Wabunge aina ya Aden Rage hawatatufikisha popote kimaendeleo

Mkuu Eschelichia Coliform aka EColi, hebu nifafanulie vizuri maana mimi kila nikikutana na watu wa Tabora wananiambia hali ni mbaya zaidi, Barabara iliyowekewa lami ambayo na watu wasio wataalam wasiojua hata CBR
Mkuu kama unazungumzia ubora hapo utakuwa sawa lakini kama tunazungumzia uwepo basi mji huu una barabara za mjini kushinda mikoa mingi sana ya Tanzania, tatizo ni utamaduni wa sisi wanyamwezi kulialia kila siku ndio maana mtu kama hajafika tbr anaweza kufikiri ni jehanamu flani hivi. Inaonekana upo fiti lakini data zako ni outdated enzi za akina kaserkandis na diamond talkies.
 
Amesababisha Ndimbo ajiuuzuru U-Afisa habari simba kwa kumwingilia madaraka yake.Anadai eti wameshamwambia ndimbo aache utangazaji ch 10.Mbona yeye ni mbunge halafu mwenyekiti wa simba.Yeye anaifanya simba kama ya kwake vile yeye ndio kila kitu. Matokeo yake simba ilpoenda kongo kucheza na motema pembe,walikaa walizuiwa kiwanja cha ndege kwa muda mrefu kwa sababu timu ilikuwa haijafanya mawasiliano na wenyeji wao kazi ambayo inapaswa kufanywa na afsa habari.
Alimtukana Ndimbo alimwita KARANI
 
Mkuu kama unazungumzia ubora hapo utakuwa sawa lakini kama tunazungumzia uwepo basi mji huu una barabara za mjini kushinda mikoa mingi sana ya Tanzania, tatizo ni utamaduni wa sisi wanyamwezi kulialia kila siku ndio maana mtu kama hajafika tbr anaweza kufikiri ni jehanamu flani hivi. Inaonekana upo fiti lakini data zako ni outdated enzi za akina kaserkandis na diamond talkies.

Mkuu ninapozungumza miaka hiyo sina maana kuwa nipo outdated japo last time Kutembelea Tabora was 2005. Hebu nieleze ni nini kipya kimefanyika tokea mwaka 2006 mpaka leo?. Kama hutumii simu kwa kuogopa megabyte charges fungua hiyo link ya google, halafua niambie kuwa nini kimeongezeka. Uwanja wa mpira umemalizika?, hizo barabara za mitaani huko gongongini, ng'ambo, National zote zimerudishiwa lami aliyoiacha mkoloni?, Kiwanda cha nyuzi kimefufuka?, Chuo cha ufugaji nyuki afrika mashariki na kati kilicho hamilishiwa olmotonyi Arusha kimerushwa?, Kiwanda cha kusindika asali kipalapala kinafanya kazi? barabara za Urambo, Sikonge zinapitika majira yote ya nchi?. Lumumba bar pale karibu na Tanzania hotel karibu na kwa mbunge wako pako active kama enzi za Kiko kids, Tabora Jazz ya kina Shem Kalenga na Marehemu Sudi Kiko?, Ule mchezo wa kuwafilisi wapinzani wa siasa wa CCM kama ulivyofanyika kwa S M Said kwa kutumia TRA umeisha?. Mkuu kwa Tabora ambapo nilikaa miaka zaidi ya nane huwezi nidanganya kitu kipya. Ukweli ni kwamba Tabora is an isolated region, Na Rage alijue hilo kama hata pigania wana Tabora 2015 CCM wataweka msanii mwingine ili kuwazuga wanatabora kuwa huenda atawaletea maendeleo. Huenda wewe utakuwa unauza mchele hapo soko kuu au una ajira serikalini ndiyo maana hujui kama kuna watu, wa Cheyo, Lwanzali, Isukamahela, Izimbili, Umanda, Igombe, Kasela, usule, Puge, ndono, kasisi, Ntalikwa, Kipalapala, masimba, Inara, Wembele, Kasisi, Ulimakafu, kalunde, Itetemia, tumbi, ufumila, you name it! Ukiacha wale wa mjini hapo kama wewe ambao wanapata mlo mmoja kwa siku.
 
Nchi ambayo Hussein bashe anatokea
Rage ni Raia wa Somalia, kama alivyo Al-Bashir. Mikoa kama Tabora wameishazoea kugalagazwa, hata enzi za watumwa wanyamwezi ndio walikuwa wa kwanza kusalimu amri, hadi watu wanasema mzigo mzito mbebeshe mnyamwezi. ndio wanabeba hivyo mizigo kama Rage. Sishangai kwa nini wameng'ang'ania CCM, utumwa bado unawaathiri
 
jamani, kauli hii sio nzuri, siipendi ina element za kibaguzi.

Mpaka watu wa Tabora na sehemu nyingine kama Singida na Morogoro mtakapozinduka usingizini na kuacha kuwachagua waarabu, wahindi na wasomali ndipo mtakapoanza kuona mabadiliko. Inashangaza nyie watu mnaacha kuwachagua watu wenu mnafurahia kuwachagua wageni kwasababu wamewapa khanga, pombe na t-shirt! zindukeni walah mtaipata vilivyo!
 
wAsomali ni hatari hata kenya wanatishia usalama sana Nairobi halafu watu wa tabora mnawapa ubunge? kweli mpo nyuma!
 
Tabora is a sleeping giant! Ni mkoa mkubwa kuliko yote kieneo sasa na una ardhi nzuri sana kwa kilimo na ufugaji na una watu wengi sana wenye afya na guvu lakini tatizo lipo kwenye thinking ya watu. nadhani watu wa tabora wamehifadhiwa zoo kwa ajili ya manufaa ya kisiasa na kifedha ya watu wachache. Kataeni hili jambo wanatabora!
 
Ukiacha wale wa mjini hapo kama wewe ambao wanapata mlo mmoja kwa siku.
Mkuu pamoja na kutaja vitongoji vyote vya tbr bado huna taarifa mpya za tbr. Hizo kiko kids zako zimekufa kitambo kama vile marquiz na bendi nyingine za enzi za mwalimu, toka 2006 mabadiliko makubwa ni barabara za lami kutoka milambo sekondari kule hadi town, lami kutoka town pale total hadi lwanzari, lami kutoka pale CCM wilaya hadi kitete hospital, imejengwa stendi mpya ya mabasi karibu na kachoma halafu vile vilabu vyote vya pombe za kienyeji vimefunga ni bar mna pub kibao zimefunguliwa, tbr sasa kuna chuo kikuu. Mkuu sijawahi kusikia au kuona familia imekula mlo mmoja kwa kukosa chakula tbr mjini.
 
Mkuu pamoja na kutaja vitongoji vyote vya tbr bado huna taarifa mpya za tbr. Hizo kiko kids zako zimekufa kitambo kama vile marquiz na bendi nyingine za enzi za mwalimu, toka 2006 mabadiliko makubwa ni barabara za lami kutoka milambo sekondari kule hadi town, lami kutoka town pale total hadi lwanzari, lami kutoka pale CCM wilaya hadi kitete hospital, imejengwa stendi mpya ya mabasi karibu na kachoma halafu vile vilabu vyote vya pombe za kienyeji vimefunga ni bar mna pub kibao zimefunguliwa, tbr sasa kuna chuo kikuu. Mkuu sijawahi kusikia au kuona familia imekula mlo mmoja kwa kukosa chakula tbr mjini.

Hii stendi niliikuta 2005. Anyway ninajua ni ile program yenu mliyotumwa ya kutetea tui kuwa ni maziwa. Tabora ya leo ipo nyuma mara 100 ya Tabora ya kati ya 1958 mpaka 1975. Kwa ujumla Tabora inarudi nyuma badala ya kusonga mbele. Tabora ni locked region, mzuunguuko wa pesa mdogo, watu wansubiri msimu wa tumbaku ndiyo wanaanza biashara msimu ukiisha nao wanatoweka. Tabora ni mkoa kati ya mikoa ya mwisho kwa elimu, shule kama Tabora School, Tabora gilrs na Mirambo wamejaa watoto wa nje ya mkoa tu.

Kama unachotetea ni Lami ya kutokea makokola mpaka soko kuu mita 250, na wewe ndiyo unaweza hata kutumia internet unakubali kuwa hayo ni maendeleo kwa kipindi cha miaka mitano basi I have doubt na judgement ya watu wa sample yako ambao naamini mpo wachache sana Tabora na mnatetea kwa kuwa mmehakikishika kula mara mbili au tatu kwa siku kwa kazi ya kupiga propaganda.

Kwa heri mkuu! tukutane kwenye thread nyingine siyo hii nilikuwa nakupa big time kwa kukuonesha kuwa hakuna ukijuacho kwa Tabora ambacho mimi sikijui.
 
Kama unachotetea ni Lami ya kutokea makokola mpaka soko kuu mita 250,.
Mkuu sasa nimekupata, mm sipigi siasa na wala sipo hapa kutetea chama au upuuzi wowote wa aina huo, mm sio mtu wa aina ya kudanganya eti umbali wa makokola hadi stendi ni mita 250. Na kwa taarifa yako hakuna mbwa yeyote aliyeko kwenye siasa za tanzania anaweza kunituma mimi. Hao wanafiki wanaweza kuwa badilisha watu wazuri kuwa waongo mm siwapendi na hata siku moja maisha yangu hayajawahi kuwategemea ila wao ndio wananitegemea kuwasaidia finacially..eat dat for dinner
 
Sikieni alichokisema jana; kuwa anawashukuru sana watu wa manicipal ya Tabora kwa kumchagua kuwa mbunge... nafasi ambayo amekuwa akitafuta kwa muda mrefu...Kwamba Tabora hawadanganyiki kwa kuwa hakuna jimbo hata moja lilochukuliwa na upinzani. Kauli ya Rage kwamba amekuwa akitafuta ubunge kwa muda mrefu inaonyesha kuwa lengo ni personal zaidi ya jamii iliyomchahua... amethibitisha tu kuwa alitaka kuwa mbungeSwala la kusema Tabora hawandanyiki ni dharau kwa watanzania. Nimuulize Rage vipi kuhusu ahadi mbalimbali ambazo zinatolewa na CCM zingine over 20 yrs old mpaka leo hazijatekelezwa je si kuwadanganya wananchi? Vp swala la umeme? Ubora wa elimu? Matatizo ya malipo ya walimu ni ahadi ya mwaka gani? Maisha bora six years later social services zinakuwa worse je si kuwadanya wananchi?Nimalize kwa kusema kama ni track record ya kudanganya basi CCM itakuwa inaongoza... after all upinzani haujawi kushika madaraka.Wabunge wasifanye bunge kuwa kijiwe cha majigambo juu ya vyama vyao na nani ni nani kamwe hawatasaidia kuleta maendeleo nchini TZ.

Waachieni wana Tabora magamba yao manake ndio mkoa unaoongoza kwa maendeleo na uchumi mzuri kuliko yooote bongo. Kumbuka mtaji wa magamba......
 
Jamani mim nimesoma tbr form 1-6 pale Mihayo secondari na Milambo. Tbr pia ni nyumbani lakin ukweli n mkoa wa kuusikitikia! Wewe Ecoli unasema barabara za lami zipi? Zile mbovu ambazo kwa mwaka zinakarabatiwa mara 2-3. Kwanza iliyongezeka ni ile ya National mpaka bank ya damu na yenyewe lami yake ni yakipuuzitu nyingine ni zile alizojenga mchina, kitete road na ile ya Line polisi na ndio barabara imara pekee mkoani.CHEYO ndio eneo la matajiri kidogo lakin halijawahi kuwa na barabara za lami tangu mkoloni aondoke.Soko kuu kuna nuka ni bovu na limechoka,uwanja wa A.Mwinyi upo vilevile! Nyumba katikati ya mji bado ni za miti na zimechoka!.,ECOLI ukiendelea kubisha ntarudi tena.
 
huyu Rage wakati wa kura za maoni kule National alisema ''jimbo hili limeongozwa na wasomi maprofesa na madokta lakini halijaendelea sasa nipeni na mimi mnaeniita msanii msanii muone ntafanya nini'' kwa hiyo anajijua ni msanii na wananchi wanamjua msanii so wamezoeana. Tabora mna safari ndefu ila kawaida yao Wanyamwezi wamezoea mizigo... ''Mzigo mzito mpe mnyamwezi'' no wonder wanyamwezi wamechagua mizigo ka Rage, Rostam Azizi, Prof. Kapuya, Hamis Kigwangalah a.k.a Said Nassoro Bagaile
 
Kwa aina ya wabunge wa akina Rage,manispaa ya Tbr itazidi kudorora! Jamaa ni bingwa wa kuongea na kujitapa tu.Huku anafikiria simba,mara mwenyekiti wa TFF mkoa ,mara mwenyekiti wa jumuia ya wazazi mkoa sasa hv n msemaji wa simba!(anawaza kukata rufaa) Kwa mjukumu haya ni mtu wa kufuata posho Dodoma halafu ndo anaamua akae Msimbazi au ofis za ccm mkoa! Hana muda wa kutumikia wananchi.
 
Nashukuru sana wana JF kuibua hoja kama hii, huyu jamaa hafai hata kidogo, muda mwingi yeye na Simba sport wala hajui matatizo ya wananchi wa Tabora kabisa, Manispaa ya Tabora ni moja manispaa zenye shida nyingi ikiwa pamoja na uongozi mbovu sana. Upande wa Elimu idara ya Sekondari kuna matatizo makubwa ambayo yamefumbiwa macho, matatizo kama pesa za likizo walimu hawalipwi, Walimu waliopo masomoni hawapati hata senti moja iwe nauli au pesa ya ghalama za masomo Rage anapiga usingizi Bungeni tu, Idara ya Afya pale Kitete nafikiri mnafahamu watu hujifungulia sakafuni, miundo mbinu kama barabara ovyo kila mwaka zina paluliwa tu hamna kinachofanyika. Rage hafai hafai hafai labda akaongeze simba.
 
Back
Top Bottom