Ndama Jeuri
JF-Expert Member
- Jul 9, 2015
- 1,503
- 1,473
HahahaNa sisi tuliolea watoto wa wanaume wenzetu kisha wakatukimbia baada ya kufanikiwa, wakawatafuta baba zao halisi, unatushauri nini?
HahahaNa sisi tuliolea watoto wa wanaume wenzetu kisha wakatukimbia baada ya kufanikiwa, wakawatafuta baba zao halisi, unatushauri nini?
Wakati mwengine mama zetu ndo tatizo,hili jambo kwa kweli sio la kutoa lawama kwa upande mmoja tu wababa, wanawake wengine vichomi,tena ukimuacha akiwa anakuhitajiHio situation ipo na kwangu,nimeamua kutulia na mwisho wa siku nimemwambia huyo mwanamke acha mm nibaki baba jina
Wapo sahihiHivyo ndivyo watoto wakiume ukiwatelekeza wanavyo-act.
Wapo wengi mtaani ambao sio mashuhuri na karibu wote wanamtazamo Kama wa Ommy
Aliombwa amzae?Anatakiwa amtafute, kwa sababu kinachotokea kina sababu; kama mzee asingepoteza muda wake kuchepuka, angezaliwa?
Je yuko tayari arudishwe kwenye suruali?Aliombwa amzae?
huu msumari wa moto sana natamani baba yangu angekuja kuusoma... amenivuruga utotoni baadae nishakuwa mkubwa amekuja kusikia mwanaye nipo zangu canada nakula maisha anahangaika kuwasumbua ndugu kutaka nimtafute how comes? ikiwa alinitelekeza mimi na mama yangu mzazi ? ubarikiweeAnaandika, Robert Heriel
Sakata la Ommy Dimpoz na baba yake linanifanya na mimi nipigilie msumari kusisitiza.
Kuna wanaume wenye tabia za kizamani kuwa ati, anaacha kwa makusudi kabisa kulea mtoto wake halafu anakuwa na mtazamo kuwa; "Akikua atanitafuta, atamtafuta baba yake". Hiyo tabia ipo na baadhi ya sisi wanaume.
Mtoto haramu,
Mtoto wa uzinzi,
Mtoto wa single mother,
Mtoto chokoraa,
Mtoto asiye na baba,
Mtoto wa nje!
Na majina mengine kama hayo licha ya kuwa yalikuwa adhabu kwa mtoto wako, hukupata muda wa kumfariji na kumuonyeshea ukaribu wako kama baba. Wewe kama baba ukachangia kwa sehemu kubwa kumuumiza mtoto kwa kile kiitwacho kutafuta maisha, kile kiitwacho ujana, kile kiitwacho magomvi yako na mama yake na sababu zingine.
Leo mtoto anakuwa, anajiweza, unafikiri atakuheshimu, unafikiri atakupenda, unafikiri atakuchukulia wewe ni baba yake? Kama wewe hukumchukulia kama mtoto wake ni ngumu yeye kukuchukulia kama baba yake. Yeye anakuona kama watu wengine, kama wewe ulivyomuona kama watoto wengine.
Ooh! Hujajua maisha, ooh huyo ni baba yako. Ndiyo ni baba lakini simchukulii kama baba, kama yeye alivyokuwa hanichukulii kama mwanaye. Mila na desturi za kijingajinga kuendekeza upuuzi ndiyo zimeifikisha Afrika hapa ilipo. Unafiki unafiki kila mahali.
Kama ulisema mtoto atakutafuta kaa usubiri mpaka utafutwe na mwanao sio usubiri amekua na kujiweza ndio uanze kumsumbua dogo.
Na dunia ilivyombaya sasa, yule uliyemtelekeza ndio Mungu anapigilia baraka hukohuko, ili akufundishe.
Mtoto wako ambaye mara nyingi ulikuwa unamuona hana msaada kwako ndiye mara nyingi baadaye huwa jiwe kuu la msingi katika sehemu ambayo wengine wote hawana uwezo wa kukusaidia.
Wanaume tujitahidi kulea watoto wetu, iwe waliozaliwa kwa bahati nasibu au wale tuliopanga. Na kama tutaamua kutelekeza basi tusisumbue watoto wetu tuliowatelekeza.
Msamaha sio lazima. Msamaha ni neema tuu ambayo siyo haki ya mkosaji. Hivyo mtoto atakavyotuchukulia ni sawa tuu, tusiwe watu wa kulalamika.
Huwezi hukumiwa na Mungu kwa kushindwa kusamehe watu. Hakuna sheria ya hivyo. Kama vile Mungu anavyosamehe apendavyo ndivyo na wewe/mimi unatoa msamaha vile upendavyo na siyo kwa shinikizo.
Mwisho, watoto waliotelekezwa kama itawapendeza mnaweza wasamehe wazazi wenu. Ingawaje najua hakuna uwezekano wa kuwa na ukaribu au mazoea ya mzazi aliyekutelekeza. Siyo baba tu hata mama. Kama hajakulea ni ngumu kuwa na ukaribu na upendo naye.
Hivyo ndivyo karma inavyofanya kazi.
Robert Heriel,
Taikon wa Fasihi,
Kwa sasa Dar es Salaam.
Ukitelekeza unakua umemfungulia njia ya mafanikio?
umemaliza kila kitu.Sio kweli.
Watoto wengi waliokataliwa ni talented na Gifted
Hizi mambo zimewahi kunikuta nikiwa mdogo,baada ya kuachana wazazi,mama yangu hakutaka msaada wowote ule wa baba,ilifikia hatua hata mshua akileta nguo alizichoma moto,baadae mshua akaamua kukaa pembeni na kutojihusisha na kutoa matunzo yoyote yale kwangu,ulipofika umri wa shule alinipa majina ya baba wa kambo aliyemuoa wakati huo,nilisoma mpaka chuo kikuu nikitumia hayo majina,nimebahtika kupata ajira,sasa nikipata kidgo namtumia biological father,hiyo hali ya kumtumia pesa baba yangu mzazi,mama yangu imekuwa inamkera mno ni vile tu nimekuwa mtu mzima anashindwa kunikemea au kunipangia ila anaumia sana! So wakati mwengine mama zetu huchangia hiyo hali,ndo maana mimi siwezi kutupa lawama kwa baba yake dimpoz,hatujui huko walikuwaje na mzazi mwenzake.
Na sisi tuliolea watoto wa wanaume wenzetu kisha wakatukimbia baada ya kufanikiwa, wakawatafuta baba zao halisi, unatushauri nini?
Wanawake ndio wanamezesha sumu. Mtoto wangu wa kwanza mama yake anampa sumu sana kuhusu mimi wakati huwa namtafuta kwenda kumjulia hali na hela natoa ila mama sababu tuna ugomvi anaihamisha hadi kwa mtoto.
Nami kwa jeuri hata akinikataa huko mbele ni poa tu.
Ndio mama yako alivyofanya?Wanawake ndio utoa lecture ya kumdis mshua iliaonekana shetani namba mbili.
Ndio mama yako alivyofanya?
Na wewe mama yako alikupandikiza chuki?Wakati mwengine mama zetu ndo tatizo,hili jambo kwa kweli sio la kutoa lawama kwa upande mmoja tu wababa, wanawake wengine vichomi,tena ukimuacha akiwa anakuhitaji
Nimemuuliza makusudi najua hajalelewa na mama ila watu kama huyu ndio wanaongeza kusema akina mama wanapandikiza chuki Kwa watoto.Muulize Mama yake akifanya Jambo Baya au Baba yake akifanya Jambo Baya Hana uwezo wa kuliona?
Ni kweli mtoto anaweza kudanganywa lakini kuna umri akifika hasa umri wa kupevuka anaanza kujua mbivu na mbichi.
Tukubali tuu kuwa kama kuna watoto tumetelekeza iwe Kwa sababu yoyote basi tukubali matokeo tuu
Nimemuuliza makusudi najua hajalelewa na mama ila watu kama huyu ndio wanaongeza kusema akina mama wanapandikiza chuki Kwa watoto.
Sana tu! Tena ilifikia hatua wakishirikiana na baba wa kambo ambaye nilikuwa natumia majina yake shuleni,walikuwa wananimbia negative kuhusu mzee,mara mshirikina,nikimuona nisimsalimie,na kweli ilifika kipindi nikienda likizo kumuona auncle,akija nilikuwa simsalimii kabisa! Na nilikuwa namkimbia.hahahahaNa wewe mama yako alikupandikiza chuki?
Hizi mambo zimewahi kunikuta nikiwa mdogo,baada ya kuachana wazazi,mama yangu hakutaka msaada wowote ule wa baba,ilifikia hatua hata mshua akileta nguo alizichoma moto,baadae mshua akaamua kukaa pembeni na kutojihusisha na kutoa matunzo yoyote yale kwangu,ulipofika umri wa shule alinipa majina ya baba wa kambo aliyemuoa wakati huo,nilisoma mpaka chuo kikuu nikitumia hayo majina,nimebahtika kupata ajira,sasa nikipata kidgo namtumia biological father,hiyo hali ya kumtumia pesa baba yangu mzazi,mama yangu imekuwa inamkera mno ni vile tu nimekuwa mtu mzima anashindwa kunikemea au kunipangia ila anaumia sana! So wakati mwengine mama zetu huchangia hiyo hali,ndo maana mimi siwezi kutupa lawama kwa baba yake dimpoz,hatujui huko walikuwaje na mzazi mwenzake.