Just Nana
JF-Expert Member
- Jul 27, 2023
- 500
- 1,001
Hiki ni kisa kinamuhusu mmoja wetu humu Jf...alisoma story ya Bella akaomba anisimulie story yake nami niiandike muisome...anaomba radhi kwa atakaowakwaza , yalishatokea ,anapambana kujisamehe....twende kazi....
Naitwa Peter ( sio jina halisi)...hadi wakati huu namudu kusimulia kisa changu kupitia Nana ,niko na miaka 43, ni mkristo niliyekulia na kulelewa kwenye familia ya dini sana, naijua dini na kuiheshimu, nimesoma shule za seminary kuanzia kidato cha kwanza hadi cha sita, nikisema naijua dini naomba muelewe, ilifikia kipindi wazazi walihisi labda nitakua Padre kwa namna nilivyokua naenenda, nilikua na utii sana, kwa Mungu na wanadamu, nikiri tu nilikua mmoja wa wale waliobahatika kupata malezi bora, sina la kuwalaumu wazazi wala walimu kwa haya yaliyonisibu, nitakachoenda kusimulia hakitowafurahisha, ila hakuna namna ya kubadilisha njano kua buluu, 'that's me...'I made that mistake and I am paying for it '...
Kutokana na kuishi maisha ya dini na ile hofu ya kutenda dhambi ilisababisha kuchelewa sana kuyafahamu mapenzi, si kwamba sikua na hisia nayo hapana...kama mwanaume rijali nilikua napata matamanio lakini kuna hofu unaipata kila ukiwaza ngono, ilinisaidia kuchelewa kuanza sanaa nzima ya mahusiano, naiita sanaa maana kama huna ufundi thabiti lazma yakutoe kwenye mchezo.
Nakumbuka nilikua safarini kurudi nyumbani Mbeya baada ya kufunga shule nikiwa kidato cha tano , kwenye siti ya basi nililokua nimepanda alikaa binti mrembo sana, hadi wakati huo sikua na mahusiano kabisa, wapo mabinti waliokua wananitumia kadi na barua shuleni ambao tulibahatika kufahamiana kupitia matamasha ya kidini, na mialiko ya hapa na pale ya kishule, lakini sikua nimeamua rasmi kuingia mapenzini, nilikua napata faraja tu kupokea barua zao, nasoma, nafurahia ila sikuwahi kujibu, wanasema mwanaume hajisifii muonekano, ila nikiri kua nilikua na muonekano fulani ivi wa kumfanya kiumbe wa kike aniangalie mara mbili kila apatapo nafasi ya kupishana nami, najua kua niliwatesa sana dada zetu maana sio kwa zile barua na kadi za maua zenye jumbe za kuvutia.
Turudi kwenye basi, safari ilitaradadi, kuna mda yule dada alikua anasinzia, kwa bahati mbaya au niseme nzuri, alinogewa na usingizi akanilalia mabegani, mabasi ya kipindi kile hayakua ya kisasa saaana, katikati ya siti na siti hapakua na ule mkono wa kutenga siti, kwa hiyo mkikaa lazma mtagusana, na mtu akisinzia kama akizidiwa na usingizi lazma atakulalia, ndicho kilichotokea. Kuna namna fulani hivi ya kama umeme ulipita maungoni mwangu, nikiri tu kua sikuwahi kukaribiana na kiumbe wakike kwa ukaribu wa kupitiliza kama siku ile.
Nilitamani ile safari isiishe, kuna raha ya ajabu sana niliipata kutokana na mguso ule, gari ilipofika sehemu ya kupata chakula, baada ya matangazo na kuona binti hana dalili ya kuamka, ikabidi nimuamshe. Aliamka akaniangalia kwa aibu za kike, akaomba radhi kwa kunisumbua na kuniegemea, nikamwambia usijali, tukashuka kwa ajili ya kupata chakula na kujistiri , baada ya dakika kadhaa tukarejea safarini kuendelea na safari.
Alirudi na mazaga kibao ya kula, mfukoni sikua vizuri, tiketi yenyewe nilifanya kukatiwa na mwalimu wangu wa darasa baada ya kufanya mawasiliano na wazazi na kutopata mrejesho kwa wakati. Mawasiliano kipindi kile ilikua ni kwa njia ya barua , ilikua ukishaituma , usubiri hadi wiki tatu ndipo upate majibu. Kama wazazi walituma pesa ya nauli basi nilipishana nayo, kwa msaada wa mwalimu nikafanikiwa kusafiri.
Binti alinikaribisha kwa chakula, ule ustaarabu wa kitanzania kukataa mara ya kwanza unapokaribishwa mlo nami niliutumia, ila kiuhalisia nilikua na njaa isiyo kifani, mfukoni nilibakiwa na pesa kidogo ambayo nilifanya utaratibu nikanywa chai na maandazi mawili kisha nikarudi kwenye basi, kwahiyo nikisema kua nilikua sina njaa nitakua muongo, binti alikua katika msisitizo nikajikuta nimeopoa kipaja cha kuku, mara viazi vya kukaanga maarufu kama chipsi, mara kajuice, ghafla tukajikuta tunapiga story za hapa na pale huku tukishambulia chakula pamoja.
Tulifika Mbeya usiku wa saa nne, mimi nilikua nimefika lakini binti alitakiwa kulala ili kesho aelekee kwao Sumbawanga, kumbuka nyumbani hawana taarifa Kama nipo safarini, nikaona sio jambo la busara kumuacha mtoto mrembo kama yule alale peke yake nyumba ya kulala wageni. Binti aliomba kampani yangu , Mimi ni nani nikatae wapendwa, ukizingatia bado nilihitaji kujua kinachoendelea baada ya kusikia kale kamvutano ka umeme kalikotokea kwenye gari, nikasema leo ndio siku ya kufanya majaribio yangu.
Naitwa Peter ( sio jina halisi)...hadi wakati huu namudu kusimulia kisa changu kupitia Nana ,niko na miaka 43, ni mkristo niliyekulia na kulelewa kwenye familia ya dini sana, naijua dini na kuiheshimu, nimesoma shule za seminary kuanzia kidato cha kwanza hadi cha sita, nikisema naijua dini naomba muelewe, ilifikia kipindi wazazi walihisi labda nitakua Padre kwa namna nilivyokua naenenda, nilikua na utii sana, kwa Mungu na wanadamu, nikiri tu nilikua mmoja wa wale waliobahatika kupata malezi bora, sina la kuwalaumu wazazi wala walimu kwa haya yaliyonisibu, nitakachoenda kusimulia hakitowafurahisha, ila hakuna namna ya kubadilisha njano kua buluu, 'that's me...'I made that mistake and I am paying for it '...
Kutokana na kuishi maisha ya dini na ile hofu ya kutenda dhambi ilisababisha kuchelewa sana kuyafahamu mapenzi, si kwamba sikua na hisia nayo hapana...kama mwanaume rijali nilikua napata matamanio lakini kuna hofu unaipata kila ukiwaza ngono, ilinisaidia kuchelewa kuanza sanaa nzima ya mahusiano, naiita sanaa maana kama huna ufundi thabiti lazma yakutoe kwenye mchezo.
Nakumbuka nilikua safarini kurudi nyumbani Mbeya baada ya kufunga shule nikiwa kidato cha tano , kwenye siti ya basi nililokua nimepanda alikaa binti mrembo sana, hadi wakati huo sikua na mahusiano kabisa, wapo mabinti waliokua wananitumia kadi na barua shuleni ambao tulibahatika kufahamiana kupitia matamasha ya kidini, na mialiko ya hapa na pale ya kishule, lakini sikua nimeamua rasmi kuingia mapenzini, nilikua napata faraja tu kupokea barua zao, nasoma, nafurahia ila sikuwahi kujibu, wanasema mwanaume hajisifii muonekano, ila nikiri kua nilikua na muonekano fulani ivi wa kumfanya kiumbe wa kike aniangalie mara mbili kila apatapo nafasi ya kupishana nami, najua kua niliwatesa sana dada zetu maana sio kwa zile barua na kadi za maua zenye jumbe za kuvutia.
Turudi kwenye basi, safari ilitaradadi, kuna mda yule dada alikua anasinzia, kwa bahati mbaya au niseme nzuri, alinogewa na usingizi akanilalia mabegani, mabasi ya kipindi kile hayakua ya kisasa saaana, katikati ya siti na siti hapakua na ule mkono wa kutenga siti, kwa hiyo mkikaa lazma mtagusana, na mtu akisinzia kama akizidiwa na usingizi lazma atakulalia, ndicho kilichotokea. Kuna namna fulani hivi ya kama umeme ulipita maungoni mwangu, nikiri tu kua sikuwahi kukaribiana na kiumbe wakike kwa ukaribu wa kupitiliza kama siku ile.
Nilitamani ile safari isiishe, kuna raha ya ajabu sana niliipata kutokana na mguso ule, gari ilipofika sehemu ya kupata chakula, baada ya matangazo na kuona binti hana dalili ya kuamka, ikabidi nimuamshe. Aliamka akaniangalia kwa aibu za kike, akaomba radhi kwa kunisumbua na kuniegemea, nikamwambia usijali, tukashuka kwa ajili ya kupata chakula na kujistiri , baada ya dakika kadhaa tukarejea safarini kuendelea na safari.
Alirudi na mazaga kibao ya kula, mfukoni sikua vizuri, tiketi yenyewe nilifanya kukatiwa na mwalimu wangu wa darasa baada ya kufanya mawasiliano na wazazi na kutopata mrejesho kwa wakati. Mawasiliano kipindi kile ilikua ni kwa njia ya barua , ilikua ukishaituma , usubiri hadi wiki tatu ndipo upate majibu. Kama wazazi walituma pesa ya nauli basi nilipishana nayo, kwa msaada wa mwalimu nikafanikiwa kusafiri.
Binti alinikaribisha kwa chakula, ule ustaarabu wa kitanzania kukataa mara ya kwanza unapokaribishwa mlo nami niliutumia, ila kiuhalisia nilikua na njaa isiyo kifani, mfukoni nilibakiwa na pesa kidogo ambayo nilifanya utaratibu nikanywa chai na maandazi mawili kisha nikarudi kwenye basi, kwahiyo nikisema kua nilikua sina njaa nitakua muongo, binti alikua katika msisitizo nikajikuta nimeopoa kipaja cha kuku, mara viazi vya kukaanga maarufu kama chipsi, mara kajuice, ghafla tukajikuta tunapiga story za hapa na pale huku tukishambulia chakula pamoja.
Tulifika Mbeya usiku wa saa nne, mimi nilikua nimefika lakini binti alitakiwa kulala ili kesho aelekee kwao Sumbawanga, kumbuka nyumbani hawana taarifa Kama nipo safarini, nikaona sio jambo la busara kumuacha mtoto mrembo kama yule alale peke yake nyumba ya kulala wageni. Binti aliomba kampani yangu , Mimi ni nani nikatae wapendwa, ukizingatia bado nilihitaji kujua kinachoendelea baada ya kusikia kale kamvutano ka umeme kalikotokea kwenye gari, nikasema leo ndio siku ya kufanya majaribio yangu.