Mangandula
Senior Member
- Nov 30, 2011
- 184
- 37
Wafanyabiashara wa maduka yanayozunguka soko kuu Makambako, leo wameandamana na kuziba barabara zote kuu za songea, mbeya na Iringa. Tatizo ni walinzi waliowaweka wao wenyewe kwa ajili ya kulinda maduka usiku kukutwa na funguo bandia pia kuwafuma wakiwa ndani ya maduka yao usiku wa saa 8, hii ilitokana na mlinzi mwenzao kuwajulisha wenye mali! Vulugu zimeanza baada ya polisi kuwaachia watuhumiwa jioni hii na kumkamata m/kiti wa soko na kumsweka ndani, hapo ndipo peoples power ilipoanza, polisi wamelazimika kuita FFU kutoka Iringa na Njombe, hivi ninavyo andika post hii mabomu ya machozi yanapigwa hovyo na watu wanakimbia hovyo. Chanzo cha habari- wananchi Makambako.