Vurugu Makambako

Wafanyabiashara wa maduka yanayozunguka soko kuu Makambako, leo wameandamana na kuziba barabara zote kuu za songea, mbeya na Iringa. Tatizo ni walinzi waliowaweka wao wenyewe kwa ajili ya kulinda maduka usiku kukutwa na funguo bandia pia kuwafuma wakiwa ndani ya maduka yao usiku wa saa 8, hii ilitokana na mlinzi mwenzao kuwajulisha wenye mali! Vulugu zimeanza baada ya polisi kuwaachia watuhumiwa jioni hii na kumkamata m/kiti wa soko na kumsweka ndani, hapo ndipo peoples power ilipoanza, polisi wamelazimika kuita FFU kutoka Iringa na Njombe, hivi ninavyo andika post hii mabomu ya machozi yanapigwa hovyo na watu wanakimbia hovyo. Chanzo cha habari- wananchi Makambako.

Hawa askari wetu vipi,mbona wao ndio waliosababisha vurugu zote hizi kwa kuwaachia watuhumiwa?Ni kweli wao wana mabomu na wananchi hawana kitu.Hivi nyie maaskari mnawafundisha nini watanzania,mnataka kusema hii ndiyo nja mwafaka ya kuleta amani katika nchi?Wafanyabiashara wameibiwa mali zao na ninyi bila huruma mnacheka na wezi,mnadhani ni rahisi kuwanyamazisha wafanyabiashara kwa mabomu ya machozi?ole wenu mnaotetea watuhumiwa,ipo siku nanyi nguvu ya umma utawashukia msijue cha kufanya.
 
imenibidi niongee na rafiki yangu ambaye ni mfanyabiashara hapo nijue kulikoni? huu mchezo wa walinzi kuiba usiku baada ya wenye mali kuondoka ulikuwa unafanyika kwa muda mrefu ila baadhi ya walinzi hawakuufurahia na hivyo kutoshiriki. walichofanya ni kuwataarifu viongozi wa soko nini huendelea usiku na kuwaahidi kuwa punde wakiwabip usiku basi wajue kazi imeanza. Viongozi wa soko wakapata missed call na kwenda sokoni wakawakuta baadhi ya walinzi wakiwa na master keys wamefungua duka na wanaiba bidhaa. viongozi wa soko wakawashushia kipigo kizito walinzi wezi na kuwaita polisi. polisi walichofanya walipofika eneo la tukio waliwachukua wale walinzi pamoja na viongozi wa soko. walipofika kituoni wakawaweka ndani viongozi wa soko na wale walinzi wakapelekwa hospitali ambako wamelzwa mpaka sasa hali zao zikiwa mbaya. wafanyabiashara wengine wamekasirishwa na kitendo cha polisi kuwaweka ndani viongozi wao ndipo akapelekea kufungwa kwa barabara kushinikiza viongozi wao kuachiwa na hatimaye polisi ikatii kutokana na vurugu hizo. kwa sasa viongozi wametolewa na walinzi bado wapo hospitali wakiwa mahututi na pingu mkononi.

Mistari yako inasomeka na kueleweka vizuri sana, keep it up whenever informing anything esp. to jf
 
Wafanyabiashara wa maduka yanayozunguka soko kuu Makambako, leo wameandamana na kuziba barabara zote kuu za songea, mbeya na Iringa. Tatizo ni walinzi waliowaweka wao wenyewe kwa ajili ya kulinda maduka usiku kukutwa na funguo bandia pia kuwafuma wakiwa ndani ya maduka yao usiku wa saa 8, hii ilitokana na mlinzi mwenzao kuwajulisha wenye mali! Vulugu zimeanza baada ya polisi kuwaachia watuhumiwa jioni hii na kumkamata m/kiti wa soko na kumsweka ndani, hapo ndipo peoples power ilipoanza, polisi wamelazimika kuita FFU kutoka Iringa na Njombe, hivi ninavyo andika post hii mabomu ya machozi yanapigwa hovyo na watu wanakimbia hovyo. Chanzo cha habari- wananchi Makambako.

Tafsiri ya neno 'vurugu' ni kuvuruga utaratibu,kanuni mengine mtajazia wadau.Hapa polisi wanahusika na kuvuruga utaratibu kanuni kwa watuhumiwa waliowakamata,kesho ktk vyombo vya habari atakuja IGP akiwahimiza wananchi watii sheria bila shuruti.
 
walinzi wawaweke wenyewe waandamane kwa serikali!
Huu upuuzi wa maandamano ulioanzishwa na hawa jamaa bila elimu ya kutosha unaleta shida sana.

hapa inanilazimu kukuuliza wewe ni wa aina gani,usikurupuke soma kitu uelewe ndio uchangie mada.Kimandolu wewe.
 
walinzi wawaweke wenyewe waandamane kwa serikali!
Huu upuuzi wa maandamano ulioanzishwa na hawa jamaa bila elimu ya kutosha unaleta shida sana.
[h=6]Dunia yako chaguo lako.. Chagua kutukana matusi, chagua kuomba radhi.. Kudadadeki.[/h]
 
Back
Top Bottom