Vodacom Tanzania: Support thread (Maswali, malalamiko na Ushauri)

Nina miezi sasa,kila nikipiga huduma kwa wateja umefikia ukomo kupiga simu huduma kwa wateja,wanataka nitumie namba ya kulipia,nayo nawapigia sipati ufumbuzi,na ukiacha salio wanachukua!
Airtel nao majanga mwezi wa tatu sasa nikitaka huduma ya airtel Yatosha Noma(airtel to Airtel) inagoma ,ila kifurushi cha airtel kwenda mitandao yote inakubali,ambayo sihitaji,nawapigia CC wanataka tsh 60 kuungoea na mhudumu,nakubali wananikata...ila mhudumu hana uwezo wowote...hii ni tatatizo la shirika letu la Umma kufa TTCL wangekua wamejiamilisha mambo yangekua poa
 
Nina miezi sasa,kila nikipiga huduma kwa wateja umefikia ukomo kupiga simu huduma kwa wateja,wanataka nitumie namba ya kulipia,nayo nawapigia sipati ufumbuzi,na ukiacha salio wanachukua!
Airtel nao majanga mwezi wa tatu sasa nikitaka huduma ya airtel Yatosha Noma(airtel to Airtel) inagoma ,ila kifurushi cha airtel kwenda mitandao yote inakubali,ambayo sihitaji,nawapigia CC wanataka tsh 60 kuungoea na mhudumu,nakubali wananikata...ila mhudumu hana uwezo wowote...hii ni tatatizo la shirika letu la Umma kufa TTCL wangekua wamejiamilisha mambo yangekua poa

Hii ndo Tanzania bwana, yaani kila kitu kiko kwenye auto pilot kinajiendea tu, marubani wote wamekata mbonji ila tutafika tu.

Vodacom kazi ni kwako
Airtel baba lao
Tigo kabaaang
TTCL ilishajifia
sijui twende wapi?
 
Vodacom majanga,, ya kwangu nimeacha kuiwekea vocha mwezi sasa na sina mpango kabisa. Aitel ndo mpango mzima najirusha cha wiki natumia saafii mpk vinakutana.
 
Si kweli KWA wiki mbili mfululizo nimepata Hilo tatizo, NA hela inakwenda
Habari Bijou tafadhali tutumie namba yako ya simu tufuatilie suala hili katika mifumo yetu. Ni kwamba hakuna kifurushi cha mteja kinaminywa/punguzwa.
 
Last edited by a moderator:
bora umekuja mkuu, sijui siku izi mmekuaje, jana nimenunua kifurushi kwa ajili ya modem yangu, kwa ajili ya wyf na kwa ajili ya simu yangu ikiwa ni pamoja na dakika na sms, simu ya wyf ilikuwa na data ON, haikukaa nusu saa kikakata, nimechomeka Modem kudownlod Whatsapp app yenye MB 15 tu ila bunndle ikikata apo apo. Nimebaki na bundle ya simu yangu tu, nimeamua kuipa adhabu line yangu, ntakuwa nachomoa line ya simu ili nitumie kifurushi icho tu wiki nzima mpaka kiishe.

COMPLAIN 2
VodaCom siku izi mnakuwa wasanii, nilinunua simu kwenye duka lenu moja/naliifadhi, izo smartphone nilichukua mbili, moja iko poa ila nyingine Vodafone 875 black ni kimeo, ukipiga simu inakata netowrk apo apo, niliporudisha simu ilikuwa kimbembe kunielewa kuwa network ni mgogoro, bahati nzuri simu ikaita niko mbele ya maafisa wenu ikakata na kuandika EMERGENCE CALLS ONLY, apo ndo wakanielewa ila baada ya kutumia energy kuuubwa!!

Simu wakasema niwaachie ili irudishwe then watanipa jibu, wiki ya pili sasa kimya, yani najipanga nikirudi patachimbika,kwa nini mnazingua ivo?? Na sitakubali simu ile ile kama mmeenda kuirekebisha kama kuchomelea network Ic, nimenote specifications pembeni ikirudi ile kwa kweli sitawaelewa, pia mjue mtu akinunua kitu kibofu dawa ni kumpa kipya si kumzungusha, pia mimi sikununua simu makao makuu, iweje mniambie nisubiri ipelekwe makao makuu,nimeweka line pembeni nikisubiri simu wiki kibao............rekebisha aisee, otherwise nitakuwa balozi mbaya wa Vodacom!!!
Habari Gsana kuhusiana na masuala haya tafadhali tutumie namba ya simu kwa mawasiliano zaidi.
 
Last edited by a moderator:
kweli mkuu, siku nilipopiga simu mdada kanibishia then anasema...nona unielewi,asante kwa kupga vodacom, akakata simu...nlishangaa sana

Hapa atakuja mr Vodacom Tanzania akupige Kiswahili weee mpaka ushangae. Ukimwambia habari za huduma kwa wateja anajifanya kupotezea na badala yake anakuja na habari za mafundi wao. Mi nimeamua kumnyamazia tu maana kampeni yangu ya kuwahamasisha ndugu, jamaa na marafiki wahame huko imefikia 76% mpaka sasa. Sipigizani kelele tena na huduma kwa wateja wa voda, niko mtandao wenye kujali shida za wateja.
Wakuu maswala haya yote yanazingatiwa na kuchukuliwa hatua ikiwemo kuwawajibisha watoa huduma wenye kauli zisizostahili kwasababu simu zote zinarekodiwa. Ahsanteni
 
hivi ni nani atatuokoa kutoka kwenye ulaghai na wizi wa Voda?

nimekuwa mteja wa Vodacom tangu waanze biashara yao nchini. Hii kampuni inaendeshwa kiulaghai-laghai sana na sijui tutawezaje kuwapa somo wawe wakweli.

Kuna ofa ya uongo ya HAPPY hour, miongoni mwa uongo mwingine chungu nzima. Labda hapa sasa utakumbuka na lile tangazo lao eti swala anamfukuza chui. Yaani voda ni wadanganyifu, ni wadanganyifu sana! Nimechagua dakika 60 kwa 200/- mara nyingi. Hiyo ndo happy hour yenyewe. Nikiongea dakika 7 inakata. NDUGU MTEJA KIFURUSHI CHAKO KIMEKWISHA. Mbona mimi naona dakika 60 ni nyingi kuzidi dakika 7?

Leo saa 1.30 nimechagua HAPPY hour ya dakika 20 kwa sh. 100 kujaribu hiyo. nusu saa baadaye nimeletewa ujumbe NDUGU MTEJA KIFURUSHI CHAKO KIMEKWISHA.

Hivi vifurushi vya VODA vinaliwa na nani? Mbona mie siwaelewi hawa? Au hawa watu wanaona Tanzania hatujui kuhesabu dakika?

Au nyie wenzangu vifurushi vyenu vinadumu?

Habari tzbiz pole sana kwa suala hili na tunaomba kufafanua namna Happy Hour inavyokuwa. Ni kwamba huduma hii inakupa dakika 60 kupiga simu kuanzia muda uliojiunga, hii inaamanisha kuwa ukijiunga saa 2 asubuhi huduma yako itakwisha dakika 60 kutoka saa 2 asubuhi kwa maana ya saa 3. Ukipiga simu saa 2 dk 40 unakuwa umebakiza dakika 20 kufikia mwisho wa kifurushi chako.

Kwahiyo kifurushi ulichojiunga saa 1:30 cha dakika 20 ilikuwa ni sahihi kupokea ujumbe kuwa kifurushi chako kimekwisha dakika 30 baada ya kujiunga.Tunaimani maelezo haya yamefafanua vyema suala hili
 
Last edited by a moderator:
Mkuu tzbiz,

I second you, hivi karibuni kuwekuwa na wizi wa ajabu Vodacom kwa wateja, binafsi nimekuwa nikijiunga na vifurushi vya kila siku kwa muda sasa, na matumizi hayajaongezeka lakini hivi karibu(wiki tatu sasa) kila nikijiunga within no time naambiwa "muda/ Salio wa kifurushi chako umekwisha" ninejaribu kujiunga vifurusgi vyote viwili vya wiki pamoja na vile vya siku kuthibitisha lakini bado 'mchezo mchafu' ni ule ule.


Vodacom you have to step up.

Habari hippocratessocrates tafadhali tutumie namba ya simu kwa mawasiliano zaidi.
 
Habari Gsana kuhusiana na masuala haya tafadhali tutumie namba ya simu kwa mawasiliano zaidi.

mkuu sisi apa jf members ni segment ndogo sana tunawakilisha jamii, sasa namba za simu utachukua ngapi? Ningekushauri uchukue complains zote zfanyiwe kazi then jamii itaona mrejesho ila utamaliza tatizo langu then kesho kwa mwingine, hope unanielewa mkuu.
 
Last edited by a moderator:
Habari Gsana kuhusiana na masuala haya tafadhali tutumie namba ya simu kwa mawasiliano zaidi.

sawa mkuu ila nakuomba solve ili tatizo, mtu anakuja kununua simu, anapewa simu mbovu like touch screen, network issue, au kujizima, anairudisha then anaambiwa hakuna simu kupewa nyingine mpaka simu ipelekwe makao makuu then anaambiwa asubirie simu nyingine au jibu toka head office, iyo ni biashara gani mkuu??

Nadhani inafaa mjipange au pia uzeni simu zilizokuwa tested tayari sio kumuacha mtu akagundue tatizo mbele ya safari, inapunduza confidence na reputation ya kampuni.

Nasubiria simu yangu kwanza, isipoletwa au kiswahili kingine then ndo ntarudi kwako...
 
Last edited by a moderator:
Wakuu maswala haya yote yanazingatiwa na kuchukuliwa hatua ikiwemo kuwawajibisha watoa huduma wenye kauli zisizostahili kwasababu simu zote zinarekodiwa. Ahsanteni
Kwa sasa naiogopa voda hakuna mfano, itoshe tu kusema nimenyosha mikono.
 
Vodacom ni wezi sana yaani hiyo cheka bombastic kifurushi muda wa maongezi umepunguzwa lakini hela ya manunuzi ni Ile ile.Kinachoniudhi kupitia kiasi ni mb yaani ukiangalia video hata sek 30 unaambiwa kifurushi cha mb kimeisha yaani mnakera sana.Pia wahudumu wa voda ni wezi na matapeli kama pale mlimani city nishawahi kutapeliwa tshs 40000
 
Wamekuwa wakiiba hela kwenye account yangu, mfano jana sh. 500 ikapotea bila sababu.
Leo tena sh. 132 sijui imeenda wapi? Mnatia aibu sana vodacom.
Kuna thread nyingi sana humu, zikiwalalamikia voda lakini mbona hamjirekebishi?? Angrrrrrrr....
 
Back
Top Bottom