kisugujira
JF-Expert Member
- Aug 13, 2012
- 774
- 196
WanaJF,
Kutokana na usumbufu wa mawasiliano uliotokea tarehe 16/8/2013, Vodacom wameamua kuwaomba radhi wateja wao kwa kuwatumia ujumbe wa maneno unaosema, "Ndugu mteja,Tunapenda kukutaarifu kuwa huduma zetu zimerejea.Tunaomba radhi kwa usumbufu uliotokea tarehe 16/8/2013.Endelea kufurahia huduma za Vodacom."
Kuomba radhi wateja kwa kutuma ujumbe mfupi wa maneno peke yake hakutoshi! Vodacom wanatakiwa kutuambia ni vipi wataturudishia wateja wao vifurushi vya internet vya masaa tulivyokuwa tumevinunua na kupotea bila kutumika kutokana na kutokuwepo kwa mawasiliano! Bila kufanya hivyo Vodacom wataendelea kuonekana wezi! Waturudishie vifurushi vyetu ili tuendelee kufurahia huduma za Vodacom!
Kutokana na usumbufu wa mawasiliano uliotokea tarehe 16/8/2013, Vodacom wameamua kuwaomba radhi wateja wao kwa kuwatumia ujumbe wa maneno unaosema, "Ndugu mteja,Tunapenda kukutaarifu kuwa huduma zetu zimerejea.Tunaomba radhi kwa usumbufu uliotokea tarehe 16/8/2013.Endelea kufurahia huduma za Vodacom."
Kuomba radhi wateja kwa kutuma ujumbe mfupi wa maneno peke yake hakutoshi! Vodacom wanatakiwa kutuambia ni vipi wataturudishia wateja wao vifurushi vya internet vya masaa tulivyokuwa tumevinunua na kupotea bila kutumika kutokana na kutokuwepo kwa mawasiliano! Bila kufanya hivyo Vodacom wataendelea kuonekana wezi! Waturudishie vifurushi vyetu ili tuendelee kufurahia huduma za Vodacom!