kuna post nilisoma juzi kati humu kuwa mashine ya kuchoma moto mabaki ya binadam muhimbili haifanyi kazi,yawezekana yametoka huko, Mtazamo wangu
Wataalamu wanasema mawili....
1..aidha madaktari wanafunzi ambao wanajifunza zaidi kuhusu maiti ndio wamemeliza masomo yao now ndo wanazitupa
2..mpango wa kubadilishana maiti kwa ajili ya kujifunza....hivo mafunzo yameisha na wamezitupa.
Swali...
nimeenda kuzishuhudia ni nyingi sana, halafu ni vipande vipande, kuna zinazovuja damu, kuna zilizokauka, kuna zilizochunwa ngozi.
Dereva aliyekuwa anaendesha hiyo Hilux amekamatwa yuko police Bunju A.....wananchi wamekizingira kituo wanataka wamuue dereva aliyetumwa kazi hiyo ya kumwaga mabaki ya miili.
Bunju hali sasa si shwari, risasi zinapigwa, watu wamebeba silaha za jadi wanataka kubomoa kituo ili wamuue dereva.
Picha na video ninazo ila niko mbali na laptop.
Daah sasa hawa wananchi wakimuua huyo dereva tutawajuaje wahusika. Inabidi polisi wafanye kazi yao hadi wahusika kamili wapatikane. Huyo dereva ni mtumwa tu
Wameenda mpaka hiyo nyumba waliyohifadhia hizo maiti, watu wamesepa.
Ila inawezekana zimetoka Hospitali
Mkuu nakula bia hapa delighton jirani na kituo cha polisi bunju A na nipo na baadhi ya maafande wa pale....Bunju pako shwari kabisa.....mimi mwenyewe napata news hapa JF
Mkuu nakula bia hapa delighton jirani na kituo cha polisi bunju A na nipo na baadhi ya maafande wa pale....Bunju pako shwari kabisa.....mimi mwenyewe napata news hapa JF
Basi hao muhimbili ndio wana kesi hapo, kwa nini watupe mabaki kienyeji hivyo?
Mkuu hili ni tukio la muda huu au mapema kidogo?
usilete Ubishi sema tu Bunju iko Dar, kwani wewe unajua Matejoo, Madizini, Kitwiru, Busweru, Isevya au Mwakibete ziko wapi?Kukaa simanjiro haina maana usiijue bunju.
Mi mbona nakaa Simanjiro na hadi Magwepande napafahamu ingawa sijang'olewa kucha.
Basi hao muhimbili ndio wana kesi hapo, kwa nini watupe mabaki kienyeji hivyo?
ustake kunambia umeunga dots ndo hao viungo vyao vimekutwa bunju