bibikuku
JF-Expert Member
- Feb 16, 2011
- 832
- 495
Baada ya Juzi Sofia Simba kukanusha kuhusika moja kwa moja na mabadiliko ya mchakato wa kupata wabunge wa viti maalum, sasa Mama Kilango ametoka UK na kuwawahi wenyeviti wa mikoa na wilaya huhohuko Dodoma na kuwaandalia dinner ambayo iliambatana na manywaji na nauli kwa washiriki wote. Lengo ni kupata uungwaji mkono ikiwa ni maandalizi ya uchaguzi mkuu. Endelea kujihabarisha hapa..........
Wagombea UWT waanza kupigana vijembe | Send to a friend |
Thursday, 15 March 2012 20:08 |
0diggsdigg Habel Chidawali, Dodoma HOMA ya Uchaguzi ndani ya Umoja wa Wanawake (UWT) wa CCM imepanda huku baadhi yao wakianza kuvurugana ingawa muda wa kampeni haujafika. Katika kikao cha Wenyeviti wa Mikoa na Wilaya kilichomalizika juzi usiku mjini hapa, baadhi ya wagombea walikuwa wakipita huku na kule kwa ajili ya kuwasaka wapiga kura huku vikao vya usiku vikifanyika na fedha nyingi zikitembezwa. Mbali na hilo, baadhi ya wenyeviti hao kwa nyakati tofauti walieleza kuwa joto liko juu kwa wagombea kwani baadhi yao wameshaanza kampeni hata kabla ya ratiba ya chama huku wakirushiana vijembe vya wazi. Hilo sio la siri, ni kweli tumeitwa katika Ukumbi wa Kilimani Barabara ya Ntyuka ambako tumekula na kunywa na pia tumewezeshwa vijinauli kidogo, lakini hayo siyo ya kuandika gazetini we waambie tulikuwa na mambo yetu, alisema mmoja wa Wenyeviti wa Mikoa ya Kanda ya Ziwa ambaye hakutaka jina lake liandikwe. Mwenyekiti huyo alimtuhumu mmoja wa wagombea kuwa alipanda ndege kutoka Uingereza na kuja nchini kwa ajili ya kukiwahi kikao hicho huku akimwacha mumewe huko lengo kubwa likiwa ni kuwaona wajumbe waliokuwa wakishirikia kikao mjini Dodoma. Baadhi ya watu wanaotajwa kugombea nafasi ya Mwenyekiti wa UWT Taifa ni pamoja na Mbunge wa Same Mashariki, Anne Kilango Malecele na Mwenyekiti wa Sasa Sophia Simba huku ikielezwa kuwa kutakuwa na mpambano wa visasi kwa wagombea hao. Mmoja wa wenyeviti wa Wilaya za Mkoa wa Dodoma ambaye hakutaka jina lake kuandikwa gazetini, alisema Watu wengine wamekuwa ni wapambanaji wa kupinga ufisadi, lakini wao ndio wa kwanza kutoa fedha, jana kuna mtu alitoa Sh 30,000 kwa kila mjumbe eti kwa ajili ya kutusalimia tu, yaani ndio maana wakizipata nafasi hizi wanatutelekeza kwani fedha wanatumia nyingi mno kuzisaka. Aliongeza kuwa katika vijembe hivyo, mgombea huyo aliwataka wanawake kuachana na kumchagua Mwenyekiti wa sasa Sophia Simba kwa madai kuwa ameshindwa kuwatetea wanawake tangu alipoingia madarakani miaka minne iliyopita. Katika ujumbe wa simu ya mkononi ambao Mwananchi iliuona jana uliandikwa Huyo kinyogoli wenu ametoka nje ya nchi na kumuacha mumewe, lengo ni kufanya kampeni na leo atakutana na wajumbe katika Ukumbi wa Kilimani mjini hapo hivyo kuweni makini ninyi wa upande wa Mwenyekiti. Akizungumzia jambo hilo Mwenyekiti wa UWT Sophia Simba alikiri kulisikia jambo hilo na kueleza kuwa mgombea huyo si mara ya kwanza kukutana na wajumbe na kufanya kampeni. Ni kweli hata mimi nimesikia na hizo message nimezisoma baadhi, lakini mimi niliwaita Wenyeviti katika kikao halali kabisa cha kazi ili tuweze kupanga mambo yetu lakini kama wenzangu wanatumia nafasi hiyo kufanya kampeni wafanye lakini wakumbuke muda bado,alisema Simba. Mwenyekiti huyo alisema kuwa wanawake wa sasa si wa kudanganywa kama inavyodhaniwa kwani wanajua kuchagua pumba na mchele na hivyo akasema hana wasiwasi kwa kuwa wanatambua hukumu ya mwisho itakavyokuwa. Akizungumzia suala la ukomo wa wabunge wa viti maalumu ambalo limeisumbua UWT kwa muda mrefu sasa alisema hiyo ni ajenda ambayo hata yeye aliikuta lakini kwa sasa ni wakati wake kuzungumzwa. Ajenda hiyo sikuileta mimi lakini naikubali kwa moyo mmoja, shida ni kwamba baadhi ya wabunge wanaogopa kupoteza vitumbua vyao na ndio maana anaipigia debe iondolewe, lakini mimi nataka wajiamini na kugombea majimboni kwani tayari wana nguvu,alisisitiza Simba |