major mkandala
Member
- Mar 6, 2010
- 74
- 0
POLEN SANA ILA MNGEANZA KUSAFISHANA KWANZA KABLA YA MGOMO MCHAWI YUMO HUMO HUMO NDANI
Wakati chama cha wafanyakazi kikipanga mgomo na kukataa uwakilishi wa serikali siku ya mei mossi...napenda kutoa wito wao kwa wao kwanza kuanza kusafishana....vyama vya tucta ,cotwu,chodawu vimekuwa mstari wa mbele kununuliwa na waajiri hasa wakati linapokuja mfanyakazi kudai haki yake,..swala hili nimeliona likipenyeza karibu kila shirika na yasiyo ya umma.viongozi hawa wamekuwa wakinunuliwa kwa pesa ndogo sana na waajiri kufikiria kusaini ama mkataba ama waraka wa kuwafukuza watu pasipokujua wanakuja watoto wao wanakuja kuathirka na mkataba ule ule waliosaini wenyewe ;so pengine serikali kukaa kimya wanajivunia baadhi yenu wakijua hata huo mgomo ausaidii kitu kama wataweza kuwakamata mkononi MWENYEKITI na KATIBU wa vyama vya wafanyakazi sehemu husika...michezo hii imeathiri maisha ya wengi huku wengine wakifurahia kuwa wajasiriamali..swala linaloumiza ni jinsi ya malipo wanayolipwa wanapostaafu ama kuachishwa kwa manufaa ya umma...ni vyema nyie wenyewe mkaanza kujisafisha ....ninao mfano mdogo sana hapo chini...
WAFANYAKAZI 128 wa Kiwanda cha Nyuzi cha New Tabora Textiles Ltd akiwemo Mwenyekiti wa Tawi la Chama cha Wafanyakazi (TUICO) kiwandani humo, Ramadhani Wakulichombe, wamefukuzwa kazi kwa tuhuma za kugoma kupinga menejimenti ya kiwanda hicho kuiingiza Jumapili kama siku ya kazi, badala ya mapumziko.
Hatua hiyo ilifikiwa na Tume ya Usuluhishi na Uamuzi Idara ya Kazi mkoani hapa, Novemba 3, mwaka jana, baada ya TUICO kufungua kesi katika Idara ya Kazi baada ya wafanyakazi wote 345 kiwandani hapo kushindwa kuafikiana na Menejimenti ya kiwanda juu ya kufanya kazi Jumapili ambayo kawaida ni siku ya mapumziko.
Aidha, katika hukumu hiyo, Tume hiyo chini ya kifungu cha 89 cha Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini Namba 6 ya mwaka 2004 pamoja kanuni na mwongozo wa usuluhishi na uamuazi, kimezingatia tangazo la serikali la Namba 67 la mwaka 2007 kuwa wafanyakazi 128 kati ya 345 walikaa nyumbani kupinga kufanya kazi siku ya Jumapili huku wafanyakazi 217 wakiridhia na kurudi kujaza mikataba ya kufanya kazi siku hiyo.
Wakati chama cha wafanyakazi kikipanga mgomo na kukataa uwakilishi wa serikali siku ya mei mossi...napenda kutoa wito wao kwa wao kwanza kuanza kusafishana....vyama vya tucta ,cotwu,chodawu vimekuwa mstari wa mbele kununuliwa na waajiri hasa wakati linapokuja mfanyakazi kudai haki yake,..swala hili nimeliona likipenyeza karibu kila shirika na yasiyo ya umma.viongozi hawa wamekuwa wakinunuliwa kwa pesa ndogo sana na waajiri kufikiria kusaini ama mkataba ama waraka wa kuwafukuza watu pasipokujua wanakuja watoto wao wanakuja kuathirka na mkataba ule ule waliosaini wenyewe ;so pengine serikali kukaa kimya wanajivunia baadhi yenu wakijua hata huo mgomo ausaidii kitu kama wataweza kuwakamata mkononi MWENYEKITI na KATIBU wa vyama vya wafanyakazi sehemu husika...michezo hii imeathiri maisha ya wengi huku wengine wakifurahia kuwa wajasiriamali..swala linaloumiza ni jinsi ya malipo wanayolipwa wanapostaafu ama kuachishwa kwa manufaa ya umma...ni vyema nyie wenyewe mkaanza kujisafisha ....ninao mfano mdogo sana hapo chini...
WAFANYAKAZI 128 wa Kiwanda cha Nyuzi cha New Tabora Textiles Ltd akiwemo Mwenyekiti wa Tawi la Chama cha Wafanyakazi (TUICO) kiwandani humo, Ramadhani Wakulichombe, wamefukuzwa kazi kwa tuhuma za kugoma kupinga menejimenti ya kiwanda hicho kuiingiza Jumapili kama siku ya kazi, badala ya mapumziko.
Hatua hiyo ilifikiwa na Tume ya Usuluhishi na Uamuzi Idara ya Kazi mkoani hapa, Novemba 3, mwaka jana, baada ya TUICO kufungua kesi katika Idara ya Kazi baada ya wafanyakazi wote 345 kiwandani hapo kushindwa kuafikiana na Menejimenti ya kiwanda juu ya kufanya kazi Jumapili ambayo kawaida ni siku ya mapumziko.
Aidha, katika hukumu hiyo, Tume hiyo chini ya kifungu cha 89 cha Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini Namba 6 ya mwaka 2004 pamoja kanuni na mwongozo wa usuluhishi na uamuazi, kimezingatia tangazo la serikali la Namba 67 la mwaka 2007 kuwa wafanyakazi 128 kati ya 345 walikaa nyumbani kupinga kufanya kazi siku ya Jumapili huku wafanyakazi 217 wakiridhia na kurudi kujaza mikataba ya kufanya kazi siku hiyo.