nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
[h=2][/h]ALHAMISI, JULAI 12, 2012 04:24 ELIZABETH MJATTA NA ASIFIWE GEORGE, DAR ES SALAAM
*Wadai hawaonyeshi dalili za kutaka usuluhishi
*Watishia kuwafikisha mahakamani waliogoma
VIONGOZI wa Baraza la Kiislamu Tanzania (BAHIKITA) wamejitoa katika kushughulikia suala la mgomo wa madaktari kwa kile wanachodai kuwa madaktari hawaonyeshi dalili za kutaka suluhisho.
Baraza hilo kupitia Katibu wake, Said Mwaipopo pia limesema linajadiliana na wanasheria wake kuangalia namna ya kuwafungulia mashitaka ya mauaji madaktari wote walioshiriki katika mgomo ambao umesababisha vifo vya wagonjwa katika Haspitali ya Taifa ya Muhimbili.
Sisi tuliingilia kati mgomo huu kwa nia njema ya kutapata suluhu kati ya madaktari na serikali lakini baada ya taarifa zetu kutoka kwenye vyombo vya habari Ikulu ilitoa tamko la kukataa kukutana na sisi
...lakini Ikulu walieleza vizuri kwamba hawajawahi kukataa kukutana na viongozi wa madaktari kwa maana hiyo basi serikali imeonekana dhahiri kutaka suluhu.
Baada ya taarifa hizo sisi tuliwatafuta viongozi wa MAT ambao tuliwaeleza kwamba kutokana na taarifa hizo wao waombe msamaha kwa serikali na umma wa watanzania kwa kuendesha mgomo ambao umesababisha vifo.
Lakini baada ya kuwaeleza hivyo hawa viongozi wa MAT hawakukubali sisi kama viongozi ambao lengo letu ilikuwa kutafuta suluhu tukaona hawa vijana (madaktari) wana nia mbaya.
Lakini sisi si kujitoa tu bali tutawafungulia mashtaka ya mauaji wote walioshiriki katika mgomo huo. Tutafanya hivyo ili fundisho kwa wengine ambao wana nia kama za madaktari wanaoendesha migomo.
Kwa hiyo sisi tunaunga mkono kufikishwa mahakamani kwa Rais wao ni njia sahihi kabisa ya kurudisha nidhamu, lakini pia tunaunga mkono matamko yote yaliyotolewa na serikali dhidi ya madaktari,alisema Mwaipopo.
Akijibu hoja hizo, Katibu wa MAT, Dk. Edwin Chitage amesema hawaogopi kufikishwa mahakamani na kwamba wao waliwapokea viongozi hao kwa nia njema wakiamini ni viongozi wa dini.
Kama wamesema watatufikishwa mahakamani wao waende halafu tutakutana nao sisi tuliwapokea kwa nia njema kabisa kwa sababu walituomba wenyewe..lakini baada ya kikao cha Jumamosi siku ya Jumapili wakatupigia simu kuomba tukutane nao,sisi tulikutana nao lakini cha kushangaza walitueleza kwamba wamepigiwa simu na mtu wa Ikulu akiwataka kutuambia kwamba inabidi tuandike barua ya kuomba msamaha halafu tuwape wao ili waipeleke sisi tulishangaa jambo hili sisi hatutafanyi kazi hiyo, alisema Dk.Chitage.
Wakati huohuo, siku moja baada ya Rais wa MAT, Dk. Namala Mkopi kufikishwa mahakamani kwa madai ya kuchochea mgomo, chama hicho kimesema hali hiyo imewashtua na lolote linaweza kutokea.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Katibu wa MAT, Dk. Edwin Chitage alisema hali hiyo imeongeza hasira na kushusha morali wa madaktari.
Kweli hiki kitendo cha Dk. Mkopi kufikishwa mahakamani kimetushtua na ukweli kimesababisha kuwepo na fukuto la chinichini.
Madaktari wamekatishwa tama lakini kitendo hiki pia kimeshusha morali ya wale ambao walirudi kazini kwa hiyo wapo madaktari ambao wapo kazini kwa maana ya eneo la kazi lakini wanachokifanya hiyo wanajua wao,alisema Chitage.
Akizungumzia suala la madaktari wa walioko katika mafunzo (Interns) 390 kufutiwa leseni alisema kitendo hicho walikitegemeakilitegemewa na hakikuwashtua kwa sababu ni kitu ambacho tayari kilipangwa.
Kwetu sisi tulitegemea jambo hilo kwa hiyo hatukushtuka sana kwetu hiki ni kitu kidogo sana, kwa sasa viongozi wa Interns wanafanya kikao na wanasheria wao wanaangalia jinsi uamuzi huo ulivyotolewa na baadaye tutakutana nao kwa ajili ya kuangalia ni namna gani tutalifanyia katika suala hili,alisema Dk. Chitage.
Akizungumzia hali ya Dk.Stephen Ulimboka alisema kwa sasa hali yake inaendelea vizuri na ameanza kutembea na kufanya mazoezi vizuri.
Hivi sasa hali yake imeanza kuimarika. Anaweza kutembea na anafanya mazoezi yake vizuri.
Kinachoendelea kumkalisha hospitali ni uangalizi wa karibu wa figo lakini ingekua si figo angekuwa amesharudi nchini, alisema.
*Wadai hawaonyeshi dalili za kutaka usuluhishi
*Watishia kuwafikisha mahakamani waliogoma
VIONGOZI wa Baraza la Kiislamu Tanzania (BAHIKITA) wamejitoa katika kushughulikia suala la mgomo wa madaktari kwa kile wanachodai kuwa madaktari hawaonyeshi dalili za kutaka suluhisho.
Baraza hilo kupitia Katibu wake, Said Mwaipopo pia limesema linajadiliana na wanasheria wake kuangalia namna ya kuwafungulia mashitaka ya mauaji madaktari wote walioshiriki katika mgomo ambao umesababisha vifo vya wagonjwa katika Haspitali ya Taifa ya Muhimbili.
Sisi tuliingilia kati mgomo huu kwa nia njema ya kutapata suluhu kati ya madaktari na serikali lakini baada ya taarifa zetu kutoka kwenye vyombo vya habari Ikulu ilitoa tamko la kukataa kukutana na sisi
...lakini Ikulu walieleza vizuri kwamba hawajawahi kukataa kukutana na viongozi wa madaktari kwa maana hiyo basi serikali imeonekana dhahiri kutaka suluhu.
Baada ya taarifa hizo sisi tuliwatafuta viongozi wa MAT ambao tuliwaeleza kwamba kutokana na taarifa hizo wao waombe msamaha kwa serikali na umma wa watanzania kwa kuendesha mgomo ambao umesababisha vifo.
Lakini baada ya kuwaeleza hivyo hawa viongozi wa MAT hawakukubali sisi kama viongozi ambao lengo letu ilikuwa kutafuta suluhu tukaona hawa vijana (madaktari) wana nia mbaya.
Lakini sisi si kujitoa tu bali tutawafungulia mashtaka ya mauaji wote walioshiriki katika mgomo huo. Tutafanya hivyo ili fundisho kwa wengine ambao wana nia kama za madaktari wanaoendesha migomo.
Kwa hiyo sisi tunaunga mkono kufikishwa mahakamani kwa Rais wao ni njia sahihi kabisa ya kurudisha nidhamu, lakini pia tunaunga mkono matamko yote yaliyotolewa na serikali dhidi ya madaktari,alisema Mwaipopo.
Akijibu hoja hizo, Katibu wa MAT, Dk. Edwin Chitage amesema hawaogopi kufikishwa mahakamani na kwamba wao waliwapokea viongozi hao kwa nia njema wakiamini ni viongozi wa dini.
Kama wamesema watatufikishwa mahakamani wao waende halafu tutakutana nao sisi tuliwapokea kwa nia njema kabisa kwa sababu walituomba wenyewe..lakini baada ya kikao cha Jumamosi siku ya Jumapili wakatupigia simu kuomba tukutane nao,sisi tulikutana nao lakini cha kushangaza walitueleza kwamba wamepigiwa simu na mtu wa Ikulu akiwataka kutuambia kwamba inabidi tuandike barua ya kuomba msamaha halafu tuwape wao ili waipeleke sisi tulishangaa jambo hili sisi hatutafanyi kazi hiyo, alisema Dk.Chitage.
Wakati huohuo, siku moja baada ya Rais wa MAT, Dk. Namala Mkopi kufikishwa mahakamani kwa madai ya kuchochea mgomo, chama hicho kimesema hali hiyo imewashtua na lolote linaweza kutokea.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Katibu wa MAT, Dk. Edwin Chitage alisema hali hiyo imeongeza hasira na kushusha morali wa madaktari.
Kweli hiki kitendo cha Dk. Mkopi kufikishwa mahakamani kimetushtua na ukweli kimesababisha kuwepo na fukuto la chinichini.
Madaktari wamekatishwa tama lakini kitendo hiki pia kimeshusha morali ya wale ambao walirudi kazini kwa hiyo wapo madaktari ambao wapo kazini kwa maana ya eneo la kazi lakini wanachokifanya hiyo wanajua wao,alisema Chitage.
Akizungumzia suala la madaktari wa walioko katika mafunzo (Interns) 390 kufutiwa leseni alisema kitendo hicho walikitegemeakilitegemewa na hakikuwashtua kwa sababu ni kitu ambacho tayari kilipangwa.
Kwetu sisi tulitegemea jambo hilo kwa hiyo hatukushtuka sana kwetu hiki ni kitu kidogo sana, kwa sasa viongozi wa Interns wanafanya kikao na wanasheria wao wanaangalia jinsi uamuzi huo ulivyotolewa na baadaye tutakutana nao kwa ajili ya kuangalia ni namna gani tutalifanyia katika suala hili,alisema Dk. Chitage.
Akizungumzia hali ya Dk.Stephen Ulimboka alisema kwa sasa hali yake inaendelea vizuri na ameanza kutembea na kufanya mazoezi vizuri.
Hivi sasa hali yake imeanza kuimarika. Anaweza kutembea na anafanya mazoezi yake vizuri.
Kinachoendelea kumkalisha hospitali ni uangalizi wa karibu wa figo lakini ingekua si figo angekuwa amesharudi nchini, alisema.