Habari ya kazi wana jf, chadema wameingia ndani ya ifakara kama nusu saa iliyopita tumewapokea mapokezi ya kufa mtu hadi nyinyiemu wamechanganyikiwa, mana ofisi yangu iko jiran na barabra basi ni hatari tu bodaboda na wat wa miguu ni wengi sana, katika pitapita yang nimekutana na mwenyekiti wa wa kata flani maeneo haya anaongea na wana ccm wenzake kuwa wananchi wa ifakara hawana mpango na chadema kwani wameshaona serikali ya chama cha mapinduzi inawajali sana na imeamua kuwaletea trekta hivyo saizi wananch wanajirudi, mara akatokea mpitanjia akawajibu trekta tumeletewa sisi au wanajeshi? Habari ndo hiyo saizi naelekea kiungani ambako ndo uliko uwanja wanaoenda kuhutubia chadema na uwanja uko pua na mdom na kituo cha polisi hivyo spati picha itakuwaje. Nitaendelea kuwajuza kinachoendelea.