Vijana acheni pombe, kwenye pombe ni fedheha

Mpigamimba

Senior Member
Nov 26, 2022
198
235
Tabia ya unywaji pombe uliokithiri inaleta ndoto za ajabu ajabu. Mbali na ndoto hizo naona kabisa kuna ushetani unaniletea kivuli. Inapotokea umelala umelewa alfajiri unaota ujinga wa kukaa bar na kupoteza waleti, kutembea kifua wazi, ni dalili ya ukichaa.

Pombe inamadhara akilini, wakati unawaza ukatafute hela umelala una hangover ni ishara mbaya hata kama unahela benki.

Nina kazi na pesa napata, nina nyumba 3 siyo vibanda, usafiri Upo, tatizo ulevi. Huu ni shida na sifurahii hii kitu na sina sababu yoyote ya kufanya hivi vitu. Vijana epukeni pombe. Walah siyo useme utakunywa kaisi, hakuna cha kiasi.

Nilianza unywaji kidogo kidogo, nikazidisha, nikapunguza, nikaongeza, naona nazidisha na siwezi kuacha.

Wakati mwingine inanisabishia matukio ya hovyo hovyo njiani, kwenye vyombo ya usafiri, makutanoni, madaladalani najikuta nafyatua, na kuniletea kero.

Katika mahusiano wakati fulani najiona naweza acha danga hili narukia lile. Nakumbwaga na UTI za kutosha, naandikiwa mimadawa ya ajabu ajabu.

Baadhi ya bar nimepigwa stop kwa kuingia na mashine na kutishia watu. Naona kabisa siyo uungwana na utaratibu.

Vijana acheni pombe. Asikuambie mtu, pombe haina afya hata kidogo, hakuna cha marafiki, wala heshima, kwenye pombe ni fedheha.
 
Tabia ya unywaji pombe uliokithiri inaleta ndoto za ajabu ajabu. Mbali na ndoto hizo naona kabisa kuna ushetani unaniletea kivuli. Inapotokea umelala umelewa alfajiri unaota ujinga wa kukaa bar na kupoteza waleti, kutembea kifua wazi, ni dalili ya ukichaa.

Pombe inamadhara akilini, wakati unawaza ukatafute hela umelala una hangover ni ishara mbaya hata kama unahela benki.
Jiambie mwenyewe!
 
Sio mie Mkuu. Mimi ni yule spidi mia nyumbani, mia kazini, mia bar, mia Kwa madem, mia Benki, mia Kwa wakala pochi ikivuja, mia Chachi nikijistukia kama hivi, nikirudi mia. Yaani ni 100mia
😄😄😄 speed mia mia nimeikubaLi hyo mkuu
 
Ila pombe sio kabisa, kuna job mates kama wawili hapa Mara aje kazini na makovu usoni,Mara kavunjika mkono,Mara kavimba shavu na kuacha hataki.

Mwingine Mara atafute balimi,Mara amix na ugolo.

Wanafanya wakat wenzao tunahaha kumiliki mikwanja,mashamba na biashara,
 
Tabia ya unywaji pombe uliokithiri inaleta ndoto za ajabu ajabu. Mbali na ndoto hizo naona kabisa kuna ushetani unaniletea kivuli. Inapotokea umelala umelewa alfajiri unaota ujinga wa kukaa bar na kupoteza waleti, kutembea kifua wazi, ni dalili ya ukichaa.

Pombe inamadhara akilini, wakati unawaza ukatafute hela umelala una hangover ni ishara mbaya hata kama unahela benki.

Nina kazi na pesa napata, nina nyumba 3 siyo vibanda, usafiri Upo, tatizo ulevi. Huu ni shida na sifurahii hii kitu na sina sababu yoyote ya kufanya hivi vitu. Vijana epukeni pombe. Walah siyo useme utakunywa kaisi, hakuna cha kiasi.

Nilianza unywaji kidogo kidogo, nikazidisha, nikapunguza, nikaongeza, naona nazidisha na siwezi kuacha.

Wakati mwingine inanisabishia matukio ya hovyo hovyo njiani, kwenye vyombo ya usafiri, makutanoni, madaladalani najikuta nafyatua, na kuniletea kero.

Katika mahusiano wakati fulani najiona naweza acha danga hili narukia lile. Nakumbwaga na UTI za kutosha, naandikiwa mimadawa ya ajabu ajabu.

Baadhi ya bar nimepigwa stop kwa kuingia na mashine na kutishia watu. Naona kabisa siyo uungwana na utaratibu.

Vijana acheni pombe. Asikuambie mtu, pombe haina afya hata kidogo, hakuna cha marafiki, wala heshima, kwenye pombe ni fedheha.
Mkuu pitia hata izo tafsiri uone jinsi Muumba wetu anavotupenda kuliko sisi tunavojipenda

( يَسْأَلُونَكَ عَنِ الْخَمْرِ وَالْمَيْسِرِ ۖ قُلْ فِيهِمَا إِثْمٌ كَبِيرٌ وَمَنَافِعُ لِلنَّاسِ وَإِثْمُهُمَا أَكْبَرُ مِن نَّفْعِهِمَا ۗ وَيَسْأَلُونَكَ مَاذَا يُنفِقُونَ قُلِ الْعَفْوَ ۗ كَذَٰلِكَ يُبَيِّنُ اللَّهُ لَكُمُ الْآيَاتِ لَعَلَّكُمْ تَتَفَكَّرُونَ )

البقرة (219) Al-Baqara

Wanakuuliza juu ya ulevi na kamari. Sema: Katika hivyo zipo dhambi kubwa na manufaa kwa watu. Lakini dhambi zake ni kubwa zaidi kuliko manufaa yake. Na wanakuuliza watoe nini? Sema: Kilicho chepesi. Namna hivi Mwenyezi Mungu anakubainishieni Aya zake mpate kufikiri--


( يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِنَّمَا الْخَمْرُ وَالْمَيْسِرُ وَالْأَنصَابُ وَالْأَزْلَامُ رِجْسٌ مِّنْ عَمَلِ الشَّيْطَانِ فَاجْتَنِبُوهُ لَعَلَّكُمْ تُفْلِحُونَ )

المائدة (90) Al-Maaida

Enyi mlio amini! Bila ya shaka ulevi, na kamari, na kuabudu masanamu, na kupiga ramli, ni uchafu katika kazi ya Shet'ani. Basi jiepusheni navyo, ili mpate kufanikiwa.



( إِنَّمَا يُرِيدُ الشَّيْطَانُ أَن يُوقِعَ بَيْنَكُمُ الْعَدَاوَةَ وَالْبَغْضَاءَ فِي الْخَمْرِ وَالْمَيْسِرِ وَيَصُدَّكُمْ عَن ذِكْرِ اللَّهِ وَعَنِ الصَّلَاةِ ۖ فَهَلْ أَنتُم مُّنتَهُونَ )

المائدة (91) Al-Maaida

Hakika Shet'ani anataka kutia kati yenu uadui na chuki kwa ulevi na kamari, na akuzuieni kumkumbuka Mwenyezi Mungu na kusali. Basi je, mmeacha?
 
Wale wasioweza kunywa kistaarabu ndo dhahama kama hizi za mleta mada zinawakumba, vinginevyo pombe sawa na bangi vinaathiri watu kwa njia tofauti tofauti kulingana na level za ukichaa walizonazo......
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom