Vifo vya wanasiasa kuelekea uchaguzi mkuu Oktoba 2015

1.Anatufundisha kuwa uhai watoka
kwake.
2.Anatufundisha kutozushia wenzetu
vifo.
3.Anatufundisha kuwa AFYA yatoka
kwake.
4.Anatufundisha kupendana na
kuheshimiana.
5.Anatufundisha kuwavumilia wenzetu
daima.
6.Anatufundisha kuwa tayari daima kwa
matendo mema yanayompendeza yy
aliye mwema na mtakatifu.
7.Anatufundisha kutenda haki kwa watu
wote.
8.Anatufundisha kujitenga na unafiki na
badala yake kutawaliwa na kweli kwa
maneno na matendo yetu.

MUNGU IBARIKI TANZANIA NA AFRIKA.
UCHAGUZI UKAWE WA HAKI MAANA SAUTI YA WENGI NI SAUTI YA MUNGU.
WOTE WALIOTUTANGULIA WAPUMZIKE KWA AMANI.
 
Mpaka leo tumebakiza siku 8 kabla ya uchaguzi mkuu kufanyika, lakini mpaka leo hii tumepoteza wanasiasa tisa tayari. Wanasiasa tuliowapoteza ni, Mohamed Mtoi (CHADEMA), Estomi Malla (ACT WAZALENDO), Celina Kombani (CCM), Mch. Christopher Mtikila (DC), Abdalah Kigoda (CCM), Emmanuel Makaidi (NLD), Deo Filikunjombe (CCM) na kuna madiwani wawili mmoja wa CCM na mwingine wa ACT, majina yao nimesahau. Munga Baba zilaze roho za marehemu hawa mahali pema peponi.

Kuna watu watasema ni mipango ya Mungu, wengi watasema hivi, lakini mimi sitaki kila kitu tuseme ni mipango ya Mungu. Hivi Mungu ni muuaji??? Mungu wetu ni katili namna hii??? Labda niulize swali, akitokea jambazi akakupiga risasi ukafa papo hapo, tutasema ni mipango ya Mungu??? Inamaana Mungu atakuwa amepanga jambazi akupige risasi?? Halafu mwisho wa siku Mungu huyo huyo aliyepanga ufe kwa kupigwa risasi na jambazi, atamuhukumu huyo jambazi aliyekupiga risasi au jambazi akitubu basi Mungu huyo huyo atamsamehe? Hapana, mimi binafsi sitaki kuamini kuwa vifo vyote ni mipango ya Mungu, hapana.

Ni kweli tunaishi na kuna siku ikifika ni lazima tufe. Hakuna ubishi hapo lazima kifo kitatuchukua, lakini kuna vifo vinasababishwa na sisi binadamu wenyewe. Katika maisha kuna harakati nyingi sana, na moja ya harakati hizo ni za kutafuta utawala na maslahi. Hizi ni harakati hatari sana katika maisha ya binadamu. Wote tunafahamu kuwa Ubunge au Urais au Udiwani kwa sasa hivi hapa Tanzania ni issue kubwa, ni dili hasa. Siwezi kushangaa kama kuna watu watafanya wawezanyo hata ikibidi kutoa roho za wenzao ili mradi tu wapate nafasi hizo. Hatuwezi tukabisha katika hili, wote tumeshuhudia Albino wakiuawa kikatili na wengine kunyofolewa viungo vyao kisa watu tu wanataka utajiri na mafanikio kisiasa. Tunalijua hili, wakati wa kuelekea uchaguzi mkuu ushirikina, upigaji ramli na utabiri wa wanaojiita manabii huwa unashamiri sana. Viongozi wengi sana ni washirikina na hili halina ubishi hata kama hakuna ushahidi wa wazi wazi.

Sina maana ya kusema kuwa vifo vyote hivyo vya hao wanasiasa vilivyotokea ni matokeo ya kibinadamu, la hasha, lakini kuna mashaka sana. Kuna vifo vimetokea katika mazingira ya kutatanisha sana. Kuna maswali mengi sana ya kujiuliza. Is it fate or coincidence? Is it fate or it is just survival of the fittest?

Tumebakiza siku 8 kufika tarehe 25 October. I have a bad feeling about this election. Siku 8 zilizobakia ni nyingi sana. Kwa jinsi mambo yanavyokwenda sijui, tutegemee kusikia lolote lile.

Mwenyezi Mungu, Baba wa rehema tuepushe na mabalaa na utuokoe kutoka kwa yule muovu.

By Son of Gamba.

Nadhani baada ya kuona viungo vya albino imekuwa balaa waganga wamebadili mbinu sasa dili ni kutengeneza ajali.
 
1. Anatukumbusha kwamba sisi ni mavumbi na mavumbini tutarudi.
2. Tuliumbwa kwa udongo na tutarudi kwa udongo.
3. Uhai wa binadamu bado ni fumbo ambalo mwanadamu hana nafasi ya kulifumbua.
4. Anayejua ni Yeye tu mzima kuwa mfu na mgonjwa kuwa salama.
5. Uhai wa mwanadamu upo kwa Mungu peke yake na sio vinginevyo.
 
Taarifa za Deo zimenifanya nikumbuke kawimbo flani sijui unaitwa je wala mwimbaji simjui...moja ya kionjo chake ni

🎵🎶🎼nimashaka na mahangaiko🎵wema hawana maisha🎵🎶🎼
Pumzika kwa Amani #Deo #Nkwera (DPLO Tarime) na wengineo
 
Yule mama alikufa kwa Presha baada ya kumuhonga Mgombea wa Ubunge Chadema ili apite bila kupingwa cha kushangaa jamaa hela yake alichukua na fomu ya kugombea akachukua ndio mama kuanguka na kupelekwa India. Madalaka Matamu
 
ss wale wa matusi na kashfa za ooh cjui fulani mgonjwa endeleeni....

christine ibrahim unamaana gani kusema hvyo?
Unataka kuniambia hvi vifo ni mungu amechukia kitendo cha kumwita mtu mgonjwa?

Lakn ngoja tumwachie yeye. Ila hvi vifo kama ni mpango wa Mungu basi hatuna neno lakn kama ni mkono wa mtu.
Hizi damu zitamlilia milele na atakukufa akijiona anaoza hakika kifo lazma kimkimbie kwa mda ili mateso ya damu hizo zimrudie
 
Last edited by a moderator:
Naona uchaguzi angalau Vifo vya albino hatujasikia 2005 na 2010 ilikua balaa

Tuendelee kumuomba MUNGU na kuombea uchaguzi huku bila unafiki tukikemea uovu hadharani bila kutukana,maana haiingii akilini CCM ndio chama kinachoongoza kwa uchafu wa aina zote tunaoufahamu kimaadili alafu badala ya kuomba Huruma ya MUNGU wao kila kona ni MATUSI kuwatukana wenzao mambo hayo MUNGU anakerekwa nayo sana,kiburi kilichopo ndani ya CCM kilichojaa kutokujali Mwisho wake umeonekana dhahiri.
 
Vifo Hivi vinasura Tatu..AU none

1. mapenzi ya Mungu
2. Uadui wa kisiasa ..uliozalishwa na kura ZA maoni vyama vyote
3.Kumkufuru Mungu kwa kukashifiana kulikopitiliza kwa mambo ambayo binadamu Hana uwezo nayo
4. Msongo wa mawazo na uchovu Hasa kutokana na ugumu wa ratiba , kukataliwa na WANANCHI na kuleta sononeko , kutumia gharama Kubwa na kuishiwa pesa kabisa pia kunaweza kuleta msongo wa mawazo

huenda L A A N A Y A M A U A J I Y A A L B I N O inatuandama pia
 
Ni kweli matukio ya vifo vya wanasiasa yamekuwa mengi kwa muda mfupi. Mungu aturehemu, tunakuwa na wasiwasi mwingi juu vifo hivi, hata leo nadiriki kuuliza je! ni salama nchini kwetu Jumamosi ya leo?
 
Hata mm cjui kama jmosi ya leo ni salama. Ila tuombe mungu sn kuna vitu si vya kawaida
 
Back
Top Bottom