kapotolo
JF-Expert Member
- Sep 19, 2010
- 3,727
- 2,214
Hivi waziri Mwinyi, unataka wangapi wafe chini ya wizara unazoziongoza ndipo uwajibike?
Milipuko ya mbagala iliua watu, ukasema kamwe hujiuzulu
Ulipoteuliwa kama waziri wa afya, ukasema utahakikisha migomo haipo tena kwenye wizara hiyo, lakini madaktari wakagoma, watu wakafa, na hukuona sababu ya kuwajibika.
Mara zikaingia dawa feki za ARVs, wanaoishi na virusi vya ukimwi wakafa, ukaendelea kufurahia viyoyozi vya ofisini bila hata kushtuka, unakuja kwa waandishi wa habari kwamba umefunga kiwanda kumbe ni hadaa hata barua hujawaandikia na bado wanaendelea kutengeneza dawa za kuua watu. Kwa nini lakini?
Na sasa zimeingia dawa feki za aina ya cloxacilline, tena kupitia MSD, watu wanakufa hili sijalisikia hata ukilisemea, maana halijakushtua. Likushtue kwa lipi, kwani wanaokufa ni binadamu, au wanakuhusu.
Hawa wanaokufa wangekuwa dada zako, wajomba zako, wakwe zako, kweli ungeendelea kufurahia hiyo ofisi, hivi huzioni roho za watu wanaokufa chini ya wizara unazoziongoza zikizunguka ofisini kwako na zikuogofye na kuacha ofisi. Au ni kweli serikali hii ya awamu ya nne ni kweli inatoa watanzania kafaraiendelee kutawala?
Waziri Mwinyi, wafe wangapi uwajibike?
Milipuko ya mbagala iliua watu, ukasema kamwe hujiuzulu
Ulipoteuliwa kama waziri wa afya, ukasema utahakikisha migomo haipo tena kwenye wizara hiyo, lakini madaktari wakagoma, watu wakafa, na hukuona sababu ya kuwajibika.
Mara zikaingia dawa feki za ARVs, wanaoishi na virusi vya ukimwi wakafa, ukaendelea kufurahia viyoyozi vya ofisini bila hata kushtuka, unakuja kwa waandishi wa habari kwamba umefunga kiwanda kumbe ni hadaa hata barua hujawaandikia na bado wanaendelea kutengeneza dawa za kuua watu. Kwa nini lakini?
Na sasa zimeingia dawa feki za aina ya cloxacilline, tena kupitia MSD, watu wanakufa hili sijalisikia hata ukilisemea, maana halijakushtua. Likushtue kwa lipi, kwani wanaokufa ni binadamu, au wanakuhusu.
Hawa wanaokufa wangekuwa dada zako, wajomba zako, wakwe zako, kweli ungeendelea kufurahia hiyo ofisi, hivi huzioni roho za watu wanaokufa chini ya wizara unazoziongoza zikizunguka ofisini kwako na zikuogofye na kuacha ofisi. Au ni kweli serikali hii ya awamu ya nne ni kweli inatoa watanzania kafaraiendelee kutawala?
Waziri Mwinyi, wafe wangapi uwajibike?