Waziri Ummy Mwalimu na Wizara ya Afya kwa ujumla, chukueni ushauri huu msipotoshwe mtakosea

Prof Koboko

JF-Expert Member
Aug 15, 2020
350
2,549
SOMO/USHAURI KWA WIZARA YA AFYA NA WAFAMASIA NCHINI KUHUSU OPOTOSHWAJI UNAOFANYWA MAKUSUDI NA BAADHI YA WATAALAM WASIOKUA WAMINIFU.

Na Prof Patrick Koboko(MD,MMED,MPH,MBA, PhD in Human Anatomy
)

Wasalaam!

Kwanza nitoe pongezi kwa serikali yangu inavyojitahidi katika kulinda usalama wa afya za wananchi wake hususani waziri wa Afya Ummy Mwalimu kwa jinsi anavyopambana ndani ya wizara ya Afya ingawa bado kuna watu wanaomzunguka wanampotosha kwa makusudi ili kulinda maslahi yao binafsi. Kupitia somo hili, naamini serikali itachukua maoni yangu na kuyafanyia kazi, wataalam wa dawa nao watajifunza hususani wale wanaopotosha umma wa watanzania kwa makusudi kulinda maslahi yao binafsi.

UPOTOSHWAJI WA MAKUSUDI UNAOFANYWA KWA WANANCHI.

Kwanza ifahamike kwamba hakuna chuki baina ya taaluma moja dhidi ya nyingine kwenye kada ya Afya, tatizo kubwa ni baadhi ya Wataalam kwa sababu ya njaa zao au ubinafsi usiokua sababu kutaka kufanya kila kitu kisiasa na kuipotosha jamii kitu ambacho huenda baadaye kikaleta madhara makubwa nchini kwa baadaye.

Nimetoa ushauri sana kwa kuandika humu ndani kama moja ya mtandao pendwa pamoja na mitandao mingine maarufu ya kijamii ambako ujumbe unaweza kuifikia jamii na mamlaka kwa haraka zaidi. Kama nilivyosema siku moja humu kwamba tuna tatizo kubwa sana la mifumo ya elimu yetu nchini, uelewa ni tatizo kubwa sana kwa baadhi ya wataalamu (siyo wote), mfumo tuliojengewa ni ule wa watu kupenda kujipatia vipato kwa njia za mkato na kujitapa kwa sababu wamesoma badala ya kuzalisha, mtu anamaliza shule badala ya kwenda kuzalisha, anafikiria cheti chake kikakae dukani kwa mwenzake ili alipwe pesa anayotaka yeye,hafikirii kwenda kuanzisha hata kiwanda kidogo za kuzalisha dawa ndogo ndogo za baridi au kuingia porini kufanya utafiti wa dawa za kutibu maradhi mbali mbali ili kulinusuru taifa na uagizaji wa dawa kutoka nje. Tunazalisha wanataaluma wazembe wanaowaza kukaa ofisini kupulizwa na viyoyozi badala ya kwenda porini kwenye Magome ya miti huko kutafuta suluhisho la maradhi ambayo yamekua yakiibuka kila uchwao. Hapa ndiko tatizo liliko.

Niwaombe wanataaluma wenzangu hasa wanazuoni wa kada hizi za Afya, tuzalishe wanataaluma wenye kujitegemea na siyo wanaowaza kukaa maofisini kuwaza vyeti vyao kutumika kufungulia maduka ya dawa au vituo vya afya na mahospitali. Tuwe na wataalam wenye tija wanaowaza kuzalisha na kuleta mapinduzi katika sekta ya Afya nchini. Mifumo ya Wanavyofanya kazi watanzania katika sekta ya Afya ni tofauti kabisa na ninayoiona hapa Afrika Kusini na hata Egypt nilikokaa takribani miaka 7 nikiwa mwalimu wa chuo kikuu na mwanafunzi huko.
Wenzetu wamejikita zaidi katika kuzalisha zaidi na siyo kukaa maofisini tu kubishana na kulalama na ndiyo maana dawa nyingi tunaingiza kutoka kwao.

HAKUNA UKWELI WOWOTE WALA HOJA YA KISAYANSI KUA MFAMASIA PEKEE NDIYE ANAYETAKIWA KUUZA AU KUTOA DAWA.

Kama nilivyosema awali ni kweli ndio uhalisia wenyewe ya kwamba Mfamasia anafanya kazi Hosptalini, Kwenye tafiti mbali mbali za dawa, Kiwandani, kua Mwalimu wa chuo kama mimi, Kwenye Godowns na stoo za kuhifadhia Dawa, maduka ya dawa na kwenye jamii pia . Daktari pia anafanya kazi Hosptalini, kua mwalimu wa chuo, Kiwandani, kwenye tafiti mbali mbali mbali, Godowns za kuhifadhia dawa, maduka ya kuuzia dawa na kwenye jamii pia, Muuguzi hali kadhalika. Katika maeneo haya kila mmoja ana jukumu lake kulingana na kuhitajika kwake.

Juzi tu tulikua kwenye utafiti wa Chanjo ya ugonjwa wa Corona, utakubaliana nami kua kulikua na madaktari wengi ndio na Wafamasia ndio wanaohangaika sana kwenye ugunduzi wa dawa na chanjo na dawa ya gonjwa hili, jiulize ni kwanini timu za madaktari na wafamasia ndizo zilikua mstari wa mbele kuhangaika juu ya dawa na chanjo ya gonjwa hili? Na bado utafiti unaendelea. Kwahiyo kazi bila team work haiwezi kwenda.

Nilisema ni ubinafsi mkubwa na ni upotoshwaji mkubwa unaofanywa na wachumia tumbo wachache katika taaluma ya Famasia nchini na wamefanikiwa kumpotosha hata waziri kua Wafamasia pekee ndio wanaopaswa kuuza dawa.

Kwanini wao tu ndio wanaotaka wakae madukani wauze dawa wakati hata mahospitalini tunafanya kazi na wao pamoja? Kwanini kwenye maduka nako tusifanye kazi as a team? Kuna sababu yeyote kimsingi au kisayansi kumzuia daktari au nesi kuuza dawa ikiwa yeye ndio amechagua kukaa kwenye duka la dawa badala ya kufanya kazi hospitani. Kila mtu anafanya kazi kwa choice yake, kuna Mfamasia anapenda afanye kazi hospitalini na mwingine kiwandani au kwenye maduka ya dawa, hali kadhalika kwa daktari na nesi hivyo hivyo, kuna shida pia kufanya kazi kama team kufanya kazi kwenye maduka?

Mnajua kua kwenye viwanda vya dawa wanafanya kazi as a team kama ilivyo kwa hospitali kama ambavyo mimi niliwahi kufanya kazi kwenye kiwanda kimoja cha dawa huko Tanzania nikiwa daktari? Wafamasia wachache waache ubinafsi na shida zao binafsi kuipotosha serikali na umma kwa ujumla.

NI MADUKA MANGAPI YANATOA DAWA ZINAZOHITAJI VYETI VYA MADAKTARI NCHINI?

Labda nimwambie Mhe Waziri Ummy kama alikua hajui, ni 99% ya maduka ya famasi nchini ambayo sheria inayataka yatoe dawa zinazohitaji maelekezo ya daktari (Dr's Prescriptions) hayafanyi hivyo. Kama ninadanganya atume timu yake ya siri kufanya uchunguzi huo kama hawatafungia maduka yote nchini. Kulaumu kua wauza dawa wasiokua wafamasia ndio wanaoharibu utaratibu huu na kuingiza afya za watanzania matatatani siyo kweli, Zile video clips zilizokua zikisambazwa mitandaoni kuonesha kuna watoa dawa hawana taaluma zilikua ni propaganda zilizoanzishwa na Wakaguzi wachache wachumia tumbo na ndiyo maana utaona hazikuowaonesha waliokua wakihoji maswali, wafanye uchunguzi wajionnee waache kupotoshwa na wachumia matumbo wachache, kabla sijaja kuandika humu nikiwa nchini nilifanya utafiti huu na hata sasa kuna vijana wangu walioko huko Tanzania wakifanya uchunguzi juu ya hili ili ninapotoa ushauri niseme vitu vya ukweli na uhakika.

SWALI:(1). Kama kwenye famasi mgonjwa ameenda kununua dawa kali yenye uhitaji wa cheti cha daktari na hana cheti hicho, atamhudumia au atamrudisha hospitali akaandikiwe na daktari kisha arudi dukani? Atawezaje kumhudumia wakati yeye siyo daktari na hawezi kuandika prescription?

Maana kuna hoja ya Kijinga hapa kua Mfamasia anaweza kuandika prescription kwa sababu anaweza kuisoma ile ya daktari eti kwa sababu amesoma Anatomy, Physiology, Pathology na Pharmacology na dio Upotoshaji mkubwa inakoanzia hapa.
Daktari ama tabibu Pathophysiology au history taking kwake ni masomo yanayojitegemea na yana principles na utaratibu wake achilia mbali Physiology na Anatomy au Pathology. Mfamasia anajua maana ya Main Complain, HPI na SOCRATES? amesomea wapi kama kuna mwenye kuthibisha hili aseme humu humu.

(2) .Kama waziri anashauriwa Wafamasia ndio wanaotakiwa kukaa mpaka kwenye maduka ya dawa muhimu ama DLDM ambayo hayahitaji cheti cha Mfamasia wala cheti cha daktari, ni kwa msingi upi sasa wakati dawa zenyewe hazihitaji Mfamasia wala cheti cha daktari?

Kama daktari au muuguzi aliyesomea kozi yake akafuzu vyema anauza DLDM, tatizo liko wapi hasa?

Kwanini tunaweka urasimu na siasa kwenye mambo muhimu kiasi hiki?

NI MADUKA MANGAPI YA DAWA TANZANIA WAFAMASIA HUBAKIA DUKANI MUDA WOTE WA KAZI?

Toka awali nilisema kwamba upotoshaji wa makusudi ukiendelea, kuna mambo yasiyosemwa tutaweka hadharani ili kusudi watanzania wajue nini kinajiri kwenye maduka haya ya dawa na ni kwa nia njema wala hakuna chuki hapa. Kila mtanzania ana haki ya kukinda afya ya mwenzake....

Ni 99.99% Tanzania ya maduka ya dawa ambayo yanatakiwa kusimamiwa na wataalam wa dawa wenye viwango vya elimu kuanzia na shahada ya kwanza hawakai kwenye maduka hayo kama sheria inavyowataka. Wanalipwa pesa nyingi ambazo hazikatwi Kodi kuanzia na milioni moja(1,000,000+) na kuendelea. Kama wizara ilikua hailijui hili basi wafanye uchunguzi wataelewa tu. Nchi inalia na mapato lakini kuna watu wanapokea pesa taslim bila makato ya kodi wakati kila mfanyakazi nchini, ni lazima na ni sheria kwa kila mfanyakazi kukatwa kodi. TRA na wizara ya fedha waliangalie hili serikali inapoteza pesa nyingi sana. Hata kama wanalipia leseni zao lakini taaluma zingine zinalipa vile vile na linapokuja suala kulipwa kwa kufanya kazi kodi ni lazima kwa taratibu za nchi yetu.

Ukaguzi wa kina wa Wizara ya Afya, Wizara ya Fedha na TRA kwa ujumla.

Kama nchi nzima ina wafamasia zaidi ya 1000 wenye level ya degree wanaosimamia maduka ya dawa na wanalipwa mishahara yao bila kukatwa kodi, ni kiasi gani taifa linapoteza kwa mwaka badala ya kuhangaika na tozo hizi ambazo zinaumiza zaidi watu wa chini?

KATI YA BARAZA LA WAFAMASIA NA TMDA NI NANI ANATAKIWA KUKAGUA DAWA NCHINI?

Huu nao ni mkanganyiko mkubwa sana Tanzania na Waziri anapotoshwa makusudi tu kwa vile labda siyo Mtaalam wa Afya maana wakati Wizara inaongozwa na Waziri mtaalam hatukuona haya, sijajua kazi ya Naibu waziri na Katibu mkuu ambao ni wataalam kwanini hawatoi ushauri huu kwa waziri.

Duniani kote, FDA au TMDA kwa kwetu Tanzania hizi ndizo taasisi pekee zinazotakiwa kukagua usalama wa dawa kisheria na taasisi hizi ndani yake utakuta kuna Wafamasia, Madaktari, Wauguzi, Wakemia, wataalam wa lishe na wataalam wengineo mpaka wanasheria kila mtu na eneo lake katika utendaji wake, and this is according to international standards, kwa Tz sijui kuna tatizo gani ndugu zangu hii kazi wanapewa Baraza la Wafamasia (Pharmacy council) ambalo hili ni baraza la kitaaluma ambalo kimsingi kazi yake ni kusajili wataalam na kuwapatia leseni za kazi, yaani sawa na kusema MCT au TANNA wafanye kazi za kukagua mahospitali ili hali haya ni mabaraza ya kitaaluma na yana kazi zake za msingi, labda wapitie kukagua leseni na vyeti vya wataalam wao waliowasajili. Sasa huku Tanzania Baraza la Wafamasia ndio wanakagua dawa, wanasajili Maduka ya dawa, huku wanasajili wataalam, yaani mambo Changanyikeni. Kama watapita kwenye kwenye maduka ya dawa na mahospitalini au viwandani kukagua leseni za wataalam hapo sawa maana kuna zinazogushiwa na ziingine kumalizika muda wake.

USAHURI wangu kwenye hili ni kwamba kazi ya kutoa vibali vya kufungua maduka ya dawa pamoja na ukaguzi wa madawa na maduka waachiwe TMDA ambao ndio kazi zao kimsingi na kama wataalam hawatoshi Wizara iajiri tu taasisi itimie na ifanye kazi kwa weledi waache kufanya mambo kienyeji. Baraza la Wafamasia ni Baraza la kitaaluma liachwe lifanye kazi zake za kimsingi ambazo ni kusajili wataalam, kuwapima na kuwapatia leseni za taaluma hiyo, wakague pia lesini zao ikiwa ni za kweli au bado ni valid.


HITIMISHO: Naiomba sana Wizara ya Afya na Mamlaka zizingatie za serikali ushauri huu ni muhimu sana, kuna upotoshwaji mkubwa unaofanywa na baadhi ya wataalam wanaokiuka maadili yao ya kazi. Tunapoteza pesa nyingi sana na umakini katika eneo hili muhimu ambalo liliachwa nyuma muda mrefu.

Ni ushauri pia kwa wataalam wa kada za Afya zaidi Wafamasia wazingatie, tuache kufanya kazi kwa mazoea, tuzingatie maadili ya kitaaluma. Tuzalishe ili taifa letu kidonge mbele.
Mimi sijikwezi na wala sina tatizo na taaluma ya mtu, naziheshimu taaluma za watu wengine na ndio tunaofanya kazi kwa pamoja kama timu ili kulinda afya ya jamii kama viapo vyetu vinavyotaka.

Ahsanteni!

Prof Partick Koboko(MD,MMED,MPH,MBA, PhD in Human Anatomy)
kobokopatricdr@gmail.com
 
Mimi nimeuchukia sana uongozi mzima wa Wizara ya Afya kwa kutudanganya kuwa wananchi wanatakiwa kutibiwa bure kwenye hospitali zetu za Serikali. Hakuna huduma ya bure kwenye hospitali za Serikali na wananchi kwanza wanatozwa bima ya afya ya papo kwa papo halafu anaambiwa kwenda kununua dawa kwenye maduka ya binafsi. Wasiwe wanadudanganya na mbwe mbwe zao kule Bungeni wakijinasibu kuwa kuwa Serikali imetoa mabilioni kadhaa kwa ajili ya madawa na huduma kwa wananchi. Binafsi nimewachukia sana na huyo Waziri anatakiwa aondolewe kwenye nafasi yake.
 
Mimi nimeuchukia sana uongozi mzima wa Wizara ya Afya kwa kutudanganya kuwa wananchi wanatakiwa kutibiwa bure kwenye hospitali zetu za Serikali. Hakuna huduma ya bure kwenye hospitali za Serikali na wananchi kwanza wanatozwa bima ya afya ya papo kwa papo halafu anaambiwa kwenda kununua dawa kwenye maduka ya binafsi. Wasiwe wanadudanganya na mbwe mbwe zao kule Bungeni wakijinasibu kuwa kuwa Serikali imetoa mabilioni kadhaa kwa ajili ya madawa na huduma kwa wananchi. Binafsi nimewachukia sana na huyo Waziri anatakiwa aondolewe kwenye nafasi yake.
Mimi nimepeleka mke wangu kujifungua kwa opereseheni hospitali ya serikali nikapigiwa 300,000 jumla
 
Ni 99.99% Tanzania ya maduka ya dawa ambayo yanatakiwa kusimamiwa na wataalam wa dawa wenye viwango vya elimu kuanzia na shahada ya kwanza hawakai kwenye maduka hayo kama sheria inavyowataka. Wanalipwa pesa nyingi ambazo hazikatwi Kodi kuanzia na milioni moja(1,000,000+) na kuendelea. Kama wizara ilikua hailijui hili basi wafanye uchunguzi wataelewa tu. Nchi inalia na mapato lakini kuna watu wanapokea pesa taslim bila makato ya kodi wakati kila mfanyakazi nchini, ni lazima na ni sheria kwa kila mfanyakazi kukatwa kodi. TRA na wizara ya fedha waliangalie hili serikali inapoteza pesa nyingi sana. Hata kama wanalipia leseni zao lakini taaluma zingine zinalipa vile vile na linapokuja suala kulipwa kwa kufanya kazi kodi ni lazima kwa taratibu za nchi yetu.
Ukaguzi wa kina wa Wizara ya Afya, Wizara ya Fedha na TRA kwa ujumla.
Kama nchi nzima ina wafamasia zaidi ya 1000 wenye level ya degree wanaosimamia maduka ya dawa na wanalipwa mishahara yao bila kukatwa kodi, ni kiasi gani taifa linapoteza kwa mwaka badala ya kuhangaika na tozo h
Prof kwa hii paragraph ninaona kabisa ni unachuki kali sana kwa wafamasia, naanza kuamini kuwa hizi hoja unazoibua kuhusu pharmacist tanzania ni za kimaslahi tu basi.

1: Kama mfamasia akai dukani kwa mujibu wa sheria hilo ni tatizo la taaluma nzima ya famasi au ni tatizo la mtu mmoja mmoja ? Huoni kuwa hapo anaepaswa kuchukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria zao ni muhusika na sio kutupia lawama kada nzima ya pharmacist.

2: kama lengo lako ni kusaidia jamii na kuishauri wizara kuhusu mambo ya kiafya za watanzania kupitia hizi famasi, haya masula ya kodi, kutaka pesa wanayolipwa wafamasia kupitia izo pharamacy zikatwe kodi yanaibuka vipi ? Inamahusiano gani na hoja zako za awali kuhusu afya na usalama wa wagonjwa kwenywe pharmacy zetu ? Ninaona kabisa prof kuandika haya izi kelele unazopiga ni unasukumwa na chuki zako, wivu na inshu za kimaslahi tu basi.
 
Mwanzoni nilidhani una nia njema kumbe ni maslahi binafsi.
Hii paragraph imeonesha wazi rangi halisi ya huyu prof koboko na malengo ya izi kelele zote anazopiga.
Ni 99.99% Tanzania ya maduka ya dawa ambayo yanatakiwa kusimamiwa na wataalam wa dawa wenye viwango vya elimu kuanzia na shahada ya kwanza hawakai kwenye maduka hayo kama sheria inavyowataka. Wanalipwa pesa nyingi ambazo hazikatwi Kodi kuanzia na milioni moja(1,000,000+) na kuendelea. Kama wizara ilikua hailijui hili basi wafanye uchunguzi wataelewa tu. Nchi inalia na mapato lakini kuna watu wanapokea pesa taslim bila makato ya kodi wakati kila mfanyakazi nchini, ni lazima na ni sheria kwa kila mfanyakazi kukatwa kodi. TRA na wizara ya fedha waliangalie hili serikali inapoteza pesa nyingi sana. Hata kama wanalipia leseni zao lakini taaluma zingine zinalipa vile vile na linapokuja suala kulipwa kwa kufanya kazi kodi ni lazima kwa taratibu za nchi yetu.
Ukaguzi wa kina wa Wizara ya Afya, Wizara ya Fedha na TRA kwa ujumla.
Kama nchi nzima ina wafamasia zaidi ya 1000 wenye level ya degree wanaosimamia maduka ya dawa na wanalipwa mishahara yao bila kukatwa kodi, ni kiasi gani taifa linapoteza kwa mwaka badala ya kuhangaika na tozo hizi ambazo zinaumiza zaidi watu wa chini?
 
Prof kwa hii paragraph ninaona kabisa ni unachuki kali sana kwa wafamasia, naanza kuamini kuwa hizi hoja unazoibua kuhusu pharmacist tanzania ni za kimaslahi tu basi.

1: Kama mfamasia akai dukani kwa mujibu wa sheria hilo ni tatizo la taaluma nzima ya famasi au ni tatizo la mtu mmoja mmoja ? Huoni kuwa hapo anaepaswa kuchukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria zao ni muhusika na sio kutupia lawama kada nzima ya pharmacist.

2: kama lengo lako ni kusaidia jamii na kuishauri wizara kuhusu mambo ya kiafya za watanzania kupitia hizi famasi, haya masula ya kodi, kutaka pesa wanayolipwa wafamasia kupitia izo pharamacy zikatwe kodi yanaibuka vipi ? Inamahusiano gani na hoja zako za awali kuhusu afya na usalama wa wagonjwa kwenywe pharmacy zetu ? Ninaona kabisa prof kuandika haya izi kelele unazopiga ni unasukumwa na chuki zako, wivu na inshu za kimaslahi tu basi.
Wewe mwenzako ameleta hoja na akatoa facts kwanini unamshambulia yeye binafsi? Mjibu hoja yake kama ni kweli au laah
 
Wewe mwenzako ameleta hoja na akatoa facts kwanini unamshambulia yeye binafsi? Mjibu hoja yake kama ni kweli au laah
Hoja yake kuhusu nini
Hoja zake kuhusu maslahi yake binafsi au

Kama TRA hainikati kodi, tatizo ni langu au la TRA ?.

Kama nalipwa afu sikai dukani kwani hawana baraza lao linaloshughulikia kesi kama izo kwa mujibu wa sheria zao. Wakulalamika hapa ilipaswa awe bosi anaemlipa hiyo pesa huyo pharmacist na sio huyu prof kpboko. Huyu ni masalahi yake tu binafsi yanamsumbua.
 
Prof kwa hii paragraph ninaona kabisa ni unachuki kali sana kwa wafamasia, naanza kuamini kuwa hizi hoja unazoibua kuhusu pharmacist tanzania ni za kimaslahi tu basi.

1: Kama mfamasia akai dukani kwa mujibu wa sheria hilo ni tatizo la taaluma nzima ya famasi au ni tatizo la mtu mmoja mmoja ? Huoni kuwa hapo anaepaswa kuchukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria zao ni muhusika na sio kutupia lawama kada nzima ya pharmacist.

2: kama lengo lako ni kusaidia jamii na kuishauri wizara kuhusu mambo ya kiafya za watanzania kupitia hizi famasi, haya masula ya kodi, kutaka pesa wanayolipwa wafamasia kupitia izo pharamacy zikatwe kodi yanaibuka vipi ? Inamahusiano gani na hoja zako za awali kuhusu afya na usalama wa wagonjwa kwenywe pharmacy zetu ? Ninaona kabisa prof kuandika haya izi kelele unazopiga ni unasukumwa na chuki zako, wivu na inshu za kimaslahi tu basi.
Ndugu yangu, sina shida ndogo ndogo hizo. Kwa level yangu si wa kumiliki DLDM au kutembea na ADDO. Mimi ni mwanataaluma, kazi zangu za utafiti tu zinanitosha hata nisipofundisha.Kazi yangu ni kulisaidia taifa na kulinda afya za watanzania kwa kiapo changu kwa taifa na Mungu wa Mbinguni.

Ninachosema humu ni ukweli usiopingika kua Wafamasia wanalipwa pesa nyingi zisizokatwa kodi na wengi wao 99% hawakai kwenye maduka yao wanaosimamia.Ninesema 99% kama una akili unaelewa namaanisha nini, hiyo 1% iliyobakia ndio wanaobakia kwenye maduka yao wanayosimami. Ni wote pesa wanayolipwa kaikatwi
Prof kwa hii paragraph ninaona kabisa ni unachuki kali sana kwa wafamasia, naanza kuamini kuwa hizi hoja unazoibua kuhusu pharmacist tanzania ni za kimaslahi tu basi.

1: Kama mfamasia akai dukani kwa mujibu wa sheria hilo ni tatizo la taaluma nzima ya famasi au ni tatizo la mtu mmoja mmoja ? Huoni kuwa hapo anaepaswa kuchukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria zao ni muhusika na sio kutupia lawama kada nzima ya pharmacist.

2: kama lengo lako ni kusaidia jamii na kuishauri wizara kuhusu mambo ya kiafya za watanzania kupitia hizi famasi, haya masula ya kodi, kutaka pesa wanayolipwa wafamasia kupitia izo pharamacy zikatwe kodi yanaibuka vipi ? Inamahusiano gani na hoja zako za awali kuhusu afya na usalama wa wagonjwa kwenywe pharmacy zetu ? Ninaona kabisa prof kuandika haya izi kelele unazopiga ni unasukumwa na chuki zako, wivu na inshu za kimaslahi tu basi.
Ndugu yangu, shina shida ndogo ndogo hizo. Kwa level yangu si wa kumiliki DLDM au kutembea na ADDO. Mimi ni mwanataaluma, kazi zangu za utafiti tu zinanitosha hata nisipofundisha.Kazi yangu ni kulisaidia taifa na kulinda afya za watanzania kwa kiapo changu kwa taifa na Mungu wa Mbinguni.

Ninachosema humu ni ukweli usiopingika kua Wafamasia wanalipwa pesa nyingi zisizokatwa kodi na wengi wao 99% hawakai kwenye maduka yao wanaosimamia.Ninesema 99% kama una akili unaelewa namaanisha nini, hiyo 1% iliyobakia ndio wanaobakia kwenye maduka yao wanayosimamia. Ni wote pesa wanayolipwa kaikatwi kodi. Thibitisho uongo wangu hapa hapa.
 
Hoja yake kuhusu nini
Hoja zake kuhusu maslahi yake binafsi au

Kama TRA hainikati kodi, tatizo ni langu au la TRA ?.

Kama nalipwa afu sikai dukani kwani hawana baraza lao linaloshughulikia kesi kama izo kwa mujibu wa sheria zao. Wakulalamika hapa ilipaswa awe bosi anaemlipa hiyo pesa huyo pharmacist na sio huyu prof kpboko. Huyu ni masalahi yake tu binafsi yanamsumbua.
Tunatahitaji kuona taratibu zinafuatwa katika kila sekta kwa mujibu wa shetia. Tumeona kuna shemu mnalalamika ya kwamba mnalisaidia sana taifa, hivi kuna msaada mkubwa kwa taifa kama kulipa kodi?

Kama kuna Wafamasia hawakai kwenye maduka wanayoyasimamia na hawalipi kodi huenda wewe inalipa na unakaa dukani , lakini ni wajibu wa sisi watanzania wazalendo kuzikumbusha mamlaka kwa wale wasiofanya hivyo.
Upotoshwaji unaozungumziwa ni ule wa kudai kua Mfamasia ndiye anayepaswa kuuza dawa pekee na wengine wakitaka eti wasome ADDO, huu ni uongo na hauna hoja z msingi.
 
We koboko nimejaribu kufatilia nimeanza hisi Una tatizo binafsi juu ya wafamasia na nahisi Una information chache sana kuhusu wafamasia nimekuwekea pharmacy act Yao hapa chini usome uelewe mfamasia ana nafasi gani kwenye biashara ya dawa
Na kwanini anahitajika zaidi kwenye usimamizi na sheria zinasemaje

Nakushauri usijaribu kuyafahamu haya Mambo haya Kwa chuki hutoyaelewa kaa chini jifunze utaelewa vizuri makosa ya wafamasia wachache usigeneralize Kada nzima Kwani ni madaktari wangapi tunasikia wanafanya abortion ,madaktari wangapi ni walevi wakupindukia madaktari wangapi ni unethical kwenye sehem zao za kazi lakini makosa Yao hayajumuishi Baraza zima la madaktari Tanzania
Jiheshimu sanaaa koboko wewe toa chuki utafahamu unayotaka kufahamu
 

Attachments

  • THE PHARMACY ACT-2011.pdf
    5.4 MB · Views: 8
SOMO/USHAURI KWA WIZARA YA AFYA NA WAFAMASIA NCHINI KUHUSU OPOTOSHWAJI UNAOFANYWA MAKUSUDI NA BAADHI YA WATAALAM WASIOKUA WAMINIFU.

Na Prof Patrick Koboko(MD,MMED,MPH,MBA, PhD in Human Anatomy
)

Wasalaam!

Niwaombe Mods wa JF muache uzi huu ujitegemee, kuna mambo muhimu.Mimi ni mdau muhimu humu!

Kwanza nitoe pongezi kwa serikali yangu inavyojitahidi katika kulinda usalama wa afya za wananchi wake hususani waziri wa Afya Umy Mwalimu kwa jinsi anavyopambana ndani ya wizara ya Afya ingawa bado kuna watu wanaomzunguka wanampotosha kwa makusudi ili kulinda maslahi yao binafsi. Kupitia somo hili, naamini serikali itachukua maoni yangu na kuyafanyia kazi, wataalam wa dawa nao watajifunza hususani wale wanaopotosha umma wa watanzania kwa makusudi kulinda maslahi yao binafsi.

UPOTOSHWAJI WA MAKUSUDI UNAOFANYWA KWA WANANCHI.

Kwanza ifahamike kwamba hakuna chuki baina ya taaluma moja dhidi ya nyingine kwenye kada ya Afya, tatizo kubwa ni baadhi ya Wataalam kwa sababu ya njaa zao au ubinafsi usiokua sababu kutaka kufanya kila kitu kisiasa na kuipotosha jamii kitu ambacho huenda baadaye kikaleta madhara makubwa nchini kwa baadaye.

Nimetoa ushauri sana kwa kuandika humu ndani kama moja ya mtandao pendwa pamoja na mitandao mingine maarufu ya kijamii ambako ujumbe unaweza kuifikia jamii na mamlaka kwa haraka zaidi. Kama nilivyosema siku moja humu kwamba tuna tatizo kubwa sana la mifumo ya elimu yetu nchini, uelewa ni tatizo kubwa sana kwa baadhi ya wataalamu (siyo wote), mfumo tuliojengewa ni ule wa watu kupenda kujipatia vipato kwa njia za mkato na kujitapa kwa sababu wamesoma badala ya kuzalisha, mtu anamaliza shule badala ya kwenda kuzalisha, anafikiria cheti chake kikakae dukani kwa mwenzake ili alipwe pesa anayotaka yeye,hafikirii kwenda kuanzisha hata kiwanda kidogo za kuzalisha dawa ndogo ndogo za baridi au kuingia porini kufanya utafiti wa dawa za kutibu maradhi mbali mbali ili kulinusuru taifa na uagizaji wa dawa kutoka nje. Tunazalisha wanataaluma wazembe wanaowaza kukaa ofisini kupulizwa na viyoyozi badala ya kwenda porini kwenye Magome ya miti huko kutafuta suluhisho la maradhi ambayo yamekua yakiibuka kila uchwao. Hapa ndiko tatizo liliko.

Niwaombe wanataaluma wenzangu hasa wanazuoni wa kada hizi za Afya, tuzalishe wanataaluma wenye kujitegemea na siyo wanaowaza kukaa maofisini kuwaza vyeti vyao kutumika kufungulia maduka ya dawa au vituo vya afya na mahospitali. Tuwe na wataalam wenye tija wanaowaza kuzalisha na kuleta mapinduzi katika sekta ya Afya nchini. Mifumo ya Wanavyofanya kazi watanzania katika sekta ya Afya ni tofauti kabisa na ninayoiona hapa Afrika Kusini na hata Egypt nilikokaa takribani miaka 7 nikiwa mwalimu wa chuo kikuu na mwanafunzi huko.
Wenzetu wamejikita zaidi katika kuzalisha zaidi na siyo kukaa maofisini tu kubishana na kulalama na ndiyo maana dawa nyingi tunaingiza kutoka kwao.

HAKUNA UKWELI WOWOTE WALA HOJA YA KISAYANSI KUA MFAMASIA PEKEE NDIYE ANAYETAKIWA KUUZA AU KUTOA DAWA.

Kama nilivyosema awali ni kweli ndio uhalisia wenyewe ya kwamba Mfamasia anafanya kazi Hosptalini,Kwenye tafiti mbali mbali za dawa, Kiwandani, kua Mwalimu wa chuo kama mimi, Kwenye Godowns na stoo za kuhifadhia Dawa,maduka ya dawa na kwenye jamii pia . Daktari pia anafanya kazi Hosptalini, kua mwalimu wa chuo, Kiwandani,kwenye tafiti mbali mbali mbali, Godowns za kuhifadhia dawa, maduka ya kuuzia dawa na kwenye jamii pia, Muuguzi hali kadhalika. Katika maeneo haya kila mmoja ana jukumu lake kulingana na kuhitajika kwake.

Juzi tu tulikua kwenye utafiti wa Chanjo ya ugonjwa wa Corona, utakubaliana nami kua kulikua na madaktari wengi ndio na Wafamasia ndio wanaohangaika sana kwenye ugunduzi wa dawa na chanjo na dawa ya gonjwa hili, jiulize ni kwanini timu za madaktari na wafamasia ndizo zilikua mstari wa mbele kuhangaika juu ya dawa na chanjo ya gonjwa hili? Na bado utafiti unaendelea. Kwahiyo kazi bila team work haiwezi kwenda.

Nilisema ni ubinafsi mkubwa na ni upotoshwaji mkubwa unaofanywa na wachumia tumbo wachache katika taaluma ya Famasia nchini na wamefanikiwa kumpotosha hata waziri kua Wafamasia pekee ndio wanaopaswa kuuza dawa.

Kwanini wao tu ndio wanaotaka wakae madukani wauze dawa wakati hata mahospitalini tunafanya kazi na wao pamoja? Kwanini kwenye maduka nako tusifanye kazi as a team? Kuna sababu yeyote kimsingi au kisayansi kumzuia daktari au nesi kuuza dawa ikiwa yeye ndio amechagua kukaa kwenye duka la dawa badala ya kufanya kazi hospitani.Kila mtu anafanya kazi kwa choice yake, kuna Mfamasia anapenda afanye kazi hospitalini na mwingine kiwandani au kwenye maduka ya dawa, hali kadhalika kwa daktari na nesi hivyo hivyo, kuna shida pia kufanya kazi kama team kufanya kazi kwenye maduka?

Mnajua kua kwenye viwanda vya dawa wanafanya kazi as a team kama ilivyo kwa hospitali kama ambavyo mimi niliwahi kufanya kazi kwenye kiwanda kimoja cha dawa huko Tanzania nikiwa daktari?.Wafamasia wachache waache ubinafsi na shida zao binafsi kuipotosha serikali na umma kwa ujumla.

NI MADUKA MANGAPI YANATOA DAWA ZINAZOHITAJI VYETI VYA MADAKTARI NCHINI?

Labda nimwambie Mhe Waziri Ummy kama alikua hajui, ni 99% ya maduka ya famasi nchini ambayo sheria inayataka yatoe dawa zinazohitaji maelekezo ya daktari (Dr's Prescriptions) hayafanyi hivyo. Kama ninadanganya atume timu yake ya siri kufanya uchunguzi huo kama hawatafungia maduka yote nchini. Kulaumu kua wauza dawa wasiokua wafamasia ndio wanaoharibu utaratibu huu na kuingiza afya za watanzania matatatani siyo kweli, Zile video clips zilizokua zikisambazwa mitandaoni kuonesha kuna watoa dawa hawana taaluma zilikua ni propaganda zilizoanzishwa na Wakaguzi wachache wachumia tumbo na ndiyo maana utaona hazikuowaonesha waliokua wakihoji maswali , wafanye uchunguzi wajionnee waache kupotoshwa na wachumia matumbo wachache,kabla sijaja kuandika humu nikiwa nchini nilifanya utafiti huu na hata sasa kuna vijana wangu walioko huko Tanzania wakifanya uchunguzi juu ya hili ili ninapotoa ushauri niseme vitu vya ukweli na uhakika.

SWALI:(1). Kama kwenye famasi mgonjwa ameenda kununua dawa kali yenye uhitaji wa cheti cha daktari na hana cheti hicho, atamhudumia au atamrudisha hospitali akaandikiwe na daktari kisha arudi dukani? Atawezaje kumhudumia wakati yeye siyo daktari na hawezi kuandika prescription?

Maana kuna hoja ya Kijinga hapa kua Mfamasia anaweza kuandika prescription kwa sababu anaweza kuisoma ile ya daktari eti kwa sababu amesoma Anatomy, Physiology,Pathology na Pharmacology na dio Upotoshaji mkubwa inakoanzia hapa.
Daktari ama tabibu Pathophysiology au history taking kwake ni masomo yanayojitegemea na yana principles na utaratibu wake achilia mbali Physiology na Anatomy au Pathology. Mfamasia anajua maana ya Main Complain, HPI na SOCRATES? amesomea wapi kama kuna mwenye kuthibisha hili aseme humu humu.

(2) .Kama waziri anashauriwa Wafamasia ndio wanaotakiwa kukaa mpaka kwenye maduka ya dawa muhimu ama DLDM ambayo hayahitaji cheti cha Mfamasia wala cheti cha daktari, ni kwa msingi upi sasa wakati dawa zenyewe hazihitaji Mfamasia wala cheti cha daktari?
Kama daktari au muuguzi aliyesomea kozi yake akafuzu vyema anauza DLDM, tatizo liko wapi hasa?
Kwanini tunaweka urasimu na siasa kwenye mambo muhimu kiasi hiki?

NI MADUKA MANGAPI YA DAWA TANZANIA WAFAMASIA HUBAKIA DUKANI MUDA WOTE WA KAZI?

Toka awali nilisema kwamba upotoshaji wa makusudi ukiendelea, kuna mambo yasiyosemwa tutaweka hadharani ili kusudi watanzania wajue nini kinajiri kwenye maduka haya ya dawa na ni kwa nia njema wala hakuna chuki hapa.Kila mtanzania ana haki ya kukinda afya ya mwenzake....

Ni 99.99% Tanzania ya maduka ya dawa ambayo yanatakiwa kusimamiwa na wataalam wa dawa wenye viwango vya elimu kuanzia na shahada ya kwanza hawakai kwenye maduka hayo kama sheria inavyowataka. Wanalipwa pesa nyingi ambazo hazikatwi Kodi kuanzia na milioni moja(1,000,000+) na kuendelea. Kama wizara ilikua hailijui hili basi wafanye uchunguzi wataelewa tu. Nchi inalia na mapato lakini kuna watu wanapokea pesa taslim bila makato ya kodi wakati kila mfanyakazi nchini, ni lazima na ni sheria kwa kila mfanyakazi kukatwa kodi. TRA na wizara ya fedha waliangalie hili serikali inapoteza pesa nyingi sana. Hata kama wanalipia leseni zao lakini taaluma zingine zinalipa vile vile na linapokuja suala kulipwa kwa kufanya kazi kodi ni lazima kwa taratibu za nchi yetu.
Ukaguzi wa kina wa Wizara ya Afya, Wizara ya Fedha na TRA kwa ujumla.
Kama nchi nzima ina wafamasia zaidi ya 1000 wenye level ya degree wanaosimamia maduka ya dawa na wanalipwa mishahara yao bila kukatwa kodi, ni kiasi gani taifa linapoteza kwa mwaka badala ya kuhangaika na tozo hizi ambazo zinaumiza zaidi watu wa chini?

KATI YA BARAZA LA WAFAMASIA NA TMDA NI NANI ANATAKIWA KUKAGUA DAWA NCHINI?

Huu nao ni mkanganyiko mkubwa sana Tanzania na Waziri anapotoshwa makusudi tu kwa vile labda siyo Mtaalam wa Afya maana wakati Wizara inaongozwa na Waziri mtaalam hatukuona haya, sijajua kazi ya Naibu waziri na Katibu mkuu ambao ni wataalam kwanini hawatoi ushauri huu kwa waziri.

Duniani kote, FDA au TMDA kwa kwetu Tanzania hizi ndizo taasisi pekee zinazotakiwa kukagua usalama wa dawa kisheria na taasisi hizi ndani yake utakuta kuna Wafamasia,Madaktari,Wauguzi,Wakemia,wataalam wa lishe na wataalam wengineo mpaka wanasheria kila mtu na eneo lake katika utendaji wake, and this is according to international standards, kwa Tz sijui kuna tatizo gani ndugu zangu hii kazi wanapewa Baraza la Wafamasia(Pharmacy council) ambalo hili ni baraza la kitaaluma ambalo kimsingi kazi yake ni kusajili wataalam na kuwapatia leseni za kazi, yaani sawa na kusema MCT au TANNA wafanye kazi za kukagua mahospitali ili hali haya ni mabaraza ya kitaaluma na yana kazi zake za msingi, labda wapitie kukagua leseni na vyeti vya wataalam wao waliowasajili. Sasa huku Tanzania Baraza la Wafamasia ndio wanakagua dawa, wanasajili Maduka ya dawa, huku wanasajili wataalam, yaani mambo Changanyikeni.Kama watapita kwenye kwenye maduka ya dawa na mahospitalini au viwandani kukagua leseni za wataalam hapo sawa maana kuna zinazogushiwa na ziingine kumalizika muda wake.

USAHURI wangu kwenye hili ni kwamba kazi ya kutoa vibali vya kufungua maduka ya dawa pamoja na ukaguzi wa madawa na maduka waachiwe TMDA ambao ndio kazi zao kimsingi na kama wataalam hawatoshi Wizara iajiri tu taasisi itimie na ifanye kazi kwa weledi waache kufanya mambo kienyeji.Baraza la Wafamasia ni Baraza la kitaaluma liachwe lifanye kazi zake za kimsingi ambazo ni kusajili wataalam, kuwapima na kuwapatia leseni za taaluma hiyo, wakague pia lesini zao ikiwa ni za kweli au bado ni valid.


HITIMISHO: Naiomba sana Wizara ya Afya na Mamlaka zizingatie za serikali ushauri huu ni muhimu sana, kuna upotoshwaji mkubwa unaofanywa na baadhi ya wataalam wanaokiuka maadili yao ya kazi. Tunapoteza pesa nyingi sana na umakini katika eneo hili muhimu ambalo liliachwa nyuma muda mrefu.

Ni ushauri pia kwa wataalam wa kada za Afya zaidi Wafamasia wazingatie, tuache kufanya kazi kwa mazoea, tuzingatie maadili ya kitaaluma. Tuzalishe ili taifa letu kidonge mbele.
Mimi sijikwezi na wala sina tatizo na taaluma ya mtu, naziheshimu taaluma za watu wengine na ndio tunaofanya kazi kwa pamoja kama timu ili kulinda afya ya jamii kama viapo vyetu vinavyotaka.

Ahsanteni!

Prof Partick Koboko(MD,MMED,MPH,MBA, PhD in Human Anatomy)
kobokopatricdr@gmail.com
Mkuu naomba kuyajuwa madawa yanayopaswa kutolewa kwa maelezo ya daktari nijuwe.
 
Huo utafiti wako wakichuki chuki umeufanyia wapi ,unajua mfamasia asipitokea kwenye pharmacy siku kadhaa tu inamletea shida yeye na leseni yake unajua kwamba kuna signing books za mfamasia kwenye kila pharmacy ambazo wanazisign unajua pharmacy council wanavojitahid kufatilia maswala hayo ya kumbana mfamasia mpaka wanafikiria kuja na mbinu mbalimbali Kwa wafamasia

Kaa Kwa kutulia shughulika na addo yako uza dawa zako na ufate Sheria ukikiuka Sheria tutakuja kufunga kiduka chako cha dawa natumai umenifahamu koboko
 
Ninachosema humu ni ukweli usiopingika kua Wafamasia wanalipwa pesa nyingi zisizokatwa kodi na wengi wao 99% hawakai kwenye maduka yao wanaosimamia.Ninesema 99% kama una akili unaelewa namaanisha nini, hiyo 1% iliyobakia ndio wanaobakia kwenye maduka yao wanayosimamia. Ni wote pesa wanayolipwa kaikatwi kodi. Thibitisho uongo wangu hapa hapa.
Prof koboko acha kujidhalilisha.

Kilichopo hapa sio kuthibitisha kuwa ni kweli au uongo kwa ulichokisema kuhusu mambo ya kodi na pesa wanazolipwa pharmacist, tufanye basi ni 100% wote hawakai kwenye izo duka, maana kama ni wizi, ukiritimba na ukwepaji kodi upo katika sekta na taasisi nyingi sana, kama hoja zako ni masuala ya kodi, wizi na inshu kama izo, why pharmacist pekee ? Huoni kuwa ni unachuki zako binafsi na hao watu ?

Mada yako ya msingi kabisa na
Hoja zako za msingi tangu awali kwenye bandiko zako zote ni kuhusu afya za watanzania kiujumla kupitia izi famasi zetu. Na umezungumzia mambo mengi kiwemo addo, baraza la famasia, waziri pamoja na wizara ya afya, sasa haya masuala unayoibua leo ya kodi, kuwa 99% hawakai kwenye izo pharamcy ni yanakuharibia hata hoja zako msingi zilizobeba maandiko yako, maana yanakufunua wazi hapa kuwa ni una jnshu za kimaslahi tuuu.

Huko kwingine kama kukaa viwandani na kuzalisha madawa ninakubaliana nawewe 100% maana hata nchi za wenzetu hao watu pharmacist wengi wao asilimia kubwa wapo kwenye uzalishaji wa madawa viwandani. Ninawasiwasi tu ni muda mrefu sana hujakaa tanzania au huijui vizuri, ivi tanzania inawiwanda vingapi vya madawa, ni imewekeza kiasi gani upande huo wa kuzalisha madawa ?. Usibaki kulaumu na kutupia mzigo tu pharmacist kila kukicha akati hali ya uwekezaji upande wa afya na madawa wa serikali yako unaifahamu.
 
SOMO/USHAURI KWA WIZARA YA AFYA NA WAFAMASIA NCHINI KUHUSU OPOTOSHWAJI UNAOFANYWA MAKUSUDI NA BAADHI YA WATAALAM WASIOKUA WAMINIFU.

Na Prof Patrick Koboko(MD,MMED,MPH,MBA, PhD in Human Anatomy
)

Wasalaam!

Niwaombe Mods wa JF muache uzi huu ujitegemee, kuna mambo muhimu.Mimi ni mdau muhimu humu!

Kwanza nitoe pongezi kwa serikali yangu inavyojitahidi katika kulinda usalama wa afya za wananchi wake hususani waziri wa Afya Umy Mwalimu kwa jinsi anavyopambana ndani ya wizara ya Afya ingawa bado kuna watu wanaomzunguka wanampotosha kwa makusudi ili kulinda maslahi yao binafsi. Kupitia somo hili, naamini serikali itachukua maoni yangu na kuyafanyia kazi, wataalam wa dawa nao watajifunza hususani wale wanaopotosha umma wa watanzania kwa makusudi kulinda maslahi yao binafsi.

UPOTOSHWAJI WA MAKUSUDI UNAOFANYWA KWA WANANCHI.

Kwanza ifahamike kwamba hakuna chuki baina ya taaluma moja dhidi ya nyingine kwenye kada ya Afya, tatizo kubwa ni baadhi ya Wataalam kwa sababu ya njaa zao au ubinafsi usiokua sababu kutaka kufanya kila kitu kisiasa na kuipotosha jamii kitu ambacho huenda baadaye kikaleta madhara makubwa nchini kwa baadaye.

Nimetoa ushauri sana kwa kuandika humu ndani kama moja ya mtandao pendwa pamoja na mitandao mingine maarufu ya kijamii ambako ujumbe unaweza kuifikia jamii na mamlaka kwa haraka zaidi. Kama nilivyosema siku moja humu kwamba tuna tatizo kubwa sana la mifumo ya elimu yetu nchini, uelewa ni tatizo kubwa sana kwa baadhi ya wataalamu (siyo wote), mfumo tuliojengewa ni ule wa watu kupenda kujipatia vipato kwa njia za mkato na kujitapa kwa sababu wamesoma badala ya kuzalisha, mtu anamaliza shule badala ya kwenda kuzalisha, anafikiria cheti chake kikakae dukani kwa mwenzake ili alipwe pesa anayotaka yeye,hafikirii kwenda kuanzisha hata kiwanda kidogo za kuzalisha dawa ndogo ndogo za baridi au kuingia porini kufanya utafiti wa dawa za kutibu maradhi mbali mbali ili kulinusuru taifa na uagizaji wa dawa kutoka nje. Tunazalisha wanataaluma wazembe wanaowaza kukaa ofisini kupulizwa na viyoyozi badala ya kwenda porini kwenye Magome ya miti huko kutafuta suluhisho la maradhi ambayo yamekua yakiibuka kila uchwao. Hapa ndiko tatizo liliko.

Niwaombe wanataaluma wenzangu hasa wanazuoni wa kada hizi za Afya, tuzalishe wanataaluma wenye kujitegemea na siyo wanaowaza kukaa maofisini kuwaza vyeti vyao kutumika kufungulia maduka ya dawa au vituo vya afya na mahospitali. Tuwe na wataalam wenye tija wanaowaza kuzalisha na kuleta mapinduzi katika sekta ya Afya nchini. Mifumo ya Wanavyofanya kazi watanzania katika sekta ya Afya ni tofauti kabisa na ninayoiona hapa Afrika Kusini na hata Egypt nilikokaa takribani miaka 7 nikiwa mwalimu wa chuo kikuu na mwanafunzi huko.
Wenzetu wamejikita zaidi katika kuzalisha zaidi na siyo kukaa maofisini tu kubishana na kulalama na ndiyo maana dawa nyingi tunaingiza kutoka kwao.

HAKUNA UKWELI WOWOTE WALA HOJA YA KISAYANSI KUA MFAMASIA PEKEE NDIYE ANAYETAKIWA KUUZA AU KUTOA DAWA.

Kama nilivyosema awali ni kweli ndio uhalisia wenyewe ya kwamba Mfamasia anafanya kazi Hosptalini,Kwenye tafiti mbali mbali za dawa, Kiwandani, kua Mwalimu wa chuo kama mimi, Kwenye Godowns na stoo za kuhifadhia Dawa,maduka ya dawa na kwenye jamii pia . Daktari pia anafanya kazi Hosptalini, kua mwalimu wa chuo, Kiwandani,kwenye tafiti mbali mbali mbali, Godowns za kuhifadhia dawa, maduka ya kuuzia dawa na kwenye jamii pia, Muuguzi hali kadhalika. Katika maeneo haya kila mmoja ana jukumu lake kulingana na kuhitajika kwake.

Juzi tu tulikua kwenye utafiti wa Chanjo ya ugonjwa wa Corona, utakubaliana nami kua kulikua na madaktari wengi ndio na Wafamasia ndio wanaohangaika sana kwenye ugunduzi wa dawa na chanjo na dawa ya gonjwa hili, jiulize ni kwanini timu za madaktari na wafamasia ndizo zilikua mstari wa mbele kuhangaika juu ya dawa na chanjo ya gonjwa hili? Na bado utafiti unaendelea. Kwahiyo kazi bila team work haiwezi kwenda.

Nilisema ni ubinafsi mkubwa na ni upotoshwaji mkubwa unaofanywa na wachumia tumbo wachache katika taaluma ya Famasia nchini na wamefanikiwa kumpotosha hata waziri kua Wafamasia pekee ndio wanaopaswa kuuza dawa.

Kwanini wao tu ndio wanaotaka wakae madukani wauze dawa wakati hata mahospitalini tunafanya kazi na wao pamoja? Kwanini kwenye maduka nako tusifanye kazi as a team? Kuna sababu yeyote kimsingi au kisayansi kumzuia daktari au nesi kuuza dawa ikiwa yeye ndio amechagua kukaa kwenye duka la dawa badala ya kufanya kazi hospitani.Kila mtu anafanya kazi kwa choice yake, kuna Mfamasia anapenda afanye kazi hospitalini na mwingine kiwandani au kwenye maduka ya dawa, hali kadhalika kwa daktari na nesi hivyo hivyo, kuna shida pia kufanya kazi kama team kufanya kazi kwenye maduka?

Mnajua kua kwenye viwanda vya dawa wanafanya kazi as a team kama ilivyo kwa hospitali kama ambavyo mimi niliwahi kufanya kazi kwenye kiwanda kimoja cha dawa huko Tanzania nikiwa daktari?.Wafamasia wachache waache ubinafsi na shida zao binafsi kuipotosha serikali na umma kwa ujumla.

NI MADUKA MANGAPI YANATOA DAWA ZINAZOHITAJI VYETI VYA MADAKTARI NCHINI?

Labda nimwambie Mhe Waziri Ummy kama alikua hajui, ni 99% ya maduka ya famasi nchini ambayo sheria inayataka yatoe dawa zinazohitaji maelekezo ya daktari (Dr's Prescriptions) hayafanyi hivyo. Kama ninadanganya atume timu yake ya siri kufanya uchunguzi huo kama hawatafungia maduka yote nchini. Kulaumu kua wauza dawa wasiokua wafamasia ndio wanaoharibu utaratibu huu na kuingiza afya za watanzania matatatani siyo kweli, Zile video clips zilizokua zikisambazwa mitandaoni kuonesha kuna watoa dawa hawana taaluma zilikua ni propaganda zilizoanzishwa na Wakaguzi wachache wachumia tumbo na ndiyo maana utaona hazikuowaonesha waliokua wakihoji maswali , wafanye uchunguzi wajionnee waache kupotoshwa na wachumia matumbo wachache,kabla sijaja kuandika humu nikiwa nchini nilifanya utafiti huu na hata sasa kuna vijana wangu walioko huko Tanzania wakifanya uchunguzi juu ya hili ili ninapotoa ushauri niseme vitu vya ukweli na uhakika.

SWALI:(1). Kama kwenye famasi mgonjwa ameenda kununua dawa kali yenye uhitaji wa cheti cha daktari na hana cheti hicho, atamhudumia au atamrudisha hospitali akaandikiwe na daktari kisha arudi dukani? Atawezaje kumhudumia wakati yeye siyo daktari na hawezi kuandika prescription?

Maana kuna hoja ya Kijinga hapa kua Mfamasia anaweza kuandika prescription kwa sababu anaweza kuisoma ile ya daktari eti kwa sababu amesoma Anatomy, Physiology,Pathology na Pharmacology na dio Upotoshaji mkubwa inakoanzia hapa.
Daktari ama tabibu Pathophysiology au history taking kwake ni masomo yanayojitegemea na yana principles na utaratibu wake achilia mbali Physiology na Anatomy au Pathology. Mfamasia anajua maana ya Main Complain, HPI na SOCRATES? amesomea wapi kama kuna mwenye kuthibisha hili aseme humu humu.

(2) .Kama waziri anashauriwa Wafamasia ndio wanaotakiwa kukaa mpaka kwenye maduka ya dawa muhimu ama DLDM ambayo hayahitaji cheti cha Mfamasia wala cheti cha daktari, ni kwa msingi upi sasa wakati dawa zenyewe hazihitaji Mfamasia wala cheti cha daktari?
Kama daktari au muuguzi aliyesomea kozi yake akafuzu vyema anauza DLDM, tatizo liko wapi hasa?
Kwanini tunaweka urasimu na siasa kwenye mambo muhimu kiasi hiki?

NI MADUKA MANGAPI YA DAWA TANZANIA WAFAMASIA HUBAKIA DUKANI MUDA WOTE WA KAZI?

Toka awali nilisema kwamba upotoshaji wa makusudi ukiendelea, kuna mambo yasiyosemwa tutaweka hadharani ili kusudi watanzania wajue nini kinajiri kwenye maduka haya ya dawa na ni kwa nia njema wala hakuna chuki hapa.Kila mtanzania ana haki ya kukinda afya ya mwenzake....

Ni 99.99% Tanzania ya maduka ya dawa ambayo yanatakiwa kusimamiwa na wataalam wa dawa wenye viwango vya elimu kuanzia na shahada ya kwanza hawakai kwenye maduka hayo kama sheria inavyowataka. Wanalipwa pesa nyingi ambazo hazikatwi Kodi kuanzia na milioni moja(1,000,000+) na kuendelea. Kama wizara ilikua hailijui hili basi wafanye uchunguzi wataelewa tu. Nchi inalia na mapato lakini kuna watu wanapokea pesa taslim bila makato ya kodi wakati kila mfanyakazi nchini, ni lazima na ni sheria kwa kila mfanyakazi kukatwa kodi. TRA na wizara ya fedha waliangalie hili serikali inapoteza pesa nyingi sana. Hata kama wanalipia leseni zao lakini taaluma zingine zinalipa vile vile na linapokuja suala kulipwa kwa kufanya kazi kodi ni lazima kwa taratibu za nchi yetu.
Ukaguzi wa kina wa Wizara ya Afya, Wizara ya Fedha na TRA kwa ujumla.
Kama nchi nzima ina wafamasia zaidi ya 1000 wenye level ya degree wanaosimamia maduka ya dawa na wanalipwa mishahara yao bila kukatwa kodi, ni kiasi gani taifa linapoteza kwa mwaka badala ya kuhangaika na tozo hizi ambazo zinaumiza zaidi watu wa chini?

KATI YA BARAZA LA WAFAMASIA NA TMDA NI NANI ANATAKIWA KUKAGUA DAWA NCHINI?

Huu nao ni mkanganyiko mkubwa sana Tanzania na Waziri anapotoshwa makusudi tu kwa vile labda siyo Mtaalam wa Afya maana wakati Wizara inaongozwa na Waziri mtaalam hatukuona haya, sijajua kazi ya Naibu waziri na Katibu mkuu ambao ni wataalam kwanini hawatoi ushauri huu kwa waziri.

Duniani kote, FDA au TMDA kwa kwetu Tanzania hizi ndizo taasisi pekee zinazotakiwa kukagua usalama wa dawa kisheria na taasisi hizi ndani yake utakuta kuna Wafamasia,Madaktari,Wauguzi,Wakemia,wataalam wa lishe na wataalam wengineo mpaka wanasheria kila mtu na eneo lake katika utendaji wake, and this is according to international standards, kwa Tz sijui kuna tatizo gani ndugu zangu hii kazi wanapewa Baraza la Wafamasia(Pharmacy council) ambalo hili ni baraza la kitaaluma ambalo kimsingi kazi yake ni kusajili wataalam na kuwapatia leseni za kazi, yaani sawa na kusema MCT au TANNA wafanye kazi za kukagua mahospitali ili hali haya ni mabaraza ya kitaaluma na yana kazi zake za msingi, labda wapitie kukagua leseni na vyeti vya wataalam wao waliowasajili. Sasa huku Tanzania Baraza la Wafamasia ndio wanakagua dawa, wanasajili Maduka ya dawa, huku wanasajili wataalam, yaani mambo Changanyikeni.Kama watapita kwenye kwenye maduka ya dawa na mahospitalini au viwandani kukagua leseni za wataalam hapo sawa maana kuna zinazogushiwa na ziingine kumalizika muda wake.

USAHURI wangu kwenye hili ni kwamba kazi ya kutoa vibali vya kufungua maduka ya dawa pamoja na ukaguzi wa madawa na maduka waachiwe TMDA ambao ndio kazi zao kimsingi na kama wataalam hawatoshi Wizara iajiri tu taasisi itimie na ifanye kazi kwa weledi waache kufanya mambo kienyeji.Baraza la Wafamasia ni Baraza la kitaaluma liachwe lifanye kazi zake za kimsingi ambazo ni kusajili wataalam, kuwapima na kuwapatia leseni za taaluma hiyo, wakague pia lesini zao ikiwa ni za kweli au bado ni valid.


HITIMISHO: Naiomba sana Wizara ya Afya na Mamlaka zizingatie za serikali ushauri huu ni muhimu sana, kuna upotoshwaji mkubwa unaofanywa na baadhi ya wataalam wanaokiuka maadili yao ya kazi. Tunapoteza pesa nyingi sana na umakini katika eneo hili muhimu ambalo liliachwa nyuma muda mrefu.

Ni ushauri pia kwa wataalam wa kada za Afya zaidi Wafamasia wazingatie, tuache kufanya kazi kwa mazoea, tuzingatie maadili ya kitaaluma. Tuzalishe ili taifa letu kidonge mbele.
Mimi sijikwezi na wala sina tatizo na taaluma ya mtu, naziheshimu taaluma za watu wengine na ndio tunaofanya kazi kwa pamoja kama timu ili kulinda afya ya jamii kama viapo vyetu vinavyotaka.

Ahsanteni!

Prof Partick Koboko(MD,MMED,MPH,MBA, PhD in Human Anatomy)
kobokopatricdr@gmail.com
Ni ukiritimba wa hao wapuuzi wanaojiita wafamasia..

Vigezo na masharti tuu ndio yazingatiwe,tukienda kwa staili hii wanayotaka hao mafamasia uchwara italazimu ukitaka kujenga utafute Mkandarasi kama sheria inavyotaka.
 
Tunatahitaji kuona taratibu zinafuatwa katika kila sekta kwa mujibu wa shetia. Tumeona kuna shemu mnalalamika ya kwamba mnalisaidia sana taifa, hivi kuna msaada mkubwa kwa taifa kama kulipa kodi?

Kama kuna Wafamasia hawakai kwenye maduka wanayoyasimamia na hawalipi kodi huenda wewe inalipa na unakaa dukani , lakini ni wajibu wa sisi watanzania wazalendo kuzikumbusha mamlaka kwa wale wasiofanya hivyo.
Upotoshwaji unaozungumziwa ni ule wa kudai kua Mfamasia ndiye anayepaswa kuuza dawa pekee na wengine wakitaka eti wasome ADDO, huu ni uongo na hauna hoja z msingi.
Basi next time uje na madudu yanayofanywa na madokta na manesi.
 
Prof koboko acha kujidhalilisha.

Kilichopo hapa sio kuthibitisha kuwa ni kweli au uongo kwa ulichokisema kuhusu mambo ya kodi na pesa wanazolipwa pharmacist, tufanye basi ni 100% wote hawakai kwenye izo duka, maana kama ni wizi, ukiritimba na ukwepaji kodi upo katika sekta na taasisi nyingi sana, kama hoja zako ni masuala ya kodi, wizi na inshu kama izo, why pharmacist pekee ? Huoni kuwa ni unachuki zako binafsi na hao watu ?

Mada yako ya msingi kabisa na
Hoja zako za msingi tangu awali kwenye bandiko zako zote ni kuhusu afya za watanzania kiujumla kupitia izi famasi zetu. Na umezungumzia mambo mengi kiwemo addo, baraza la famasia, waziri pamoja na wizara ya afya, sasa haya masuala unayoibua leo ya kodi, kuwa 99% hawakai kwenye izo pharamcy ni yanakuharibia hata hoja zako msingi zilizobeba maandiko yako, maana yanakufunua wazi hapa kuwa ni una jnshu za kimaslahi tuuu.

Huko kwingine kama kukaa viwandani na kuzalisha madawa ninakubaliana nawewe 100% maana hata nchi za wenzetu hao watu pharmacist wengi wao asilimia kubwa wapo kwenye uzalishaji wa madawa viwandani. Ninawasiwasi tu ni muda mrefu sana hujakaa tanzania au huijui vizuri, ivi tanzania inawiwanda vingapi vya madawa, ni imewekeza kiasi gani upande huo wa kuzalisha madawa ?. Usibaki kulaumu na kutupia mzigo tu pharmacist kila kukicha akati hali ya uwekezaji upande wa afya na madawa wa serikali yako unaifahamu.
Kosa la mtu mwingine lisikupelekee na wewe kuvunja sheria ndugu. Huu ni ukweli mtupu na wala hakuna chuki na mtu kama ambavyo mmekuwa mkifikiria kua maslahi yenu yamegeuzwa. Msiipotoshe serikali simsmieni katika ukweli.

Mbona hamjibu hoja ya ushauri kua duniani kote ukaguzi wa dawa hufanywa na FDAs au TMDA kwà Tanzania na Pharamacy Council ibakie na kazi za kusajili wataalam kama yalivyo mabaraza mengine nchini?
 
Back
Top Bottom