binti kiziwi
JF-Expert Member
- Aug 4, 2014
- 8,905
- 22,296
Sasa katika hali ya kawaida, Yeye kujenga shule Tz kama malengo yake ya muda mrefu ya kushinda miss world Sisi kama Tz tunapata hasara gani zaidi ya faida ya kujengewa shule?Pamoja na ubinafsi wa viongozi, kuna hulka huwa tunayo kwamba wanaokuja kutusaidia kuna wanachopata. Hii husemwa hasa pale mtoa msaada akiwa na ngozi nyeupe, japo hata mwezetu akianzosha taasisi ya kusaidia jamii, tunakimbilia kusema ni dili anafukuzia hela za wazungu. Sijui tunataka wenye mahitaji kwenye jamii yetu wasaidiwe na nani. Kuhusu huyu miss world, nimeona twitter mtu kaandika wazungu huwa wa mikakati sana, kwamba msaada aliotupa miaka minne iliyopita anakuja kuutumia kushinda miss world. Kwamba binti mwenye miaka 18 alikuwa na foresight ya kwenda sehemu ngeni kabisa kwake, kijijini ndani ndani, akajenga shule watoto wasome, Ili miaka ya mbeleni pengine vitamsaidia ashinde miss world. Hao watoto wanaosomeshwa elimu waliyopata si kitu, issue ni binti kashinda miss world Kwa kuwatumia.
Wakati huo huo sisi watoto ambao wala hatuhitaji kwenda mbali kuona wanavyoishi hatuna msaada kwao. Tunawafungia vioo wakija kutuoshea vioo vya magari barabarani, wakituomba hela tukiwa kwenye foleni tunasema wanatumiwa, ni mradi wa mtu, zikianzishwa harakati kupambania uboreshwaji wa maisha kwa wote, sio tu hatuungi mkono, tunabeza.
Aliyeargue hivyo atakuwa kiongozi mwenye wivu kuwa yeye hajafanya chochote na binti wa miaka 18 amefanya kitu.
Na bado this time akija kuleta msaada mwingine atasindikizwa na msafara wa V8 new model kama kumi hivi za viongozi zilizonunuliwa kwa kodi ya mtanzania……
Shame on us!