Mmawia
JF-Expert Member
- Aug 20, 2013
- 121,955
- 95,276
Mkuu ukisikia kuishiwa mipango ndio huko watahangaika sana hao ma dc maana mbunge ni chaguo la wananchi wenyewehii ni too low kwa ccm. yaani wanajipa hata haki miliki ya kutoa misaada?
Mkuu ukisikia kuishiwa mipango ndio huko watahangaika sana hao ma dc maana mbunge ni chaguo la wananchi wenyewehii ni too low kwa ccm. yaani wanajipa hata haki miliki ya kutoa misaada?
Huyo kasesera anajitafutia kufa njaa''Mimi nimechaguliwa na wananchi, wewe umeletwa na Rais''-Msigwa.
''Manispaa niya kwetu, huyu ameletwa tu-Msigwa
''Leo ninakutolea uvivu na waandishi wa habari wanachukua-Msigwa.
''Kila kwenye kikao cha CCM unanisema, acha mambo ya kishamba shamba-Msigwa.
''Sasa hivi nitapambana na wewe serially''-Msigwa
''Maafa sio ya kwako, maafa niya Watanzania wote''-Msigwa
''Si una power ya kuniweka ndani, kaniweke basi ndani''-Msigwa
''Sina shida ya kukuweka ndani''-Kasesera
''Sikiliza, mimi ninakuheshimu sana ndio maana sina shida ya kubishana na wewe''-Kasesera.
Politicians and politics at its best!
Wanasiasa wetu wanataka kutwangana ngumi, kisa nani anakuwa mbele mbele katika kutoa misaada ya wahanga wa mvua ya el nino!
Vurumai hizo zilizotokea baada ya Msigwa kukasirishwa na kitengo cha DC kutaka kumuengua ili asionekane anatoa msaada kwa watu wa jimbo lake
Inaelekea hawa maDC wanafikiria njia ya kupata attention ya Magufuli na kuonekana wanafanya kazi ni kuwakorofisha wabunge wa wilaya zao na wao kuonekana kwenye luninga wanapogombana ; naamini Rais hataingia kwenye huu mtego kuwa wale wanaojionesha kwenye luninga na kugombana na wabunge ndio watabaki kuwa maDc au kupandishwa kuwa ma RC kama alivyoahidiwa Makonda !!!
View attachment 324104
View attachment 324105
View attachment 324106
Kumetokea mabishano makali sana kati ya Mbunge Msigwa na DC Kasesera eneo la Iringa Mjini baada kuwa wamewatembelea wahanga wa nyumba zilizoezuliwa na mvua kubwa na kusababisha baadhi ya watu ktk Tarafa ya Nduli
Vurumai hizo zilizotokea baada ya Msigwa kukasirishwa na kitengo cha DC kutaka kumuengua ili asionekane anatoa msaada kwa watu wa jimbo lake bali DC ndio ionekane anajali wananchi.Shutuma zilienda mbali baada ya Msigwa kumueleza DC kuwa anajuwa anamhujumu na amekuwa anapanga mikakati ya siri ya kumfanyia hujuma ili aonekane hafanyi kazi jimboni kwake.
Juhudi hizo zimefanyika week iliyopita ambapo DC kwa kushirikiana na Humphley Polepole waliandaa "mdahalo" na wanafunzi wa vyu vikuu mkoani Iringa na kuanza kumsema vibaya Mbunge Msigwa,katika mdahalo huo Polepole amerekodiwa akisema Iringa awalikosea sana kumchagua Msigwa sbb alikuwa anamuunga mkono "fisadi" Lowassa
Wakati DC Kasesera alimshutumu Mb Msigwa kutokwenda Tarafa ya Pawaga kusaidia wahanga wa mafuriko na Msigwa akamjibu kuwa aanze kumwambia Lukuvi kwanini hajaenda maana Tarafa ya Pawaga ipo ndani ya Jimbo la Isimani,na hata yeye akienda sio lazima DC ajue,kama ambavyo yeye anaenda na kupiga picha na kurusha Facebook akimbeba mpiga picha ambaye haitaji msaada wa kubebwa.
Vurugu hizo ziliamuliwa na diwani na Meya wa Mji. Mwishoni Msigwa akamwambia DC awaite polisi wamuweke ndani maana katika viako vya CCM DC Kasesera amekuwa akisema lazima amuweke ndani Msigwa kumtia adabu
Kazi kweli kweli......
Kasesera ni mpita njia huyo,msigwa ndiye chaguo la wana wa iringaHa ha ha. Cheki Msigwa anavyovua koti lake. Eti "...everywhere, in Facebook sijui wapi...I use strategies..." Huyu mchungaji aache kupanic. Mwisho wa siku yeye ndio ataonekana kichaa. Kasesera kamseti na yeye kaingia kichwa kichwa.
Mkuu minyoo hilo tatizo la wakuu wa wilaya nafikiri wanakuwa wanatekeleza maagizo ya wakubwa zao kutoka juuH
hakuna cha kichwa kichwa hapo Mkuu wa wilaya alimkosea Mbunge kwa kutaka kumdhalilisha ni vyema wakuu wa wilaya wakawaheshimu wabunge pasipo kuweka itikadi za Vyama vyao mbele.
Hakuna mtu wa kumwajibisha mbunge zaidi ya wananchi walio mchagua tu,dc akilikoroga aliye mchagua anamtupa tuHasira hasara.
Upo sahihi mkuu na huo ndio uawala bora tunategemea kuona kutoka kwa viongozi wetuKamchana live huo ndiyo ukweli, lazima tufike mahali tuachane na kasumba za kuendekeza Majungu na itikadi za ccm kwenye shida zinazowahusu wananchi wote.
Ccm ni majanga sanama ccm lazima yapewe za uso live ndio yataelewa jinsi ya kushirikiana kujenga taifa.
swissme
Nashindwa kujua hawa wakuu wa wilaya wanakuwa wanatumia busara zipi hadi kupelekea kutaka kumdharau mbunge wa sehemu husika wakati huyo mbunge ndiye chaguo la wananchi wa hapoSafi sana Mchungaji Msigwa. Siku nyingine akileta tena ungese ungese mchape kibao. Hilo kuu la wilaya jinga kabisa
Kwani kupanic ni dhambi?Ni kweli.
Ila naona alishindwa kudhibiti hasira zake mpaka ameshindwa kutoa maneno kwa ufasaha. Huyu kasesera anaonekana ni mtu mwenye dharau au nyodo tuseme kwahiyo mtu unapaswa uwe technical kidogo kumvaa. Hapo mbunge kaonekana kama amepanick au analalamika, jambo ambalo DC kalichukulia poa tu.
Inasikitisha sana kwa kiongozi kuwa na mambo ya ajabu kama hayaHuyo mkuu wa wilaya kabla ya kuteuliwa alikuwa ni mtu mngwana sana tokea akiwa shuleni Azania hadi akiwa kwenye harakati zingine nimeshangaa kumwona kaaza ukorofi kwa kuwaiga akina Polepole ambao ni Watumishi wa Benard Membe adui namba moja wa Lowasa.