Varangati: Mbunge Msigwa na DC Kasesela nusura ngumi zichapwe

barafu

JF-Expert Member
Apr 28, 2013
6,726
32,820
image.jpeg


image.jpeg


image.jpeg




Kumetokea mabishano makali sana kati ya Mbunge Msigwa na DC Kasesera eneo la Iringa Mjini baada kuwa wamewatembelea wahanga wa nyumba zilizoezuliwa na mvua kubwa na kusababisha baadhi ya watu ktk Tarafa ya Nduli

Vurumai hizo zilizotokea baada ya Msigwa kukasirishwa na kitengo cha DC kutaka kumuengua ili asionekane anatoa msaada kwa watu wa jimbo lake bali DC ndio ionekane anajali wananchi.Shutuma zilienda mbali baada ya Msigwa kumueleza DC kuwa anajuwa anamhujumu na amekuwa anapanga mikakati ya siri ya kumfanyia hujuma ili aonekane hafanyi kazi jimboni kwake.

Juhudi hizo zimefanyika week iliyopita ambapo DC kwa kushirikiana na Humphley Polepole waliandaa "mdahalo" na wanafunzi wa vyu vikuu mkoani Iringa na kuanza kumsema vibaya Mbunge Msigwa,katika mdahalo huo Polepole amerekodiwa akisema Iringa awalikosea sana kumchagua Msigwa sbb alikuwa anamuunga mkono "fisadi" Lowassa

Wakati DC Kasesera alimshutumu Mb Msigwa kutokwenda Tarafa ya Pawaga kusaidia wahanga wa mafuriko na Msigwa akamjibu kuwa aanze kumwambia Lukuvi kwanini hajaenda maana Tarafa ya Pawaga ipo ndani ya Jimbo la Isimani,na hata yeye akienda sio lazima DC ajue,kama ambavyo yeye anaenda na kupiga picha na kurusha Facebook akimbeba mpiga picha ambaye haitaji msaada wa kubebwa.

Vurugu hizo ziliamuliwa na diwani na Meya wa Mji. Mwishoni Msigwa akamwambia DC awaite polisi wamuweke ndani maana katika viako vya CCM DC Kasesera amekuwa akisema lazima amuweke ndani Msigwa kumtia adabu
 
Duh no wonder wananchi hawakuingiza madarakani hawa viongozi wa manyumbu, yani mbunge na mchungaji anakosa busara namna hii,big up kasesela kwa kuonyesha busara nidham na umakini wa hali ya juu , thank god ur reputation is intact cause u didn't stoop so low to that nyumbus level.
 
''Mimi nimechaguliwa na wananchi, wewe umeletwa na Rais''-Msigwa.

''Manispaa niya kwetu, huyu ameletwa tu-Msigwa

''Leo ninakutolea uvivu na waandishi wa habari wanachukua-Msigwa.

''Kila kwenye kikao cha CCM unanisema, acha mambo ya kishamba shamba-Msigwa.

''Sasa hivi nitapambana na wewe serially''-Msigwa

''Maafa sio ya kwako, maafa niya Watanzania wote''-Msigwa

''Si una power ya kuniweka ndani, kaniweke basi ndani''-Msigwa

''Sina shida ya kukuweka ndani''-Kasesera

''Sikiliza, mimi ninakuheshimu sana ndio maana sina shida ya kubishana na wewe''-Kasesera.

Politicians and politics at its best!

Wanasiasa wetu wanataka kutwangana ngumi, kisa nani anakuwa mbele mbele katika kutoa misaada ya wahanga wa mvua ya el nino!
 
Ha ha ha. Cheki Msigwa anavyovua koti lake. Eti "...everywhere, in Facebook sijui wapi...I use strategies..." Huyu mchungaji aache kupanic. Mwisho wa siku yeye ndio ataonekana kichaa. Kasesera kamseti na yeye kaingia kichwa kichwa.
 
H
Ha ha ha. Cheki Msigwa anavyovua koti lake. Eti "...everywhere, in Facebook sijui wapi...I use strategies..." Huyu mchungaji aache kupanic. Mwisho wa siku yeye ndio ataonekana kichaa. Kasesera kamseti na yeye kaingia kichwa kichwa.
hakuna cha kichwa kichwa hapo Mkuu wa wilaya alimkosea Mbunge kwa kutaka kumdhalilisha ni vyema wakuu wa wilaya wakawaheshimu wabunge pasipo kuweka itikadi za Vyama vyao mbele.
 
H

hakuna cha kichwa kichwa hapo Mkuu wa wilaya alimkosea Mbunge kwa kutaka kumdhalilisha ni vyema wakuu wa wilaya wakawaheshimu wabunge pasipo kuweka itikadi za Vyama vyao mbele.
Hasira hasara.
 
''Mimi nimechaguliwa na wananchi, wewe umeletwa na Rais''-Msigwa.

''Manispaa niya kwetu, huyu ameletwa tu-Msigwa

''Leo ninakutolea uvivu na waandishi wa habari wanachukua-Msigwa.

''Kila kwenye kikao cha CCM unanisema, acha mambo ya kishamba shamba-Msigwa.

''Sasa hivi nitapambana na wewe serially''-Msigwa

''Maafa sio ya kwako, maafa niya Watanzania wote''-Msigwa
Kamchana live huo ndiyo ukweli, lazima tufike mahali tuachane na kasumba za kuendekeza Majungu na itikadi za ccm kwenye shida zinazowahusu wananchi wote.
 
Mb

Mbunge kachoka na hujuma lazima aseme Ukweli.
Ni kweli.
Ila naona alishindwa kudhibiti hasira zake mpaka ameshindwa kutoa maneno kwa ufasaha. Huyu kasesera anaonekana ni mtu mwenye dharau au nyodo tuseme kwahiyo mtu unapaswa uwe technical kidogo kumvaa. Hapo mbunge kaonekana kama amepanick au analalamika, jambo ambalo DC kalichukulia poa tu.
 
Nidhamu au ndo amekuwa mdogo kama piritoni? Anakuwa mjanja Msigwa asipokuwepo, lakini amenywea walipokutana. By the way wakuu wa wilaya sio chaguo la wananchi, yaani ilikuwa riziwani akipeleka jina tu kwa mshua kesho unapewa cheo
Huyo mkuu wa wilaya kabla ya kuteuliwa alikuwa ni mtu mngwana sana tokea akiwa shuleni Azania hadi akiwa kwenye harakati zingine nimeshangaa kumwona kaaza ukorofi kwa kuwaiga akina Polepole ambao ni Watumishi wa Benard Membe adui namba moja wa Lowasa.
 
Back
Top Bottom