Halafu mkuu wa wilaya has nothing to loose msigwa has so many to loose kwenye hiyo saga ya msigwa na huyo mkuu wa wilaya kwa hiyo lazima ajitetee kumbuka msigwa yuko mbele ya waajiri wake akizubaa ataonekana hashugulikii changamoto zilizoko jimboni kwake sasa kama mwenyewe anajituma halafu mtu anataka kumfitini kwa hila na ghiliba kwa nini asitetee kibarua chake.Kweli huo ni mtazamo wako,uko huru na "sahihi",lkn ungewahi kuonja changamoto za kuwa mwanasiasa wa Upinzani ndani ya nchi ambacho chama dola ndio mpinzani wako mkuu...hilo jambo alilofanya Msigwa ni kawaida sana...Too much obidience is stupidity!!Wakati mwingine ni kujivika "uchizi" tu kidogo
Anayetetea ugali si dc ni msigwa kumbuka dc ni discretion ya rais.Huyo mkuu wa wilaya anaweza akabebana na waandishi wa habari. Lakini rais akaona hajajikomba kwake akampiga chini akachagua washikaji zake.It works other way round kwa mbunge.Muacheni DC atetee Ugali jamani.
unajua hata mimi nilitaka kuuliza hiyo misaada kwani imetoka wapi ? ndio wagombee kuigawambna ndo vizuri km wanagombea kutoa misaada me naunga mkono waendelee tu huyu akileta mabati 20 mwingne aonyeshe umwamba analeta mabati 50 hapo ndo uanaume utaonekana araf sisi wananchi tutaamua nani mshindi nani anatujali
BUT MSHINDI LAZIMA APATIKANE NI YULE ALOLETA VITU VINGI so endeleeni kugombana tu WAKUU
lazima aweke maslahi ya chama chake kilichomuweka kama msigwa alivyoteuliwa na chama chake kugombea ubungeH
hakuna cha kichwa kichwa hapo Mkuu wa wilaya alimkosea Mbunge kwa kutaka kumdhalilisha ni vyema wakuu wa wilaya wakawaheshimu wabunge pasipo kuweka itikadi za Vyama vyao mbele.
Ni kweli.
Ila naona alishindwa kudhibiti hasira zake mpaka ameshindwa kutoa maneno kwa ufasaha. Huyu kasesera anaonekana ni mtu mwenye dharau au nyodo tuseme kwahiyo mtu unapaswa uwe technical kidogo kumvaa. Hapo mbunge kaonekana kama amepanick au analalamika, jambo ambalo DC kalichukulia poa tu
View attachment 324104
View attachment 324105
View attachment 324106
Kumetokea mabishano makali sana kati ya Mbunge Msigwa na DC Kasesera eneo la Iringa Mjini baada kuwa wamewatembelea wahanga wa nyumba zilizoezuliwa na mvua kubwa na kusababisha baadhi ya watu ktk Tarafa ya Nduli
Vurumai hizo zilizotokea baada ya Msigwa kukasirishwa na kitengo cha DC kutaka kumuengua ili asionekane anatoa msaada kwa watu wa jimbo lake bali DC ndio ionekane anajali wananchi.Shutuma zilienda mbali baada ya Msigwa kumueleza DC kuwa anajuwa anamhujumu na amekuwa anapanga mikakati ya siri ya kumfanyia hujuma ili aonekane hafanyi kazi jimboni kwake.
Juhudi hizo zimefanyika week iliyopita ambapo DC kwa kushirikiana na Humphley Polepole waliandaa "mdahalo" na wanafunzi wa vyu vikuu mkoani Iringa na kuanza kumsema vibaya Mbunge Msigwa,katika mdahalo huo Polepole amerekodiwa akisema Iringa awalikosea sana kumchagua Msigwa sbb alikuwa anamuunga mkono "fisadi" Lowassa
Wakati DC Kasesera alimshutumu Mb Msigwa kutokwenda Tarafa ya Pawaga kusaidia wahanga wa mafuriko na Msigwa akamjibu kuwa aanze kumwambia Lukuvi kwanini hajaenda maana Tarafa ya Pawaga ipo ndani ya Jimbo la Isimani,na hata yeye akienda sio lazima DC ajue,kama ambavyo yeye anaenda na kupiga picha na kurusha Facebook akimbeba mpiga picha ambaye haitaji msaada wa kubebwa.
Vurugu hizo ziliamuliwa na diwani na Meya wa Mji. Mwishoni Msigwa akamwambia DC awaite polisi wamuweke ndani maana katika viako vya CCM DC Kasesera amekuwa akisema lazima amuweke ndani Msigwa kumtia adabu
Hivi ukiwa na ISIS, kuna kutumia diplomasia hapo?Yaani Msigwa haelewi maana ya diplomasia? Huyu si ndio waziri kivuli wa kimataifa. Sasa kama Ukawa wangeshinda na yeye kuchukua nafasi ya Mahiga na hiyo mihasira si Umoja wa Mataifa pangekuwa hapatoshi?
Kama hujui Geography ya Iringa ni vyema usiseme chochote!Duh no wonder wananchi hawakuingiza madarakani hawa viongozi wa manyumbu, yani mbunge na mchungaji anakosa busara namna hii,big up kasesela kwa kuonyesha busara nidham na umakini wa hali ya juu , thank god ur reputation is intact cause u didn't stoop so low to that nyumbus level.
Bwana minyoo hoja dhumuni lake ni maendeleo sio kutafuta mshindi....tuweke akiba ya maneno japo mpumbavu na mwenye hekima tumewajuwa.H
hasara hakuna hapo Mkuu wa wilaya kaambiwa Ukweli na yeye kakubali kasema yaishe basi waendelee na kazi.
Ndiyo maana wananchi wengi kupitia tume ya Warioba walitoa maoni kupinga hawa wakuu wa mikoa na wilaya, hawana umuhimu zaidi ya majungu na fitina za watawala.Mkuu wa wilaya alizidi kuendekeza majungu, fitna na sifa zisizo na maana, mfano ile ya kumbeba Mwandishi mzima na kupiga naye picha ilikuwa na tija gani? Kupiga picha na misaada huku ukimtenga Mbunge inamsaidia nini? Tufike mahala hizi kasumba ziishe kama kweli ccm wamedhamilia kubadilika na kuijenga Nchi hii, Magufuli ni wakati wa kuangalia upya hiki cheo cha ukuu wa wilaya ikibidi atumbue Majipu wakuu wa wilaya woote wanaodharau upinzani.