Uwt- ccm ficheni upumbavu wenu msifiche hekima zenu

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,956
22,150
UWT zibeni mpasuko wenu, malumbano hayana tija






LISEMWALO lipo na kama halipo linakuja. Hivi karibuni, Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) umekuwa gumzo kutokana na madai ya kuwepo mgogoro unaohusisha viongozi wa juu.

Yapo mengi yanayosemwa juu ya viongozi hao ambao ni Mwenyekiti wa umoja huo, Sophia Simba na Katibu Mkuu wake, Husna Mwilima.

Inawezekana yanayosemwa ama yasiwepo au yakaongezwa chumvi. Lakini hilo haliondoi ukweli kwamba hali ni tete katika umoja huo.

Mimi siyo hakimu wa kubainisha hali ilivyo na kutoa hukumu. Lakini hakuna ubishi kwamba mazingira yanaonesha kwamba mpasuko ndani ya umoja huo upo.

Kwa mfano, kitendo cha baadhi ya viongozi wa umoja huo juzi kutoa taarifa ya kukanusha kuwepo mgogoro, bila kumhusisha Katibu Mkuu, Mwilima anayetajwa kuwa sehemu ya mgogoro huo wakati alikuwepo ofisini, ni mazingira tosha kuonesha kwamba lipo tatizo.

Inafahamika wazi kwamba UWT ni umoja wa kichama. Lakini katika kufuatilia historia yake, ni umoja ambao unahitaji kuwa na nguvu kubwa kwa kuzingatia kwamba unawakilisha chama tawala chenye sera za kitaifa katika kuwakomboa wanawake wote.

Nanukuu hotuba ya Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete katika ufunguzi wa mkutano mkuu maalumu wa UWT uliofanyika Dodoma, Julai 27, 2007: “UWT ni chombo cha ukombozi wa mwanamke wa Tanzania na taifa kwa jumla.

Ni chombo cha kupigania haki na maendeleo ya wanawake na jamii kwa ujumla." Chombo hiki historia yake inatajwa tangu enzi za kupigania uhuru na ukombozi wa nchi kutokana na wanawake kusimama kidete, wakiwa bega kwa bega na wanaume kupambana na ukoloni na utawala wa kisultani.


Wapo wanawake wengi waasisi wa UWT ambao sifa zao tunaendelea kuzisikia hadi leo. Kwa kuzingatia hilo, Rais Kikwete katika mkutano huo aliendelea kusema, ‘Jukumu la msingi la UWT kwa sasa ni kuendelea kutumia uhalali huo wa kihistoria na mtandao mkubwa ilionao nchi nzima kuendelea kupigania haki, usawa na maendeleo ya kiuchumi na kijamii ya wanawake wa Tanzania na jamii zao wanamoishi.

Siyo nia yangu kuainisha historia ndefu ya UWT, mafanikio au changamoto zinazoukabili umoja huo kwani wahusika, hususan viongozi, wanafahamu ukweli.

Hiki ni kioo pia cha wanawake wa nchi nzima japokuwa hata vyama vingine vya siasa vina vyombo vyao.

Ndiyo maana tunaona Mwenyekiti wake, Simba, ni kiongozi wa kitaifa tena katika nafasi nyeti ya utawala bora.


Kwa mantiki hii, ina maana inapotokea aina yoyote ya mpasuko, mgogoro au kuaibishana baina ya wanachama, suala hilo haliwezi kuishia ngazi ya umoja huo, bali linavuka mipaka hadi serikalini.


Kwa kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utawala bora), Simba ndiye mwenyekiti na ambaye amekuwa akihusishwa katika mgogoro huo, ni vyema atumie busara na nguvu ya wadhifa alio nao serikalini kumaliza hali hiyo.

Pamoja na kwamba migogoro siyo jambo geni katika taasisi au mkusanyiko wowote wa watu, lakini ni vyema UWT isikubali kuchafua sifa yake.

Umoja huo uepuke kutoa nafasi kwa jamii inayoamini katika mfumo dume, kuibeza UWT kwa kuhalalisha dhana potofu kwamba wanawake hawapendani na wanaoneana wivu.

Hatua zichukuliwe haraka kukomesha hali hii kwani mwanamke wa kijijini hana manufaa yoyote na malumbano haya.


Vikao vibaki kuwa vya kujadili masuala yenye tija ya kumwendeleza mwanamke na si vya kusutana na kupashana.
 
UWT=CCM=complications!

wanayoongea hawa wanawake mtaweza kuyajadili humu! wakati Sofia Simba anamwaga upupu wake wanampigia makofi, JF mnasema ajiuzulu

mtawaweza hawa!

Kabali ya mikono inakunyima pumzi, kabali ya between legs inakunyima pumzi, akili, uhuru, utu...name it

Tuwaache hawa jamani
 
UWT zibeni mpasuko wenu, malumbano hayana tija






LISEMWALO lipo na kama halipo linakuja. Hivi karibuni, Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) umekuwa gumzo kutokana na madai ya kuwepo mgogoro unaohusisha viongozi wa juu.





Yapo mengi yanayosemwa juu ya viongozi hao ambao ni Mwenyekiti wa umoja huo, Sophia Simba na Katibu Mkuu wake, Husna Mwilima.

Inawezekana yanayosemwa ama yasiwepo au yakaongezwa chumvi. Lakini hilo haliondoi ukweli kwamba hali ni tete katika umoja huo.

Mimi siyo hakimu wa kubainisha hali ilivyo na kutoa hukumu. Lakini hakuna ubishi kwamba mazingira yanaonesha kwamba mpasuko ndani ya umoja huo upo.

Kwa mfano, kitendo cha baadhi ya viongozi wa umoja huo juzi kutoa taarifa ya kukanusha kuwepo mgogoro, bila kumhusisha Katibu Mkuu, Mwilima anayetajwa kuwa sehemu ya mgogoro huo wakati alikuwepo ofisini, ni mazingira tosha kuonesha kwamba lipo tatizo.

Inafahamika wazi kwamba UWT ni umoja wa kichama. Lakini katika kufuatilia historia yake, ni umoja ambao unahitaji kuwa na nguvu kubwa kwa kuzingatia kwamba unawakilisha chama tawala chenye sera za kitaifa katika kuwakomboa wanawake wote.

Nanukuu hotuba ya Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete katika ufunguzi wa mkutano mkuu maalumu wa UWT uliofanyika Dodoma, Julai 27, 2007: “UWT ni chombo cha ukombozi wa mwanamke wa Tanzania na taifa kwa jumla.

Ni chombo cha kupigania haki na maendeleo ya wanawake na jamii kwa ujumla." Chombo hiki historia yake inatajwa tangu enzi za kupigania uhuru na ukombozi wa nchi kutokana na wanawake kusimama kidete, wakiwa bega kwa bega na wanaume kupambana na ukoloni na utawala wa kisultani.


Wapo wanawake wengi waasisi wa UWT ambao sifa zao tunaendelea kuzisikia hadi leo. Kwa kuzingatia hilo, Rais Kikwete katika mkutano huo aliendelea kusema, ‘Jukumu la msingi la UWT kwa sasa ni kuendelea kutumia uhalali huo wa kihistoria na mtandao mkubwa ilionao nchi nzima kuendelea kupigania haki, usawa na maendeleo ya kiuchumi na kijamii ya wanawake wa Tanzania na jamii zao wanamoishi.

Siyo nia yangu kuainisha historia ndefu ya UWT, mafanikio au changamoto zinazoukabili umoja huo kwani wahusika, hususan viongozi, wanafahamu ukweli.

Hiki ni kioo pia cha wanawake wa nchi nzima japokuwa hata vyama vingine vya siasa vina vyombo vyao.

Ndiyo maana tunaona Mwenyekiti wake, Simba, ni kiongozi wa kitaifa tena katika nafasi nyeti ya utawala bora.


Kwa mantiki hii, ina maana inapotokea aina yoyote ya mpasuko, mgogoro au kuaibishana baina ya wanachama, suala hilo haliwezi kuishia ngazi ya umoja huo, bali linavuka mipaka hadi serikalini.

Kwa kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utawala bora), Simba ndiye mwenyekiti na ambaye amekuwa akihusishwa katika mgogoro huo, ni vyema atumie busara na nguvu ya wadhifa alio nao serikalini kumaliza hali hiyo.

Pamoja na kwamba migogoro siyo jambo geni katika taasisi au mkusanyiko wowote wa watu, lakini ni vyema UWT isikubali kuchafua sifa yake.

Umoja huo uepuke kutoa nafasi kwa jamii inayoamini katika mfumo dume, kuibeza UWT kwa kuhalalisha dhana potofu kwamba wanawake hawapendani na wanaoneana wivu.

Hatua zichukuliwe haraka kukomesha hali hii kwani mwanamke wa kijijini hana manufaa yoyote na malumbano haya.


Vikao vibaki kuwa vya kujadili masuala yenye tija ya kumwendeleza mwanamke na si vya kusutana na kupashana.

Mkuu


hivi naweza kupindisha hii ishuu, hivi-
  • Apolitical ?
  • Social class nightmare?
  • A socialeconomic organ at the helm of power mongering?
What has CCM got to do with it? hekima au upumbavu?
Wanawake siku zote kusutana tu na kupashana-wataelewana "frienemies" hawa.
Apolitical.
 
kwa style hii ya hapo juu nahisi kizunguzungu cha ajabu watu kama wakina pdidy bado wanangangania kadi za uvccm...ccm
kazi kweli kweli
 
Kama kiongozi wake ni Sophia Simba unategemea nini zaidi ya hayo yanayojiri? Je unadhani SS anabusara yakuweza kusuluhisha migogoro ndani ya UWT zaidi ya kuikoleza?
 
Kama kiongozi wake ni Sophia Simba

That is fact. Mkuu ulichosema ni ukweli mtupu, huwezi kutegemea kingine zaidi ya mipasho kutoka kwa Sophia Simba. Anastahili atunikiwe Phd ya kusasambua kwenye kitchen party.
 
Nani mwenye habari zozote? Huyu mama alifuata ule ushauri wa Mzee Malechela, au aliamua kuukalia?
 
Hapo ngoma kwisha ni kuwatimuwa wote wawili,kwani kwa jinsi nijuavyo ni watu wa mipasho sana watu hawa.
 
Back
Top Bottom