Hekima Ufunuo
JF-Expert Member
- May 28, 2009
- 220
- 11
Inapotokea serikali iliyopo madarakani kuvunja katiba ya nchi au mhimili mmojawapo wa nchi kuvunja katiba ni hatua gani zinachukuliwa na ni nani anayechukua hizo hatua? Nahitaji elimu hii kwa sababu kuna matukio ambayo mimi nayaona kama uvunjaji wa katiba ya nchi. Natoa mifana ili muone ni nini mtizamo wangu.
1. Katiba ya Zanzibar inategea sana katiba ya muungano, ili kuwa na uhalali wa kuibadilisha hasa vipengele ambavyo vinaihusu pia katiba ya muungano ni lazima kwanza urekebishe katiba ya muungano ndiyo ubadili katiba ya zanzibar. Kilichotokea mwaka juzi ni wazi kuwa kinakinzana na katiba ya Muungano. Hili si ni uvunjaji wa katiba ya muungano?
2. Mwaka jana Chadema wamewafukuza uanachama madiwani wa Arusha, huku nyuma Waziri wa Tamisemi akasema waendelee na udiwani wao, ili hali wamepoteza sifa kikatiba. Je huu si uvunjaji wa katiba?
3. Mwaka jana NCCR-Mageuzi wamemfukuza mbunge wao wa kigoma kusini uanachama kwa yale wanayoyajua wao. leo bunge linasema linamtambua mpaka mahakama itakapoamua. Lakini katika kesi ya mbunge huyo, hakuna mahali popote ambapo bunge limetajwa. Je huo siyo uvunjaji wa katiba.
4. Juzi karibu na mwisho wa mwaka CUF wamemfukuza uanachama mbunge wao wa wawi, lugha ya mhimili huu wa kutunga sheria ni ile ile. Kwenye matukio haya katiba inasimamiwa na nani?
Nipeni elimu jamani.
1. Katiba ya Zanzibar inategea sana katiba ya muungano, ili kuwa na uhalali wa kuibadilisha hasa vipengele ambavyo vinaihusu pia katiba ya muungano ni lazima kwanza urekebishe katiba ya muungano ndiyo ubadili katiba ya zanzibar. Kilichotokea mwaka juzi ni wazi kuwa kinakinzana na katiba ya Muungano. Hili si ni uvunjaji wa katiba ya muungano?
2. Mwaka jana Chadema wamewafukuza uanachama madiwani wa Arusha, huku nyuma Waziri wa Tamisemi akasema waendelee na udiwani wao, ili hali wamepoteza sifa kikatiba. Je huu si uvunjaji wa katiba?
3. Mwaka jana NCCR-Mageuzi wamemfukuza mbunge wao wa kigoma kusini uanachama kwa yale wanayoyajua wao. leo bunge linasema linamtambua mpaka mahakama itakapoamua. Lakini katika kesi ya mbunge huyo, hakuna mahali popote ambapo bunge limetajwa. Je huo siyo uvunjaji wa katiba.
4. Juzi karibu na mwisho wa mwaka CUF wamemfukuza uanachama mbunge wao wa wawi, lugha ya mhimili huu wa kutunga sheria ni ile ile. Kwenye matukio haya katiba inasimamiwa na nani?
Nipeni elimu jamani.