nickname
JF-Expert Member
- Dec 20, 2009
- 544
- 147
UVCCM-Mara waitaka serikali itangaze kuwa DOWANS ni kampuni hewa, wahamashishana kama vijana waamke na kuwashauri viongozi wa CCM waibane serikali iwajali wananchi wake na wasitangaze takwimu za uongo za maendeleo wakati ukweli unaonekana.Walalamikia CCM kuogopa midahalo ya kitaifa na pia wawakilishi wa CCM na jumuiya zake kukosekana kwenye mdahalo wa katiba mpya uliofanyika UDSM.Pia UVCCM waitaka serikali ya CCM itoe kweli ajira kwa vijana kupitia kilimo cha umwagiliaji.
Tafsiri yangu: Hili ni jambo jema liilooneshwa na UVCCM mkoani Mara.Nimegundua kitu kuwa watu wa mkoa wa Mara ni wana mabadiliko na wasio waoga kusema ukweli,safi sana hii inatakiwa kuigwa na viongozi wa UVCCM wa mikoa mingine pamoja na wakitaifa wakiwemo Beno na Riz1
UVCCM WAITAKA CCM KUTOA TAMKO
Wakati huo huo, wajumbe wa Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Mkoa wa Mara, wamekitaka chama hicho kuitaka Serikali kutamka kuwa Dowans ni kampuni hewa ambayo hastahili kulipwa kiasi chochote cha fedha za walipakodi wa Tanzania.
Wamesema kukaa kimya kwa CCM wakati serikali yake ikiendelea na mchakato wa kuliipa Dowans fedha hizo kutatafsiriwa kuwa kinahusika moja kwa moja na njama hizo za wizi wa fedha za umma.
Wakizungumza katika mkutano ulioitishwa na Mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Mara kupitia UVCCM, Esther Bulaya, kwa ajili ya kuwashukuru, wajumbe hao walisema kama Bunge lilibaini kuwa kampuni ya kufua umeme ya Richmond ni kampuni hewa, iweje leo Dowans iliyorithi mikoba yake ikawa ni kampuni halali ya kulipwa fedha hizo.
"Tumefika mahali kama vijana wa CCM kukitaka chama chetu kitamke kwa kuitaka serikali kusitisha malipo kwa Dowans. Dowans leo inapataje uhalali wa kulipwa mabilioni ya Watanzania wakati Richmond tulielezwa ni kampuni hewa. Hivi CCM inataka kuwaambia nini Watanzania ambao wengi hawawezi kuwa na uwezo wa kupata mlo wa siku?" alihoji Fidelis Manyerere, mjumbe wa Baraza Kuu wa umoja huo mkoa wa Mara na kushangiliwa.
Manyerere alisema ili kulinda heshima ya CCM ambayo imejengwa kwa miaka mingi, lazima viongozi wakuu wakaishauri serikali kuacha kuilipa Dowans na kutahadharisha kuwa ikiwa fedha hizo zitalipwa kwa Dowans chama hicho kitakuwa katika wakati mgumu hasa kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2015.
Mjumbe huyo pia alishauri CCM kuacha kutoa taarifa zinazopingana kwa wananchi. Mjumbe mwingine Marwa Mirumbe, pamoja na kueleza kukerwa na mambo mbalimbali yanayoendelea likiwemo la malipo kwa Dowans, alimuomba mbunge huyo kutumia Bunge kuomba kuharakishwa kwa ujenzi wa barabara ya lami kutoka Makutano-Musoma hadi Mto wa Mbu mkoani Arusha hatua ambayo pia alisema itachangia ukuaji wa uchumi wa maeneo hayo.
Mjumbe mwingine kutoka Wilaya ya Tarime, Denis Zacharia, akizungumzia suala la katiba mpya, alisema inasikitisha kwa kiasi kikubwa kwa chama hicho kutozungumzia suala hilo wakati wakitambua wazi hoja hiyo ni ya Taifa zima kwa sasa.
"Juzi kulikuwa na mdahalo kuhusu katiba pale Chuo Kikuu ambao ulirushwa hewani na ITV, lakini ilinisikitisha kuona hakuna hata mwakilishi wa chama wala jumuiya zake. Hivi kwanini tunapenda kufanyia mzaha kiasi hiki jambo la kitaifa, tunakwepa kujitokeza nasi tuzungumze mnadhani wananchi wanatuelewa vipi wakati wote tunajua matizo mengi ya nchi yako ndani ya katiba?"alihoji na kuongeza:
"CCM tunaanza kuogopa makongamano ya kitaifa, tunaogopa mijadala, jamani tufike mahali tubadilike ili sisi pia tushiriki mijadala ya kitaifa na kutoa michango yetu kuhusu mambo muhimu ya nchi, tusiwaachie wapinzani kazi hizi," alisema Zacharia.
Alisema woga huo umesababisha vijana wa CCM kukosa uthubutu hata wa kuhutubia ama kuelezea mafanikio ya serikali katika mikusanyiko ya watu, jambo ambalo alisema ni hatari kwa chama.
Kwa upande wake, mwenyekiti wa UV-CCM mkoa wa Mara, Marwa Mathayo, alisema wakati umefika kwa vijana kujipanga vizuri kwa kuwashauri viongozi wa CCM kuibana serikali yake kutekeleza mambo mbalimbali yanawakabili wananchi ili kuepuka kuhojiwa wakati wa chaguzi.
Mathayo alisema jambo hilo limekuwa likisababisha kushindwa na wapinzani katika kata, majimbo hata kupunguza kura za rais.
"Vijana wanahoji tunataka ajira, na viongozi wa serikali wanatamba kuwa wamezalisha ajira ambazo hazionekani. Wasomi wanataka maabara, mnasema hakuna fedha huku serikali ikitumia mamilioni ya fedha kununulia Ma-VX," alisema na kuongeza:
"Hivi chama kimeshindwa kuibana serikali yake sababu sasa tumeshaona baadhi ya viongozi wa serikalini ambao wanaendesha hujuma katika kuhakikisha CCM inaondoka madarakani na CCM yenyewe inakaa kimya."
Mjumbe mwingine, Rudia Mareza, alisema serikali ya CCM ina kila sababu ya kuhakikisha inatengeneza mazingira mazuri ya ajira kwa vijana kwa kujiajiri wenyewe baada ya kuhitimu masomo ya sekondari na vyuo vikuu badala ya kutegemea ajira toka serikalini.
Alisema sehemu kubwa ambayo inaweza kutoa ajira kubwa kwa vijana ni kilimo kwa kuwawezesha vijana kushiriki kikamilifu katika sekta hiyo kwa kupewa nyenzo ambazo zitakazotumika katika kuendesha kilimo cha umwagiliaji badala ya kutegemea mvua, jambo ambalo litachangia vijana kuzalisha wakiwa vijijini.
Source : Nipashe
Tafsiri yangu: Hili ni jambo jema liilooneshwa na UVCCM mkoani Mara.Nimegundua kitu kuwa watu wa mkoa wa Mara ni wana mabadiliko na wasio waoga kusema ukweli,safi sana hii inatakiwa kuigwa na viongozi wa UVCCM wa mikoa mingine pamoja na wakitaifa wakiwemo Beno na Riz1
UVCCM WAITAKA CCM KUTOA TAMKO
Wakati huo huo, wajumbe wa Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Mkoa wa Mara, wamekitaka chama hicho kuitaka Serikali kutamka kuwa Dowans ni kampuni hewa ambayo hastahili kulipwa kiasi chochote cha fedha za walipakodi wa Tanzania.
Wamesema kukaa kimya kwa CCM wakati serikali yake ikiendelea na mchakato wa kuliipa Dowans fedha hizo kutatafsiriwa kuwa kinahusika moja kwa moja na njama hizo za wizi wa fedha za umma.
Wakizungumza katika mkutano ulioitishwa na Mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Mara kupitia UVCCM, Esther Bulaya, kwa ajili ya kuwashukuru, wajumbe hao walisema kama Bunge lilibaini kuwa kampuni ya kufua umeme ya Richmond ni kampuni hewa, iweje leo Dowans iliyorithi mikoba yake ikawa ni kampuni halali ya kulipwa fedha hizo.
"Tumefika mahali kama vijana wa CCM kukitaka chama chetu kitamke kwa kuitaka serikali kusitisha malipo kwa Dowans. Dowans leo inapataje uhalali wa kulipwa mabilioni ya Watanzania wakati Richmond tulielezwa ni kampuni hewa. Hivi CCM inataka kuwaambia nini Watanzania ambao wengi hawawezi kuwa na uwezo wa kupata mlo wa siku?" alihoji Fidelis Manyerere, mjumbe wa Baraza Kuu wa umoja huo mkoa wa Mara na kushangiliwa.
Manyerere alisema ili kulinda heshima ya CCM ambayo imejengwa kwa miaka mingi, lazima viongozi wakuu wakaishauri serikali kuacha kuilipa Dowans na kutahadharisha kuwa ikiwa fedha hizo zitalipwa kwa Dowans chama hicho kitakuwa katika wakati mgumu hasa kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2015.
Mjumbe huyo pia alishauri CCM kuacha kutoa taarifa zinazopingana kwa wananchi. Mjumbe mwingine Marwa Mirumbe, pamoja na kueleza kukerwa na mambo mbalimbali yanayoendelea likiwemo la malipo kwa Dowans, alimuomba mbunge huyo kutumia Bunge kuomba kuharakishwa kwa ujenzi wa barabara ya lami kutoka Makutano-Musoma hadi Mto wa Mbu mkoani Arusha hatua ambayo pia alisema itachangia ukuaji wa uchumi wa maeneo hayo.
Mjumbe mwingine kutoka Wilaya ya Tarime, Denis Zacharia, akizungumzia suala la katiba mpya, alisema inasikitisha kwa kiasi kikubwa kwa chama hicho kutozungumzia suala hilo wakati wakitambua wazi hoja hiyo ni ya Taifa zima kwa sasa.
"Juzi kulikuwa na mdahalo kuhusu katiba pale Chuo Kikuu ambao ulirushwa hewani na ITV, lakini ilinisikitisha kuona hakuna hata mwakilishi wa chama wala jumuiya zake. Hivi kwanini tunapenda kufanyia mzaha kiasi hiki jambo la kitaifa, tunakwepa kujitokeza nasi tuzungumze mnadhani wananchi wanatuelewa vipi wakati wote tunajua matizo mengi ya nchi yako ndani ya katiba?"alihoji na kuongeza:
"CCM tunaanza kuogopa makongamano ya kitaifa, tunaogopa mijadala, jamani tufike mahali tubadilike ili sisi pia tushiriki mijadala ya kitaifa na kutoa michango yetu kuhusu mambo muhimu ya nchi, tusiwaachie wapinzani kazi hizi," alisema Zacharia.
Alisema woga huo umesababisha vijana wa CCM kukosa uthubutu hata wa kuhutubia ama kuelezea mafanikio ya serikali katika mikusanyiko ya watu, jambo ambalo alisema ni hatari kwa chama.
Kwa upande wake, mwenyekiti wa UV-CCM mkoa wa Mara, Marwa Mathayo, alisema wakati umefika kwa vijana kujipanga vizuri kwa kuwashauri viongozi wa CCM kuibana serikali yake kutekeleza mambo mbalimbali yanawakabili wananchi ili kuepuka kuhojiwa wakati wa chaguzi.
Mathayo alisema jambo hilo limekuwa likisababisha kushindwa na wapinzani katika kata, majimbo hata kupunguza kura za rais.
"Vijana wanahoji tunataka ajira, na viongozi wa serikali wanatamba kuwa wamezalisha ajira ambazo hazionekani. Wasomi wanataka maabara, mnasema hakuna fedha huku serikali ikitumia mamilioni ya fedha kununulia Ma-VX," alisema na kuongeza:
"Hivi chama kimeshindwa kuibana serikali yake sababu sasa tumeshaona baadhi ya viongozi wa serikalini ambao wanaendesha hujuma katika kuhakikisha CCM inaondoka madarakani na CCM yenyewe inakaa kimya."
Mjumbe mwingine, Rudia Mareza, alisema serikali ya CCM ina kila sababu ya kuhakikisha inatengeneza mazingira mazuri ya ajira kwa vijana kwa kujiajiri wenyewe baada ya kuhitimu masomo ya sekondari na vyuo vikuu badala ya kutegemea ajira toka serikalini.
Alisema sehemu kubwa ambayo inaweza kutoa ajira kubwa kwa vijana ni kilimo kwa kuwawezesha vijana kushiriki kikamilifu katika sekta hiyo kwa kupewa nyenzo ambazo zitakazotumika katika kuendesha kilimo cha umwagiliaji badala ya kutegemea mvua, jambo ambalo litachangia vijana kuzalisha wakiwa vijijini.
Source : Nipashe