Wana Jf
Jana Mwenyekiti wa Kamati ya REFORMS UVCCM, Hussein Bashe akiwa katika Mkutano Mkuu wa Uvccm Mkoa wa Dar es Salaam, alitoa Onyo kwa UVCCM na Chama Cha Mapinduzi, Bashe alisema Wakati CCM na UVCCM wakisahau wajibu wao kwa Jamii na Kubaki Kulumbana na Kutuhumiana wenzeao CDM wako busy katika kukijenga Chama Chao.
Bashe alitumia muda Mwingi kueleza kwanini CCM inapoteza uhalali wake, alisema CCM imesahau kutekeleza wajibu wake na hasa Kusimamia SOCIAL JUSTICE, na akasema wasipotekeleza wajibu wao CCM itaondolewa madarakani na watanzania. Bashe alisema watanzania wengi leo wanahali ngumu, Maisha yanazidi kupanda nchi ina Nyemelewa na Njaa.
Alitoa Mfano kwao Nzega kati ya kata 130 za wilaya ya Nzega kata 90 zina upungufu wa chakula, Bei ya Mchele leo 1600 kipindi cha mavuno Bashe pia alisema leo Nchi ipo ktk Mgao zaidi ya Mika 6 viongozi wanalumbana badala ya kutatua tatizo la Umeme. Bashe alisema Mafuta yanapanda kwakuwa duniani yamepanda lakini ni wajibu wa serekali kutafuta Njia ya kupunguza makali. Maharage 1,500, Sembe 1,000 anashangaa chama hakiibani serikali wako busy kujibizana na Slaa na CHADEMA, alisema wana CCM wengi hawaijui ITIKADI ya Chama Chao inatekelezekaje ktk ulimwengu wa Mfumo wa soko.
Bashe alionya CCM isipokuwa makini Itaondoka Madarakani na kuwataka vijana wenzie wa UVCCM kuamka na kukibana chama kisimamie serekali ili tuwatendee haki wananchi,Bashe aliwashangaa Viongozi wa Chama chake badala kutumia Muda mrefu kutatua kero za watanzania wao wako BUSY kukomoana na Kutuhumiana Mara. FULANI Fisadi atoke, Fulani CCJ alishiriki kuandaa katiba,alisema watanzania wanataka uhakika wa Ajira, Masoko ya Bidhaa zao,uimara wa Shilingi na Uchumi, kuliko matakwimu ambayo hayaonekani ktk maisha ya kila siku ,Afya ya Uhakika, Maji ya Uhakika sio porojo za fulani fisadi fulani CCJ, Bashe pia aliwaahidi wajumbe hao uhuru wa kutoa maoni na kamati yake haita chakachua lolote .
Pia katika hotuba yake Bashe alimpa Ujumbe Kijana aneitwa Matefu,kumwambia asikubali kuwa Sauti ya watu Flani lazima ahoji kila anachoambiwa kusema ili hata akisema Basi awe amekiamini na kukijua.
Bashe alionya Pia Tabia ya Viongozi kutumia UDINI na UKABILA kuhalalisha hoja zao za kisiasa ama kutafuta Political Legitimacy (uhalali wa kisiasa), Bashe alisema Leo kiongozi anakituhumu chama flani kuwa ni cha wachaga alihoji ama chadema tunawatuhumu kuwa ni cha wakristo.
Jamani huu ni ujuha, wendawazimu na ulevi kwa kijana wa CCM kuongea ama kuwaza haya, Dhambi hii itatuumiza kama Chama na Nchi. Alisema je wachaga na wakristo wote wakihamia chadema itakuwaje, tunataka kuvuruga nchi, ama tunataka kuwaambia watanzania CCM hakitaki wachaga na wakristo, alionya UVCCM wasiongee mawazo hayo dhaifu na Mabovu yasiyo kuwa na mashiko.
Bashe wakati akifunga Mkutano aliwaahidi vijana yale waliomueleza atayafikisha katika Baraza kuu Bila kuchakachua,Bashe alionya Mfumo mbovu wa chama ambao viongozi wamekaa kiuchaguzi chaguzi utakimaliza chama alisema CCM ni P na Serekali ni Agent,lazima Chama kiisimamie serekali kutekeleza wajibu wake na kuwataka Viongozi wa Chama na Jumuiya kuacha Mara moja Tabia ya Kuchokonoana kwani itavunja heshima ya Chama alitoa Mfano wa kesi ya Mahalu akasema hiyo iwe Shule kwani leo Rais mkapa anatakiwa mahakamani,Rais kikwete anatakiwa mahakamani hii ni aibu
Alisema Tuwatumikie watanzania tuache kuwa watumwa wa Historia,makosa ya Nyuma yatumike kurekebisha Future. Alisema Urais 2015 usitumike kukimaliza Chama Viongozi watimize wajibu wao waache kuwaza mfumo wa kushughulikiana,alisema Communication Strategy (mfumo wa mawasiliano) wa Chama ni Mbovu Magazeti, Radio za chama hazina Mvuto kwa watu kwakua hatuelezi vitu vya maana zaidi ya Mipasho na Porojo,Watanzania wamechoka kusikiliza Porojo lazima kila Mwana ccm atekeleze wajibu wake kukisaidia chama na si kusaidia kundi lake, aliwataka Vijana waungane kujenga Jumuiya Imara.
Alisema wasitumie muda Mwingi kujadili chadema tutumie muda mwingi kujenga chama chetu na kutimiza wajibu wetu, alimaliza kuwaasa vijana wasiwaze kuwa CCM ni watawala alisema dhana hiyo ni mbovu,bali alisema dhana sahihi ni kujenga Fikra kuwa CCM ni chama kinachoongoza ni si Tawala. Alisema leo CCM inaimba Nyimbo za Chadema na akasema Tumeingia katika POLITICAL TRAP ya chadema tunafanyia kazi ya kwao na kuacha ya kwetu 2015 tutaulizwa yakwetu tutakua hatuna majibu, alisema CCM tumekua REACTIVE badala ya PROACTIVE,badala ya kuwa Viongozi sasa Tunaongozwa,Tumebaki kuwaza Madaraka Badala ya kuwaza Namna Gani tutamiza wajibu wetu.
Aliwataka UVCCM kubadilika na kusema Maslahi ya Nchi na Chama yatalindwa kwa sisi kutekeleza wajibu wetu na kuacha UROHO wa Madaraka bila ya hivo tutaivuruga Nchi na Chama chetu alishangaa Tabia sikuhizi ccm kila mtu anasharubu na Kutoa Matamko.
Alisema Kamati yake itapokea maoni kupitia Email, akatangaza email address (maoniuvccm@yahoo.com) pia ukurusa wa Facebook ( maoni uvccm reforms)pia sms alisema kila wilaya wametuma madodoso 100 ambayo yatajazwa na wana uvccmm alisema watafanya mikutano ya namna hiyo ktk miko kumi na moja watakutana na wasomi wa Vyuo Vikuu.
Alisema atatumia JamiiForums ataongea na Viongozi wa mtandao huo wapate fursa ya kupokea maoni kwa Njia hiyo, aliwataja viongozi wastaafu wote alisema anawaomba vijana wasigubikwe na ugonjwa wa rushwa na kusema leo kila Mwana CCM hataki kutekeleza wajibu wake mpaka apewe Pesa aliomba Tuweke maslahi ya Chama na kukilinda na Kukijenga Chama Na Nchi yetu.
Jana Mwenyekiti wa Kamati ya REFORMS UVCCM, Hussein Bashe akiwa katika Mkutano Mkuu wa Uvccm Mkoa wa Dar es Salaam, alitoa Onyo kwa UVCCM na Chama Cha Mapinduzi, Bashe alisema Wakati CCM na UVCCM wakisahau wajibu wao kwa Jamii na Kubaki Kulumbana na Kutuhumiana wenzeao CDM wako busy katika kukijenga Chama Chao.
Bashe alitumia muda Mwingi kueleza kwanini CCM inapoteza uhalali wake, alisema CCM imesahau kutekeleza wajibu wake na hasa Kusimamia SOCIAL JUSTICE, na akasema wasipotekeleza wajibu wao CCM itaondolewa madarakani na watanzania. Bashe alisema watanzania wengi leo wanahali ngumu, Maisha yanazidi kupanda nchi ina Nyemelewa na Njaa.
Alitoa Mfano kwao Nzega kati ya kata 130 za wilaya ya Nzega kata 90 zina upungufu wa chakula, Bei ya Mchele leo 1600 kipindi cha mavuno Bashe pia alisema leo Nchi ipo ktk Mgao zaidi ya Mika 6 viongozi wanalumbana badala ya kutatua tatizo la Umeme. Bashe alisema Mafuta yanapanda kwakuwa duniani yamepanda lakini ni wajibu wa serekali kutafuta Njia ya kupunguza makali. Maharage 1,500, Sembe 1,000 anashangaa chama hakiibani serikali wako busy kujibizana na Slaa na CHADEMA, alisema wana CCM wengi hawaijui ITIKADI ya Chama Chao inatekelezekaje ktk ulimwengu wa Mfumo wa soko.
Bashe alionya CCM isipokuwa makini Itaondoka Madarakani na kuwataka vijana wenzie wa UVCCM kuamka na kukibana chama kisimamie serekali ili tuwatendee haki wananchi,Bashe aliwashangaa Viongozi wa Chama chake badala kutumia Muda mrefu kutatua kero za watanzania wao wako BUSY kukomoana na Kutuhumiana Mara. FULANI Fisadi atoke, Fulani CCJ alishiriki kuandaa katiba,alisema watanzania wanataka uhakika wa Ajira, Masoko ya Bidhaa zao,uimara wa Shilingi na Uchumi, kuliko matakwimu ambayo hayaonekani ktk maisha ya kila siku ,Afya ya Uhakika, Maji ya Uhakika sio porojo za fulani fisadi fulani CCJ, Bashe pia aliwaahidi wajumbe hao uhuru wa kutoa maoni na kamati yake haita chakachua lolote .
Pia katika hotuba yake Bashe alimpa Ujumbe Kijana aneitwa Matefu,kumwambia asikubali kuwa Sauti ya watu Flani lazima ahoji kila anachoambiwa kusema ili hata akisema Basi awe amekiamini na kukijua.
Bashe alionya Pia Tabia ya Viongozi kutumia UDINI na UKABILA kuhalalisha hoja zao za kisiasa ama kutafuta Political Legitimacy (uhalali wa kisiasa), Bashe alisema Leo kiongozi anakituhumu chama flani kuwa ni cha wachaga alihoji ama chadema tunawatuhumu kuwa ni cha wakristo.
Jamani huu ni ujuha, wendawazimu na ulevi kwa kijana wa CCM kuongea ama kuwaza haya, Dhambi hii itatuumiza kama Chama na Nchi. Alisema je wachaga na wakristo wote wakihamia chadema itakuwaje, tunataka kuvuruga nchi, ama tunataka kuwaambia watanzania CCM hakitaki wachaga na wakristo, alionya UVCCM wasiongee mawazo hayo dhaifu na Mabovu yasiyo kuwa na mashiko.
Bashe wakati akifunga Mkutano aliwaahidi vijana yale waliomueleza atayafikisha katika Baraza kuu Bila kuchakachua,Bashe alionya Mfumo mbovu wa chama ambao viongozi wamekaa kiuchaguzi chaguzi utakimaliza chama alisema CCM ni P na Serekali ni Agent,lazima Chama kiisimamie serekali kutekeleza wajibu wake na kuwataka Viongozi wa Chama na Jumuiya kuacha Mara moja Tabia ya Kuchokonoana kwani itavunja heshima ya Chama alitoa Mfano wa kesi ya Mahalu akasema hiyo iwe Shule kwani leo Rais mkapa anatakiwa mahakamani,Rais kikwete anatakiwa mahakamani hii ni aibu
Alisema Tuwatumikie watanzania tuache kuwa watumwa wa Historia,makosa ya Nyuma yatumike kurekebisha Future. Alisema Urais 2015 usitumike kukimaliza Chama Viongozi watimize wajibu wao waache kuwaza mfumo wa kushughulikiana,alisema Communication Strategy (mfumo wa mawasiliano) wa Chama ni Mbovu Magazeti, Radio za chama hazina Mvuto kwa watu kwakua hatuelezi vitu vya maana zaidi ya Mipasho na Porojo,Watanzania wamechoka kusikiliza Porojo lazima kila Mwana ccm atekeleze wajibu wake kukisaidia chama na si kusaidia kundi lake, aliwataka Vijana waungane kujenga Jumuiya Imara.
Alisema wasitumie muda Mwingi kujadili chadema tutumie muda mwingi kujenga chama chetu na kutimiza wajibu wetu, alimaliza kuwaasa vijana wasiwaze kuwa CCM ni watawala alisema dhana hiyo ni mbovu,bali alisema dhana sahihi ni kujenga Fikra kuwa CCM ni chama kinachoongoza ni si Tawala. Alisema leo CCM inaimba Nyimbo za Chadema na akasema Tumeingia katika POLITICAL TRAP ya chadema tunafanyia kazi ya kwao na kuacha ya kwetu 2015 tutaulizwa yakwetu tutakua hatuna majibu, alisema CCM tumekua REACTIVE badala ya PROACTIVE,badala ya kuwa Viongozi sasa Tunaongozwa,Tumebaki kuwaza Madaraka Badala ya kuwaza Namna Gani tutamiza wajibu wetu.
Aliwataka UVCCM kubadilika na kusema Maslahi ya Nchi na Chama yatalindwa kwa sisi kutekeleza wajibu wetu na kuacha UROHO wa Madaraka bila ya hivo tutaivuruga Nchi na Chama chetu alishangaa Tabia sikuhizi ccm kila mtu anasharubu na Kutoa Matamko.
Alisema Kamati yake itapokea maoni kupitia Email, akatangaza email address (maoniuvccm@yahoo.com) pia ukurusa wa Facebook ( maoni uvccm reforms)pia sms alisema kila wilaya wametuma madodoso 100 ambayo yatajazwa na wana uvccmm alisema watafanya mikutano ya namna hiyo ktk miko kumi na moja watakutana na wasomi wa Vyuo Vikuu.
Alisema atatumia JamiiForums ataongea na Viongozi wa mtandao huo wapate fursa ya kupokea maoni kwa Njia hiyo, aliwataja viongozi wastaafu wote alisema anawaomba vijana wasigubikwe na ugonjwa wa rushwa na kusema leo kila Mwana CCM hataki kutekeleza wajibu wake mpaka apewe Pesa aliomba Tuweke maslahi ya Chama na kukilinda na Kukijenga Chama Na Nchi yetu.