Uuzwaji nyumba za Serikali: John Magufuli, Mussa Magufuli, Sundi Malomo kushtakiwa (Raia Mwema)

Mnapoteza muda kufikiria kwamba huyu wa sasa ataishi kwa huruma ya ajaye.

Jana ijumaa yamemalizika mafunzo maalum ya viongozi wa juu 60 pale bahari beach jeshini.

JPM analiandaa vyema kiuongozi kundi lake litakalokuwa na nguvu kuanzia 2020 - 25, na kwa taarifa yako marais wamekuwa wakishindwa kuwaweka viongozi chaguo lao kwa sababu wao wenyewe wamekuwa hawaaminiki.

JPM anaaminika kwa wananchi, na wananchi wanawakubali wale ambao ni chaguo lake la moja kwa moja, rejea Kassim Majaliwa Majaliwa.

Usishangae 2025 JPM akaweka mtu wake na akaungwa mkono na chama.

mwaka 2025 aweke mtu wake asiweke mtu wake haimsaidii, ataendelea kuishi kwa huruma ya huyo atakayemuweka. Na Uraisi huwa hauna ubia, ukishakizoea kiti ukajua chaneli zinavyokwenda basi hata yule aliyekuweka asije kujifanya kuingia kwenye 18 zako unaweza kumshughulikia!.
Hata Mwalimu Nyerere alikuja kuujua ukweli huu baadae sana kwenye maisha yake pale mtu aliyempigania kwa nguvu na akili zake zote BWM alipoamua kuuza NBC na mashirika mengineyo bila kujali JKN anaumia au haumii, sasa hilo ni dogo, kama JKN angechonga kama alivyokuwa akichonga kipindi cha mstaarabu AHM naye angejua tu ni nini nguvu ya kiti alichowahi kukikalia yeye mwenyewe
 
mwaka 2025 aweke mtu wake asiweke mtu wake haimsaidii, ataendelea kuishi kwa huruma ya huyo atakayemuweka. Na Uraisi huwa hauna ubia, ukishakizoea kiti ukajua chaneli zinavyokwenda basi hata yule aliyekuweka asije kujifanya kuingia kwenye 18 zako unaweza kumshughulikia!.
Hata Mwalimu Nyerere alikuja kuujua ukweli huu baadae sana kwenye maisha yake pale mtu aliyempigania kwa nguvu na akili zake zote BWM alipoamua kuuza NBC na mashirika mengineyo bila kujali JKN anaumia au haumii, sasa hilo ni dogo, kama JKN angechonga kama alivyokuwa akichonga kipindi cha mstaarabu AHM naye angejua tu ni nini nguvu ya kiti alichowahi kukikalia yeye mwenyewe
Mawazo ya fisi, anausubiri mkono uanguke mpaka anakufa. JPM alichokifanya ni kuliondoa daraja lilikuwepo kati ya mkuu wa nchi na wananchi, sio mwanadiplomasia ni mtendaji.

Rais anayefuatilia maagizo yake, hafanani kabisa na BWM au JMK, na kizuri kwake ni kwamba aliwafuata wananchi mwaka 2015 bila ya chembechembe za pesa za matajiri.

Ana uchungu na maisha ya mtu wa kawaida, na mtu wa kawaida amemuelewa, hao wazee wawili waliomtangulia walikubali kuwa sehemu ya siasa za makundi, wakawa ni watumwa wa makundi, hawakuwa na nafsi huru kama JPM.
 
Ila kws hiki lazima aje ashtakiwe. Huo ni uwizi ambao JK aliufumbia macho.
Kweli ukipenda chongo utaita kengeza...yaani hata kivuko chakavu cha bilioni 8 anapakaziwa Magufuli!

unnamed%2B(36).jpg

Kama huyo si yeye, basi kweli watu hufanana!​
 
Ila kws hiki lazima aje ashtakiwe. Huo ni uwizi ambao JK aliufumbia macho.

Halafu jamaa akapeleka hili dude jeshini ili watu wasiseme! hahaha, ngoja naye atoke madarakani watu waanze kumuitia press conference kuponda mambo yake ya zamani na leo. Muosha huoshwa!
 
Ok, so wewe ambacho hukitaki ni jiwe kuwajibishwa juu ya ufisadi wake au ni nini?
Mnatumia nguvu kubwa kuwa against JPM lakini hamna mnachoweza kukifanya kikamdhuru.

Ukishaapishwa pale uwanja wa uhuru Hakuna sisimizi anayeweza kukupeleka mahakamani.
 
Yatasemwa mengi sana kipindi hiki tunapokaribia UCHAGUZI MKUU...hamna mluzi utaopoteza mbwa hata mmoja this time around maana Tuna fuga ma German shephard sio wale mmbwa koko...hao tushaacha kuwafuga kitambo sana maana hawajui tofautisha mluzi wa mwnye nyumba na mpita njia.
 
Mnatumia nguvu kubwa kuwa against JPM lakini hamna mnachoweza kukifanya kikamdhuru.

Ukishaapishwa pale uwanja wa uhuru Hakuna sisimizi anayeweza kukupeleka mahakamani.

Mkuu inaonekana mimi na wew tunachojadili ni vitu tofauti. Acha niseme kuwa umeshinda.
 
Huyu bwana ni mwivi,mdini, mbinafsi na mkabila kupindukia,
Tuungane kumuondoa ktk sanduku la kura 2020 hata kama ni kwa kuwaunga mapanya buku kina makamba na membe ili mradi totoe joka hili pangoni.
Mdini ,mkabila utaungana na nani kumuondoa?
 
Mnatumia nguvu kubwa kuwa against JPM lakini hamna mnachoweza kukifanya kikamdhuru.

Ukishaapishwa pale uwanja wa uhuru Hakuna sisimizi anayeweza kukupeleka mahakamani.

Sasa hii haifuti tuhuma za kuhonga nyumba ya serikali na aibu yake

Ana uwezo gani serious wa kupambana na ufisadi mtu wa namna hii?
 
Sasa hii haifuti tuhuma za kuhonga nyumba ya serikali na aibu yake

Ana uwezo gani serious wa kupambana na ufisadi mtu wa namna hii?
Ungeujua upigaji wa Obama na bado kaongoza marekani vipindi viwili usingeandika hayo uliyoyaandika.

Ungeujua upigaji wa Trump na kundi lake unaoendelea sasa hivi usingekuwa na mawazo uliyonayo kichwani.

Huwa hatuchagui malaika pale ikulu, anakwenda mtu kama wewe mwenye udhaifu kama wa kwako.

Ndege kumi ndani ya miaka minne sio kitu kidogo mkuu, watatu waliomtangulia walikuwa wanaliangalia tu shirika bila ya kuwa na ujanja wa kulifufua.

Hakuna nchi ambayo ina kiongozi mkuu ambaye hajawahi kupiga pesa, kuanzia zile serikali za kia Herode enzi za Yesu mpaka leo hii. Hawapo na bado ni hao hao wanaopambana na rushwa na ufisadi.
 
Huyu Ndiye Pombe Magufuli:

- Wasema nyumba 8,000 kauza kwa mkono wake mwenyewe
- Apuuza maonyo ya wataalamu- Mafaili ya Sundi na Musa aliyabeba kwapani

ALIYEKUWA Waziri wa Ujenzi, John Magufuli, katika Serikali ya awamu ya tatu, aliteka madaraka na kuwa mwenyekiti wa zoezi la kuuza nyumba za serikali ambazo hadi sasa, zimeshauzwa 8,288 imefahamika.

Habari zilizopatikana ndani ya wakala wa Majengo ya Serikali (TBA), zimethibitishia Rai wiki hii kwamba Magufuli alihakikisha anashiriki kama Mwenyekiti katika zoezi zima la kuuza nyumba, ambalo kimsingi lilistahili kusimamiwa na Mtendaji Mkuu wa TBA.

Kwa mujibu wa vyanzo kadhaa vya habari ndani ya TBA, Magufuli alifanya kila aina ya fujo katika zoezi la kuuza nyumba hizo, wakati mwingine akibatilisha maamuzi yaliyofanywa na Kamati ya TBA ya kuuza nyumba hizo, akiwapangia watu nyumba kwa utashi wake na wakati mwingine akiwakemea wale wote waliomshauri kinyume na matakwa.

Ni chini ya utaratibu huo, habari zinaeleza kwamba Magufuli, aliyabeba yeye mwenyewe mafaili ya ndugu zake; Musa Magufuli ambaye ni mdogo wake, na Sundi Malomo ambaye ni mzazi mwenzake na kuwalazimisha watendaji wa TBA wafuate matakwa yake katika kuwapatia nyumba ndugu zake hao.

Habari hizo zinaeleza kwamba awali Mtendaji Mkuu wa TBA alimshauri Magufuli kwamba suala la mauzo ya nyumba kwa ndugu zake ni kinyume cha utaratibu. Hata hivyo, imeelezwa kwamba Magufuli alilazimisha huku akisema mdogo wake hana tatizo kwa sababu alikuwa tayari mfanyakazi wa Serikali.

Musa aliajiriwa kwa mkataba wa miezi mitatu, baada ya mwezi mmoja akauziwa nyumba na baada ya miezi miwili akaacha kazi.

Kwa upande wa Sundi, kwanza ilikuwa Sundi auziwe nyumba moja kwa moja. Lakini Magufuli alipoonywa akashtuka na kusema suala hilo aachiwe yeye mwenyewe. Na ndipo akaibuka na jina la Stanley Manongi kwamba ndiye mnunuzi halisi na baba yake Sundi, vinasema vyanzo hivyo vya habari, vingine ambavyo vilishiriki moja kwa moja katika mchakato wa uuzaji nyumba hizo.

Habari hizo zinaendelea kueleza kwamba baadaye, Sundi alishtuka akitilia shaka uaminifu wa Manongi, kwamba angeweza kumdhulumu nyumba hiyo.

Ndipo Magufuli aliibuka na mpango wa Sundi kuwa mtoto wa Manongi na mrithi wake na kisha kwa kuhakikisha kwamba hakuna dhuluma yoyote, mtoto wa Sundi naye akarithishwa na kama mrithi wa pili, chanzo hicho cha habari kinaeleza.

Chini ya sheria ya Executive Agency Act No. 30 ya mwaka 1997, TBA ilipewa madaraka yote ya kuuza nyumba za Serikali, kujenga nyumba mpya, kuzikarabati zilizopo pamoja na kugawa nyumba za madaraja A, B na C kwa wafanyakazi wa Serikali.

Sheria hiyo inaipa mamlaka ya kipekee ya kufanya shughuli zote bila kuingiliwa na chombo chochote.

Chini ya sheria hiyo, Waziri anaruhusiwa kuteua wajumbe wa bodi ya ushauri watakaomshauri Katibu Mkuu wa Wizara juu ya namna nzuri ya TBA kusimamia mamlaka yake.

Hadi Machi mwaka huu, wajumbe hao walikuwa ni J. Kijazi, E. Lipambila, E. Lugwisha, Msangi, E. Mwakalinga, D. Kisasi, P. Ncheye, F. Werema na A. Bukuku.

Hata hivyo, sheria haitoi nafasi yoyote kwa Waziri kusimamia shughuli za uuzwaji au upangaji wa nyumba za serikali.

Mtendaji Mkuu wa TBA Togolayi Makumba Kimweri, alipoulizwa kupitia kwa Katibu Muhtasi wake, alimwambia mwandishi wa Rai aandike maswali kisha asubiri kuruhusiwa kuingia ndani ya ofisi.

Hata hivyo, baada ya kusubiri kwa muda wa saa moja, mwandishi alipokwenda kuuliza akaambiwa kwamba Kimweri tayari alikwishaondoka ofisini kupitia mlango wa nyuma na asingeweza kurudi ofisini.

Lakini baadhi ya wafanyakazi wa TBA wameiambia Rai kwamba kinachoandikwa kwenye magazeti kuhusu ushiriki wa Magufuli kuuza nyumba za Serikali ni kidogo mno kuliko hali halisi.

Kama ilivyokuwa kwa mdogo wake Musa, waziri Magufuli alishinikiza mtoto wa dada yake anayeitwa James Doto Mgosha auziwe nyumba za serikali kwa kumtengenezea ajira ya muda mfupi katika TANROADS.

Tofauti na Musa, Doto ameuziwa nyumba hiyo kwa jina la mtu mwingine lakini anaishi katika nyumba hiyo, namba 64 iliyopo Kinondoni Flats.

Habari kutoka TBA zinaonyesha jina la mtu mwingine (tunalihifadhi) kuwa ndiye aliyeuziwa nyumba hiyo mtu huyo alipata kupitia utaratibu wa Magufuli kupeleka jina lake kwenye wakala wa majengo na kulazimisha apewe nyumba.

Alipoulizwa kwa njia ya simu, Doto alisema suala la ajira na nyumba waulizwe waliomwajiri na kumpa nyumba. Akakata simu.

Mfanyakazi mwingine alieleza Rai kwamba msichana mwingine (jina tunalihifadhi) akiwa na miezi minne tu kazini alipelekwa na Magufulikatika Wakala wa Majengo akilazimisha auziwe nyumba hata kabla ya kuthibitishwa kazini. Nyumba hiyo iko Block A, Ocean Road.

Hata hivyo, habari hizo zinaeleza kwamba msichana huyo ambaye hadi sasa anaishi na wazazi wake, ameipangisha nyumba hiyo kwa mfanyakazi mmoja wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa na analipwa kwa dola za kimarekani.

Kuuza nyumba za serikali sawa, lakini kweli katika mtindo huu? Sisi tunaoshiriki kuzikagua na kuziratibu tukiomba hatupati, lakini wengine wanaingia serikalini miezi miwili wanapata nyumba. Na wengine hata si wafanyakazi, wanapata, hii si sahihi, alilalamika mfanyakazi mmoja aliyeandikia Rai kwa njia ya barua pepe.

Hadi Machi mwaka huu Wakala wa Majengo wa Serikali (TBA) walishauza nyumba 8,288 ambazo hata hivyo zilitakiwa kuuzwa kwa watumishi wa serikali.

Katika mauzo hayo, Serikali ilitarajia kupata jumla ya shilingi 60,016,556,439.00. Hata hivyo hadi sasa Serikali imepata shilingi 22,684,108,115.08.

Kwa sasa, Serikali imebakiwa na nyumba 1,098 zinazosimamiwa na TBA. Kati ya hizo, nyumba 692 zimetengwa kwa wafanyakazi wa Serikali, nyumba 675 kama tied quarters, nyumba 111 zinatumika kama Rest House za Serikali, wakati nyumba 40 zinatumika kama state lodges. Nyumba 24 zinatumika kama ofisi na nyingine 29 ni kama karakana na bohari.

SALVA RWEYEMAMU
RAI

Acheni upotoshaji.Magufuli hakuuza nyumba kama Magufuli,ilikuwa uamuzi wa serikali,kwa hiyo yeye alikuwa anatekeleza maamuzi ya serikali collectively.Hii ina maana kwamba hawezi kuwa held responsible as an individual katika uuzwaji wa nyumba hizo.Tutumie akili kidogo.
 
Acheni upotoshaji.Magufuli hakuuza nyumba kama Magufuli,ilikuwa uamuzi wa serikali,kwa hiyo yeye alikuwa anatekeleza maamuzi ya serikali collectively.Hii ina maana kwamba hawezi kuwa held responsible as an individual katika uuzwaji wa nyumba hizo.Tutumie akili kidogo.

Kama zoezi aliliendesha hovyo hadi "michepuko" ikatake advantage basi anaweza kuwa held accountable!

Soma tena taarifa ya uuzwaji wa nyumba hizo ngoja nikuwekee tena sehemu ya kipande:

Kwa mujibu wa vyanzo kadhaa vya habari ndani ya TBA, Magufuli alifanya kila aina ya fujo katika zoezi la kuuza nyumba hizo, wakati mwingine akibatilisha maamuzi yaliyofanywa na Kamati ya TBA ya kuuza nyumba hizo, akiwapangia watu nyumba kwa utashi wake na wakati mwingine akiwakemea wale wote waliomshauri kinyume na matakwa.

Ni chini ya utaratibu huo, habari zinaeleza kwamba Magufuli, aliyabeba yeye mwenyewe mafaili ya ndugu zake; Musa Magufuli ambaye ni mdogo wake, na Sundi Malomo ambaye ni mzazi mwenzake na kuwalazimisha watendaji wa TBA wafuate matakwa yake katika kuwapatia nyumba ndugu zake hao.

Habari hizo zinaeleza kwamba awali Mtendaji Mkuu wa TBA alimshauri Magufuli kwamba suala la mauzo ya nyumba kwa ndugu zake ni kinyume cha utaratibu. Hata hivyo, imeelezwa kwamba Magufuli alilazimisha huku akisema mdogo wake hana tatizo kwa sababu alikuwa tayari mfanyakazi wa Serikali.

Musa aliajiriwa kwa mkataba wa miezi mitatu, baada ya mwezi mmoja akauziwa nyumba na baada ya miezi miwili akaacha kazi.

Kwa upande wa Sundi, kwanza ilikuwa Sundi auziwe nyumba moja kwa moja. Lakini Magufuli alipoonywa akashtuka na kusema suala hilo aachiwe yeye mwenyewe. Na ndipo akaibuka na jina la Stanley Manongi kwamba ndiye mnunuzi halisi na baba yake Sundi, vinasema vyanzo hivyo vya habari, vingine ambavyo vilishiriki moja kwa moja katika mchakato wa uuzaji nyumba hizo.

Habari hizo zinaendelea kueleza kwamba baadaye, Sundi alishtuka akitilia shaka uaminifu wa Manongi, kwamba angeweza kumdhulumu nyumba hiyo.

Ndipo Magufuli aliibuka na mpango wa Sundi kuwa mtoto wa Manongi na mrithi wake na kisha kwa kuhakikisha kwamba hakuna dhuluma yoyote, mtoto wa Sundi naye akarithishwa na kama mrithi wa pili, chanzo hicho cha habari kinaeleza.

Chini ya sheria ya Executive Agency Act No. 30 ya mwaka 1997, TBA ilipewa madaraka yote ya kuuza nyumba za Serikali, kujenga nyumba mpya, kuzikarabati zilizopo pamoja na kugawa nyumba za madaraja A, B na C kwa wafanyakazi wa Serikali.


Sheria hiyo inaipa mamlaka ya kipekee ya kufanya shughuli zote bila kuingiliwa na chombo chochote.
 
Kama zoezi aliliendesha hovyo hadi "michepuko" ikatake advantage basi anaweza kuwa held accountable!

Soma tena taarifa ya uuzwaji wa nyumba hizo ngoja nikuwekee tena sehemu ya kipande:

Kwa mujibu wa vyanzo kadhaa vya habari ndani ya TBA, Magufuli alifanya kila aina ya fujo katika zoezi la kuuza nyumba hizo, wakati mwingine akibatilisha maamuzi yaliyofanywa na Kamati ya TBA ya kuuza nyumba hizo, akiwapangia watu nyumba kwa utashi wake na wakati mwingine akiwakemea wale wote waliomshauri kinyume na matakwa.

Ni chini ya utaratibu huo, habari zinaeleza kwamba Magufuli, aliyabeba yeye mwenyewe mafaili ya ndugu zake; Musa Magufuli ambaye ni mdogo wake, na Sundi Malomo ambaye ni mzazi mwenzake na kuwalazimisha watendaji wa TBA wafuate matakwa yake katika kuwapatia nyumba ndugu zake hao.

Habari hizo zinaeleza kwamba awali Mtendaji Mkuu wa TBA alimshauri Magufuli kwamba suala la mauzo ya nyumba kwa ndugu zake ni kinyume cha utaratibu. Hata hivyo, imeelezwa kwamba Magufuli alilazimisha huku akisema mdogo wake hana tatizo kwa sababu alikuwa tayari mfanyakazi wa Serikali.

Musa aliajiriwa kwa mkataba wa miezi mitatu, baada ya mwezi mmoja akauziwa nyumba na baada ya miezi miwili akaacha kazi.

Kwa upande wa Sundi, kwanza ilikuwa Sundi auziwe nyumba moja kwa moja. Lakini Magufuli alipoonywa akashtuka na kusema suala hilo aachiwe yeye mwenyewe. Na ndipo akaibuka na jina la Stanley Manongi kwamba ndiye mnunuzi halisi na baba yake Sundi, vinasema vyanzo hivyo vya habari, vingine ambavyo vilishiriki moja kwa moja katika mchakato wa uuzaji nyumba hizo.

Habari hizo zinaendelea kueleza kwamba baadaye, Sundi alishtuka akitilia shaka uaminifu wa Manongi, kwamba angeweza kumdhulumu nyumba hiyo.

Ndipo Magufuli aliibuka na mpango wa Sundi kuwa mtoto wa Manongi na mrithi wake na kisha kwa kuhakikisha kwamba hakuna dhuluma yoyote, mtoto wa Sundi naye akarithishwa na kama mrithi wa pili, chanzo hicho cha habari kinaeleza.

Chini ya sheria ya Executive Agency Act No. 30 ya mwaka 1997, TBA ilipewa madaraka yote ya kuuza nyumba za Serikali, kujenga nyumba mpya, kuzikarabati zilizopo pamoja na kugawa nyumba za madaraja A, B na C kwa wafanyakazi wa Serikali.


Sheria hiyo inaipa mamlaka ya kipekee ya kufanya shughuli zote bila kuingiliwa na chombo chochote.
Hayo yote kama kweli yalifanyika,si yalifanyika wakati serikali imeshafanya maamuzi ya kuziuza hizo nyumba?Sasa yeye atalaumiwaje kwa kufanya maamuzi ya kuziuza?Frankly commonsense tells me kwamba hawezi kulaumiwa kwa maamuzi ya kuuza nyumba za serikali,at most he can be blamed for implenting the government decision harphazardly,if it happened at all.
 
Hayo yote kama kweli yalifanyika,si yalifanyika wakati serikali imeshafanya maamuzi ya kuziuza hizo nyumba?Frankly commonsense tells me kwamba hawezi kulaumiwa kwa maamuzi ya kuuza nyumba za serikali,at most he can be blamed for implenting the government decision harphazardly,if it happened at all.

Uamuzi wa kuziuza ni jambo moja na kuziuza kinyume cha sheria kwa maslahi ya ndugu na michepuko ni jambo jingine.
TBA ndo ilikuwa na mamlaka ya kuziuza na siyo Waziri
 
Back
Top Bottom