Uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu Mpya wa TISS, Said H. Masoro, na Mtazamo wangu

Yericko Nyerere

JF-Expert Member
Dec 22, 2010
16,987
20,271
Pengine huu ni mwanzo mpya wa mageuzi ya Idara ya Usalama wa Taifa. Mabadiliko haya ya uongozi yana maana kubwa sana kwa Idara yetu, ni matumaini yangu kwamba mabadiliko yatakwenda mbali zaidi kuguza muundo wa idara, mfumo wa idara, sheria na kanuni za idara ili kuendana na ulimwengu mpya wa dunia ya sayansi na teknolojia.

DGIS mpya Ndugu Said Masoro si mtu maarufu katika korido za Ujasusi Dar es Salaam ukimlinganisha na mtangulizi wake Athuman Diwani ambae umaarufu wake ulijengwa akiwa Intelijensia ya Polisi, DCI na katibu Tawala, Masoro anaweza kuwa chachu ya magezi ya chombo hiki muhimu na uti wa mgongo wa taifa letu ikiwa hataruhusu kumezwa na siasa chafu za Dar na Dodoma.

Moja ya Sababu kuu mimi kuamua kuandika kitabu cha Ujasusi wa Kidola na Kiuchumi, ilikuwa ni "kuhimiza mageuzi ya idara ya Usalama Tanzania na mfumo mzima wa ulinzi na Usalama nchini".

Nilifanya hivyo baada ya utafiti mkubwa nilioufanya na kujiridhisha kwamba mfumo uliopo hauwezi kulisaidia taifa katika ulimwengu huu mpya zaidi ya kulirudisha nyuma na kudumaza utu na fikra za kijamii huku dunia ikisonga mbele katika mageuzi ya kilimwengu.

Katika kitabu, nimeeleza mageuzi makuu matatu ya muhimu na ya lazima kwa Idara ya Usalama wa Taifa kama tunalitakia mema taifa hili. Mageuzi hayo ni; kwanza yaanze kwenye Sheria iliyounda chombo hiki, pili ni Muundo wa Chombo hiki, na tatu ni Sera ya chombo hiki adhimu kwa uhai wa taifa letu.

Kwa mjibu wa Katiba ya Tanzania ya 1977 Idara ya Usalama haitajwi moja kwa moja kwenye katiba hii tofauti na majeshi mengine yote ya Nchi. Yaani Katiba ya Tanzania haitambuwi uwepo wa Idara ya Usalama wa Taifa.

Badala yake Chombo hiki kinatambuliwa na sheria ya Usalama wa Taifa ya 20 January 1997 iliyosainiwa na Benjamin William Mkapa, Rais wa Tanzania. Kwa maoni yangu hili ni moja ya makosa, Katiba Mpya inatakiwa kutambua na kuipa nguvu idara/taasisi hii pamoja na kwamba Chombo chochote cha usalama kinachoanzishwa kwa mjibu wa sheria ya Tanzania au katiba ya Tanzania, chombo hicho kitakuwa mali ya Tanzania na kitafanya kazi kwa maslahi ya Taifa na si vinginevyo.

Katika Kitabu cha Ujasusi nimeainisha mapendekezo yangu kwenye sheria ya Usalama wa Taifa ambayo nafikiri kwasasa sheria hiyo ni lazima ifanyiwe marekebisho ili kuendana na mageuzi ya dunia ya leo, tuko karne ya 21 sio enzi za zamadamu.

Moja ya vifungu katika Sheria ya Usalama wa Taifa iliyosainiwa 20 January 1997 na Rais Hayati Benjamiji W. Mkapa ambavyo ni muhimu sana kufanyiwa marekebisho ni. Mfano, kifungu 14 -(1), (2),(3), (4)-(a) na (b). Kifungu cha 15 -(1),(2), (3) -(a) na (b). Kifungu cha 16-(1) (a)na (b), (2) na (3).

Katika kitabu nimehimiza muundo wa Idara ambao umepitwa na wakati ubadilike, muundo huu unahusu kuanzia uajiri (recruiting) na mengineyo, Mfumo wa chama kimoja wa 1962 ulikuwa ndio mfumo wa uajiri wa vyombo vyote vya ulinzi na usalama, na ndio ulikuwa mfumo wa ajira zingine, ilikuwa huwezi kuingia katika vyombo vya ulinzi na usalama bila kupita TANU YOUTH League/UVCCM.

Hadi ilipofika 1992 ndipo mfumo huo ulianza kutoweka katika sekta zingine, lakini katika vyombo vya dola haukutoweka kabisa, Hivi leo watumishi wa vyombo vya dola wengi walioingia kazini kuanzia 1992 kurudi nyuma hadi 1962, hawa ni makada wa chama cha mapinduzi 100%.

Wengi wao leo ni watu wazima ndio ma RPC, OCD na wakuu wa vitengo mbalimbali katika vyombo vya utumishi na vya dola, Hivyo ukimuona RPC anashangilia ccm ikishinda sio kosa lake bali itikadi kwake imekolea na aliingia jeshini kwa tiketi ya chama na sio professional yake.

Kizazi kilichoingia kwenye vyombo vya ulinzi na Usalama miaka ya karibuni angalau hiki msingi wa kuingia kwao ni elimu, undugulaizesheni na kuipenda kazi husika, japo ukada bado una nguvu ndani ya vyombo hivyo, kwamba leo unaweza kuona maajabu RPC anastaafu leo na kesho akagombea uenyekiti wa ccm mkoa au Ubunge utajiuliza lini aliuwa mwanachama kama katiba ya ccm inavyotaka awe mwanachama angalau miaka miwili.

Sera ama Malengo makuu ya Ujasusi Tanzania yanatakiwa kujikita katika Uchumi kwakuwa hakuna njia ya mkato ya kufikia mafanikio ya Taifa kiuchumi bila kuruhusu uchumi wetu uongozwe katika misingi ya Idara ya Usalama wa Taifa na Jeshi la Wananchi Tanzani (TISS na MI).

Hapa ieleweke sana, sina maana biashara na makampuni ya uwekezaji yawe ya vyombo hivyo vya ulinzi, au yawe ya serikali, la hasha, nina maana pana zaidi kwamba ushughulikiaji wa taarifa za biashara na uchumi utiliwe mkazo zaidi kuliko ilivyo sasa taarifa za kisiasa ndizo zenye nguvu ya nchi, Mapendekezo ni TISS itilie mkazo taarifa za uchumi na biashara zaidi na kuzipa ulinzi shughuli na biashara zote za uwekezaji wa ndani na nje na wawekezaji wake. Hawa waitwe rasmi kuwa ni (asset).

Tanzania iwe na shirika la Ujasusi linaloangalia siasa kama njia tu, na sio msingi imara wa kulinda TAIFA, wanausalama watakao kuwa makini kuona kofia ya siasa haizidi kofia ya nguvu ya umma au TAIFA. Ni wakati mwafaka wa kutambua NCHI ndio nguzo ya UTAIFA na sio siasa kuwa ndio UTAIFA wenyewe.

Kusimamia Demokrasi kwa jicho la ndani na sio jicho la upendeleo wa kiitikadi bali kuongozwa na kusimamia maadilli ya NCHI dhidi ya siasa. Inatakiwa Shirika ambalo halitatumika kwa faida ya chama, Mtu au kikundi cha watu bali ukweli uwe Taifa lianitaji nini kutoka kwenye siasa. Nchi inaishi katika lindi la unafi hasa vijana.

Kwa undani zaidi, soma kitabu cha Ujasusi wa Kidola na Kiuchumi popote ulipo duniani.


IMG_20230104_081530_808.jpg
 
Pengine huu ni mwanzo mpya wa mageuzi ya Idara ya Usalama wa Taifa. Mabadiliko haya ya uongozi yana maana kubwa sana kwa Idara yetu, ni matumaini yangu kwamba mabadiliko yatakwenda mbali zaidi kuguza muundo wa idara, mfumo wa idara, sheria na kanuni za idara ili kuendana na ulimwengu mpya wa dunia ya sayansi na teknolojia.

DGIS mpya Ndugu Said Masoro si mtu maarufu katika korido za Ujasusi Dar es Salaam ukimlinganisha na mtangulizi wake Athuman Diwani ambae umaarufu wake ulijengwa akiwa Intelijensia ya Polisi, DCI na katibu Tawala, Masoro anaweza kuwa chachu ya magezi ya chombo hiki muhimu na uti wa mgongo wa taifa letu ikiwa hataruhusu kumezwa na siasa chafu za Dar na Dodoma.

Moja ya Sababu kuu mimi kuamua kuandika kitabu cha Ujasusi wa Kidola na Kiuchumi, ilikuwa ni "kuhimiza mageuzi ya idara ya Usalama Tanzania na mfumo mzima wa ulinzi na Usalama nchini".

Nilifanya hivyo baada ya utafiti mkubwa nilioufanya na kujiridhisha kwamba mfumo uliopo hauwezi kulisaidia taifa katika ulimwengu huu mpya zaidi ya kulirudisha nyuma na kudumaza utu na fikra za kijamii huku dunia ikisonga mbele katika mageuzi ya kilimwengu.

Katika kitabu, nimeeleza mageuzi makuu matatu ya muhimu na ya lazima kwa Idara ya Usalama wa Taifa kama tunalitakia mema taifa hili. Mageuzi hayo ni; kwanza yaanze kwenye Sheria iliyounda chombo hiki, pili ni Muundo wa Chombo hiki, na tatu ni Sera ya chombo hiki adhimu kwa uhai wa taifa letu.

Kwa mjibu wa Katiba ya Tanzania ya 1977 Idara ya Usalama haitajwi moja kwa moja kwenye katiba hii tofauti na majeshi mengine yote ya Nchi. Yaani Katiba ya Tanzania haitambuwi uwepo wa Idara ya Usalama wa Taifa.

Badala yake Chombo hiki kinatambuliwa na sheria ya Usalama wa Taifa ya 20 January 1997 iliyosainiwa na Benjamin William Mkapa, Rais wa Tanzania. Kwa maoni yangu hili ni moja ya makosa, Katiba Mpya inatakiwa kutambua na kuipa nguvu idara/taasisi hii pamoja na kwamba Chombo chochote cha usalama kinachoanzishwa kwa mjibu wa sheria ya Tanzania au katiba ya Tanzania, chombo hicho kitakuwa mali ya Tanzania na kitafanya kazi kwa maslahi ya Taifa na si vinginevyo.

Katika Kitabu cha Ujasusi nimeainisha mapendekezo yangu kwenye sheria ya Usalama wa Taifa ambayo nafikiri kwasasa sheria hiyo ni lazima ifanyiwe marekebisho ili kuendana na mageuzi ya dunia ya leo, tuko karne ya 21 sio enzi za zamadamu.

Moja ya vifungu katika Sheria ya Usalama wa Taifa iliyosainiwa 20 January 1997 na Rais Hayati Benjamiji W. Mkapa ambavyo ni muhimu sana kufanyiwa marekebisho ni. Mfano, kifungu 14 -(1), (2),(3), (4)-(a) na (b). Kifungu cha 15 -(1),(2), (3) -(a) na (b). Kifungu cha 16-(1) (a)na (b), (2) na (3).

Katika kitabu nimehimiza muundo wa Idara ambao umepitwa na wakati ubadilike, muundo huu unahusu kuanzia uajiri (recruiting) na mengineyo, Mfumo wa chama kimoja wa 1962 ulikuwa ndio mfumo wa uajiri wa vyombo vyote vya ulinzi na usalama, na ndio ulikuwa mfumo wa ajira zingine, ilikuwa huwezi kuingia katika vyombo vya ulinzi na usalama bila kupita TANU YOUTH League/UVCCM.

Hadi ilipofika 1992 ndipo mfumo huo ulianza kutoweka katika sekta zingine, lakini katika vyombo vya dola haukutoweka kabisa, Hivi leo watumishi wa vyombo vya dola wengi walioingia kazini kuanzia 1992 kurudi nyuma hadi 1962, hawa ni makada wa chama cha mapinduzi 100%.

Wengi wao leo ni watu wazima ndio ma RPC, OCD na wakuu wa vitengo mbalimbali katika vyombo vya utumishi na vya dola, Hivyo ukimuona RPC anashangilia ccm ikishinda sio kosa lake bali itikadi kwake imekolea na aliingia jeshini kwa tiketi ya chama na sio professional yake.

Kizazi kilichoingia kwenye vyombo vya ulinzi na Usalama miaka ya karibuni angalau hiki msingi wa kuingia kwao ni elimu, undugulaizesheni na kuipenda kazi husika, japo ukada bado una nguvu ndani ya vyombo hivyo, kwamba leo unaweza kuona maajabu RPC anastaafu leo na kesho akagombea uenyekiti wa ccm mkoa au Ubunge utajiuliza lini aliuwa mwanachama kama katiba ya ccm inavyotaka awe mwanachama angalau miaka miwili.

Sera ama Malengo makuu ya Ujasusi Tanzania yanatakiwa kujikita katika Uchumi kwakuwa hakuna njia ya mkato ya kufikia mafanikio ya Taifa kiuchumi bila kuruhusu uchumi wetu uongozwe katika misingi ya Idara ya Usalama wa Taifa na Jeshi la Wananchi Tanzani (TISS na MI).

Hapa ieleweke sana, sina maana biashara na makampuni ya uwekezaji yawe ya vyombo hivyo vya ulinzi, au yawe ya serikali, la hasha, nina maana pana zaidi kwamba ushughulikiaji wa taarifa za biashara na uchumi utiliwe mkazo zaidi kuliko ilivyo sasa taarifa za kisiasa ndizo zenye nguvu ya nchi, Mapendekezo ni TIFF itilie mkazo taarifa za uchumi na biashara zaidi na kuzipa ulinzi shughuli na biashara zote za uwekezaji wa ndani na nje na wawekezaji wake. Hawa waitwe rasmi kuwa ni (asset).

Tanzania iwe na shirika la Ujasusi linaloangalia siasa kama njia tu, na sio msingi imara wa kulinda TAIFA, wanausalama watakao kuwa makini kuona kofia ya siasa haizidi kofia ya nguvu ya umma au TAIFA. Ni wakati mwafaka wa kutambua NCHI ndio nguzo ya UTAIFA na sio siasa kuwa ndio UTAIFA wenyewe.

Kusimamia Demokrasi kwa jicho la ndani na sio jicho la upendeleo wa kiitikadi bali kuongozwa na kusimamia maadilli ya NCHI dhidi ya siasa. Inatakiwa Shirika ambalo halitatumika kwa faida ya chama, Mtu au kikundi cha watu bali ukweli uwe Taifa lianitaji nini kutoka kwenye siasa. Nchi inaishi katika lindi la unafi hasa vijana.

Kwa undani zaidi, soma kitabu cha Ujasusi wa Kidola na Kiuchumi popote ulipo duniani.


View attachment 2468314
Hivi huwa ni lazima wavae miwani?
 
Sera ama Malengo makuu ya Ujasusi Tanzania yanatakiwa kujikita katika Uchumi kwakuwa hakuna njia ya mkato ya kufikia mafanikio ya Taifa kiuchumi bila kuruhusu uchumi wetu uongozwe katika misingi ya Idara ya Usalama wa Taifa na Jeshi la Wananchi Tanzani (TISS na MI).

Hapa ieleweke sana, sina maana biashara na makampuni ya uwekezaji yawe ya vyombo hivyo vya ulinzi, au yawe ya serikali, la hasha, nina maana pana zaidi kwamba ushughulikiaji wa taarifa za biashara na uchumi utiliwe mkazo zaidi kuliko ilivyo sasa taarifa za kisiasa ndizo zenye nguvu ya nchi, Mapendekezo ni TIFF itilie mkazo taarifa za uchumi na biashara zaidi na kuzipa ulinzi shughuli na biashara zote za uwekezaji wa ndani na nje na wawekezaji wake. Hawa waitwe rasmi kuwa ni (asset).
View attachment 2468314

Hiki ulichoandika hapa sio kazi kuu za Idara za Usalama wa Taifa/Ujasusi duniani. Kazi za majususi ni ulinzi na usalama wa nchi masuala ya uchumi na biashara yataingizwa huko katika majuku yao kama ni kitisho cha usalama wa nchi zao au kama yataleta matokeo fulani kiusalama.

Hizi kazi za uchumi na biashara katika nchi ni kazi kuu za Wizara ya Fedha na Benki Kuu.
 
Pengine huu ni mwanzo mpya wa mageuzi ya Idara ya Usalama wa Taifa. Mabadiliko haya ya uongozi yana maana kubwa sana kwa Idara yetu, ni matumaini yangu kwamba mabadiliko yatakwenda mbali zaidi kuguza muundo wa idara, mfumo wa idara, sheria na kanuni za idara ili kuendana na ulimwengu mpya wa dunia ya sayansi na teknolojia.

DGIS mpya Ndugu Said Masoro si mtu maarufu katika korido za Ujasusi Dar es Salaam ukimlinganisha na mtangulizi wake Athuman Diwani ambae umaarufu wake ulijengwa akiwa Intelijensia ya Polisi, DCI na katibu Tawala, Masoro anaweza kuwa chachu ya magezi ya chombo hiki muhimu na uti wa mgongo wa taifa letu ikiwa hataruhusu kumezwa na siasa chafu za Dar na Dodoma.

Moja ya Sababu kuu mimi kuamua kuandika kitabu cha Ujasusi wa Kidola na Kiuchumi, ilikuwa ni "kuhimiza mageuzi ya idara ya Usalama Tanzania na mfumo mzima wa ulinzi na Usalama nchini".

Nilifanya hivyo baada ya utafiti mkubwa nilioufanya na kujiridhisha kwamba mfumo uliopo hauwezi kulisaidia taifa katika ulimwengu huu mpya zaidi ya kulirudisha nyuma na kudumaza utu na fikra za kijamii huku dunia ikisonga mbele katika mageuzi ya kilimwengu.

Katika kitabu, nimeeleza mageuzi makuu matatu ya muhimu na ya lazima kwa Idara ya Usalama wa Taifa kama tunalitakia mema taifa hili. Mageuzi hayo ni; kwanza yaanze kwenye Sheria iliyounda chombo hiki, pili ni Muundo wa Chombo hiki, na tatu ni Sera ya chombo hiki adhimu kwa uhai wa taifa letu.

Kwa mjibu wa Katiba ya Tanzania ya 1977 Idara ya Usalama haitajwi moja kwa moja kwenye katiba hii tofauti na majeshi mengine yote ya Nchi. Yaani Katiba ya Tanzania haitambuwi uwepo wa Idara ya Usalama wa Taifa.

Badala yake Chombo hiki kinatambuliwa na sheria ya Usalama wa Taifa ya 20 January 1997 iliyosainiwa na Benjamin William Mkapa, Rais wa Tanzania. Kwa maoni yangu hili ni moja ya makosa, Katiba Mpya inatakiwa kutambua na kuipa nguvu idara/taasisi hii pamoja na kwamba Chombo chochote cha usalama kinachoanzishwa kwa mjibu wa sheria ya Tanzania au katiba ya Tanzania, chombo hicho kitakuwa mali ya Tanzania na kitafanya kazi kwa maslahi ya Taifa na si vinginevyo.

Katika Kitabu cha Ujasusi nimeainisha mapendekezo yangu kwenye sheria ya Usalama wa Taifa ambayo nafikiri kwasasa sheria hiyo ni lazima ifanyiwe marekebisho ili kuendana na mageuzi ya dunia ya leo, tuko karne ya 21 sio enzi za zamadamu.

Moja ya vifungu katika Sheria ya Usalama wa Taifa iliyosainiwa 20 January 1997 na Rais Hayati Benjamiji W. Mkapa ambavyo ni muhimu sana kufanyiwa marekebisho ni. Mfano, kifungu 14 -(1), (2),(3), (4)-(a) na (b). Kifungu cha 15 -(1),(2), (3) -(a) na (b). Kifungu cha 16-(1) (a)na (b), (2) na (3).

Katika kitabu nimehimiza muundo wa Idara ambao umepitwa na wakati ubadilike, muundo huu unahusu kuanzia uajiri (recruiting) na mengineyo, Mfumo wa chama kimoja wa 1962 ulikuwa ndio mfumo wa uajiri wa vyombo vyote vya ulinzi na usalama, na ndio ulikuwa mfumo wa ajira zingine, ilikuwa huwezi kuingia katika vyombo vya ulinzi na usalama bila kupita TANU YOUTH League/UVCCM.

Hadi ilipofika 1992 ndipo mfumo huo ulianza kutoweka katika sekta zingine, lakini katika vyombo vya dola haukutoweka kabisa, Hivi leo watumishi wa vyombo vya dola wengi walioingia kazini kuanzia 1992 kurudi nyuma hadi 1962, hawa ni makada wa chama cha mapinduzi 100%.

Wengi wao leo ni watu wazima ndio ma RPC, OCD na wakuu wa vitengo mbalimbali katika vyombo vya utumishi na vya dola, Hivyo ukimuona RPC anashangilia ccm ikishinda sio kosa lake bali itikadi kwake imekolea na aliingia jeshini kwa tiketi ya chama na sio professional yake.

Kizazi kilichoingia kwenye vyombo vya ulinzi na Usalama miaka ya karibuni angalau hiki msingi wa kuingia kwao ni elimu, undugulaizesheni na kuipenda kazi husika, japo ukada bado una nguvu ndani ya vyombo hivyo, kwamba leo unaweza kuona maajabu RPC anastaafu leo na kesho akagombea uenyekiti wa ccm mkoa au Ubunge utajiuliza lini aliuwa mwanachama kama katiba ya ccm inavyotaka awe mwanachama angalau miaka miwili.

Sera ama Malengo makuu ya Ujasusi Tanzania yanatakiwa kujikita katika Uchumi kwakuwa hakuna njia ya mkato ya kufikia mafanikio ya Taifa kiuchumi bila kuruhusu uchumi wetu uongozwe katika misingi ya Idara ya Usalama wa Taifa na Jeshi la Wananchi Tanzani (TISS na MI).

Hapa ieleweke sana, sina maana biashara na makampuni ya uwekezaji yawe ya vyombo hivyo vya ulinzi, au yawe ya serikali, la hasha, nina maana pana zaidi kwamba ushughulikiaji wa taarifa za biashara na uchumi utiliwe mkazo zaidi kuliko ilivyo sasa taarifa za kisiasa ndizo zenye nguvu ya nchi, Mapendekezo ni TIFF itilie mkazo taarifa za uchumi na biashara zaidi na kuzipa ulinzi shughuli na biashara zote za uwekezaji wa ndani na nje na wawekezaji wake. Hawa waitwe rasmi kuwa ni (asset).

Tanzania iwe na shirika la Ujasusi linaloangalia siasa kama njia tu, na sio msingi imara wa kulinda TAIFA, wanausalama watakao kuwa makini kuona kofia ya siasa haizidi kofia ya nguvu ya umma au TAIFA. Ni wakati mwafaka wa kutambua NCHI ndio nguzo ya UTAIFA na sio siasa kuwa ndio UTAIFA wenyewe.

Kusimamia Demokrasi kwa jicho la ndani na sio jicho la upendeleo wa kiitikadi bali kuongozwa na kusimamia maadilli ya NCHI dhidi ya siasa. Inatakiwa Shirika ambalo halitatumika kwa faida ya chama, Mtu au kikundi cha watu bali ukweli uwe Taifa lianitaji nini kutoka kwenye siasa. Nchi inaishi katika lindi la unafi hasa vijana.

Kwa undani zaidi, soma kitabu cha Ujasusi wa Kidola na Kiuchumi popote ulipo duniani.


View attachment 2468314
Asante SANA kwa ufafanuzi huu
 
Lakini kabla ya yote, mimi niliwahi kuandika humu, tanzania hatutaweza kuwa na demokrasia kamili kama tusipo tegua kitendawili cha muungano.

Kwasasa, namna pekee ya kuhakikisha uhai wa Muungano na uhai wa taifa upo, ni lazima chama kinachoshika uongozi wa JMT pia kishike na Zanzibar.

Hata wanausalama wakiwa wapenda demokrasia kwa namna gani, hawawezi kuruhusu serikali ya Mapinduzi iwe chama tofauti na serikali ya JMT.

Wakati wa Mwinyi kipindi kile cha mchafuko wa hali ya hewa, ilibidi nguvu ya ziada kutoka kwa mwalimu akisaidiwa na wazalendo kunusuru uhai wa taifa. Imagine kama rais wa Zanzibar wa kipindi kile angekuwa wa chama kingine, ingebidi yajirudie yaleyale ya hayati naliliu... yule babu yake na yule mwanasheria maarufu, Jambo ambalo ni risk kubwa kwani linaweza kupasua taifa kabisa.

Natumaini huyo boss mpya atamshauri vizuri Mheshimiwa kwenye umuhimu wa katiba mpya na kuhakikisha inaulinda muungano.
 
Kusimamia Demokrasi kwa jicho la ndani na sio jicho la upendeleo wa kiitikadi bali kuongozwa na kusimamia maadilli ya NCHI dhidi ya siasa. Inatakiwa Shirika ambalo halitatumika kwa faida ya chama, Mtu au kikundi cha watu bali ukweli uwe Taifa lianitaji nini kutoka kwenye siasa. Nchi inaishi katika lindi la unafi hasa vijana.
Hili halitekelezeki chini ya Ccm.
 
Hiki ulichoandika hapa sio kazi kuu za Idara za Usalama wa Taifa/Ujasusi duniani. Kazi za majususi ni ulinzi na usalama wa nchi masuala ya uchumi na biashara yataingizwa huko katika majuku yao kama ni kitisho cha usalama wa nchi zao au kama yataleta matokeo fulani kiusalama.

Hizi kazi za uchumi na biashara katika nchi ni kazi kuu za Wizara ya Fedha na Benki Kuu.
Alichoandika sio kazi kuu ya usalama wa taifa, ila ni kazi mojawapo. Mambo mengine yanafanyika, ulinzi na usalama wanafanya bado ujasusi wa kiuchumi.
Hao unaosema BoT na Finance hawawezi kufanya crandestine operations.

Wasovieti walioiba blueprints za atomic bomb kutoka Los Alamos pale Marekani sio wanasayansi wala watumishi wa jeshi, serikali ya Stalin ingeamua kusubiri jopo la wanasayansi lifanye testing na kila kitu wangetumia gharama kubwa mno na muda mwingi zaidi kupata breakthrough.

Wamarekani walioiba Lunik ya USSR ikiwa kwenye world tour hawakuwa wanasayansi wa NASA, walipiga picha na kukamilisha kazi yao kisha NASA wakatumia hizo taarifa.

Basically TISS isingekuwa na maana kama haitakiwi kufanya kazi fulani maana kila kazi ina wizara. Ulinzi na usalama si zina wizara zake, mambo ya ndani na ile ya ulinzi. TISS kamilifu inatakiwa iweze kusaidia popote pale, hata kampuni ya hapa nchini ikitaka kutengeneza pikipiki ikakwama kutengeneza injini, TISS inabidi iwe na uwezo wa kupata wapi pa kupata ujuzi wa kutengeneza injini kwa namna yoyote ile. Ndio vitu duniani wanafanya, China mara nyingi tu unasikia wameiba TB za data kuhusu kitu fulani. Survival of the fittest
 
Kuna similarities and connections baina ya Usalama wa Taifa na Uchumi wetu tena sana ila wengi hawajui

Salute mkuu kwa mada hii
Kuna watu wanarudisha nyuma maendeleo ya nchi ili wao wafaidi na mama zao

Bila Usalama kuwa na nguvu na kuwashughulikia hata paka siku moja na kanchi kake kadogo atatupita
 
TISS na Jeshi hawawezi kuukwamua uchumi wetu, hakuna maendeleo yoyote duniani ya kiuchumi yamepatikana kwa njia hii.
Huo wizi ulioiutaja hapa hauhusiani na uchumi. Maendeleo ya uchumi yanahitaji uongozi na mfumo mzuri wa kisiasa pamoja wachumi nguli wanaopewa uhuru kutimiza majukumu yao.
Alichoandika sio kazi kuu ya usalama wa taifa, ila ni kazi mojawapo. Mambo mengine yanafanyika, ulinzi na usalama wanafanya bado ujasusi wa kiuchumi.
Hao unaosema BoT na Finance hawawezi kufanya crandestine operations.

Wasovieti walioiba blueprints za atomic bomb kutoka Los Alamos pale Marekani sio wanasayansi wala watumishi wa jeshi, serikali ya Stalin ingeamua kusubiri jopo la wanasayansi lifanye testing na kila kitu wangetumia gharama kubwa mno na muda mwingi zaidi kupata breakthrough.

Wamarekani walioiba Lunik ya USSR ikiwa kwenye world tour hawakuwa wanasayansi wa NASA, walipiga picha na kukamilisha kazi yao kisha NASA wakatumia hizo taarifa.

Basically TISS isingekuwa na maana kama haitakiwi kufanya kazi fulani maana kila kazi ina wizara. Ulinzi na usalama si zina wizara zake, mambo ya ndani na ile ya ulinzi. TISS kamilifu inatakiwa iweze kusaidia popote pale, hata kampuni ya hapa nchini ikitaka kutengeneza pikipiki ikakwama kutengeneza injini, TISS inabidi iwe na uwezo wa kupata wapi la kupata ujuzi wa kutengeneza injini kwa namna yoyote ile. Ndio vitu duniani wanafanya, China mara nyingi tu unasikia wameiba TB za data kuhusu kitu fulani. Survival of the fittest
 
Back
Top Bottom