Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 15,280
- 9,719
Ndugu zangu Watanzania,
Hiyo ndio habari kuwa Rais wetu mpendwa kipenzi cha watanzania Mama Samia Suluhu Hasssan mama wa shoka, chuma cha Reli, shujaa wa Afrika, jasiri muongoza njia, simba wa nyika, komandoo wa vita, nyota ya matumaini na nuru ya wanyonge amemteua ndugu Ephraim Mafuru kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya utalii Tanzania.
Kabla ya uteuzi huo ndugu mafuru alikuwa ni mkurugenzi mtendaji wa kituo cha mikutano cha kimataifa Arusha. Anachukua nafasi ya ndugu Damas mfugale ambaye uteuzi wake umetenguliwa.
Nampongeza ndugu Mafuru kwa kupata heshima hii ya kipekee kabisa kuteuliwa kuongoza bodi ya utalii Tanzania kama mkurugenzi wake Mkuu. Rai yangu ni kumuomba kwenda kuchapa kazi kwa bidii ,maarifa na juhudi kubwa sana na kutoa mchango wake chanya katika kuhakikisha kuwa Secta ya utalii inaendelea kufanya vyema na watalii wanakuja kwa wingi nchini.
Hasa kwa kuzingatia ukweli kuwa tuna vivutio vingi sana vya utalii kuanzia mbuga za wanyama wa kila aina,milima,Kimondo cha Mbozi,n.k.ambapo tukivitagaza vizuri kimataifa basi tutafikisha watalii hadi million 5 kwa mwaka kutoka wa sasa ambao ni million moja na laki nane kwa mwaka.
Kikubwa ni kutumia watu wenye weledi na uzoefu na maarifa ya kutosha katika Secta hii ya utalii katika kutangaza vivutio vyetu. Mheshimiwa Rais tayari alishafungua njia katika kutangaza nchi yetu na vivutio vyake kupitia royal tour,kwa hiyo kazi iliyobaki kwa watendaji ni kuanzia pale alipoishia Mheshimiwa Rais.
Tuhakikishe kuwa Secta ya utalii inatupatia pesa za kigeni za kutosha,ajira kwa wingi kwa vijana wetu na mambo mengine mengi sana.wakati mwingine unawashawishi watu maarufu kama wacheza mpira wa kimataifa na wenye majina makubwa au wanamziki wa kimataifa au watu maarufu katika Secta Tofauti tofauti kuja nchini kutembelea vivutio vyetu bure kabisa .
ili wao wafanye kazi ya kututangazia vivutio vyetu kupitia kurasa zao za mitandao pomoja na matangazo kupitia video .kikubwa ni ubunifu katika kuhakikisha kuwa Tanzania inakuwa chaguo namba moja la watalii wanaotaka kuja kutembelea Bara la Afrika.
Lakini hapa pia ni lazima kama nchi tuhakikishe tunaboresha huduma za hoteli ,kwa kuhakikisha kuwa tunakuwa na hoteli za kisasa na hadhi ya kimataifa na zenye kutoa huduma bora na za kisasa.yaani mtu asijute kulipia dollar zake kuja nchini. Kuboresha miundombinu ya kwenda mbugani kwa kuhakikisha kuwa njia zinapitika bila shida msimu wote Masika na kiangazi,usalama kwa watalii,uaminifu kwa wafanyakazi wanaowapokea,kuwaongoza na kuwahudumia watalii ili hata wakirejea makwao basi waiseme e mema nchi yetu na kuwashawishi wengine kuja nchini.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
Hiyo ndio habari kuwa Rais wetu mpendwa kipenzi cha watanzania Mama Samia Suluhu Hasssan mama wa shoka, chuma cha Reli, shujaa wa Afrika, jasiri muongoza njia, simba wa nyika, komandoo wa vita, nyota ya matumaini na nuru ya wanyonge amemteua ndugu Ephraim Mafuru kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya utalii Tanzania.
Kabla ya uteuzi huo ndugu mafuru alikuwa ni mkurugenzi mtendaji wa kituo cha mikutano cha kimataifa Arusha. Anachukua nafasi ya ndugu Damas mfugale ambaye uteuzi wake umetenguliwa.
Nampongeza ndugu Mafuru kwa kupata heshima hii ya kipekee kabisa kuteuliwa kuongoza bodi ya utalii Tanzania kama mkurugenzi wake Mkuu. Rai yangu ni kumuomba kwenda kuchapa kazi kwa bidii ,maarifa na juhudi kubwa sana na kutoa mchango wake chanya katika kuhakikisha kuwa Secta ya utalii inaendelea kufanya vyema na watalii wanakuja kwa wingi nchini.
Hasa kwa kuzingatia ukweli kuwa tuna vivutio vingi sana vya utalii kuanzia mbuga za wanyama wa kila aina,milima,Kimondo cha Mbozi,n.k.ambapo tukivitagaza vizuri kimataifa basi tutafikisha watalii hadi million 5 kwa mwaka kutoka wa sasa ambao ni million moja na laki nane kwa mwaka.
Kikubwa ni kutumia watu wenye weledi na uzoefu na maarifa ya kutosha katika Secta hii ya utalii katika kutangaza vivutio vyetu. Mheshimiwa Rais tayari alishafungua njia katika kutangaza nchi yetu na vivutio vyake kupitia royal tour,kwa hiyo kazi iliyobaki kwa watendaji ni kuanzia pale alipoishia Mheshimiwa Rais.
Tuhakikishe kuwa Secta ya utalii inatupatia pesa za kigeni za kutosha,ajira kwa wingi kwa vijana wetu na mambo mengine mengi sana.wakati mwingine unawashawishi watu maarufu kama wacheza mpira wa kimataifa na wenye majina makubwa au wanamziki wa kimataifa au watu maarufu katika Secta Tofauti tofauti kuja nchini kutembelea vivutio vyetu bure kabisa .
ili wao wafanye kazi ya kututangazia vivutio vyetu kupitia kurasa zao za mitandao pomoja na matangazo kupitia video .kikubwa ni ubunifu katika kuhakikisha kuwa Tanzania inakuwa chaguo namba moja la watalii wanaotaka kuja kutembelea Bara la Afrika.
Lakini hapa pia ni lazima kama nchi tuhakikishe tunaboresha huduma za hoteli ,kwa kuhakikisha kuwa tunakuwa na hoteli za kisasa na hadhi ya kimataifa na zenye kutoa huduma bora na za kisasa.yaani mtu asijute kulipia dollar zake kuja nchini. Kuboresha miundombinu ya kwenda mbugani kwa kuhakikisha kuwa njia zinapitika bila shida msimu wote Masika na kiangazi,usalama kwa watalii,uaminifu kwa wafanyakazi wanaowapokea,kuwaongoza na kuwahudumia watalii ili hata wakirejea makwao basi waiseme e mema nchi yetu na kuwashawishi wengine kuja nchini.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.