Kigarama
JF-Expert Member
- Apr 23, 2007
- 2,492
- 1,230
Katika hatua za mapenzi kwenye mahusiano hakuna hatua ambayo ni tata kama pale kila mmoja anataka kutoka kwenye mahusiano yaliyopo lakini anajikuta anamhitaji mwenzake kwa ajili ya maisha "halisi" hivyo inambidi kubaki. Katika hatua hii ndipo baadhi ya wanandoa au walio katika mahusiano hutamani kuwa na mahusiano na watu wengine.
Lakini mahusiano hayo huwa si yale yenye lengo la kwenda mbele zaidi kwenye kuvunja mahusiano ya awali badala yake mahusiano hayo (yanaweza yasihusishe ngono) hutumika kujenga wivu kwa mume/mke au kwa Girlfriend/Boyfriend ili kufufua upendo uliopotea.
Bahati mbaya kuna watu wakiingizwa kwenye mahusiano ya aina hii wao hutaka kujenga kiota na kutamani kumpindua mhusika mpenzi wa awali. Haiwezekani kumpindua na katika mahusiano hatari na yenye kuchosha ni haya ya kuingilia kati uhusiano wenye upendo uliofiifia na wewe ukadhani utaweza kuteka moyo wa yule mliye kwenye mahusiano naye.
Kiukweli wewe unatumiwa kama Bakora tu ya kumchapia mpinzani wa huyo anayejidai uko naye kwenye mahusiano wakati yeye lengo lake ni kukutumia wewe kama silaha ya kumrejesha mpenzi wake anayeonekana kumponyoka.
Jihadhari!!
Lakini mahusiano hayo huwa si yale yenye lengo la kwenda mbele zaidi kwenye kuvunja mahusiano ya awali badala yake mahusiano hayo (yanaweza yasihusishe ngono) hutumika kujenga wivu kwa mume/mke au kwa Girlfriend/Boyfriend ili kufufua upendo uliopotea.
Bahati mbaya kuna watu wakiingizwa kwenye mahusiano ya aina hii wao hutaka kujenga kiota na kutamani kumpindua mhusika mpenzi wa awali. Haiwezekani kumpindua na katika mahusiano hatari na yenye kuchosha ni haya ya kuingilia kati uhusiano wenye upendo uliofiifia na wewe ukadhani utaweza kuteka moyo wa yule mliye kwenye mahusiano naye.
Kiukweli wewe unatumiwa kama Bakora tu ya kumchapia mpinzani wa huyo anayejidai uko naye kwenye mahusiano wakati yeye lengo lake ni kukutumia wewe kama silaha ya kumrejesha mpenzi wake anayeonekana kumponyoka.
Jihadhari!!