Usijenge kiholela, tambua mambo muhimu kuhusu kibali cha Ujenzi

figganigga

JF-Expert Member
Oct 17, 2010
25,492
54,895
USIJENGE KIHOLELA, TAMBUA MAMBO HAYA MUHIMU KUHUSU 'KIBALI CHA UJENZI'

1. KIBALI CHA UJENZI
Kulingana na sheria ya ujenzi wa majengo Mijini si ruhusa kwa mtu yeyote kujenga au kuanza kujenga jengo bila ya:-
(i) Kutuma maombi kwa mamlaka ya mji
(ii) Kuwasilisha michoro ya jengo na kumbukumbu husika
(iii) Kupata kibali kwa maandishi kinachoitwa “Kibali Cha ujenzi”

2. KIBALI CHA AWALI (Planning consent)
Inashauriwa kupata kibali cha awali kabla ya kuomba kibali cha ujenzi. Hivyo muendelezaji anatakiwa aandae mchoro wa awali (Outland plan) kwa utaratibu unaotakiwa ukionyesha aina ya ujenzi atakaokusudia kufanya ili aweze kupata ridhaa ya kuendelea na hatua za kuandaa michoro ya mwisho.
Faida:
• Kuokoa muda na gharama iwapo michoro ya mwisho itaonekana kuwa na dosari za kitaalam ambazo zitahitaji kufanyiwa marekebisho.
•Kuwa na uhakika kuhusu mahitaji muhimu ya kuzingatiwa wakati michoro inaandaliwa.

3. JINSI YA KUWASILISHA MAOMBI YA KIBALI CHA UJENZI
Baada ya michoro kukamilika, iwasilishwe ikiwa kwenye majalada kwa namna ambayo inaweza kufunguliwa na kusomeka. Michoro hiyo iwasilishwe ifuatavyo:-
• Seti tatu za michoro ya jengo (Archectural drawing)
• Seti mbili za michoro ya vyuma/mihimili (structural drawings) kwa michoro ya ghorofa

4. MICHORO ILIYOANDALIWA IONYESHE NINI
Michoro itakayoandaliwa inatakiwa ionyeshe mambo yafuatayo:-
• Namna jengo litakavyokuwa (plans, sections, elevations, foundation and roof plan)
• Namba na eneo la kiwanja kilipo
• Jina la mmilikaji ardhi inayohusika
• Jina la mchoraji, ujuzi na anwani
• Ukubwa wa jengo kwa mita za mraba
• Ujazo wa kiwanja (Plot coverage)
• Uwiano (Plot ratio)
• Matumizi yanayokusudiwa
• Idadi ya maegesho yatakayokuwepo
• Umbali wa jengo kutoka kwenye mipaka ya kiwanja (setbacks)
• Mfumo wa kutoa maji taka hadi kwenye mashimo

5. VIAMBATANISHO
• Fomu za maombi zilizojazwa kwa usahihi
• Hati ya mmiliki wa kiwanja au barua ya toleo
• Kumbumbuku nyingine zinazohusu kiwanja hicho kama hati za mauzo, makabidhiano n.k
• Nakala za risiti ya kodi ya kiwanja na kodi ya majengo
• Mabadiliko ya matumizi ya ardhi

6. HATUA ZINAZOFUATWA KATIKA KUSHUGHULIKIA MAOMBI YA KIBALI
Zifuatazo ni hatua zinazofuatwa wakati wa kuchunguza michoro hiyo:-
• Uhakiki wa miliki
• Kukaguliwa usanifu wa michoro
• Kukagua kiwanja kinachokusudiwa kuendelezwa
• Uchunguzi wa matumizi ya jengo na uwiano
• Uchunguzi wa maofisa wa afya
• Uchunguzi wa mipango ya uondoaji maji taka
• Uchunguzi wa tahadhali za moto
• Uchunguzi wa uimara wa jingo
• Kuwasilishwa kwenye kikao cha Mipangomiji na Mazingira baada ya kukamilisha taratibu zote
• Hatimaye kuandika na kutoa kibali

7. TARATIBU ZA KUFUATA BAADA YA KUPATA KIBALI CHA UJENZI

Kwa mujibu wa sheria ya ujenzi mijini ujenzi wowote ambao
umepata kibali unapaswa kukaguliwa kwa kila hatua ya ujenzi. Baada ya kupata kibali cha ujenzi mambo yafuatayo yanapaswa kufanyika:-
1. Kutoa notisi ya masaa 48 kabla ya kuanza ujenzi. Fomu ya notisi hii utapatiwa unapokabidhiwa kibali cha ujenzi
2. Kujaza fomu ya ukaguzi na kuwasilisha kwenye ofisi ya ujenzi ili hatua hiyo ya ujenzi unayotaka kufanya ikaguliwe
3. Utapatiwa “Certificate of Occupation” baada ya ujenzi wako kukamilika iwapo tu hatua muhimu za ujenzi zimekaguliwa

8. FAIDA ZA KUJENGA NYUMBA IKIWA NA KIBALI CHA UJENZI
1. Kuishi kwenye nyumba ambayo imethibitishwa kitaalamu kuwa ni salama
2. Kuwa na mazingira bora kwa kuwa na mji uliopangwa
3. Kuepuka hasara na usumbufu unaoweza kutokea iwapo ujenzi umefanyika bila kibali ikiwa pamoja na kushitakiwa mahakamani, kuvunjiwa na kulipa gharama za uvunjaji.

Hayo ndio Mambo muhimu ya kuyafahamu kuhusu 'Kibali cha Ujenzi' (Building Permit), Epuka usumbufu fuata sheria!.
 
Haya maelezo watu inapaswa tupewe na serikali za mitaa.
 
Hatua hizo ni nzuri na hongera kwa elimu hii mujarabu kabisa.

Ila tatizo , Tanroads na baadhi ya watendaji wa serikali wanajikurupukia tu na kubomoa.

Maana, wapo wengi wamefata hatua hizo zote ila leo tunavyoandika hapa wanazungumza lugha ya kuomboleza.
 
wahusika wenyewe wa kutoa kibali cha ujenzi hawaekewi haya maelekezo, ma afisa ardhi ndo kabisaaa wao wanajua kuiba viwanja na kuuuza/kujenga kinyemela

kifupi hayà mambo yapo kwenye makaratasi na sio hali halisi mtaani
 
USIJENGE KIHOLELA, TAMBUA MAMBO HAYA MUHIMU KUHUSU 'KIBALI CHA UJENZI'

1. KIBALI CHA UJENZI
Kulingana na sheria ya ujenzi wa majengo Mijini si ruhusa kwa mtu yeyote kujenga au kuanza kujenga jengo bila ya:-
(i) Kutuma maombi kwa mamlaka ya mji
(ii) Kuwasilisha michoro ya jengo na kumbukumbu husika
(iii) Kupata kibali kwa maandishi kinachoitwa “Kibali Cha ujenzi”

2. KIBALI CHA AWALI (Planning consent)
Inashauriwa kupata kibali cha awali kabla ya kuomba kibali cha ujenzi. Hivyo muendelezaji anatakiwa aandae mchoro wa awali (Outland plan) kwa utaratibu unaotakiwa ukionyesha aina ya ujenzi atakaokusudia kufanya ili aweze kupata ridhaa ya kuendelea na hatua za kuandaa michoro ya mwisho.
Faida:
• Kuokoa muda na gharama iwapo michoro ya mwisho itaonekana kuwa na dosari za kitaalam ambazo zitahitaji kufanyiwa marekebisho.
•Kuwa na uhakika kuhusu mahitaji muhimu ya kuzingatiwa wakati michoro inaandaliwa.

3. JINSI YA KUWASILISHA MAOMBI YA KIBALI CHA UJENZI
Baada ya michoro kukamilika, iwasilishwe ikiwa kwenye majalada kwa namna ambayo inaweza kufunguliwa na kusomeka. Michoro hiyo iwasilishwe ifuatavyo:-
• Seti tatu za michoro ya jengo (Archectural drawing)
• Seti mbili za michoro ya vyuma/mihimili (structural drawings) kwa michoro ya ghorofa

4. MICHORO ILIYOANDALIWA IONYESHE NINI
Michoro itakayoandaliwa inatakiwa ionyeshe mambo yafuatayo:-
• Namna jengo litakavyokuwa (plans, sections, elevations, foundation and roof plan)
• Namba na eneo la kiwanja kilipo
• Jina la mmilikaji ardhi inayohusika
• Jina la mchoraji, ujuzi na anwani
• Ukubwa wa jengo kwa mita za mraba
• Ujazo wa kiwanja (Plot coverage)
• Uwiano (Plot ratio)
• Matumizi yanayokusudiwa
• Idadi ya maegesho yatakayokuwepo
• Umbali wa jengo kutoka kwenye mipaka ya kiwanja (setbacks)
• Mfumo wa kutoa maji taka hadi kwenye mashimo

5. VIAMBATANISHO
• Fomu za maombi zilizojazwa kwa usahihi
• Hati ya mmiliki wa kiwanja au barua ya toleo
• Kumbumbuku nyingine zinazohusu kiwanja hicho kama hati za mauzo, makabidhiano n.k
• Nakala za risiti ya kodi ya kiwanja na kodi ya majengo
• Mabadiliko ya matumizi ya ardhi

6. HATUA ZINAZOFUATWA KATIKA KUSHUGHULIKIA MAOMBI YA KIBALI
Zifuatazo ni hatua zinazofuatwa wakati wa kuchunguza michoro hiyo:-
• Uhakiki wa miliki
• Kukaguliwa usanifu wa michoro
• Kukagua kiwanja kinachokusudiwa kuendelezwa
• Uchunguzi wa matumizi ya jengo na uwiano
• Uchunguzi wa maofisa wa afya
• Uchunguzi wa mipango ya uondoaji maji taka
• Uchunguzi wa tahadhali za moto
• Uchunguzi wa uimara wa jingo
• Kuwasilishwa kwenye kikao cha Mipangomiji na Mazingira baada ya kukamilisha taratibu zote
• Hatimaye kuandika na kutoa kibali

7. TARATIBU ZA KUFUATA BAADA YA KUPATA KIBALI CHA UJENZI

Kwa mujibu wa sheria ya ujenzi mijini ujenzi wowote ambao
umepata kibali unapaswa kukaguliwa kwa kila hatua ya ujenzi. Baada ya kupata kibali cha ujenzi mambo yafuatayo yanapaswa kufanyika:-
1. Kutoa notisi ya masaa 48 kabla ya kuanza ujenzi. Fomu ya notisi hii utapatiwa unapokabidhiwa kibali cha ujenzi
2. Kujaza fomu ya ukaguzi na kuwasilisha kwenye ofisi ya ujenzi ili hatua hiyo ya ujenzi unayotaka kufanya ikaguliwe
3. Utapatiwa “Certificate of Occupation” baada ya ujenzi wako kukamilika iwapo tu hatua muhimu za ujenzi zimekaguliwa

8. FAIDA ZA KUJENGA NYUMBA IKIWA NA KIBALI CHA UJENZI
1. Kuishi kwenye nyumba ambayo imethibitishwa kitaalamu kuwa ni salama
2. Kuwa na mazingira bora kwa kuwa na mji uliopangwa
3. Kuepuka hasara na usumbufu unaoweza kutokea iwapo ujenzi umefanyika bila kibali ikiwa pamoja na kushitakiwa mahakamani, kuvunjiwa na kulipa gharama za uvunjaji.

Hayo ndio Mambo muhimu ya kuyafahamu kuhusu 'Kibali cha Ujenzi' (Building Permit), Epuka usumbufu fata sheria!.


Naona process ni ndefu na gharama kubwa kuliko jengo, na hapo hujataja rushwa kwa maafisa ardhi
 
Back
Top Bottom