USHINDI wa Obama ni fundisho kwa wapinzani nchini Tanzania

Seriously wewe ni katibu mwenezi wa CCM?Why talking rubbish na mnajua chaguzi zote mnazoshiriki Tanzania ni rushwa,ngono na vurugu tupu.Usijaribu kulinganisha chaguzi za mareekani na TZ.I am sure hukupata baraka za your bosses kuandika huu uchafu ingawa nao thinking yao finyu.
 
Ni kweli iwapo CCM haitadiriki Wizi wa kura, Vitisho, Uongo na Rushwa! Muwe wakweli na Mungu atawabariki kinyume chake mtalanika

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums
 
- Now look ninatakiwa kujadili na Great Thinker anayetumia hoja za kusikia, ndio maana nikiondoka mnaaanza kulia lia rudi rudi, wewe jifunze hoja zako m,wenyewe sio za kusikia sikia maana huo ni umbeya na hapa mjini haufai sana, unaweza kuishia kuvalishwa shanga mwanaume mzima!! ha! ha! ha! ha!

le mutuz!!
babuuuuu!
 
- Now look ninatakiwa kujadili na Great Thinker anayetumia hoja za kusikia, ndio maana nikiondoka mnaaanza kulia lia rudi rudi, wewe jifunze hoja zako m,wenyewe sio za kusikia sikia maana huo ni umbeya na hapa mjini haufai sana, unaweza kuishia kuvalishwa shanga mwanaume mzima!! ha! ha! ha! ha!

le mutuz!!

halafu unajiita kiongozi wa taifa jumuiya ya wazazi kwa hizi pumba zako.!!!!!
 
Ushindi wa Obama dhidi ya Romney ni fundisho zuri kwa upinzani nchini kwetu kama wataamua kujifunza, mafunzo muhimu sana kwa washindani wa kisiasa ni pamoja na;

1. Kiwango cha utekelezaji wa ahadi mbalimbali na mipango (Ilani ya uchaguzi) kwa wananchi ina nguvu kubwa katika kuwafanya wapiga kura kuamua nani wa kumpa kura wakati wa kupiga kura..... Kupigia kura mabadiliko au la....

2. Kelele nyngi na wingi wa wapiga kelele si kigezo cha kupata kura nyingi siku ya kupigiwa kura......mikakati na ukaribu na wapiga kura ambao huonyesha ni kiasi gani Chama kiko karibu na kuzijua changamoto zinazowakabili wapiga kura ni moja ya misingi mikubwa...

3. Kutumia muda mwingi kuponda mafanikio yaliyopatikana kwenye kipindi cha mshindani wako...hasa aliyeko madarakani hakusaidii kukufanya upate kura bali wenye akili zao wataona unawadharau na kuwaona wajinga kama vile hawaoni yaliyofanyika.....ndicho kilichommaliza Romney...

4. Lakini ushindi kwa Obama ni dalili njema za kukubalika kwa fikra za kijamaa kwa Taifa kubwa na la kibepari duniani.....sasa tizameni upya itikadi zenu........


NAPE TOFAUTISHA UCHAGUZI WA USA NA TANZANIA, KAMA KWELI ZIMO KICHWANI NA UNASEMA ULISOMA INDIA DEGREE SIJUI NI YA CCM AU MASABURI. USA UWEZI LINGANISHA NA TANZANIA UCHAGUZI ULIOPITA ULIONA MATOKEO YALIVYOPINDISHWA NA TUME YA UCHAGUZI KWA MAKUSUDI KUMPA USHINDI KIKWETE NA KUMNYIMA Dr. SLAA USHINDI WAKE. KUFIKA HAPO WALIPO WAMAREKANI JASHO LILIWATOKA MAANA MAMBO YALIKUWA KAMA YA CCM LAKINI BAADA YA CIVIL WAR MAMBO YAKAWA SHWARI MPAKA LEO. NA CCM ITAENDELEA KUKANDAMIZA UPINZANI MPAKA HAPO WANANCHI WATASEMA INATOSHA NA KUAMUA KUCHUKUA RUNGU MKONONI (CIVIL WAR). NA SASA HIVI CCM IMEKUWA KAMA UONGOZI WA KIFALME ALIYE NJE YA UKOO WA KIFALME HATA KAMA NI KIPANGA KIASI GANI ATAONEKANA KAMA CHOO CHA MANZESE AU MAGOMENI MAKUTI. HATA KAMA UTAKUWA NA ELIMU KIASI GANI UWEZI PATA NAFASI YEYOTE YA MAANA SERIKALINI AU MASHIRIKA YA SERIKALI, BALI WALIYOTOKA KWENYE KOO ZA KIFALME NDO WANAPEWA NAFASI NZURI NA NYETI SERIKALINI. PIA NDO MAANA MADUDU YAMEKUWA MENGI SANA SERIKALINI KWA SABABU YA KUPEANA NAFASI KWA KUJUANA BILA KUFUATA QUALIFICATION ZA MTU NA UWEZO WAKE.
 
Nyani Ngabu
ahaaa haaa your man Mitt was scared to come out to give some words!! Never underestimates the power of Chicago political machines; can`t believe the shit Fox News was making this re election harder for Obama look at the number!

Chama
Gongo la mboto DSM
 
Ushindi wa Obama dhidi ya Romney ni fundisho zuri kwa upinzani nchini kwetu kama wataamua kujifunza, mafunzo muhimu sana kwa washindani wa kisiasa ni pamoja na;

1. Kiwango cha utekelezaji wa ahadi mbalimbali na mipango (Ilani ya uchaguzi) kwa wananchi ina nguvu kubwa katika kuwafanya wapiga kura kuamua nani wa kumpa kura wakati wa kupiga kura..... Kupigia kura mabadiliko au la....

2. Kelele nyngi na wingi wa wapiga kelele si kigezo cha kupata kura nyingi siku ya kupigiwa kura......mikakati na ukaribu na wapiga kura ambao huonyesha ni kiasi gani Chama kiko karibu na kuzijua changamoto zinazowakabili wapiga kura ni moja ya misingi mikubwa...

3. Kutumia muda mwingi kuponda mafanikio yaliyopatikana kwenye kipindi cha mshindani wako...hasa aliyeko madarakani hakusaidii kukufanya upate kura bali wenye akili zao wataona unawadharau na kuwaona wajinga kama vile hawaoni yaliyofanyika.....ndicho kilichommaliza Romney...

4. Lakini ushindi kwa Obama ni dalili njema za kukubalika kwa fikra za kijamaa kwa Taifa kubwa na la kibepari duniani.....sasa tizameni upya itikadi zenu........

Ndugu yangu Nape.
Salaaam.
Inawezekana unafahamu vizuri siasa za USA na TANZANIA, lakini kwa uzi wako unajaribu kuleta yale yasiyo na MASHIKO.
1. Siasa za USA ni za uwazi sana kuanzia mgombea mwenyewe, mali zake na pesa za kampeini zitakazotumika. NYIE CCM HILO HAMUWEZI NA HAMTAKI LIWEPO LA UWAZI NDIO MAANA HATA GAMBA ULILOTAKA WAJIVUE MAFISADI SASA HIVI UMEUZA KIBAO.
2. USA ndilo taifa linalotoa misaada mingi duniani na wanayo akiba kubwa ya raslimali (MAFUTA, MADINI NK) Hapa kwetu Tanzania pamoja kuwa tunazo raslimali kuanzia za misitu,gesi, samaki, dhahabu,tanzanite, almasi lakini hatujulikani kutoa misaada kama USA matokeo yake tunaomba huko. CCM yako imehodhi kila kitu.
3. USA wanazo sera ambazo ni za kitaifa hasa kwa maslahi yao hapa kwetu CCM kila kitu imewapa WAARABU kuanzia twiga, faru, na wanyama wengine, madini kila ajaye na sura ya kuwapa hela ya uchaguzi anapata MGODI.
4. USA hakuna sera ya kubagua jimbo la upinzani kutopeleka maendeleo, hapa CCM ikishaona kata ni ya upinzani hakuna kupeleka kitu pale, sasa mkishatoka Madarakani tunafikiri tutakaa nanyi mkiwa hampo ikulu tupange sera hizo unazotamani, mie sijaenda USA lakini wewe unaenda kama utakavyo kwa ajili ya chama.
USHINDI WA OBAMA NI KWA AJILI YA AMERIKA SIYO KWETU TANZANIA NDUGU NAPE.
 
ccm ndo wanapaswa wajifunze na huu uchaguzi,hatujasikia mabavu,rushwa,wizi wa kula, obama alikuwa tayari kwa lolote,na imekuwa bahati kashinda,sio magamba ambao wapo kuzuia kila kitu ili wahakikishe wanashinda.
 
Ama kweli Nape unachekesha!! Uchaguzi wa juzi 2010 Tido alijaribu japo kuwaweka wagombea wote kwenye Mdahalo ili wenye akili zao waweze kutumia fursa yao ya kidemokrasia kuwahoji na kuwapima uwezo wao na nia yao kugombea, na nyie CCM mlifanya nini?? Na baada ya uchaguzi mlimfanya nini Tido??
Muhimu ni sie sote tujifunze kupitia uchaguzi huu wa Marekani ili kupitia utengenezaji wa Katiba mpya tuweze kuweka mazingira ya Demokrasia ya kweli na itakayofanikisha Chaguzi zetu kuwa Huru na za Haki!!
 
Mr. Nape, nimepata wasiwasi mkubwa sana na uwezo wako wa kufikiri na kuchambua mambo haya ya kisiasa. nadhani hauna uwezo au unafanya makusudi kwa sababu ya unafiki. hivi kweli unaweza linganisha siasa huru za Marekani na siasa za Tanzania ambapo ni rahisi mshindi kunyang'anywa ushindi kwa kutumia pesa chafu (rushwa). Umesahau jinsi pesa za EPA zilivyomuingiza Kikwete Madarakani? Umesahau ushindi wa utata wa Kikwete katika kipindi chake cha pili? umesahau Dr. Ulimboka alivyopigwa karibu kufa na hakuna aliyechukuliwa hatua? Kisa kudai haki za afya! Umesahau mauaji ya wananchi na mwandishi wa habari yaliyofanywa na polisi kwa sababu za kisiasa?

nakuhakikishia Nape, kuwa kama mtaendelea kushinda si kwa haki bali kwa hila zenu zile zile za kuwahadaa wananchi. Unakumbukwa mlivyoeneza siasa za kidini kuhusu CUF kuwa ni chama cha kidini (kiislamu)? unakumbuka uchaguzi wa 2010 mlivyoeneza propaganda kuwa CDM ni chama cha kidini (Kikatoliki)?

Kama vile haitoshi chama chako kimeendelea kuonyesha udhaifu mkubwa katika kushughulikia masuala ya rushwa. rushwa imekuwa sehemu ya maisha ya wanaCCM? Suala la magamba limefikia wapi? Una msimamo gani juu ya Lowassa na wenzake? Je bado ni magamba? Katika hili ninakuona mnafiki mkubwa wa kisiasa unayetakiwa kupuuzwa na Watanzania wote.

Mungu ibariki Tanzania!
Mungu waumbue wanafiki wa kisiasa kama Nape Moses Nnauye!
Mungu tupe Ufumbuzi wa matatazo lukuki! uchumi, mfumuko wa bei, mafuta n.k.
Mungu tupe ukombozi wa kweli!
 
ushindi wa obama dhidi ya romney ni fundisho zuri kwa upinzani nchini kwetu kama wataamua kujifunza, mafunzo muhimu sana kwa washindani wa kisiasa ni pamoja na;

1. Kiwango cha utekelezaji wa ahadi mbalimbali na mipango (ilani ya uchaguzi) kwa wananchi ina nguvu kubwa katika kuwafanya wapiga kura kuamua nani wa kumpa kura wakati wa kupiga kura..... Kupigia kura mabadiliko au la....

2. Kelele nyngi na wingi wa wapiga kelele si kigezo cha kupata kura nyingi siku ya kupigiwa kura......mikakati na ukaribu na wapiga kura ambao huonyesha ni kiasi gani chama kiko karibu na kuzijua changamoto zinazowakabili wapiga kura ni moja ya misingi mikubwa...

3. Kutumia muda mwingi kuponda mafanikio yaliyopatikana kwenye kipindi cha mshindani wako...hasa aliyeko madarakani hakusaidii kukufanya upate kura bali wenye akili zao wataona unawadharau na kuwaona wajinga kama vile hawaoni yaliyofanyika.....ndicho kilichommaliza romney...

4. Lakini ushindi kwa obama ni dalili njema za kukubalika kwa fikra za kijamaa kwa taifa kubwa na la kibepari
duniani.....sasa tizameni upya itikadi zenu........
kwa hali hiyo, unataka kumfananisha vasco/jk na obama? Kumbuka obama alitoa ahadi zinazotekelezeka ila nyinyi na vasco ahadi zenu hazitekelezeki hata kama tukiwaongezea miaka mingine 50, na pia obama he is the man of determination tofauti na wewe na wezi wenzio, nb ni aibu kiongozi wa nchi anatoa madini kwa kubadilishana na vyandarua na still mnaona yupo sawa, na sashivi akimaliza kuuza rasilmali zetu atawauza na nyie mavuvuzelawake. Ok sawa mwana ccj
 
Huo ujamaa gani unaousema baada ya kuvunja azimo la Arusha na kuanzisha azimio la Zanzibar ambalo lilibariki viongozi kujichotea mali na kujitajirisha na wasihojiwe?.
Kumbuka kilichompa Obama ushindi ni kura za vijana kwa sera zake za kujenga uchumi wa Marekani kwa kuanzia na middle class. Ni tofauti na hali halisi ya sera za CCM ambazo zinamjali sana mtu wa juu, kwa viongozi au watawala kuwa na dhana potofu kuwa ndio pekee wenye haki ya kumiliki raslimali za nchi na kuchota kila kitu huku watanzania wengi wa chini wakiogelea ktk dimbwi la umaskini.
Jiulize unafiki ulioje kumkumbatia Lowasa mwenye tuhuma ya rushwa huku akiendelea kuamini kuwa atakuwa Rais wa nchi hii ajaye?. CCM kimebaki kuwa chama cha malalamiko kwa kila mtu hadi mwenyekiti rushwa, rushwa, rushwa, huku wananchi wanaendelea kudanganywa kuwa rushwa inapigwa vita na hakuna hatua na nchi inaendelea kudidimia kwa rushwa.
Suluhu wananchi waamke na mwaka 2015 waseme hapana. Miaka 50 inatosha tuangalie upande mwingine wa shillingi.
Raslimali iliyopotea potelea mbali lakini tuanze na mfumo mpya utakaomfanya kila mwananchi ajione kuwa ana haki kwa raslimali za nchi hii.




Ungekuwa na busara ungesema FUNZO KWA SIASA ZA TANZANIA ila kwa kutumia neno upinzani umeonyesha udhaifu mkubwa sana Kaka, next time jaribu kujadili mambo kwa uhalisi maana huwezi kwa Mfano kuwaita Republican ni WAPINZANI (kwa jinsi ulivyochukulia) wale ni chama cha siasa sio kama siasa zenu za CCM za Maji taka
 
Huyu jamaaanatia kinyaa.....insikitisha kwamba ameshindwa upuuzi wake a umfukuz Lowasa kwnye chama. Come 2015, NAPE atakuwa aefngwa kwenye NEPI zake mweyewe, baada ya wenye Chama kumpiga chini na kumtafutia kesi.
Uchumiatumbo Kazi kweli kweli!
 
Back
Top Bottom