Wakuu natumaini mu wazima wa afya..!!
Bila kupoteza muda nianze moja kwa moja kuwaletea habari inayonisibu kuja hapa jamvin na kuomba ushauri. Ni hivi Miezi mitano ilopita nilipata mchumba na katika mahusiano yetu ikabidi ahamie sehemu nayokaa mpaka sahizi niko nae na ana ujauzito wa miezi mitatu. sasa kama mwezi mmoja umepita nimepata rafiki wa kimarekani toka huko pande za CLEVELAND,OHIO sasa tumewasiliana kwa muda na kunambia anatafuta mchumba na kutumiana picha pia na kunipa story zake yeye ni Assistant adviser wa Ohio hospital state University na mfanyabiashara pia Yupo cute sana iseeh, she is a DIVA.
Sasa katika kuwa tunwasiliana akavutika na mimi na anasema anataka aolewe na african man. tunachati sana na ananiahidi kunitumia visa fee na airfair ticket tukiendelea vizuri na atakuja Tanzania kuniona.Kaniahidi mambo kama siku nikienda USA atanipeleka Miami Beach,hollywood,na atanionesha sehemu nyingi USA za kutembelea na kuenjoy pia atanipikia american dishes na mambo mengine mazur mazuri tu.
Sasa tatizo linakuja kwa hapa akigundua kua nina binti naish nae na ana mimba yangu sijui itakuaje. Maana naona hii pia ni kama ticket ya kutua kwa Obama, the land of opportunity. Sasa wakuu nifanyeje ili nicheze kama pele maana huyu binti wa huku siwezi kumwacha kwani atapata shida akija kujifungua na life lake kwa ujumla.
Ushauri wenu wa muhimu ndo maana nimekuja hapa.
Ahsanteni.
Unachati na Emeka Ukechukwu, wakati wa kufanya mipango ya visa, utaambiwa utume dola 200 kwa ajili ya kufanyiwa mipango ya visa. Mwee mapenzi gani hayo yamekaa kama bongo movie
Tunza hiyo mimba bana na huyo mwenzako ili ajifungue salama salmini kisha mfunge pingu za maisha. Huyo Mmarekani achana naye.
ahsante mkuu your very wise..!! sasa watu wengine maneno sijui utaolewa sijui nini? thats what i came here for.
Tunza hiyo mimba bana na huyo mwenzako ili ajifungue salama salmini kisha mfunge pingu za maisha. Huyo Mmarekani achana naye.
Namuonea huruma aliyebeba mimba"""Kaniahidimambo kama siku nikienda
USA atanipeleka Miami Beach,hollywood, naatanionesha sehemu nyingi USA za kutembelea na kuenjoy pia atanipikia american dishes na mambomengine mazur mazuri tu.""""
kwa hiyo umedata na haya manen
utaolewa
Well said mkuu... Hebu nikimbushe ile methali, Heri ndege uliyenaye mkononi kuliko ndege aliye mwituni.
Sijui kama nimepatia...