Mganguzi
JF-Expert Member
- Aug 3, 2022
- 1,032
- 2,769
Nampenda sana mke wangu, inshort ni mrembo sana na amejaaliwa kila kitu ambacho mwanaume anakitaka kwa mwanamke na nimezaa naye mtoto mmoja.
Miezi mitatu iliyopita tulikuwa katika hali ya kutaniana, mimi nilikuja na vipimo vya HIV vile vya kuweka mdomoni, kuna jamaa yangu ni daktari alinipa pakiti kumi kama zawadi tu nikawa nimezitunza ndani.
Mimi huwa sina tabia za umalaya malaya halafu najiamini sana, ila sasa mwenzangu ndio nilikuwa simuamini sana kulingana na urembo wake na hata aina ya style yake ya maisha. Tukiwa katika utani kitandani tukaamua kupima, mimi ndio nilikuwa namlazimisha yeye japokuwa alikuwa hataki.
Ile tumepima tu tunasubiria majibu mimi nikatoka kwenda chumba cha watoto, dakika kumi nimerudi namkuta analia na ameshikilia vipimo vyote viwili anasema wewe umeathirika, kuangalia kipimo kimoja kinaonyesha positive na kingine negative, mimi nikawa sijui kipi ndio changu ila yeye amekomaa kwamba kile chenye ngoma ni changu.
Nikamuuliza kwa nini umevichanganya na hatukuviwekea alama? Ameweka msimamo kwamba mimi ndio muathirika, nimemuomba twende hospitali hataki, turudie kupima hataki, kunipa mapenzi hataki, muda wote anashinda amelala na hana amani kabisa, mimi najikuta mwenye furaha kama hakuna kilichotokea.
Kinachonipa tabu ni kunyimwa unyumba miezi mitatu na sijui nifanyeje!
Miezi mitatu iliyopita tulikuwa katika hali ya kutaniana, mimi nilikuja na vipimo vya HIV vile vya kuweka mdomoni, kuna jamaa yangu ni daktari alinipa pakiti kumi kama zawadi tu nikawa nimezitunza ndani.
Mimi huwa sina tabia za umalaya malaya halafu najiamini sana, ila sasa mwenzangu ndio nilikuwa simuamini sana kulingana na urembo wake na hata aina ya style yake ya maisha. Tukiwa katika utani kitandani tukaamua kupima, mimi ndio nilikuwa namlazimisha yeye japokuwa alikuwa hataki.
Ile tumepima tu tunasubiria majibu mimi nikatoka kwenda chumba cha watoto, dakika kumi nimerudi namkuta analia na ameshikilia vipimo vyote viwili anasema wewe umeathirika, kuangalia kipimo kimoja kinaonyesha positive na kingine negative, mimi nikawa sijui kipi ndio changu ila yeye amekomaa kwamba kile chenye ngoma ni changu.
Nikamuuliza kwa nini umevichanganya na hatukuviwekea alama? Ameweka msimamo kwamba mimi ndio muathirika, nimemuomba twende hospitali hataki, turudie kupima hataki, kunipa mapenzi hataki, muda wote anashinda amelala na hana amani kabisa, mimi najikuta mwenye furaha kama hakuna kilichotokea.
Kinachonipa tabu ni kunyimwa unyumba miezi mitatu na sijui nifanyeje!