Ushauri kwa Serikali: Chagueni viongozi na watu wenye upeo/maono/hoja kutoka JamiiForums

Donatila

JF-Expert Member
Oct 23, 2014
7,557
21,515
Habari wakuu,

Husika na kichwa cha habari hapo juu,

Nimewaza na kutafakari kuwa kama Taifa la Tanzania tuna watu wenye upeo na akili kubwa sana ila ni kama wamesahaulika.

Wapo watanzania ambao wanaonekana kuwa wana maono na upeo makubwa na kama wangepewa nafasi basi wangetufikisha kama Taifa mahali pazuri.

Nimekuwa msomaji wa muda mrefu sana hasa hapa JamiiForums na nimegundua hapa kuna watu ambao hawafahamiki ila kama watapewa nafasi ya kuongoza Taifa la Tanzania watalipeleka mahali.

Kama viongozi Serikali ya Tanzania wangekuwa na muda wa kupitia na kusoma hoja za watu huku JamiiForums Kuna watu wenye michango au maoni mazuri na hoja zenye tija kwa jamii na Taifa kwa ujumla.

Ifike mahali hata Rais awe anaangalia Hawa watu wanaotoka katika platform ya JamiiForums na kuwapa vitengo.

Kuna hoja huku zinatolewa na mwisho wa siku zimekuwa zikiibiwa na viongozi wengine na wanazifanyia kazi.

Sasa ni wakati wa Viongozi kutoka katika platform hii ya JamiiForums maana wana hoja za msingi kwa maendeleo la Taifa letu pendwa la Tanzania.

Sasa tumeona huko mitandao ya Instagram kuna viongozi wamechaguliwa kupitia hiyo mitandao.

Ni wakati wa kupenda mitandao yetu kama huku JamiiForums, wao wanafahamika kwa kuandika sio sura zao.

Watu hawa wamekuwa wakiandika vitu vyenye tija kuliko wale ambao wanajulikana kwa sura zao.

Wamekuwa wabunifu, wamekuwa na hoja zenye tija sana kwa uongozi wa Tanzania katika jamii na siasa.

Serikali fungueni macho yenu, hawa waliopo huku JamiiForums wanaupeo mkubwa katika kufikisha Tanzania kwenye Ile nchi yetu ya ahadi.

Niwashukuru sana Serikali ya Tanzania hasa kwa kufanyia kazi na hoja zinazowekwa huku JamiiForums.

Ni ombi langu kuona tunawapa nafasi na hawa watu waliopo JamiiForums.


Tunaweza wataja member hapa...

Donatila
 
Unapaswa ujue kuwa humu humu jf pia kuna viongozi wakubwa serikalini,na huenda wangejulikana kwa majina halisi na sura zao kama usemavyo basi wasingechangia hoja zao positively,hofu kubwa ukiwa kwenye mfumo na ukazungumza jambo lenye mashiko haijalishi ni la kiukosoaji moja kwa moja utaonekana unambeza aliyekupa nafasi ya uongozi,jambo la msingi acha tu serikali iendelee kuzifanyia kazi hoja zetu japo miongoni mwetu ni serikali pia ila kwa nafasi zetu bado ni wachanga kivyeo. Ibaki hivyo,watoto wetu waupate wa usiku na mchana na maisha yaendelee.
 
Unapaswa ujue kuwa humu humu jf pia kuna viongozi wakubwa serikalini,na huenda wangejulikana kwa majina halisi na sura zao kama usemavyo basi wasingechangia hoja zao positively,hofu kubwa ukiwa kwenye mfumo na ukazungumza jambo lenye mashiko haijalishi ni la kiukosoaji moja kwa moja utaonekana unambeza aliyekupa nafasi ya uongozi,jambo la msingi acha tu serikali iendelee kuzifanyia kazi hoja zetu japo miongoni mwetu ni serikali pia ila kwa nafasi zetu bado ni wachanga kivyeo. Ibaki hivyo,watoto wetu waupate wa usiku na mchana na maisha yaendelee.
Sio viongozi wengi...

Bado tunataka wenye hoja zinazotolewa wapewe nafasi wakasimamia hoja zao.
 
Wanaoandika hizo hoja wengi ni watu wa serikali wamejaa humu tele labda ungezungumzia wale verified members akina Pascal Mayala wateuliwe huko serikalini
 
Hao watu unawaina wana maono kwa sababu wapo nje ya mfumo wa uongozi Serikalini.. Na siku wakipewa teuzi hawatakuwa na tofauti kwani watakuwa wanautumika mfumo ulioasisiwa na CCM.

Dr. Ayoub Rioba & Bashiru Ally kabla ya kuingia kwenye siasa walikuwa ni watu makini na wenye maono chanya, lakini baada ya kupewa teuzi na kuingia kwenye mfumo wa CCM hawana tofauti na kina Wassira au Makamba wamebaki kumsifia Rais.

Tatizo la nchi yetu si watu bali ni mfumo wa katiba uliopo wa kila atakayeteuliwa anamtumikia Rais badala ya katiba.
 
"The problem of Africans, those with ideas have no power, and those with power have no ideas."

Kutokana na kuwepo kwa hali hii, watu ambao ni Wasomi na/au Wataalamu wenye mitazamo huru ktk bara hili la Afrika Wamefanywa kuwa ni Maadui Wakubwa wa Watawala waliopo Mamlakani. Wasomi wenye mitizamo huru wanaonekana kuwa ni tishio kubwa sana kwa Watawala na Utawala kwa ujumla wake, badala yake Wasomi hao wamekuwa wakipigwa vita vibaya sana na watawala.
 
Hao watu unawaina wana maono kwa sababu wapo nje ya mfumo wa uongozi Serikalini.. Na siku wakipewa teuzi hawatakuwa na tofauti kwani watakuwa wanautumika mfumo ulioasisiwa na CCM.

Dr. Ayoub Rioba & Bashiru Ally kabla ya kuingia kwenye siasa walikuwa ni watu makini na wenye maono chanya, lakini baada ya kupewa teuzi na kuingia kwenye mfumo wa CCM hawana tofauti na kina Wassira au Makamba wamebaki kumsifia Rais.

Tatizo la nchi yetu si watu bali ni mfumo wa katiba uliopo wa kila atakayeteuliwa anamtumikia Rais badala ya katiba.
Vizuri!
 
Sio viongozi wengi...

Bado tunataka wenye hoja zinazotolewa wapewe nafasi wakasimamia hoja zao.
Kipindi cha chaguzi mnajificha mtachaguliwaje mkuu?
Tujitokeze kugombea nafasi zozote za uongozi tukajenge hoja na tuzitetee hoja zetu HAKIKA TUTALETA MABADILIKO MAKUBWA NINA IMANI
 
Hao watu unawaina wana maono kwa sababu wapo nje ya mfumo wa uongozi Serikalini.. Na siku wakipewa teuzi hawatakuwa na tofauti kwani watakuwa wanautumika mfumo ulioasisiwa na CCM.

Dr. Ayoub Rioba & Bashiru Ally kabla ya kuingia kwenye siasa walikuwa ni watu makini na wenye maono chanya, lakini baada ya kupewa teuzi na kuingia kwenye mfumo wa CCM hawana tofauti na kina Wassira au Makamba wamebaki kumsifia Rais.

Tatizo la nchi yetu si watu bali ni mfumo wa katiba uliopo wa kila atakayeteuliwa anamtumikia Rais badala ya katiba.
Absolutely!

Katiba ya nchi yetu ndio chimbuko la tatizo hili baya. Na mbaya zaidi nchi yetu inafuata Sera, Itikadi na Falsafa ya utawala za Ujamaa/Ukomunisti.

Ukomunisti unaamini kwamba 'Raia wote' katika nchi ni "Mateka" wa "Mwenyekiti, " na Mwenyekiti ndio "mtu pekee" mwenye 'akili nyingi zaidi' katika nchi kuliko mtu mwingine yeyote yule. Hii ndio sababu ya kuanzishwa kwa Kaulimbiu iliyokuwa Maarufu sana enzi za Utawala wa Awamu ya Kwanza ya Mwl. J.K. Nyerere ya "Zidumu Fikra za Mwenyekiti."
 
Kipindi cha chaguzi mnajificha mtachaguliwaje mkuu?
Tujitokeze kugombea nafasi zozote za uongozi tukajenge hoja na tuzitetee hoja zetu HAKIKA TUTALETA MABADILIKO MAKUBWA NINA IMANI
"Changamoto kubwa iliyopo katika ulimwengu wa sasa ni kwamba, watu wenye akili nzuri hawataki kujihusisha na Siasa, hivyo, kuwapa mamlaka watu wasiokuwa na akili kuwatawala watu wenye akili na watu wasiokuwa na akili."
Donald Trump, aliyekuwa Rais wa 44 wa Marekani.
 
Ata viongozi wengi tu wana upeo mkubwa ila ukijaa kwenye mfumo wa chama cha mboga mboga akili zako ziache huko kijijini kwenu.
 
Back
Top Bottom