denooJ
JF-Expert Member
- Mar 31, 2020
- 18,511
- 68,150
Salaam.
Nimepata wazo la kumshauri Makamu Mwenyekiti wa Chadema, Mheshimiwa Tundu Lissu juu ya taarifa zake anazotoa kuwalenga baadhi ya viongozi wa serikali ya CCM, hasa awapo kwenye majukwaa ya siasa.
Jambo lililonisukuma zaidi kutoa ushauri huu, ni baada ya Lissu, jana akiwa kwenye mkutano wa siasa, kutoa madai kumhusu aliyekuwa Rais wa Tanzania, awamu ya tano, Marehemu John P. Magufuli.
Lissu kwenye mkutano huo alidai kwamba, Marehemu Magufuli alikutwa na kiasi kikubwa cha pesa nyumbani kwake, takriban dola za kimarekani milioni 42, ambazo ni sawa na Tsh.bilioni 100 za kitanzania.
Madai haya nikiyatazama kwa makini, nayaona yana tofauti kubwa na mengine yanayohusu mkataba wa hovyo wa bandari, mkataba ambao wengi wetu tumeuona, hivyo kusema neno lolote kali kuhusu mkataba ule, sio mbaya kwasababu ushahidi wake upo hadharani.
Lakini madai ya kumhusu Marehemu Magufuli, haya Lissu ameyatoa naamini kwa kuzingatia zaidi maneno ya kuambiwa, na bahati mbaya zaidi, hao waliomwambia juu ya hili ni wana CCM, ambao either wako idara ya Usalama, au huko chamani.
Hawa wanajua siku zote, jukumu lao la kwanza, lililo muhimu zaidi kwao, siku zote ni kulinda maslahi ya chama chao, hivyo wako radhi kufanya chochote ili kuhakikisha wanalinda heshima ya chama chao, na viongozi wao.
Sasa kwa hali hiyo, endapo Lissu atatakiwa kuthibitisha mahakamani juu ya madai yake kumhusu Marehemu Magufuli, na ushahidi wake akataka kuupata toka kwa hao hao CCM, ambao wamekuwa wakimpa taarifa nyeti kwa siri, naanza kuona Lissu anaweza kujikuta mtegoni mbele ya safari.
Mahakamani siku zote tunatakiwa ku prove beyond reasonable doubt, huwezi kumtuhumu Magufuli kisha utetezi wako uegemee kwenye upotevu wa pesa za Plea Bargaining, au kwenye uporaji waliofanyiwa wamiliki wa Bureau de Change, kama ambavyo nimeona wengi wetu humu wakiutumia.
Kufikia hapo, CCM wanaweza kumuwekea mtego Lissu, kisha wakafanikiwa kummaliza kabisa kisiasa, pale ambapo ushahidi atakaoutaka ili kuutoa mahakamani, hao rafiki zake wa CCM watakapogoma kumpa ushirikiano, kwa kuogopa wasijulikane kwa wakubwa zao.
Namshauri Lissu awe makini na maneno ya kuambiwa kisha kuyatoa majukwaani, sio kwa hili la Magufuli pekee, bali hata na mengine yajayo, ahakikishe kabla hajazungumza anakuwa na ushahidi wa kutosha mezani, ili endapo akitakiwa kuupeleka mahakamani, iwe rahisi kwake kufanya hivyo.
Naandika haya nikijua fika Lissu ni mwanasheria mzuri, tena mwenye uzoefu wa kutosha mahakamani, lakini waswahili husema ndege mjanja siku zote hunaswa na tundu bovu, akumbuke yupo kwenye mchezo wa siasa, mchezo ambao hauna rafiki wala adui wa kudumu, rafiki wa leo, kesho anaweza kugeuka adui yako.
Pia soma: Lissu: Dola za Kimarekani Milioni 42 (takribani Tsh. Bilioni 100) zilikutwa nyumbani kwa Magufuli baada ya kufariki
Nimepata wazo la kumshauri Makamu Mwenyekiti wa Chadema, Mheshimiwa Tundu Lissu juu ya taarifa zake anazotoa kuwalenga baadhi ya viongozi wa serikali ya CCM, hasa awapo kwenye majukwaa ya siasa.
Jambo lililonisukuma zaidi kutoa ushauri huu, ni baada ya Lissu, jana akiwa kwenye mkutano wa siasa, kutoa madai kumhusu aliyekuwa Rais wa Tanzania, awamu ya tano, Marehemu John P. Magufuli.
Lissu kwenye mkutano huo alidai kwamba, Marehemu Magufuli alikutwa na kiasi kikubwa cha pesa nyumbani kwake, takriban dola za kimarekani milioni 42, ambazo ni sawa na Tsh.bilioni 100 za kitanzania.
Madai haya nikiyatazama kwa makini, nayaona yana tofauti kubwa na mengine yanayohusu mkataba wa hovyo wa bandari, mkataba ambao wengi wetu tumeuona, hivyo kusema neno lolote kali kuhusu mkataba ule, sio mbaya kwasababu ushahidi wake upo hadharani.
Lakini madai ya kumhusu Marehemu Magufuli, haya Lissu ameyatoa naamini kwa kuzingatia zaidi maneno ya kuambiwa, na bahati mbaya zaidi, hao waliomwambia juu ya hili ni wana CCM, ambao either wako idara ya Usalama, au huko chamani.
Hawa wanajua siku zote, jukumu lao la kwanza, lililo muhimu zaidi kwao, siku zote ni kulinda maslahi ya chama chao, hivyo wako radhi kufanya chochote ili kuhakikisha wanalinda heshima ya chama chao, na viongozi wao.
Sasa kwa hali hiyo, endapo Lissu atatakiwa kuthibitisha mahakamani juu ya madai yake kumhusu Marehemu Magufuli, na ushahidi wake akataka kuupata toka kwa hao hao CCM, ambao wamekuwa wakimpa taarifa nyeti kwa siri, naanza kuona Lissu anaweza kujikuta mtegoni mbele ya safari.
Mahakamani siku zote tunatakiwa ku prove beyond reasonable doubt, huwezi kumtuhumu Magufuli kisha utetezi wako uegemee kwenye upotevu wa pesa za Plea Bargaining, au kwenye uporaji waliofanyiwa wamiliki wa Bureau de Change, kama ambavyo nimeona wengi wetu humu wakiutumia.
Kufikia hapo, CCM wanaweza kumuwekea mtego Lissu, kisha wakafanikiwa kummaliza kabisa kisiasa, pale ambapo ushahidi atakaoutaka ili kuutoa mahakamani, hao rafiki zake wa CCM watakapogoma kumpa ushirikiano, kwa kuogopa wasijulikane kwa wakubwa zao.
Namshauri Lissu awe makini na maneno ya kuambiwa kisha kuyatoa majukwaani, sio kwa hili la Magufuli pekee, bali hata na mengine yajayo, ahakikishe kabla hajazungumza anakuwa na ushahidi wa kutosha mezani, ili endapo akitakiwa kuupeleka mahakamani, iwe rahisi kwake kufanya hivyo.
Naandika haya nikijua fika Lissu ni mwanasheria mzuri, tena mwenye uzoefu wa kutosha mahakamani, lakini waswahili husema ndege mjanja siku zote hunaswa na tundu bovu, akumbuke yupo kwenye mchezo wa siasa, mchezo ambao hauna rafiki wala adui wa kudumu, rafiki wa leo, kesho anaweza kugeuka adui yako.
Pia soma: Lissu: Dola za Kimarekani Milioni 42 (takribani Tsh. Bilioni 100) zilikutwa nyumbani kwa Magufuli baada ya kufariki