Nafurahi sana ninapoona filamu za kitanzania zikizidi kupata umaarufu ndani na nje ya nchi. Siku hizi filamu nyingi za kibongo zinawekwa 'subtitles' za Kiingereza ili kuongeza uelewa katika lugha hiyo pia. Lakini sasa, hicho Kiingereza jamani kinachowekwa sijui ni makusudi au bahati mbaya! Ni 'broken' balaa! Kama sio makusudi, nawashauri kabla ya kuweka hizo 'subtitles' watafute wataalamu wa hiyo lugha wawasaidie, ni kitu cha kawaida, wasione aibu!