USHAURI: Ipelekwe Hoja Binafsi Bungeni- Wananchi wote waridhike

TUJITEGEMEE

JF-Expert Member
Nov 6, 2010
23,914
23,079
Nashauri ipelekwe Hoja Binafsi Bungeni(kwa mujibu wa taratibu za Bunge) -Bunge libatilishe Azimio lile na kisha, Makubaliano yaangaliwe upya pale ambapo panapigiwa kelele na wananchi hasa kipengere cha 23(4), na pengine pia parekebishwe na wananchi waridhike kuwa Sasa makubaliano yapo sawa. Kisha Bunge lipitishe Azimio lililorekebishwa ili serikali iendelee na mchakato unaofuata.

Hili jambo lisitupotezee muda tufanye marekebisho tusonge mbele. Tuna Mambo mengi ya kufanya kwa Kila mtu kwa nafasi yake alipo kuwawezesha watanzania wote kujiletea maendeleo kiuchumi na kiteknolojia.

Naamini viongozi wetu wote Wana kiu ya kuiletea maendeleo halisi ya kiuchumi na kiteknolojia Tanzania kwa manufaa ya watanzania wote. Na kwa msingi huo hoja yangu hii wataitazama na kuifikiria kwa uzito ambao wao wanaona inastahili.

Naomba kutoa hoja.
- - -
TUJITEGEMEE 25/06/2023.
 
Nashauri ipelekwe Hoja Binafsi Bungeni(kwa mujibu wa taratibu za Bunge) -Bunge libatilishe Azimio lile na kisha, Makubaliano yaangaliwe upya pale ambapo panapigiwa kelele na wananchi hasa kipengere cha 23(4), na pengine pia parekebishwe na wananchi waridhike kuwa Sasa makubaliano yapo sawa. Kisha Bunge lipitishe Azimio lililorekebishwa ili serikali iendelee na mchakato unaofuata.

Hili jambo lisitupotezee muda tufanye marekebisho tusonge mbele. Tuna Mambo mengi ya kufanya kwa Kila mtu kwa nafasi yake alipo kuwawezesha watanzania wote kujiletea maendeleo kiuchumi na kiteknolojia.

Naamini viongozi wetu wote Wana kiu ya kuiletea maendeleo halisi ya kiuchumi na kiteknolojia Tanzania kwa manufaa ya watanzania wote. Na kwa msingi huo hoja yangu hii wataitazama na kuifikiria kwa uzito ambao wao wanaona inastahili.

Naomba kutoa hoja.
- - -
TUJITEGEMEE 25/06/2023.
Sawa peleka wewe
 
Kuna tatizo gani kupeleka hoja binafsi kama hoja hii Ina mashiko?
 
Lolote litakalo faa kuondoka kwenye hili dudu sawa tuu.
Ni kweli Mkuu. Lakini sielewi Kuna nguvu gani ambayo baadhi ya viongozi wetu inawafanya wasione kuwa Kuna tatizo katika makubaliano haya.

Mfano, nimeona clip mbunge mmoja (Ni mama) alitaka kuonyesha kuwa Bunge limekosea kwenye maamuzi yake juu ya bandari lakini alikatishwa asiendelee kutoa hoja yake nadhani Hata kabla muda haujaisha.

Inasikitisha sana na inajenga chuki dhidi ya viongozi wa namna hii. Viongozi hawa wajirekebishe lengo wananchi wote kama nchi tusonge mbele kwa tabasamu.
 
Busara za wabunge, wakirudi majimboni zitumike kusikiliza nini wananchi wanataka kuhusu rasilimali zao hasa hili swagger la bandari and then wafanye rectification.
 
Ni kweli Mkuu. Lakini sielewi Kuna nguvu gani ambayo baadhi ya viongozi wetu inawafanya wasione kuwa Kuna tatizo katika makubaliano haya.

Mfano, nimeona clip mbunge mmoja (Ni mama) alitaka kuonyesha kuwa Bunge limekosea kwenye maamuzi yake juu ya bandari lakini alikatishwa asiendelee kutoa hoja yake nadhani Hata kabla muda haujaisha.

Inasikitisha sana na inajenga chuki dhidi ya viongozi wa namna hii.
Ni kweli, nguvu inayotumika kuzima hoja ya bandari dhidi ya ile ya serikali ni kubwa sana.

Hii ni ngoma nzito, chakushangaza husikii yale majarida kama the economist yaliyokuwa yakipiga kelele kila siku, kuhusu uwekezaji Tanzania wakati wa Magu. Je huu mnyororo wa wafaidika ni mrefu kiasi gani?
 
Naamini kabisa, mpaka sasa, kuna wengi wanaoona aibu kuu kwa kuruhusu ule ujinga kutokea ndani ya ardhi ya Tanganyika yetu, wakiongozwa na Samia.
 
....husikii yale majarida kama the economist yaliyokuwa yakipiga kelele kila siku, kuhusu uwekezaji Tanzania....
Kweli inashangaza sana. Au aina hii ya uwekezaji wa "DP kuwa na haki wakati mwenye mali ndiye anawajibika bila haki" (hii ni kwa mujibu wa maelezo ya Prof. Shivji) ndiyo walikuwa wanataka ?

Kama ndiyo, jambo lifanyike.
 
....kuna wengi wanaoona aibu kuu kwa kuruhusu ule ujinga kutokea....
Wana msemo wao kuwa "hii nayo ni hewa inayotembea hivyo itapita". Sidhani kama Wana aibu. Pia katika hili mtoe Kiongozi wa nchi tafadhali maana anahimiza staha katika kutoa maoni.
 
Kweli inashangaza sana. Au aina hii ya uwekezaji wa "DP kuwa na haki wakati mwenye mali ndiye anawajibika bila haki" (hii ni kwa mujibu wa maelezo ya Prof. Shivji) ndiyo walikuwa wanataka ?

Kama ndiyo, jambo lifanyike.
Zamani tulikuwa tunawacheka wakenya na wanaigeria jinsi nchi zao zinavyotanfunwa ila sasa tumewazidi.
 
Hiawezekani, maagizo kutoka juu yashafanyika...
Inawezekana Mkuu, ushauri umeishatolewa wa namna inavyowezekana.


Niliwahi kumsikia Professor Kabudi anasema ni Bora tuwapatie Watanganyika Tanganyika Yao wakati Watanganyika bado kuihitaji kuliko kusubiri watanganyika waanze kuidai Tanganyika.

Katika hili pia ni Bora Bunge likarejea kwa hati za Dharura (nadhani Kuna namna ya utaratibu wa kuitisha Bunge kwa Dharura) ili jambo hili lirekebishwe kabla wananchi hawajataka kulilazimisha Bunge hilo kufanya kazi hiyo ya marekebisho!!

Nawaza pia.
 
Nashauri ipelekwe Hoja Binafsi Bungeni(kwa mujibu wa taratibu za Bunge) -Bunge libatilishe Azimio lile na kisha, Makubaliano yaangaliwe upya pale ambapo panapigiwa kelele na wananchi hasa kipengere cha 23(4), na pengine pia parekebishwe na wananchi waridhike kuwa Sasa makubaliano yapo sawa. Kisha Bunge lipitishe Azimio lililorekebishwa ili serikali iendelee na mchakato unaofuata.

Hili jambo lisitupotezee muda tufanye marekebisho tusonge mbele. Tuna Mambo mengi ya kufanya kwa Kila mtu kwa nafasi yake alipo kuwawezesha watanzania wote kujiletea maendeleo kiuchumi na kiteknolojia.

Naamini viongozi wetu wote Wana kiu ya kuiletea maendeleo halisi ya kiuchumi na kiteknolojia Tanzania kwa manufaa ya watanzania wote. Na kwa msingi huo hoja yangu hii wataitazama na kuifikiria kwa uzito ambao wao wanaona inastahili.

Naomba kutoa hoja.
- - -
TUJITEGEMEE 25/06/2023.
Soma lwamza 23 (3)
 
Busara za wabunge, wakirudi majimboni zitumike kusikiliza nini wananchi wanataka kuhusu rasilimali zao hasa hili swagger la bandari and then wafanye rectification.
Hii ni Taxzania sidhani kama kuna utaratibu wabunge huutumia kuongea na wanachi kujua misimamo yao ila wabunge wengi hufanya na kuzungumza mengi kwa utashi wao kisiasa na faida zao, ; mfano : mbunge analilia wizara ya maji kwa kujua atafaidika na kura za wananchi ili aendelee kupiga posho ila kwa swala la bandari tujiangalie upya namkumbuka sana Hayati Magufuli asingetupeleka huko.
 
Nashauri ipelekwe Hoja Binafsi Bungeni(kwa mujibu wa taratibu za Bunge) -Bunge libatilishe Azimio lile na kisha, Makubaliano yaangaliwe upya pale ambapo panapigiwa kelele na wananchi hasa kipengere cha 23(4), na pengine pia parekebishwe na wananchi waridhike kuwa Sasa makubaliano yapo sawa. Kisha Bunge lipitishe Azimio lililorekebishwa ili serikali iendelee na mchakato unaofuata.

Hili jambo lisitupotezee muda tufanye marekebisho tusonge mbele. Tuna Mambo mengi ya kufanya kwa Kila mtu kwa nafasi yake alipo kuwawezesha watanzania wote kujiletea maendeleo kiuchumi na kiteknolojia.

Naamini viongozi wetu wote Wana kiu ya kuiletea maendeleo halisi ya kiuchumi na kiteknolojia Tanzania kwa manufaa ya watanzania wote. Na kwa msingi huo hoja yangu hii wataitazama na kuifikiria kwa uzito ambao wao wanaona inastahili.

Naomba kutoa hoja.
- - -
TUJITEGEMEE 25/06/2023.
Prof Shivji: Bunge Linaweza kufuta Azimio lake lenye kuazimia mkataba na DP World.

Hii ni Moja ya njia chache kuvunja mkataba huu na kuanza UPYA.
 
Nashauri ipelekwe Hoja Binafsi Bungeni(kwa mujibu wa taratibu za Bunge) -Bunge libatilishe Azimio lile na kisha, Makubaliano yaangaliwe upya pale ambapo panapigiwa kelele na wananchi hasa kipengere cha 23(4), na pengine pia parekebishwe na wananchi waridhike kuwa Sasa makubaliano yapo sawa. Kisha Bunge lipitishe Azimio lililorekebishwa ili serikali iendelee na mchakato unaofuata.

Hili jambo lisitupotezee muda tufanye marekebisho tusonge mbele. Tuna Mambo mengi ya kufanya kwa Kila mtu kwa nafasi yake alipo kuwawezesha watanzania wote kujiletea maendeleo kiuchumi na kiteknolojia.

Naamini viongozi wetu wote Wana kiu ya kuiletea maendeleo halisi ya kiuchumi na kiteknolojia Tanzania kwa manufaa ya watanzania wote. Na kwa msingi huo hoja yangu hii wataitazama na kuifikiria kwa uzito ambao wao wanaona inastahili.

Naomba kutoa hoja.
- - -
TUJITEGEMEE 25/06/2023.
Ndugu, Bunge halina msaada, lile ni genge la ..................wanaojali mambo yao binafsi.
 
Nashauri ipelekwe Hoja Binafsi Bungeni(kwa mujibu wa taratibu za Bunge) -Bunge libatilishe Azimio lile na kisha, Makubaliano yaangaliwe upya pale ambapo panapigiwa kelele na wananchi hasa kipengere cha 23(4), na pengine pia parekebishwe na wananchi waridhike kuwa Sasa makubaliano yapo sawa. Kisha Bunge lipitishe Azimio lililorekebishwa ili serikali iendelee na mchakato unaofuata.

Hili jambo lisitupotezee muda tufanye marekebisho tusonge mbele. Tuna Mambo mengi ya kufanya kwa Kila mtu kwa nafasi yake alipo kuwawezesha watanzania wote kujiletea maendeleo kiuchumi na kiteknolojia.

Naamini viongozi wetu wote Wana kiu ya kuiletea maendeleo halisi ya kiuchumi na kiteknolojia Tanzania kwa manufaa ya watanzania wote. Na kwa msingi huo hoja yangu hii wataitazama na kuifikiria kwa uzito ambao wao wanaona inastahili.

Naomba kutoa hoja.
- - -
TUJITEGEMEE 25/06/2023.
Mkataba wote ufutwe Kwa azimio la Bunge, Kisha tufanye mjadala wa wazi ikiwa BANDARI ni sahihi kubinafsishwa.

Tuanzie hapo.
 
Back
Top Bottom