Ushauri: Baba mzazi hamtaki mtoto wake wala kuzungumza na mzazi mwenzake

May 30, 2023
43
130
Habari za Jumatatu,

Naomba ushauri kuhusu rafiki yangu huyu.

Huyu rafiki yangu alizaa na mpenzi wake miaka ya tisini mwishoni, lakini hawakufanikiwa kuwa pamoja, Baba alioa mwanamke mwingine, akabaki kuhudumia mtoto wake tu japo alikuwa anaishi na mama yake. Ila huyu mzazi mwenzie ambaye ni rafiki yangu naye baada ya miaka kadhaa alipata mume ambaye anamtoto wa kike, aliyezaa na mwanamke mwingine ambaye alishafariki.

Rafiki yangu akaona ni vyema hapa, coz na yeye anamtoto wa kike, hasa umri walipishana mwaka mmoja tu, aliona watakuwa marafiki baada ya kuingia kwenye ndoa. Ila baada ya kuolewa mzazi mwenzie alimfuata na kumwambia kuwa anamtaka mtoto wake ili amlee yeye mwenyewe na sio na mwanaume mwingine.

Rafiki yangu akaona hapana mtoto anataka akaenae yeye mwenye. Kwa kifupi uliibuka ugomvi mkubwa tu. Sijajua walifikia hatua gani maana namuona kama kuna vitu anaficha huyu my friend, ila naamini alimlisha maneno mtoto kuhusu baba yake, ila baadae mtoto akabaki nae na mwanaume wake aliyeolewa nae.

Mtoto alivyokuwa mkubwa akahitaji kuwa karibu na baba yake, alijaribu kuwasiliana na baba yake lakini alikuwa haonyeshi ushirikiano wowote. Alijaribu hivyo mara kadhaa lakini alishidwa kabisa, pia alijaribu hata kufika nyumbani kwake alishidwa kabisa.

Mwaka jana alihitaji kwenda kwa baba yake laini still baba hakumtaka kabisa, rafiki yangu alijaribu kuongea na baba yake, naye hakutaka hata kusikia kabisa.

Mtoto akataka kujua shida ni nini, amekuja kugundua kuwa kumbe kipindi yupo mdogo baba yake alikuwa anamtaka kumchukua ila mama aligoma kabisa na ugomvi juu.

Pia binti anamuuliza maswali mama yake anashidwa hata kumjibu mengine. Kwa sasa mtoto mwenyewe hataki kwenda hata kwa mama yake, yupo tuu mwenyewe.

Ila mimi nimeona baba yake mzazi ni mtu mwenye uwezo sana tena sana. Hata kuliko alipolelewa yeye, nafikiri mtoto kinamuumiza sana. Rafiki yangu ameshidwa nini cha kufanya.

Ila mimi naamini huenda mtoto akiwa mdogo alimlisha maneno ya kumjibu vibaya baba mtoto ili abaki nae. Yeye alisema kuwa aliona ni vyema kwa sababu mwanaume aliyemuoa nae alikuwa na mtoto wa kike, alitaka akae nae kwa sababu aliona itakiwa vyema apate mtu wa kucheza nae, na kujenga mahusiano mazuri yeye na mume wake.
 
baba ameshidwa
mama ameshidwa
mtoto ameshidwa
aunt(wewe) umeshidwa.

Nasi tumeshidwa.


By the way mtoto aliyezaliwa miaka ya 90 mwishoni yuko kwenye ~23, 24, 25 yrs, mshauri atulie tu na umesema yuko kwake means anajitegemea sasa, huko anakong'ang'ania Ni nadra sana kupendeka na kukubalika maana bond huwa inajengwa wakati akiwa anakua, so akubali hali halisi aishi, mbona ameishi kipindi alichokuwa tegemezi zaidi, kipindi alichomhitaji zaidi baba na amekua sasa.
Wakati mwingine Mungu huwa anaruhusu mambo fulani akiwa na sababu, pengine angeteswa sana huko kwa baba yake.
 
Kila mbegu unayopanda ni lazima uvune malipo yake.

Mtoto kama anajitambuwa aende kwa ndugu zake upande wa baba, haya ndio madhara ya kulisha Watoto Sumu.

Selfishness.
Kweli kabisa ndugu yangu, wazazi hasa upande wa kike wana tabia zaidi ya kuwapa watoto sumu ya kufanya Baba aonekanike mbaya sana yaani maneno yote yatakayosemwa kuhusu baba ni mabaya na kamwe siyo mazuri.

Mimi Kama mimi binafsi Nipo ktk situation kama hii na kuanzia mzazi mpaka ndugu, jamaa na marafiki wa mzazi mwenzangu wote wamejazwa maneno mabaya sana kuhusu mimi ila Mungu siku zote anachukua upande sahihi inawezekanika ikawa siyo Leo au Kesho lakini Kwa wakati wake na itakuja tuu siku hiyo.

Wazazi wa kike( mama za watoto wetu) hii kuwapa sumu watoto na kuwajaza maneno mabaya ili mradi mzazi mwenzako haonekanike mbaya ni kitu kibaya sana


Ova
 
Kweli kabisa ndugu yangu, wazazi hasa upande wa kike wana tabia zaidi ya kuwapa watoto sumu ya kufanya Baba aonekanike mbaya sana yaani maneno yote yatakayosemwa kuhusu baba ni mabaya na kamwe siyo mazuri.

Mimi Kama mimi binafsi Nipo ktk situation kama hii na kuanzia mzazi mpaka ndugu, jamaa na marafiki wa mzazi mwenzangu wote wamejazwa maneno mabaya sana kuhusu mimi ila Mungu siku zote anachukua upande sahihi inawezekanika ikawa siyo Leo au Kesho lakini Kwa wakati wake na itakuja tuu siku hiyo.

Wazazi wa kike( mama za watoto wetu) hii kuwapa sumu watoto na kuwajaza maneno mabaya ili mradi mzazi mwenzako haonekanike mbaya ni kitu kibaya sana


Ova
Usibabaishwe na mwanamke mpumbavu, ukweli huwa una tabia ya kujisimamia wenyewe daima.

Sumu na uongo ni vitu temporary tu.
 
Huyo my friend wako ni mpuuzi sana! Lazima alimfanya mtoto kitega uchumi kwa tamaa zake! Mjinga sana huyo
 
Wa
Habari za Jumatatu,

Naomba ushauri kuhusu rafiki yangu huyu.

Huyu rafiki yangu alizaa na mpenzi wake miaka ya tisini mwishoni, lakini hawakufanikiwa kuwa pamoja, Baba alioa mwanamke mwingine, akabaki kuhudumia mtoto wake tu japo alikuwa anaishi na mama yake. Ila huyu mzazi mwenzie ambaye ni rafiki yangu naye baada ya miaka kadhaa alipata mume ambaye anamtoto wa kike, aliyezaa na mwanamke mwingine ambaye alishafariki.

Rafiki yangu akaona ni vyema hapa, coz na yeye anamtoto wa kike, hasa umri walipishana mwaka mmoja tu, aliona watakuwa marafiki baada ya kuingia kwenye ndoa. Ila baada ya kuolewa mzazi mwenzie alimfuata na kumwambia kuwa anamtaka mtoto wake ili amlee yeye mwenyewe na sio na mwanaume mwingine.

Rafiki yangu akaona hapana mtoto anataka akaenae yeye mwenye. Kwa kifupi uliibuka ugomvi mkubwa tu. Sijajua walifikia hatua gani maana namuona kama kuna vitu anaficha huyu my friend, ila naamini alimlisha maneno mtoto kuhusu baba yake, ila baadae mtoto akabaki nae na mwanaume wake aliyeolewa nae.

Mtoto alivyokuwa mkubwa akahitaji kuwa karibu na baba yake, alijaribu kuwasiliana na baba yake lakini alikuwa haonyeshi ushirikiano wowote. Alijaribu hivyo mara kadhaa lakini alishidwa kabisa, pia alijaribu hata kufika nyumbani kwake alishidwa kabisa.

Mwaka jana alihitaji kwenda kwa baba yake laini still baba hakumtaka kabisa, rafiki yangu alijaribu kuongea na baba yake, naye hakutaka hata kusikia kabisa.

Mtoto akataka kujua shida ni nini, amekuja kugundua kuwa kumbe kipindi yupo mdogo baba yake alikuwa anamtaka kumchukua ila mama aligoma kabisa na ugomvi juu.

Pia binti anamuuliza maswali mama yake anashidwa hata kumjibu mengine. Kwa sasa mtoto mwenyewe hataki kwenda hata kwa mama yake, yupo tuu mwenyewe.

Ila mimi nimeona baba yake mzazi ni mtu mwenye uwezo sana tena sana. Hata kuliko alipolelewa yeye, nafikiri mtoto kinamuumiza sana. Rafiki yangu ameshidwa nini cha kufanya.

Ila mimi naamini huenda mtoto akiwa mdogo alimlisha maneno ya kumjibu vibaya baba mtoto ili abaki nae. Yeye alisema kuwa aliona ni vyema kwa sababu mwanaume aliyemuoa nae alikuwa na mtoto wa kike, alitaka akae nae kwa sababu aliona itakiwa vyema apate mtu wa kucheza nae, na kujenga mahusiano mazuri yeye na mume wake.
Wanawake wa namna yake ni mashetani yanayoishi duniani nahisi atakua ni mjita uyo maana ndio wana tabia za kua wasimbe na watoto kila mtoto na baba yake
 
Huyo baba alikua selfish na wivu wa kijinga toka mwanzo....
Kwamba yeye anaona mwanae hawezi kulelewa na mwanaume mwingine ila mke wake yeye ndo anaweza lea mtoto asiye wake (binafsi wanangu hawawezi lelewa na mtu mwingine yeyote labda nimekufa)
Mtoto anajichosha tu, since baba hana time nae astick na mama yake maisha yaendelee, kashakua mkubwa, huo muda wa kutafutana na baba asiye mtaka afocus kujenga maisha binafsi sababu soon ataanzisha familia binafsi pia
 
Kuzaa nje hakujawahi kumuacha mtu salama hata siku moja.

Yangu ni hayo tu! Mwenye masikio na asikie.

KaziKweliKweli/JobTrueTrue
 
Back
Top Bottom