Ushahidi Kagoda waitikisa Serikali

hapa vinatafutwa vidagaa ili vifungwe na nyangumi wanapeta. Hii ni serikali ya magamba katika harakati za kuwahadaa wadaganyika. Haiwezi kuingia akilini leo hii wameona eti huu ushahidi unaweza kutumika. Huu ushaidi umetengenezwa kutufanya wajinga.

Hatutadanganyikiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii.

Chadema fanyani kazi yenu bana tusibabaishane!
 
Serikali haijatikisika, wala hakuna cha maana kitakachofanyika. "utulivu na amani" vinapeta. Hii serikali ya nJA ya KAYA ni mbayuwayu kwa kwenda mbele. Ukiletewa ushahidi wa tuhuma, changanya na zako.
 
Serikali haijatikisika, wala hakuna cha maana kitakachofanyika. <strong>"utulivu na amani"</strong> vinapeta. Hii serikali ya nJA ya KAYA ni mbayuwayu kwa kwenda mbele. Ukiletewa ushahidi wa tuhuma, changanya na zako.
 
Kwa vyovyote vile Msemakweli amefanya sehemu yake kama Mzalendo (au hata kama anatumiwa). Yeye ametoa ushahidi kuonesha hizo pesa zilipokwenda (nje ya nchi), sasa akisema zilienda CCM wakati vielelezo alivyonavyo vinaonesha zilipelekwa nje si atakuwa anajichanganya? Sasa kama pesa hizo somehow zilizunguka tena na kurudi CCM au kina Manji walitoa pesa kutoka accounts nyingine na kuzipeleka CCM, hilo lingekuwa kazi vyombo vyetu kuchunguza kama wangekuwa na chembe ya uzalendo.<br />
<br />
Lakini kwa kusema ukweli kabisa hakuna nia ya dhati kwa DPP, DCI na wengine kushughulika na suala hili (they jusst reactive na kusaidia mafisadi kuzima mto kila unapotaka kuwaka). Hivi vielelezo anavyotoa Msemakweli na vingine vingi wanaweza kuvipata wao wenyewe kama wangetaka kufanya kazi kizalendo. Kwa ujumla hii yote hapa ni senema tu!
<br />
<br />
 
Hii ni vita tamu kuliko zote,ya maadui wa sasa ambao walikuwa marafiki zamani,lowasa na timu yake upande mmoja,j.k.na wapambe upande mwingine,msemakweli kasema kweli pesa za epa zilienda dubai lakini kila mwenye akili timamu anajua wamiliki wake wako tz na dubai hazikwenda kuwasaidia wananchi wa u.a.e. Na kadri ninavyofahamu wa dubai hawahitaji msaada alau kutoka tanzania,pesa zilienda kusafishwa MONEY LAUNDRY na pesa zilitumika ktk kampeni ya ccm zingine obvious walijilipa watu.mtakumbuka kampeni za kifiesta huku magari yakisomba watu toka kila kata ya nchi hii,hizo haziwezi kuwa fedha halali hakuna anaeweza kuitoa ccm lakini 2nataka ushahidi,na ushahidi wanao upande wa pili.WAPAMBE WA J.K WAMEMWAGA UGALI,TIMU YA LOWASA BAKULI LA MBOGA LIKO MBELE YENU...
 
Nadhani Serikali yetu na Sisi watanzania kwa ujumla wetu tu mbumbumbu! Inakuaje mtu anaoneka akirudisha fedha za wizi halafu tunasema wezi walioiba fedha hizo hawajulikani?? nina wasiwasi tutaingia ktk Guiness Book, kuwa ni Taifa la ajabu Duniani, kwa kubadilisha na kuukana ukweli kuwa si ukweli.
 
&lt;br /&gt;<br />
&lt;br /&gt;<br />
wasiwasi wangu ni kwamba tume iliyoundwa/itakayoundwa haitakuwa huru kusema ukweli. Issue ya kagoda Jk hakosekani, kwani ndiyo pesa zilizotumika kumwingiza JK ikulu. Vilevile nina wasiwasi wakurugenzi waliounda hii tume walishakwapua sehemu ya pesa hizo.
Sasa wewe unaanzisha thread yako au?Maana mtoa ushahidi anamwondoa kabisa jk kwa kusema pesa za kagoda hazikutumika kumwingiza jk ikulu,sasa wewe hayo ya jk kuhusika umeyapata wapi?Msemakweli amedadafua yote tena kwa ushahidi mzito.Labda hapo kwenye shaka ya hiyo task force kutotenda yale yanayopaswa wayatende nakubaliana nawe
 
hakuna kitu hapo maana jambo kama hilo lilishafanyika wakafunga majalada kwamba hakuna kitu zaidi ya kuibuka na majibu kwamba ni unknown sasa vp tena? ni maigizo tu
Mkuu nakubaliana na wewe kwamba tunachezeshewa cinema baada ya cinema. Ila watambue cinema zao haziiuziki kwani hazina mashiko.
 
Bila shaka Msemakweli ameongea kile ambacho ana ushahidi,lakini hakupaswa kuongelea kuwa CCM haihusiki wakati CCM ndio chama tawala na moja aliyemtaja ni alikuwa mhasibu wa CCM,kwa vipi CCM hapa isihusike.
 
Hii nchi utawala wake wa sheria wanitia shaka, kuna watu wapo juu ya sheria. Hayo ya EPA ni Hadithi tu!
 
Hapa ni ajabu sana ninavyofahamu mimi Raisi hana mamlaka ya kumsamehe mtu ambaye bado hajahukumiwa ilikuwaje Raisi aksemehe wezi walioliibia Taifa mabilioni ili hali kule Kijijini mtu aliiba kuku au mbuzi ananafungwa miaka mitatu?
 
Je TAKUKURU walikua hawana vithibitisho alivyowasilisha bwana msemakweli siku zote? na kama walikua navyo je walikua wanasubiri nini kuchukua hatua?....Huu ni usanii tu.
 
Kwenye huu wizi wote ni wageni wasio jua uchungu na Nchi .John Kato ni Mganda ambaye sasa anakaa kinondoni , hana kazi baada ya kumwagwa na RA lakini alikuwa Chief Accountant wa kampuni yake pale pugu Rd those days .John Kato kesha amua kuishi Tanzania na anakula bata tu kumbe ni sehemu ya Kagoda ? Kweli Tanzania ina maajaabu mno
 
Jamani kutokana na wingi wa hizi skendo za serikali yetu kuna wakati nachangayikiwa kujua ipi inahusiana na wapi. Nisaidieni kwa hili tafadhali.
1.Hivi EPA na Kagoda si ndugu hawa!!!
2. Ile tume ya IGP, DCI, PCCB aliyounda Luhanjo ishughulikie EPA, iliwahi kutoa taarifa mahali popote duniani
3. Hii tume iliyoundwa baada ya Msemakweli kusema, ina nguvu gani kisheria na inawajibika kwa nani
swali la tatu ni la msingi, na si ajabu hii tume ikawa inalipwa na R.A pamoja na Manji huku ikiwajibika kwa Rais (patata hapo!!!!!!!!!)
 
Je TAKUKURU walikua hawana vithibitisho alivyowasilisha bwana msemakweli siku zote? na kama walikua navyo je walikua wanasubiri nini kuchukua hatua?....Huu ni usanii tu.
TAKUKURU ni chaka la majangili wa nchi hii, na sioni haja ya kuwa na hiki chombo kwani kimeundwa na ma-ngumbaru
 
Back
Top Bottom