Ushahidi Kagoda waitikisa Serikali

Pamoja na kuusifu ujasiri wa Msemakweli na kumpongeza sponsor wake, ni mahali pamoja tu panaponikatisha tamaa juu yao, hili la kujikomba kwa CCM, sioni kwa nini msemakweli na sponsor wake wanahangaika sana kuonyesha kwamba fedha hiyo haina uhusiano na urais wa Kikwete, hapa nao wanakua kama hao hao wezi, wanabaka demokrasia, ni vizuri kama wanajikomba sana kwa JK, waache watanzania waamue kama hizo hela zilitumika wapi, kama msemakweli ni mkweli na msomi kama ninavyoamini, aache kabisa kukubali kuwa mpumbavu kwa kujiingiza kwenye unafiki wa sponsor wake, tunamjua na huyo sponsor pamoja na kufanyakazi nzuri tunamjua mnafiki kwa kuwa anajikomba kwa CCM tu kwa sababu ya maslahi yake binafsi. Huwezi kuwa popo kwenye ukweli na hiki ndio kina water down arguments nzuri na evidence nzuri za msemakweli. Hivi utasemaje eti hela hazikutumika kwa kuwa tarehe ya kuzihamisha ilikua baada ya uchaguzi? crap stop this rubbish, what is the relationship between tarehe ya uchaguzi na ya kuhamisha hela? hapa mngekazana na nani mwizi na yoyote aliyeshiriki ni culprit, mtatetea lakini tanzania ni ya watanzania wote siku ya siku bila kujali vyeo wala nini watafungwa tu jela watu hawa, hata mkiwauma na kupuliza, kumbuka hamuwezi kupambana na wakina Rostam na Manji mkitegemea eti kumwokoa JK, fanyeni maamuzi magumu kama mnajikomba sana kwa JK waacheni wakina Manji na Rostam wapumzike, hamuwezi kuwagusa hawa na kumponya JK wakati huo huo. neno linasema, mafuta na maji havichanganyiki, giza na mwanga vile vile, poleni sana

Kwenye Red ni kweli asilia kubwa Fedha hiyo aina uhusiano na CCM wala mgombea wa CCM,tulitaka kupumbazwa na MAFISADI kuwa ina uhusiano na CCM kumbe ndio ilikuwa iwe pona yao na kichaka chao cha kujificha.Manake Wezi wa mali ya Tanzania walio wengi wamekuwa wakijipanga na kujificha chini ya kivuli cha CCM [Kosa la Sumaye na usemi wake "Ukitaka kufanikiwa ingia CCM"].Aksante Mungu nae alimuhukumu mapema mapema na kisha sasa ni mmoja wa wafuasi wa kupigia kelele haki.

Mimi binafsi uwa nachukia sana na sipendi kusikia wakina kasuku wakilazimisha kusema pesa za EPa eti zilitumika kumuingiza Kikwete madalakani wakati kiongozi mmoja mkuu zama hizo hata yeye aliingizwa chaka bovu aliposikia taarifa hizo alipiga ukete mkubwa kushangaa maovu hayo.Mimi binafsi na jamaa zangu tulio wengi na na si ajabu hata wewe tulimchagua Kikwete asilimia 80% bila ya kupewa hata senti tano,kama wewe ulihongwa ututhibitishie.Sasa mabilioni hayao yalitumika wapi kama sio kikundi cha watu wachache,tena yakapelekwa kwao India na wanakojua wao.

Walitupumbaza sana na style ya kusema mabilioni hayo ndio yaliyomuingiza mgombea wa CCM madalakani na kuyafanya kuona ni sehemu ya Serikali na mipango ya kihayawani.

Hakika ili pia litakuwa ni fundisho kwa CCM kuanza kujitoa kwenye mikakati ya Kiserikali zaidi ibakize kuwa ni chama kinachounda Serikali na si kuacha watumishi wake [Viongozi wa CCM na Wafanyabishara majangili] kuhujumu Umma kwa mgongo wa chama Serikali au chama madalaka.

Na hakika tungeendelea kuimbishiwa na kukalilishwa nyimbo za kuwa fedha za EPA ndio zilimuingiza Rais wa tiketi ya CCM madalakani na hakika hatutafika na tusingefika hapa tulipofikia kwa akina Msemakweli.Njia sahihi ya kupambana na watu wa aina hii ya UFISADI ni kutenganisha wao na hicho cha kusema ilikuwa ni kwa faida ya CCM.

Wenzetu Nchi zingine uovu wa kitaasisi au kundi la watu au mtu mmoja mmoja daima una mtu wa kuwajibikana tatizo au kosa husika [Somone to be blame or someone is to be responsible to the matter]. Kwanini sisi uwa tunatabia ya kuweka lawama kitaasisi na sio mtu. Lawama za kitaasisi uwa wanaweka kwenye vyombo vya ulinzi na usalama,lakini pia nao aliyejua uwajibishwa ili liwe funzo kwwa walio juu kuwa makini kila wanapokuwa na crisis situation yoyote kuitazama kwa jicho kali,na kuwawajibisha wa chini yao.Lakini bongo ni tofauti hakika.
 
Jamani kutokana na wingi wa hizi skendo za serikali yetu kuna wakati nachangayikiwa kujua ipi inahusiana na wapi. Nisaidieni kwa hili tafadhali.
1.Hivi EPA na Kagoda si ndugu hawa!!!

Ndio. EPA ndio kashfa yenyewe - Kagoda ni mojawapo ya makampuni yalichukua hizo fedha za EPA na by far the largest beneficiary ikiwa imechukua bilioni 40 za ile 133! Lakini pia ni kampuni ambayo imeweza kuchukua bilioni hizo huku wenyewe wasiwepo kabisa... "wamiliki wa Kagoda hawajulikani!" ilisemwa.

2. Ile tume ya IGP, DCI, PCCB aliyounda Luhanjo ishughulikie EPA, iliwahi kutoa taarifa mahali popote duniani

Ile tume haikuwa kwa ajili ya kutoa taarifa kwa umma. Ilikuwa ni kwa ajili ya kushawishi wahusika kuzirudisha hizo fedha na wale ambao walikuwa hawana ujiko mkubwa kufikishwa mahakamani. Tume ile haikuwa na nguvu zozote za kisheria zaidi ya kuingiilai kazi za DPP na matokeo yake ndio haya ya sasa hivi ambapo tumeamua kumtaka DPP afanye kazi yake na siyo tume. Ndio maana utaona kuwa hata ripoti ya hiyo tume haijawahi kuhojiwa na Bunge au kutaka iletwe Bungeni kwa msingi ule ule wa ripoti nyingine ya tume ya Luhanjo inavyotakiwa Bungeni.

3. Hii tume iliyoundwa baada ya Msemakweli kusema, ina nguvu gani kisheria na inawajibika kwa nani

Kuna tume nyingine imeundwa?
 
Kuna tume nyingine imeundwa?
SAKATA la Kampuni ya Kagoda iliyokwapua sh bilioni 33 kutoka kwenye Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA), mali ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT), limechukua sura mpyaa baada ya ofisi ya Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai (DCI), Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP)na Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), kuunda kikosi kazi kuchunguza sakata hili
Kikosi kazi nadhani ni kama tume! Nahisi ni kubadili ladha ya maneno. Hata ile ya Luhanjo ilianza kwa jina hilo njiani tukasikia ni tume. Au nimeelewa tofauti habari iliyopo.
 
Nadhani walioandika wameweka impression isiyo sahihi. Labda ni "sub-committee" ya hiyo kamati ya awali ya Luhanjo.
 
Hakuna lolote la maana hapo. Tume inaundwa na watu toka ofisi ambazo zote hazina crdibility ya kusema ukweli sasa tutarajie nini cha maana? Another "funika kombe mwanaharamu apite"!

hivi intelijensia ya wale jamaa (usalama wa taifa na polisi) mipaka yake inaishia kwenye maandamano ya chadema peke yake tu!
 
ndio haya ya sasa hivi ambapo tumeamua kumtaka DPP afanye kazi yake na siyo tume. Ndio maana utaona kuwa hata ripoti ya hiyo tume haijawahi kuhojiwa na Bunge au kutaka iletwe Bungeni kwa msingi ule ule wa ripoti nyingine ya tume ya Luhanjo inavyotakiwa Bungeni.


Kuna tume nyingine imeundwa?

Ina maana kuna watu walimtuma Msemakweli afanye yale aliyoyafanya na wewe ni mmojawapo wa wale waliomtuma...?
 
Nadhani walioandika wameweka impression isiyo sahihi. Labda ni "sub-committee" ya hiyo kamati ya awali ya Luhanjo.
ha ha ha!
Hawa watu si walisema hawajui Kagoda ni ya nani na hawana ushihidi. Sasa hiyo 'sub commitee' inataka ichunguze nini walichoshindwa kukiona mwanzoni!! Kipi kinawashtua leo hii.
 
Mimi binafsi nimechoshwa na habari za Kagoda, naona kama mchezo wa kuvuta muda tu...tunaenda mbele hatua moja halafu nyuma tunarudi hatua tatu! Kama wakuu wote wa idara husika wangekuwa makini na kutumia professional zao hii ingekuwa closed case ages ago. Naona watu wanakazana kuunda tume ili hali majibu yote wanayo wenyewe, sasa kama siyo kupoteza muda huko ni nini? Bwana Feleshi naye anasubiri apelekewe ushahidi badala ya kuingia vitani kutafuta huo ushahidi yeye mwenyewe na team yake.

Kwa kifupi, juhudi kubwa inafanywa na idara husika kuukwepa/kuukimbia ushahidi kuliko kuutafuta!
 
Mungu anawaona sana tu cz watanzania wanateseka sana kwasababu yao ipo cku tu watakiona cha moto naendelea kupiga goti kwa ajili yao.
 
CCM ilikuwa ikiogopa bure. Waliochukuwa fedha za Kagoda , walitake advantage ya uchaguzi huo wa 2005. Walichukua fedha hizo kwa ajili ya mambo yao binafsi. Ni kweli kuna fedha za EPA nyingine zilichukuliwa na kutumiwa kwa ajili wa uchaguzi. CCM (mpya) . nadhani wamefanya thamimini upya na wamekuja kugundua kwa hakuna fedha ya Kagoda ilikwenda CCM na watakuwa wametoa baraka kwa uchunguzi ufanyike na watu mara hii watapelekwa mahakamani.
 
Tume za nini waache unafiki ,kwani wakati akina Manji si wanajulikana na ndio waliorudisha hizo pesa kiasi waache tumsikie mwendesha mashitaka naye atakuja na lipi asavali Msemakweli katuonyesha njia kwa kunfunga PAKA SHUME KENGELE,tume tume si kulikuwa na tume ya akina Mwanyika na huyo mkuu wa sijui nini eti Mkuu wa nini sijui Manumba,hayo makabrasha yao yamefukiwa na vumbi sasa ni kipi kipya cha kuunda tume juu ya mitume,hovyoo
 
ndio maana kuna gap kubwa kati ya maskini na matajiri mikopo mikuuuubwa wamepewa wao wakati pesa hizo kama wangewakopesha watanzania ambao hata ungewapa mitaji ya milioni moja moja tu ungekuwa umeinua wananchi wangapi??sera ya maisha bora ilikuwa elekekezi kwa wanyonyaji,,wadhalilishaji,na makupe>>>aaaaghhhhhhhh manji+rostam=jk
 
huu ujanja Brella wanatumia kulinda wezi siku moja wataujibia mahakamani. Hata mwadui diamond mmiliki haeleweki wanachota mali kiwiziwizi tu
 
Pamoja na kuusifu ujasiri wa Msemakweli na kumpongeza sponsor wake, ni mahali pamoja tu panaponikatisha tamaa juu yao, hili la kujikomba kwa CCM, sioni kwa nini msemakweli na sponsor wake wanahangaika sana kuonyesha kwamba fedha hiyo haina uhusiano na urais wa Kikwete, hapa nao wanakua kama hao hao wezi, wanabaka demokrasia, ni vizuri kama wanajikomba sana kwa JK, waache watanzania waamue kama hizo hela zilitumika wapi, kama msemakweli ni mkweli na msomi kama ninavyoamini, aache kabisa kukubali kuwa mpumbavu kwa kujiingiza kwenye unafiki wa sponsor wake, tunamjua na huyo sponsor pamoja na kufanyakazi nzuri tunamjua mnafiki kwa kuwa anajikomba kwa CCM tu kwa sababu ya maslahi yake binafsi. Huwezi kuwa popo kwenye ukweli na hiki ndio kina water down arguments nzuri na evidence nzuri za msemakweli. Hivi utasemaje eti hela hazikutumika kwa kuwa tarehe ya kuzihamisha ilikua baada ya uchaguzi? crap stop this rubbish, what is the relationship between tarehe ya uchaguzi na ya kuhamisha hela? hapa mngekazana na nani mwizi na yoyote aliyeshiriki ni culprit, mtatetea lakini tanzania ni ya watanzania wote siku ya siku bila kujali vyeo wala nini watafungwa tu jela watu hawa, hata mkiwauma na kupuliza, kumbuka hamuwezi kupambana na wakina Rostam na Manji mkitegemea eti kumwokoa JK, fanyeni maamuzi magumu kama mnajikomba sana kwa JK waacheni wakina Manji na Rostam wapumzike, hamuwezi kuwagusa hawa na kumponya JK wakati huo huo. neno linasema, mafuta na maji havichanganyiki, giza na mwanga vile vile, poleni sana

Can't we sober ourselves up? Mimi sijui na wala sijali kama Msemakweli anatumiwa as long as anachokizungumza ana ushahidi nacho na kinastahili kusukuma matumizi ya sheria dhidi ya wale waliohujumu uchumi na rasilimali za nchi hii. Nasikitika ndugu yangu kudhani kwamba watanzania ndiyo watakaoamua kama fedha zilitumika kwenye uchaguzi au la wakati takwimu ndizo zinazopasa ku-dictate kama kweli zilitumika kwenye uchaguzi au la. Huwezi kusema kwamba ziliztumika kwenye uchaguzi wakati fedha hizo zimetumika baada ya uchaguzi kupita. Hili haliwezi kubadilika hata kama watanzania wote watahamasishwa na kusema kwamba zilitumika katika uchaguzi wakati ukweli uko vinginevyo. Msemakweli amesaidia kumtoa paka kwenye gunia kwa kuonyesha kwamba wale walioiba wakajifinya mgongoni kwa mwammvuli wa uchaguzi wa Kikwete sasa wameumbuliwa na kwa hiyo uporaji huu ulikuwa ni kwa maslahi ya waporaji hao na si vinginevyo.

Ndugu yangu unaendelea kujionyesha consistently kwamba tatizo lako wewe ni Kikwete binafsi na siyo maovu yanayofanyika nchini. Ndiyo maana uko tayari kuona kwamba Manzi na Rostam wanaachwa huru kwa vile tu tuhuma dhidi yao hazimwingizi Kikwete. Huu ni usaliti na unafiki wa hali ya juu na mtu unashangaa mtu kama wewe anawezaje kujiita mzalendo wakati na wewe una-shield wezi. Mimi nirudie kumshukuru Msemakweli kwa hatua yake hii na kwa kweli tunahitaji kumuunga mkono na kumpa kila aina ya msaada katika harakati zake hizi dhidi ya uovu!
 
Ina maana kuna watu walimtuma Msemakweli afanye yale aliyoyafanya na wewe ni mmojawapo wa wale waliomtuma...?

Kama kweli ametumwa basi waliomtuma ni wazalendo wa kweli na sijali kama wataendelea kumtumia yeye au watu wengine katika masuala yenye maslahi kwa watanzania na taifa hili kwa ujumla.
 
Hivi hizi pesa 'walizorudisha' kuliwahi kuwepo ushahidi wa kurudishwa? Isije ikawa ni changa la macho! NAjiuliza haya mabilioni mtu anayarudishaje kama 'hard cash'? Tunaweza kujua zilitokea account gani (za aliyerudisha) na kuingia account ipi ya serikali/bot? Baadae tuliambiwa zimeenda TIB kwa Nyoni!!!???
 
Msemakweli nimekuamini sana lakini kama utaendelea kusisitiza kwamba Kagoda haihusiani na CCM sitakuamini tena.
 
Pamoja na kuusifu ujasiri wa Msemakweli na kumpongeza sponsor wake, ni mahali pamoja tu panaponikatisha tamaa juu yao, hili la kujikomba kwa CCM, sioni kwa nini msemakweli na sponsor wake wanahangaika sana kuonyesha kwamba fedha hiyo haina uhusiano na urais wa Kikwete, hapa nao wanakua kama hao hao wezi, wanabaka demokrasia, ni vizuri kama wanajikomba sana kwa JK, waache watanzania waamue kama hizo hela zilitumika wapi, kama msemakweli ni mkweli na msomi kama ninavyoamini, aache kabisa kukubali kuwa mpumbavu kwa kujiingiza kwenye unafiki wa sponsor wake, tunamjua na huyo sponsor pamoja na kufanyakazi nzuri tunamjua mnafiki kwa kuwa anajikomba kwa CCM tu kwa sababu ya maslahi yake binafsi. Huwezi kuwa popo kwenye ukweli na hiki ndio kina water down arguments nzuri na evidence nzuri za msemakweli. Hivi utasemaje eti hela hazikutumika kwa kuwa tarehe ya kuzihamisha ilikua baada ya uchaguzi? crap stop this rubbish, what is the relationship between tarehe ya uchaguzi na ya kuhamisha hela? hapa mngekazana na nani mwizi na yoyote aliyeshiriki ni culprit, mtatetea lakini tanzania ni ya watanzania wote siku ya siku bila kujali vyeo wala nini watafungwa tu jela watu hawa, hata mkiwauma na kupuliza, kumbuka hamuwezi kupambana na wakina Rostam na Manji mkitegemea eti kumwokoa JK, fanyeni maamuzi magumu kama mnajikomba sana kwa JK waacheni wakina Manji na Rostam wapumzike, hamuwezi kuwagusa hawa na kumponya JK wakati huo huo. neno linasema, mafuta na maji havichanganyiki, giza na mwanga vile vile, poleni sana

Kwa vyovyote vile Msemakweli amefanya sehemu yake kama Mzalendo (au hata kama anatumiwa). Yeye ametoa ushahidi kuonesha hizo pesa zilipokwenda (nje ya nchi), sasa akisema zilienda CCM wakati vielelezo alivyonavyo vinaonesha zilipelekwa nje si atakuwa anajichanganya? Sasa kama pesa hizo somehow zilizunguka tena na kurudi CCM au kina Manji walitoa pesa kutoka accounts nyingine na kuzipeleka CCM, hilo lingekuwa kazi vyombo vyetu kuchunguza kama wangekuwa na chembe ya uzalendo.

Lakini kwa kusema ukweli kabisa hakuna nia ya dhati kwa DPP, DCI na wengine kushughulika na suala hili (they jusst reactive na kusaidia mafisadi kuzima mto kila unapotaka kuwaka). Hivi vielelezo anavyotoa Msemakweli na vingine vingi wanaweza kuvipata wao wenyewe kama wangetaka kufanya kazi kizalendo. Kwa ujumla hii yote hapa ni senema tu!
 
Nadhani ni wakati sasa wa kuwakamata Yussuf and Rustum na kuwapeleka mahakamani and then wapewa dhamana ya "kudumu" - angalau huu mzimu wa Kagoda uta-rest in peace!
 
Brella ni ya serikali, inachekesha na kuhuzunisha serikali inaposema kuwa haiwafahamu wamiliki wa Kagoda. Hiki ni kielelezo kimoja wapo kati ya vingi kuwa wajanja wachache wameiweka serikali yetu mifukoni mwao.

sindo wwanaoamua umeme uwashwe au uzimwe ili wauze mafuta! jana niliumia sana kugundua kuwa mabonde ya kilombero yalikuwa ma hamba ya serikali, lakIni wajjanja wakagawana kama biscutes!
eeeerh Mungu Tuhurumie watanzania kutoka katika kukandamizwa huku!
 
Back
Top Bottom