Godfrey GODI
Member
- Nov 10, 2011
- 62
- 19
Mimi sio mwanahistoria mzuri lakini ninaweza kukumbuka vitu vya kihistoria katika nchi yetu hususani wakati wa ukoloni. Wanahistoria watakubaliana nami kuwa Tanganyika ilitawaliwa na wakoloni wa kijerumani. Kabla ya ukoloni, jamii zetu za kitanzania zilikuwa tayari zimejipanga katika suala la uongozi wa makabila.Wajerumani walipoingia nchini Tanganyika walipambana na upinzania mkali kutoka kwa wananchi waliokuwa wanaongozwa na viongozi wao. Mara nyingi wajerumani pekee walishindwa vibaya katika mapambano hayo.Wajerumani walibuni mbinu ya ulaghai. Waliweza kulaghai viongozi wa kabila moja ili waungane na kabila hilo kuwapiga kabila lingine katika Tanganyika. Kwa mfano, wajerumani waliungana na Mangi Sina wa Kibosho na kumpiga Mangi Meli wa Marangu. Watanganyika wakapigana wao kwa wao. Baadaye ujerumani ilimrudi Sina na kumshambulia na kumwagusha. Hila za kikoloni.Ndugu zangu, mtakubaliana nami kuwa hila hizo za mkoloni zinatumika hadi leo katika nchi yetu. Na kwa hiyo zinatumika katika siasa yetu. Kwa hali ilivyo sasa, umasikini wa mtanzania na raslimali za Tanzania ni vitu viwili tofauti. Imekuwa laana kwa mtanzania kuzaliwa katika Tanzania yenye raslimali kibao. Kupitia raslimali hizo si tu kwamba hazimnufaisha mtanzania lakini pia zimepelekea kuongezeka kwa vitendo vya uporwaji wa haki zao.Wakati hayo yanaendelea na kufanywa na serikali ya CCM, na baada ya watanzania kuanza kuhoji namna raslimali zao zilivyogeuzwa laana. CCM inatumia hila ya kikoloni, inaungana na CUF kuishambulia CHADEMA, ambacho ndicho chama kinachowatetea wananchi. CUF zaidi ya CCM ndicho kimekuwa mstari wa mbele katika kukipiga vita CHADEMA na kukifanyia hila za hapa na pale kama alivyotumiwa Sina kumpiga Meli. Cuf, historia hujirudia. Huyo bwana uliyempata ipo siku atakutariki baada ya kukutumia vya kutosha, kama iliyokuwa kwa Mangi SINA. CUF bara take care. Yetu macho na nia yetu kamwe haitabadilika. TUNATAKA UKOMBOZI WA NCHI YETU, UKOMBOZI WA RASLIMALI ZETU NA UKOMBOZI WA RAIA WETU.Nawasilisha
..