Usafiri wa Baharini Kivukoni hadi Kunduchi Beach Kumbe Inawezekenaka!!!!

bado sana kuja hiyo,lakini kupunguza foleni dar hakuwezi kutatuliwa kwa kuongeza reli,barabara na usafiri majini.NJia pekee ni kuondoa maofisi yaliyojazana pale posta na kuyatoa nje ya katikat ya mji,hii itasaidia pia kuendeleza mji kimaendeleo na kimazingira kuliko ilivyo sasa.Tazama kama kuna baadhi ya maofisi makubwa yangu kuwa bunju mengine Mbagala ama kigamboni kabisa na mengine yakabaki palepale Mjini kati foleni ingetokea wapi?wakati huo huo maeneo ambayo hayajawa planed wakayaplan kwa kuweka baranara njia nne kila upande.Tungekuwa mbali sana!
 
Wasiwasi wangu ni kujazana kwa abairia kwenye hizo ngalawa na upepo wa Msasani Penisular isije tukawa chakula cha samaki wa Magufuli
 
bado sana kuja hiyo,lakini kupunguza foleni dar hakuwezi kutatuliwa kwa kuongeza reli,barabara na usafiri majini.NJia pekee ni kuondoa maofisi yaliyojazana pale posta na kuyatoa nje ya katikat ya mji,hii itasaidia pia kuendeleza mji kimaendeleo na kimazingira kuliko ilivyo sasa.Tazama kama kuna baadhi ya maofisi makubwa yangu kuwa bunju mengine Mbagala ama kigamboni kabisa na mengine yakabaki palepale Mjini kati foleni ingetokea wapi?wakati huo huo maeneo ambayo hayajawa planed wakayaplan kwa kuweka baranara njia nne kila upande.Tungekuwa mbali sana!

Kama mdau ulivyosema kuondoa kero ya msongamano wa magari si moja tu ni nyingi. Utaona viwanda vinajengwa sehemu moja badala ya kutanua viwanda kujenga kufuata watu huko waliko badala ya watu kufuata viwanda, pengini kuanzisha maeneo mapya ambayo yatakuwa na makazi mapya pia. Kama wazo la Nyerere viwanda vingetanuliwa eneo la Kibaha, kwa vile ni eneo lenye nafasi kubwa huenda hawa wanaohangaika kubigania viwanja vya kujenga Dar ingepungua kwani watu wangeamua kuongeza makazi sehemu ambazo ajira zipo.

Serikali haina mipango kama hiyo. Wenzetu wanaweza kuamua kufungua mji fulani mpya porini kabisa kwa kujenga nyumba mpya za makazi na kiwanda kikubwa, katika muda wa nusu mwaka utakuta ni mji wa kukalika kwa vile huduma zote zitasogezwa hapo kama shopping mall, shule, makanisa, huduma za afya nk. Sisi kila kitu ni kujaza pale Darisalama.

Ningekuwa rais wa nchi hii ningesikia raha sana na kuonja fresh air ningehamia Ikulu ya Chamwino Dodoma kuliko kuendelea kuvuta moshi wa pale jiko la wachemsha samaki magogoni, harufu ya samaki, harufu ya uchafu unaotumbukizwa toka mjini kwani bomba limepita pale mtaa wa kipatu na unapoelea baharini Ikulu inavuta harufu yake.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom