URITHI; Mtoto wa nje alitaka nyumba zote ziuzwe ili apate hela kubwa. Ni shukrani gani hii?

Moronight walker

JF-Expert Member
Aug 3, 2021
3,105
4,635
Habari wana Jamii forum.

Ngoja leo nilete hii kesi niliyoishuudia kwa macho yangu.

Kulikuwa na Baba mmoja na familia yake wa watoto 4, wapili ni wakiume ambae alimzaa nje na wengine 3 Wandoa wakike alizaa na mkewe.

Niliambiwa hivi, Baada ya mkewake kujifungua mtoto wa kwanza ikapita kama mwaka hivi Baba akazaa nje mtoto wa kiume ila aliyamaliza na mkewe.

Mtoto alipofika umri wa miaka 6 mzee alimchukua na kukaa nae home.

Mke wake alikubaliana na hali na kumlea tu bila shida yoyote. Na likizo akawa anaenda kwa mama yake.

Sasa baada ya kufika utu uzima watoto wote.

Yule Baba alifariki na kuacha nyumba mbili tu. 1 aliyokuwa anaishi na mke wake nyingine walipangisha.

Sasa mtoto wa kiume wa baba ambae alimzaa nje akawa anag'ang'ania awe msimamizi wa mirathi kwa kigozo cha yeye ndiyo wa kiume ndiyo anaendeleza familia ya mzee.

Na pia analazimisha nyumba zote mbili ziuzwe wagawane ila yeye akawa anahitaji kupata asilimia kubwa.

Kesi ilikuwa kubwa mpaka kupelekana mahakamani , ila walipofika mahakamani mabinti wale watatu wakasema wao hawaitaji nyumba kuuza kwa sababu mama yao atakaa wapi.

Lakini mahakama wakamwambia jamaa wote ni watoto wa baba mmoja kwa hio wote mtapata sawa hakuna huyu wa kiume wala huyu wa kike wote mnapata kwa usawa.

Lakini mwishoni walikubaliana wauze nyumba mmoja halafu kaka yao wampe pesa zake na zingine ili wafidie ile nyumba nyingine ambayo Mama yao anakaa.

Nyumba iliuzwa 1 jamaa akachukua pesa ndefu tu ili kufidia ile nyumba nyingine ambayo mama wa mabinti alikuwa anaishi na mume wake.

Sidhani kama wanaundugu mpaka leo wa karibu.

Nafikiri jamaa alitaka ziuzwe zote bila kujali mama yule atakaa wapi.

Hiyo ni kwa sababu yule hakuwa mama yake, hata nyumba ikiuzwa yeye ataumia chochote.

Karibuni jamani mutoe uzoefu wenu kama umewahi kutana na migogoro kama hii.

Karibu.
 
Sidhani kama hii ni kweli, Baba akifa akabaki Mama, sidhani kama yeye hana haki yeyote, there is more in this story.
Ni kuulize swali?

Kwanini mtu anaponunua nyumba lazima aangalie status ya Kwa mtu ambaye anamuulia yani , yupo kwenye ndoa au la.

Mimi nimewahi kusimuliwa na mzee wangu aliniambia ilitokea mda kidogo miaka kabla ya 2008.

Kulikuwa na benk moja hapa dsm ilimkopesa Baba mchaga mmoja mkopo akaweka rehani nyumba na mkopo hukumuhusha mkewe na kwenye hati ya nyumba lipo jina la mume wake its means nyumba ni ya Baba sio mama.

Mda uliisha na mkopo hakufanikiwa kumaliza, benki ilitaka kunadisha nyumba mke wake alienda kupinga mahakamani isiuzwe na mahakama ikatoa amri isiuzwe.

Japo sasa hivi hakuna benk inafanya huo upuuzi.

Ndo maana ukinunu nyumba au kiwanja ni lazima umuhusishe mke hata kama nyumba au kiwanja jina lipo kwa mume wake.

Unajua hilo.
 
"Ulisimuliwa, there is more kwenye hayo masimulizi, najua nachosema"
Au umezaa nje???

Hata humu kuna mtu alisema mume wake alikuwa na mtoto kabla hata ya kumuoa baada ya ndoa alimchukua yeye mwenyewe na kumlea na kuwa mkubwa baada ya Baba kufaliki mtoto wa Baba hakutaka hata mke wake afike msibani hata mali kurithi aligoma kilimsaidia cheti cha ndoa tuu.
Maana walipelekana mpk mahakamani.
Usisahau yeye ndo alimlea.
 
Nilikua naitafuta
Sidhani kama hii ni kweli, Baba akifa akabaki Mama, sidhani kama yeye hana haki yeyote, there is more in this story.
Hiii
Navyojua kama mke WA ndoa yupo haziuzwi...unless Kuna kitu zaidi ya hii stor
 
Nilikua naitafuta

Hiii
Navyojua kama mke WA ndoa yupo haziuzwi...unless Kuna kitu zaidi ya hii stor
Mkuu ndo maana haikuuzwa baada kijana kupiga kulele wakaamua kumkatia cha kwake tuu kwa makubaliano ya familia yote na mama mwenyewe, nafikili umenipata.
 
Back
Top Bottom