Uraia wa nchi mbili: Maendelo na Matokeo yake!

Naendelea sasa na nitaendelea tena kesho kuupinga Uraia wa Nchi mbili . Wazungu ndiyo model yetu ya maendeleo nadhani kila mara we must site them as an example hadi kufika hapo hawakuhitaji uraia wa Nchi 2. Wamefika hapo kwa kuuthamini uraia wao na kuachana na mawazo ya kifisadi na matendo ya kifisadi. Unaweza kupeleka pesa Tanzania hata sasa na watu wamekuwa wakipeleka pesa TZ kabla ya hata wazo la uraia wa Nchi 2.

Hapa Membe anaongeza speed mtaona sasa watakavyo kuja watoto wao kuchukua madaraka na kueneleza utawala waoa kwa manufaa yao . Uraia wa Nchi 2 hivi itakuwaje kwa ajira za polisi, usalama wa Taifa , jeshini nk ?Mnaongelea Waghana kupeleka pesa hizo kwao wakati hata sisi watanzania tunapeleka na baadaye wazungu wanapeleka mabilioni lakini bado tuko hata kadi za kupiga kura ughaibuni wala access ya kuchagua ukiwa ughaibuni haipo . We are not serious na dual is never an answer.

Lunyungu,

Jibu hoja ya Waziri, je ungelikuwa wewe, utamnyima uraia huyo Mtanzania ambaye kaamua kuchukua uraia wa Canada ili watoto wake wagonjwa watibiwe?

Mifano ya namna hiyo iko mingi sana na ndio inawafanya watu wachukue uraia wa pili.

Watu hapa kila wakiambiwa wapeleke bank stament wanakuta overdraft kila mwezi zimetumika, kama ni kwenye visa jibu ni NO. Watu kama hao ndio inafika mahali wanaona ya nini shida?

Utasema watu kama hao ni watoto wa vigogo? Mtoto wa fisadi amejaza pesa bank unafikiri anahaja hata ya kuhangaika na uraia wa nchi mbili?

Mimi Watanzania ambao najua wana magamba ya hapa UK, kwa asilimia 90 ni watoto wa watu wa kawaida tu Tanzania ambao kwa sehemu kubwa hawa vijana ndio wanawasaidia hata wazazi wao kuishi kule nyumbani.
 
Katika Dunia hii Ya utandawazi tuwe makini...wakati afrika Bado Ina chechemea Mi nina fikiri Tanzania Iruhusu Uaraia wa nchi Mbili lakini iwe Ndani ya Africa..Kwanza..Unaweza ukawa Mtanzania laikini ukawa Raia wa Nchi nyingine Ya Africa!!...

Kama una akili Timamu utanielewa!! Kama Fala Itakuchukua muda sana...

Sijaambulia kitu mkuu
 
mmh baada ya muda mrefu sasa nimerejea.Uraia wa nchi kwa sasa ulimwenguni ni jambo amablo ni inevitable,vema serekali ipitishe sheria ya uraia wa nchi mbili,maana wanaokusudiwa ni Watanzania kunyakuchua uraia wa nchi nyingine na si raia wa nchi nyingine kuchukua uraia wa Tanzania.
 
Tunafikiri watz watafaidika kuchukua uraia wa nchi nyingine km Canada lakini nadhani tutapata wageni wengi wataopenda kuchukua uraia wa tz vile vile km toka Asia. Kibaya zaidi nchi yetu hata kaijaweza kumonitor na kuwatumia raia wake vizuri.

Mtu kama Mkapa akichukua gamba la Canada (akahamia huko), basi Canada haitaangalia uraia wake mwingine na tukiomba arudishwe ashitakiwe utaambiwa ni MKANADA. Wenzetu wanalinda watu wao.

Vile vile kuna raia wa nje watataka kuchua GAMBA LA TZ ili wachukue gold prospecting licenses (easy kwa mtz), kununua ardhi nk. na wote watalindwa na nchi zao.

Serikali yetu haijawahi kua makini kwa mambo mengi, na itakua hivyo hivyo kwa hili.

I say No to dual citizenship.
 
Tunafikiri watz watafaidika kuchukua uraia wa nchi nyingine km Canada lakini nadhani tutapata wageni wengi wataopenda kuchukua uraia wa tz vile vile km toka Asia. Kibaya zaidi nchi yetu hata kaijaweza kumonitor na kuwatumia raia wake vizuri.

Mtu kama Mkapa akichukua gamba la Canada (akahamia huko), basi Canada haitaangalia uraia wake mwingine na tukiomba arudishwe ashitakiwe utaambiwa ni MKANADA. Wenzetu wanalinda watu wao.

Vile vile kuna raia wa nje watataka kuchua GAMBA LA TZ ili wachukue gold prospecting licenses (easy kwa mtz), kununua ardhi nk. na wote watalindwa na nchi zao.

Serikali yetu haijawahi kua makini kwa mambo mengi, na itakua hivyo hivyo kwa hili.

I say No to dual citizenship.

Tom,

Si umeambiwa Balali ana uraia wa USA, wale wezi kwenye Radar wana uria pia wa UK. Hayo mambo yanatendek hata leo na wanaobanwa ni Watanzania watiifu tu..

Kuhusu mfano wako wa Mkapa sio sahihi. Ukiwa na dualcitizenship
na ukafanya kosa kwenye nchi mojawapo basi ile nchi nyingine haikulindi. Pia lazima ujue akina Bhutto wa Pakistan, au wale Warusi wenye pesa wanaolindwa hapa UK wala sio raia wa UK. Ukiwa na pesa utalindwa tu hata kama huna dualcitizenship.

Kwa mafisadi wa Kihindi hapo Dar, ukichunguza kila mtu ana passport zaidi ya tatu (TZ, India, UK)na hakuna anayewazuia lakini ndugu zetu wasotaji ndio tunawakea mikwara kibao.
 
Kwenye mtazamo wa sanaa yangu!! mimi bado sijawahi kufika Huko Uliko!! nikija nita warudisha!! Lakini atakae weza awe!! hata Raia wa sayari Nyingine...

Lakini tupendane-Tupende Tulipo Toka...Napenda Kua Raia wa Africa..Baadaye Nitakua Raia wa Dunia Labda Marekani au Uk- au Ulaya hivi..China japani --lakini hebu fikiri Mbona nilipo zaliwa ni Nyumbani zaidi...
sijui!!
Mara zote Viongozi wa Africa wamependa Kuona Africa Ikiwa nchi Moja-sasa hauoni Hili suala Litatusaidia kuonyesha Ndoto hizo!?!

Fala elewa...
 
Waziri Membe says, and I quote:
Akitoa mfano mmojawapo bila kutaja majina ya wahusika, Waziri Membe alisema anaifahamu familia moja ya Watanzania ambayo ililazimika kuchukua uraia wa Kanada kwa sababu za matibabu, na kwamba kuwanyang’anya uraia watu hawa ni kuwaadhibu bila kujali uhai wao...na kwamba kwa kuchukua uraia wa Kanada, matibabu hayo yanakuwa bure. Alihoji je, ni haki kuwanyang’anya uraia wao wa Tanzania.

Na hapa,
Lunyungu,
Jibu hoja ya Waziri, je ungelikuwa wewe, utamnyima uraia huyo Mtanzania ambaye kaamua kuchukua uraia wa Canada ili watoto wake wagonjwa watibiwe? Mifano ya namna hiyo iko mingi sana na ndio inawafanya watu wachukue uraia wa pili.

Kwahiyo bwana Mtanzania, wewe pamoja na waziri wako Membe mmeona hii ni tamati ya sababu ya kuleta uraia wa nchi mbili? Kwani ukishakuwa na uraia wa nchi mbili au zaidi ndio maana yake hulipi hizo costs za matibabu? Na wale watanzania waishio nchi kama US je, sababu yao ni ipi? Maana be raia or not, utalipia tu gharama za matibabu. Mister Minister, if this is your reason for supporting dual citizenship, then you are plain shallow!

Better yet, Kwanini msiboreshe huduma za afya pale Tanzania, kwasababu mkishaboresha, watu hawatakuwa na sababu za kutafuta matibabu nje kwa kasi na wingi wa sasa hivi. Je watu watachukua uraia nchi zingine kwa sababu ipi? Au hapo utakuja na sababu nyingine ya ku-validate uraia wa nchi mbili? Mkishaboresha sekta hii, then tutakuwa na listi ndogo sana ya kupeleka wagonjwa kutibiwa nje ambao watakuwa na ulazima, na wizara ya afya itaweza ku-afford hizi if need be.

“Ni kwa nini tumuadhibu huyu Mtanzania wa kuzaliwa kwa kuwa tu amechukua uraia wa nchi nyingine ili apate elimu ama ajira na kusaidia ndugu zake waliobaki Tanzania?” alihoji Waziri Membe. .

Here you go again Mister Minister, boresheni sekta za elimu, sio kukimbilia quick fixes tu. Halafu mnashangaa hao wafadhili mnaowapigia magoti kila siku walete misaada, na wakileta, wana leta quick fix type of aid. They learned from the best, they learned from you!

Mimi naona hivi, kama hii kitu ya dual citizenship ikipitishwa, which I know it will, itapitishwa kwa sababu ya ubabe na kufuata tu upepo, kwasabau kuna nchi zinafanya, basi na sisi tufanye, otherwise, reasons zinazotolewa ku-support this thing are sadly, plain shallow! I said it before, and Im saying it now, hakuna kinachosemwa hapa zaidi ya kutafuta mteremko tuuu! Dezo itatuuwa wabongo, we may as well have the Canadians et al, waje wachukue nchi na kututawala physically ili tusichukue short-cuts za kuhitaji services zao! Be that as it may, watatujengea hospitali na madikari wao waje TZ na tutapata matibabu ya bureee!
 
It was after reading this speech I personally decided, I will not seek the citizenship of another nation for my loyalty remains and will forever be to Tanzania and Tanzania only.[/url]


Mzee mwanakiji, wewe si upo nje ya nchi? watafute waTZ wawili watatu ambao wamechukua uraia wa nchi ya nje halafu uwainterview then utagundua kuwa wao na wewe hakuna tofauti yoyote katika utanzania, uraia wa nchi ya nje upo on paper and nowhere else among these tanzanians, wao bado ni wazalendo, wengine tupo nao hapa Jf wanabanana tuu na wewe na mimi, ila hakuna mtu yeyote anayewababaisha katika nchi wanazoishi, hakuna wakuwafukuza, hakuna wakuwanyima ajira kwa kisingizio cha makaratasi n.k hakuna wa kuwanyanyasa, na Tanzania wanaipenda, wakiongea wana accent ya kitanzania, pesa wanawatumia ndugu zao tanzania, yaani wanabanana kishenzi na wabongo mzee.

Immigration has been in history tangu enzi za wangoni, mbona wakoloni waliokuja tanganyika hatuwaiti wasaliti wa uingereza? mbona walituma hela na malighafi nchini mwao lakini hatukuwaita watanganyika halisi kwa sababu wameamua kuja tanganyika? hawa bado walibaki kuwa waingereza. Kama watanzania wanvyowasupport ndugu zao hapa bongo bado wao ni watanzania mzee, ila makaratasi yanasema vingine. Unafikiri mafisadi kibao pale wizara mbali mbali na BOT ukichunguza makaratasi unaweza kukuta mahesabu yote yanagawanyika lakini kiukweli mahesabu hayakamiliki jamaa wamechukua chao mapema, kwa hiyo ukiona karatasi linasema mahesabu yamekamilika usiamini sana, jamaa kiukweli wanajua kinachoendelea, kwa hiyo ukiona karatasi la mwenzio linasema muingereza wakati jamaa anaongea kiswahili fasaha kama nyerere, jamaa bibi yake analala kwenye nyumba ya udongo kule kijijini na bili ya hospitali ya bibi yake hailipwi na karamagi bali huyu "muingereza" basi weka question mark mzee.
 
Ukweli ni kwamba watu kadhaa mpaka serikalini kwetu wana uraia wa nchi mbili kwa miaka mingi tu na wanaendelea kupeta bila noma wala nini. Sidhani kama hii sheria ya sasa ya uraia tuliyonayo inakuwa enforced...

Nakumbukwa Mwalimu JKN aliwahi kusema akiwa ziarani Canada kuwa hata uchukue uraia wa wapi, Utanzania wako uko palepale maana ukoo wako uko kule hivyo hakuna atakayekuuliza ila akaongezea "lakini ukiingia kwenye siasa utakuwa unajitafutia matatizo"!
 
faida hizo haters

WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Bernard Membe, amesema serikali itahakikisha sheria ya uraia wa nchi mbili inapitishwa kwa manufaa ya Watanzania na taifa na si vinginevyo.

Akizungumza na baadhi ya Watanzania waliokutana naye mjini New York wiki iliyopita katika hoteli ya Grand Hyatt, Waziri Membe alisema lengo la serikali ni kuwasaidia Watanzania na si kugawa uraia wa Tanzania kwa wageni wenye uraia wa nchi zao.

Alisema haingii akilini ni kwa nini Mtanzania wa kuzaliwa anyang'anywe uraia wa Tanzania kwa kuwa amechukua uraia wa nchi nyingine kutafuta faida za kielimu, ajira au hata matibabu.

“Ni kwa nini tumuadhibu huyu Mtanzania wa kuzaliwa kwa kuwa tu amechukua uraia wa nchi nyingine ili apate elimu ama ajira na kusaidia ndugu zake waliobaki Tanzania?” alihoji Waziri Membe.

Waziri alisisitiza kuwa sheria hiyo itakapopitishwa haitatoa mwanya kwa kila mtu kuuvamia uraia wa Tanzania bali itawalinda Watanzania wanaotaka kuchukua uraia wa nchi za nje kwa manufaa yao na taifa kwa ujumla.

Akitoa mfano mmojawapo bila kutaja majina ya wahusika, Waziri Membe alisema anaifahamu familia moja ya Watanzania ambayo ililazimika kuchukua uraia wa Kanada kwa sababu za matibabu, na kwamba kuwanyang'anya uraia watu hawa ni kuwaadhibu bila kujali uhai wao.

Alieleza kuwa familia hiyo ina watoto wawili ambao matibabu yao hugharimu dola 2,000 kwa kila mmoja kwa mwezi, na kwamba kwa kuchukua uraia wa Kanada, matibabu hayo yanakuwa bure. Alihoji je, ni haki kuwanyang'anya uraia wao wa Tanzania?

Akitoa mfano wa manufaa yanayopatikana Ghana, Waziri Membe aliwaambia Watanzania hao kwamba ni muhimu kwa Tanzania kutumia raia wake walioko nje kwa manufaa ya taifa na siyo kuwabagua.

“Mwaka jana pekee wananchi wa Ghana walioko nje waliingiza dola bilioni 2.5 kwa njia mbalimbali halali,” na akaongeza: “Taifa dogo kama Komoro, mwaka jana lilipata dola milioni 89 kutoka kwa wananchi wake walioko Ufaransa pekee.

Akifafanua zaidi, Waziri Membe alisema wakati akiwa Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani kwa kipindi kisichofikia miaka miwili, Tanzania ilitoa uraia kwa wageni 101 na kushangaa ni kwa nini Watanzania wa kuzaliwa wapoteze uraia wao.

Waziri Membe aliwataka Watanzania kujenga umoja thabiti na kuwahakikishia kwamba serikali itakuwa pamoja nao ili kuleta maendeleo kwa taifa, na kwamba mawazo kuwa usalama wa taifa utakuwa hatarini si la jambo kuhofia iwapo sheria itatungwa vizuri.

Tanzania ina raia wake waliosambaa nchi mbalimbali duniani huku idadi kubwa ikiwa katika nchi za Kiarabu za Ghuba ambako wakati serikali ikiongeza ofisi moja ya Ubalozi nchini Oman miaka michache iliyopita ilikadiria kuwa kuna Watanzania laki tano.

Nchi nyingine ambazo Watanzania wanakadiriwa kuwa wengi ni za Marekani Kaskazini na Ulaya Magharibi ambako wako kwa maelfu, ambao wengi wao hukabiliwa pia na utata wa uraia wa watoto wao wanaozaliwa ugenini.

Mjadala wa suala la uraia wa nchi mbili umekuwa ukiendelea nchini katika siku za karibuni ambako kumeibuka kambi za wanaopinga kwa madai ya kulinda maslahi ya nchi na wanaounga mkono kwa madai hayo hayo ya kulinda maslahi ya nchi.
 
Ningependa sana kusikia toka kwa wale wanaopinga Duo citizenship wanieleze ni nchi zipi wanazifahamu wao hazina duo leo hii kisha tutaendelea kuchukua mifano hai ya nchi hizo maanake huwezi kuona faida ama hasara ya kitu kama huna mfano. Tujaribu kutumia vigezo kabla hatujatoa hukumu zetu.

Pili, hili swala la wageni kuja chukua mali zetu, hivi kuna mtu ama sheria inayowakataza wao wasichukue mali zetu wanapokuwa hawana duo ama ndio inakuwa rahisi kwao kuchukua mali hizo na kuzipeleka makwao, mifano tunayo machoni petu kila siku tunalia nao.

Kuna wale wanaosema huwezi ku serve two masters... je, kati yenu kuna mtu ambaye hakufunga ndoa nje ya ndugu zake na akaifanya hiyo kuwa familia yake?... je unapooa/olewa huwa umepoteza kabisa jina la familia yako na kwamba sasa hivi una master mpya!

Maswala ya Mathayo na sijui Yohana yanahusu nini na Uraia mbona kuna Yesu na Mungu! who said/asked who is the master!.. Hii imetoka wapi kupima uraia wa mtu kwa biblia! Nani kasema Ukiwa raia wa Uingereza basi master wako ndio kisha kuwa Muingereza!.. haya ni mawazo finyu ya watu waliotawaliwa..yaani bado tunaendeleza ukoloni wa kifikra. Ni Fikra kama hizi zimeturudisha nyuma hata tumeshindwa kuunda Umoja wa nchi za Kiafrika kwa sababu mawazo yetu siku zote hayatoki nje ya mipaka alotuwekea mkoloni. Tunaishi bado ndani ya kabati ama box kiasi kwamba hata mzee wa shamaba humkataza mwanae kutokwenda mjini mathlan Dar kwa sababu hawezi kuziona faida za mtoto huyo akiwa mbali. Yaani akili zao zimefungwa kiasi kwamba haoni huyu mtoto anaweza vipi kumsaidia akiwa mbali naye.... kuna wazee walitoa laana kwa watoto wao kuoa nje ya kabila zao kwa sababu ya hofu hiyo hiyo!..

Yoote haya yanatokana na kufungwa akili na Utumwa wa fikra!...

Kumradhini, mtanisamehe!
 
Mimi nasema hivi, huu uraia wa nchi mbili utahalalishwa tu, maana sasa hivi upo wa kimyakimya(sio kwa wahindi na waarabu tu hata kwa wabantu tena lukuki na wengine wana nyadhifa serikalini na kwingineko) hivyo muda si mrefu watahalalisha hiyo dual citizenship kwa hiyo wala msikonde...
 
Kisura,

Unapoendelea kusisitiza kuhusu - NI KITU GANI HAKIWEZI KUFANYIKA MPAKA MHUSIKA AWE NA RAIA WA NCHI MBILI?..

Umetajiwa mifano kibao na Mawaziri ikiwa ni pamoja na huyo mgonjwa ambaye kwa kukufahamisha tu ni ktk familia yangu!.

They had no choice kwani matibabu ya maradhi haya ni maelfu ya dola ambazo huwezi kabisa kuzimudu hata kama ungekuwa Karamagi 2007! kwii kwii kwii!

Nadhani Njabu ngabu katupa swali zuri sana na yabidi tujiulize kabla ya kuendelea na yote haya:- HIVI, NI NANI RAIA WA TANZANIA?...kisha tuweke mifano ya nchi ambazo hazina Uraia wa nchi mbili na faida zinazotokana na kutokuwa na Uraia huo maanake hadi sasa naziona nchi zenye Uraia wa nchi mbili zikitajwa kwa faida zake, hasara zake pia zsijaziona zikiandikwa!...

Kama hatuna msingi wa asilia ya Uraia wa Mtanzania sidhani kama tunaweza kulijadili swala hili kwa lugha isiyofungamana na Upande!...
 
Waraka wa uraia wa nchi mbili wakamilika

Na Boniface Meena


WAZIRI wa Mambo ya Ndani, Joseph Mungai amesema waraka wa mapendekezo ya mwananchi kuwa na uraia wa nchi mbili umekamilika na kufikishwa kwenye Baraka Baraza la Mawaziri.

Hata hivyo, waraka huo utapelekwa kwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) ili kupata muafaka wa pande zote mbili za Muungano.

Mugai alisema hayo jana alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuelezea mafanikio ya wizara hiyo na vitengo vyake kwa miaka miwili ya serikali ya awamu ya nne.

"Suala la uraia wa nchi mbili mchakato wake unaendelea na suala la vitambulisho vya uraia pia mchakato wake unaendelea na kwamba mchakato huo utagharimu kiasi cha dola Marekani milioni 152 (karibu 15.2 bilioni )," alisema Mungai.

Akizungumzia suala la wakimbizi, Mungai alisema idadi ya wakimbizi nchini imepungua kutoka 615,000 mwaka 2005 hadi wakimbizi 432,583 mwezi Novemba, mwaka huu baada ya zoezi la kuwarejesha makwao wakimbizi kuendelea vizuri.

Hata hivyo, alisema utafiti uliofanyika kuangalia ni asilimia ngapi ya wakimbizi hao wangependa kurudi nchini mwao hasa wale wa Burundi, imeonekana kuwa asilimia 21ya wakimbizi wa Burundi wangependa kurudi kwao na asilimia 79 wangependa kubaki nchini na hatimaye kuomba uraia.

Kwa upande wa magereza, alisema uwezo wa kisheria wa kutunza wafungwa umeongezeka kutoka wafungwa 22,6699 hadi 27,653 pia wafungwa na mahabusu wamepungua kutoka 46,416 hadi 43,262, lakini hata hivyo bado kuna tatizo la msongamano wa wafungwa na mahabusu gerezani.

Alisema sababu za msongamano katika magereza ni ongezeko la uhalifu nchini ambalo husababisha ongezeko la idadi ya wafungwa lisilowiana na ongezeko la nafasi za kuwahifadhi pamoja kesi zao kuchelewa kusikilizwa mahakamani.

Kuhusu zimamoto Mungai alisema wizara inajitahidi kuboresha miundombinu ya kikosi hicho ili kiweze kukabilia na na majanga ya moto na mengine.

Chanzo: Mwananchi
 
Bila shaka wengi tumekuwa tujiuliza nini hasa sababu ya Bunge letu kuanza mchakato wa kuwawezesha Watanzania wachache wenye nazo yaani wenye "Vijisenti" kuweza kuwa na uraia wa nchi nyingine zaidi ya hii ya sisi masikini. Bila shaka ukishakuwa na vijisenti lazima uwe raia wa UGHAIBUNI.

Swala hili limekuja akilini mwangu na nikaja kugundua kwamba hawa mamilionea watanzania wenzetu sasa wanataka kutumaliza kisha kukimbilia nje ya nchi. Katika hali isiyo ya kawaida hoja hii haikuwa na msingi wowote kiasi cha kumaliza siku kadhaa ndani ya bunge letu. Ila kulikuwa na kitu ninachoweza kukiita sherehe ya KUIGAWA TANZANIA. Baada ya kuchuma na kuridhika au kufikia hadhi ya kuwa ni mkaazi wa Ulaya na Marekani bila kusahau Asia na kwingineko bunge letu lilikubali kujadili mambo ambayo hayakuwa na manufaa kwa wananchi. ""URAIA WA NCHI MBILI""

Tujaribu kugusa hasa kwa undani faida na hasara ya mfumo kama huu, kwa watanzania waliowengi hakuna faida lakini kwa wale ambao ni walengwa na ambao ndiyo walioleta hoja hii hili lina manufaa sana kwao. Tuelewe kwamba kuwa raia wa nchi fulani huhitaji visa kwenda na mara ukisha kuwa katika nchi uliyopo.

SISI WATANZANIA BAADA YA KUGUNDUA KWAMBA VIONGOZI WETU HAMPO KWA AJILI YA MASLAHI YA TAIFA NA KWA KUWA TAYARI MMEPITISHA RASIMU AU MSWADA HUU WA KUWAWEZESHA HAWA MAFISADI KUWEZA KUHAMA NCHI WATAKAVYO; TUAMUOMBA MHESHIMIWA RAISI ASISAINI SHERIA HIYO.
 
Bubu umeongea leo...si mchezo inawezekana wamefikiria ili kujenga mazingira ya wao kutoroka kwa urahisi wakishatupiga bao ni kuwa na huo dual-citizenship maana wanajua kabisa wakichota wakabaki bongo patakuwa hapatoshi lazima tule nao sahani moja. Hapo ndipo wakati mwingine bunge letu linaponitia kichefuchefu kushabikia mambo ya hovyo kama hilo. Nadhani wengi wa mafisadi lazima wata-support tu hilo wazo la dual -citizenship. Mungu awalaaani kabisa
 
Kuna picha kubwa zaidi katika wazo la kuwa na uraia wa nchi mbili kuliko hiyo ya majambazi wetu kuhamisha hela nje ya nchi. Kwa sababu hata sasa ambapo hakuna uraia wa nchi mbili bado hatukuweza kuwazuia majambazi kuiba hela na kuzihamisha nje, kwa hiyo uraia wa nchi mbili hauwezi kuwa licence au kikwazo kwa hao majamaa katika bidii yao ya kutuibia. I hope wabunge walikuwa makini katika kujadili hili jambo.
 
Watanzania wa kawaida/asilia ndio wana uraia wa nchi moja. Mimi sidhani kama MAFISADI hawana uraia wa nchi zaidi ya moja.
 
Kuna picha kubwa zaidi katika wazo la kuwa na uraia wa nchi mbili kuliko hiyo ya majambazi wetu kuhamisha hela nje ya nchi. Kwa sababu hata sasa ambapo hakuna uraia wa nchi mbili bado hatukuweza kuwazuia majambazi kuiba hela na kuzihamisha nje, kwa hiyo uraia wa nchi mbili hauwezi kuwa licence au kikwazo kwa hao majamaa katika bidii yao ya kutuibia. I hope wabunge walikuwa makini katika kujadili hili jambo.

TUNAHITAJI HUO URAIA WA NCHI MBILI TUWEZE KUHAMISHA TECHNOLOJIA NA UFUNDI PILI IWE LAHISI KWETU KU MOVE KUKUSANYA MITAJI,PIA TUWE MACHO NA HILO TULIJADILI LISITUMIKE VIBAYA
 
Back
Top Bottom