Leo asubuhi nimefuatilia mahojiano yaliyorushwa na TBC 1 ukiwashirikisha Mwigulu Nchemba na Zitto Kabwe. Mpango wa maendeleo wa taifa uliopitisha mwaka jana na bunge na kusainiwa na raisi unaanisha wazi kwamba kwa kila bajeti serikali itatenga 35% ya mapato ya ndani kwa ajili ya mipango ya maendeleo. Zitto anaanisha wazi kwamba mwaka huu fedha iliyotengwa kutoka mapato ya ndani ni 0% kinyume na mpango huu hivyo kukiuka azimio la bunge.
Kwa upotoshaji mkubwa Nchemba anasoma mpango wa kiingereza anapotosha kuwa si 35% ya mapato ya ndani bali ni 35% ya bajeti. Ila Zitto anasoma mpango wa kiswahili ambao unaonyesha wazi ni 35% ya mapato ya ndani. Pia bado kwenye hiyo bajeti hiyo 35% ya bajeti kwenye mipango ya maendeleo haionekani. Nchemba anakusanya hadi bajeti yote ya elimu kuongezea walau apate hiyo 35% bado haifiki licha ya kuwa hela nyingi kwenye elimu si maendeleo bali matumizi ya kawaida.
Swali langu hapa je upotoshaji huu wa Nchemba ni kwa faida ya nini? Ni kwa ajili ya kutaka bajeti ipite hata kama haina uhalisia na hata kama inakiuka maazimio ambayo yamepitishwa na bunge?
Nadhani Nchemba anasahau kuwa wananchi wa sasa hivi sio wale wa kuburuzwa tu kwa faida ya chama tawala.
Kwa upotoshaji mkubwa Nchemba anasoma mpango wa kiingereza anapotosha kuwa si 35% ya mapato ya ndani bali ni 35% ya bajeti. Ila Zitto anasoma mpango wa kiswahili ambao unaonyesha wazi ni 35% ya mapato ya ndani. Pia bado kwenye hiyo bajeti hiyo 35% ya bajeti kwenye mipango ya maendeleo haionekani. Nchemba anakusanya hadi bajeti yote ya elimu kuongezea walau apate hiyo 35% bado haifiki licha ya kuwa hela nyingi kwenye elimu si maendeleo bali matumizi ya kawaida.
Swali langu hapa je upotoshaji huu wa Nchemba ni kwa faida ya nini? Ni kwa ajili ya kutaka bajeti ipite hata kama haina uhalisia na hata kama inakiuka maazimio ambayo yamepitishwa na bunge?
Nadhani Nchemba anasahau kuwa wananchi wa sasa hivi sio wale wa kuburuzwa tu kwa faida ya chama tawala.