Upande wa pili wa CCM

mtweve

Member
Mar 28, 2009
96
8
...Binafsi na kwa dhati ya moyo nakiri kuwa hali ya CCM sasa ni mbaya,imezeeka,imekuwa kichaka cha wahuni,wala rushwa,wahujumu uchumi,mafisadi wa mali za umma,mradi wa kuendelea kimaisha...imekuwa simba mzee aliyeng'ooka meno hawezi kuwinda tena. pamoja na yote haya lakn tukumbuke tulikotoka,turudishe hisia zetu mwa 1961 wakati tunaanza kujitawala wenyewe. tulikuwa na barabara ngapi za lami,wangapi walikuwa wanapata maji hata kama ya mgao,wangapi walikuwa na umeme wa gridi ya taifa,achalia ,mbali wangapi walikuwa na uwezo wa kununua jenereta au hata solar power. shule za sekondari,msingi,au hata vyuo vilikuwa vingapi?achalia mbali ubora wa elimu itolewayo. ukweli ni kuwa aliyemaliza kidato cha nne akapata sifuri si sawa na aliyeishia darasa la saba. leo watanzania wengi wanahama kutoka nyumba za tembe au nyasi au makuti wanaishi nyumba za bati ambazo ni bora zaidi ya za tembe.tuache ulimbkeni wa kisiasa,let us be critical. naunga mkono mia kwa mia kuwa kwa sasa ccm haina jipya imeeksipaya,ni vema chama kingine si lazima chadema kikachukua madaraka,ccm ijifunze kutoka huko kabla hatuja sema hayo.....tukipongeze chama cha mapinduzi kwa kazi iliyofanya nzuri japokuwa spidi yake ilikuwa na ndogo na kwa sasa gari haliiendi kabisa,limekufa injini,tutafute gari jingine tufaulishiwe huko....lakini je ni gari gani hilo? lisije likawa kama hili bovu?tukapumbazwa na maneno ya makonda na wapiga debe wake, au rangi yake na maneno ya mbele" V.I.P CLASS"
 
hebu lete gari lako tupande sasa hivi ili tuwahi hio safari yako ya kuzimu.........
 
Mpiga debe ilo gari chakavu unalo hamasisha watu wapande halifai lipo jipya la vijana!mtapata ajari huko!unapotea wewe!
 
Back
Top Bottom