Uongozi wa Nyerere na haja ya Katiba mpya

The Boss

JF-Expert Member
Aug 18, 2009
49,110
115,899
Kuna vitu viwili vinaendelea hapa tanzania
na jf pia..............

Watu wengi wanazungumzia haja na madai ya kuwepo kwa katiba
mpya...
Ambayo itakuwa ya watanzania,ya wananchi.
Itakayowapa uhuru wao na mambo mengi kwa ujumla...

Watu wengi akiwemo issa shivji,mwanakijiji na wengineo

wamedriki kusema kusema au kuunga mkono kuwa

katiba iliyopo sio tu haifai,lakini haijawahi kuwa ya wananchi......


Wakati huo huo,kuna mjadala wa kumkosoa nyerere na utawala wake

mjadala ambao cha kushangaza wale wengi wanaomtetea nyerere kuwa

alikuwa kiongozi bora na wa mfano,
na ambae alikuja kabla ya wakati wake ndio hao hao wanaodai katiba hii tuliyonayo

haifai na haijawahi kuwa ya wananchi......
Ni katiba mbovu,inayowakandamiza wananchi,haiwapi nguvu na uhuru wa kutosha
na kadhalika......

Sasa hapa swali ninalouliza ni hili.............

Inawezekanaje nyerere huyo huyo ambae alikuwa

kiongozi bora sana,na wengine mkimwita ni nabii na mtakatifu aliyekuja kabla

ya muda wake.......lakini leo katiba ile ile aliyoitumia kutawala na kuitengeneza

tuseme haifai kabisa na haina uhalali na sasa tunahitaji mpya?????????????????????????????

Mind you kuwa hatuzungumzii mabadiliko ya katiba tu
tunazungumzia katiba mpya,katiba nyingine inayofaa na sio hii ya nyerere...
 
Kila zama na kitabu chake!

Zama za katiba ya Nyerere zimepita, na na tumo kwenye era' tofauti!

Kwa wakati wake, hata kama katiba ile haikuwa ya wananchi, ilitosha, na ilifanya kazi kubwa sana inayoonekana!
Kutokana na mabadiliko ya miongo tunatamka kuwa sasa haifai, ndiyo argument hiyo!
 
Sasa kiongozi bora anatawala bila ya katiba ya wananchi????????????
 
The Boss, mie naona unauliza swali huku ukiwa na jibu.

Nyerere na katiba ni vitu viwili tofauti. Ni kweli kwamba katiba tuliyonayo haifai kabisa na si ya ki-utu. Uzuri wa Nyerere umetokana na nidhamu ya hali ya juu aliyokuwa nayo yeye kama Nyerere. Pamoja na hilo, wakati Nyerere akitawala mazingira yalikuwa ya mfumo wa chama kimoja. Sasa hivi mazingira yamebadilika sana, kuna mfumo wa vyama vingi na mambo mengi yamebadilika pia. Huwezi endesha nchi yenye vyama vingi kwa mfumo wa katiba ya chama kimoja vinginevyo unataka kuligawa taifa. Kama katiba iliyopo ni nzuri basi kusingelikuwa na haja ya serikali nayo kulikubali hili!
 
wewe hujui kitu
nyerere alikuta nchi ina vyama vingi na katiba nyingine

ni yeye alieleta chama kimoja na katiba hiii tuliyonayo....
 
Sina hakika na Shivji lakini Mwanakijiji atakuwa kwenye wakati mgumu sana hasa akifikiria kwamba katiba iliyopo ni zao la utawala wa awamu ya kwanza. Angetamani leo atamke kwamba katiba hii ilitengenezwa na Kikwete ili amtwishe mzigo huo kwa chuki tu. Thanks God ni Kikwete huyo huyo ndiye sasa aliyeamua ku-midwife upatikanaji wa katiba mpya.
 
Kuna vitu viwili vinaendelea hapa tanzania
na jf pia..............

Watu wengi wanazungumzia haja na madai ya kuwepo kwa katiba
mpya...
Ambayo itakuwa ya watanzania,ya wananchi.
Itakayowapa uhuru wao na mambo mengi kwa ujumla...

Watu wengi akiwemo issa shivji,mwanakijiji na wengineo

wamedriki kusema kusema au kuunga mkono kuwa

katiba iliyopo sio tu haifai,lakini haijawahi kuwa ya wananchi......


Wakati huo huo,kuna mjadala wa kumkosoa nyerere na utawala wake

mjadala ambao cha kushangaza wale wengi wanaomtetea nyerere kuwa

alikuwa kiongozi bora na wa mfano,
na ambae alikuja kabla ya wakati wake ndio hao hao wanaodai katiba hii tuliyonayo

haifai na haijawahi kuwa ya wananchi......
Ni katiba mbovu,inayowakandamiza wananchi,haiwapi nguvu na uhuru wa kutosha
na kadhalika......

Sasa hapa swali ninalouliza ni hili.............

Inawezekanaje nyerere huyo huyo ambae alikuwa

kiongozi bora sana,na wengine mkimwita ni nabii na mtakatifu
aliyekuja kabla

ya muda wake.......lakini leo katiba ile ile aliyoitumia kutawala na kuitengeneza

tuseme haifai kabisa na haina uhalali na sasa tunahitaji mpya?????????????????????????????

Mind you kuwa hatuzungumzii mabadiliko ya katiba tu
tunazungumzia katiba mpya,katiba nyingine inayofaa na sio hii ya nyerere...

Watanzania hawakumwita Nyerere ni nabii na mtakatifu kwa hiyari yao. Nyerere alilazimisha watu wamwite hivyo esp. mara baada ya kurudi toka China alipoonana na chairman Mao
 
Sina hakika na Shivji lakini Mwanakijiji atakuwa kwenye wakati mgumu sana hasa akifikiria kwamba katiba iliyopo ni zao la utawala wa awamu ya kwanza. Angetamani leo atamke kwamba katiba hii ilitengenezwa na Kikwete ili amtwishe mzigo huo kwa chuki tu. Thanks God ni Kikwete huyo huyo ndiye sasa aliyeamua ku-midwife upatikanaji wa katiba mpya.

SI vibaya kumsifu rais pale anapotenda jema. Lakini kwa hili la katiba, bado sana, kwa kifup, kwa sasa hastahili sifa yoyote. Kama tunataka kumwaga sifa kwa ajili ya mchakato unaoendelea wa katiba mpya, basi tuwape vyama vya upinzani (NCCR,CUF,DP-Mtikila, CDM), wanaharakati. wanahabari na wasomi.

Kwa rais wetu hili la katiba mpya halitokani na utashi wake, ameshinikizwa na ndio maana serikali yake ikaja na mswada ambao ulipingwa na kila mtu hadi kufikia hatua ya kuchanwa hadharani na pia kurudishwa serikalini na bunge. Hii maana yake ni kwamba, bado haelewi wananchi wake wanataka nini. Kiongozi mwenye utashi anajua nn cha kuwapa watu wake na hukitekeleza kwa moyo mkunjufu. Angejua umuhimu wa katiba mpya kwa sasa, angeweka kama ktk ilani ya chama chake wakat wa uchaguzi 2010.
 
wewe hujui kitu
nyerere alikuta nchi ina vyama vingi na katiba nyingine

ni yeye alieleta chama kimoja na katiba hiii tuliyonayo....

Nchi ngapi za kiafrika zina vyama vingi toka zilipopata uhuru?
 
Sina hakika na Shivji lakini Mwanakijiji atakuwa kwenye wakati mgumu sana hasa akifikiria kwamba katiba iliyopo ni zao la utawala wa awamu ya kwanza. Angetamani leo atamke kwamba katiba hii ilitengenezwa na Kikwete ili amtwishe mzigo huo kwa chuki tu. Thanks God ni Kikwete huyo huyo ndiye sasa aliyeamua ku-midwife upatikanaji wa katiba mpya.

No Mbopo,Dont go that way...you are aiming too low now.Kwa mantiki hiyo uliyoonyesha hapo juu Wewe pia hauna tofauti na Mwanakijiji kwa sababu hata wewe unamhusudu Jk kuliko.Kwa hiyo comment yako bado umeonyesha partiality,imekaa kimaslahi/kiutetezi utetezi..hata wewe uko katika tanuru zaidi!

Aisee,comment yako nimecheka sana,loh una bahati niko barabarani
 
Tupe basi hotuba aliyoitoa akiwataka Watanzania wamwite nabii na mtakatifu. Angalau tupe nukuu ya gazeti. People are busy re-writing history substituting facts for fiction.

Manung'uniko ya chinichini yalikuwa mengi mno wakati JKN alipokuwa raisi na siasa zake za ukomunisti. Hata huo ujamaa wake watu wengi hawakuutaka kabisa na waliupinga kichinichini na hakukuwa hotuba ya kulazimisha watu ila mazingira aliyoyatengeneza wakati akiongoza nchi ilikuwa huna jinsi ya kumpinga ukijaribu unapotea. Kasanga Tumbo, Kambona na wananchi wengi akiwemo mzazi wangu walijaribu na umeona waliishia wapi?
 
Manung'uniko ya chinichini yalikuwa mengi mno wakati JKN alipokuwa raisi na siasa zake za ukomunisti. Hata huo ujamaa wake watu wengi hawakuutaka kabisa na waliupinga kichinichini na hakukuwa hotuba ya kulazimisha watu ila mazingira aliyoyatengeneza wakati akiongoza nchi ilikuwa huna jinsi ya kumpinga ukijaribu unapotea. Kasanga Tumbo, Kambona na wananchi wengi akiwemo mzazi wangu walijaribu na umeona waliishia wapi?
Yeah, najua Kambona alikimbilia London, baada ya njama zake za kupindua serikali kugundulika. Kasanga Tumbo naye alitamba kuwa amepewa hela na Waingereza apindue serikali. Akaswekwa lupango. Yaliyowapata wazazi wako siyajui. Lakini nina hakika hawakuwa innocent bystanders.
 
two wrongs do not make it right

Quite correct! But that was a rhetorical question. The real question is why the idea of multi-party system only became so famous and relevant as late as 1990s? By 1990s, the World was no longer polarized. Maintaining National unity (e.g. through single party system) was no longer an issue and necessary as it was during the cold war. The West started to dominate and dictate in almost every aspect of life (politically, socially and economically). Since then, you are either for or against the West.
 
Yeah, najua Kambona alikimbilia London, baada ya njama zake za kupindua serikali kugundulika. Kasanga Tumbo naye alitamba kuwa amepewa hela na Waingereza apindue serikali. Akaswekwa lupango. Yaliyowapata wazazi wako siyajui. Lakini nina hakika hawakuwa innocent bystanders.

Kwa hiyo are u trying to say that watanzania wote walikubaliana na mawazo ya mwalimu na siasa zake?
 
Back
Top Bottom