i-store
Member
- Mar 10, 2020
- 54
- 65
Hivi kwenye ishu kama hii unafanyaje wakuu.
Huyu jamaa yangu wa siku nyingi (tumwite W) alikuwa na demu wake (tumwite D) wa kanda ya kati huko. Huyu binti alimpenda sana jamaa. Yaani alishaniambia nikiwa nachati nae private sio mara moja (Nampenda sana rafiki yako ila naona hata hanipi muda).
Inshort jamaa alikuwa anapiga tu siku ziende ukizingatia kuwa mtarajiwa alikuwa nje kimasomo. Nilijua hawezi muoa ila sikuwahi kumwambia ila yeye kila wakikosana ananipigia eti shemu W sijui nini na nini! Mi nampa pole nampigia jamaa nasolve yanaisha.
Mara hamadi demu wa nje akarudi, ikabidi jamaa ahame kimya kimya pale home akapanga mbali kidogo. Nilipata shida sana mana jamaa alinipa onyo nisije mwambia D. Yaani D alichanganyikiwa alikuwa anafanya kazi sehemu akaacha kazi akawa anashinda analala ndani hali chakula analia tu. Kila akipoa ananipigia simu nimwambie aliko W. Mimi sikutaka kuvunja kiapo nilimwambia atulie atulie ajipe muda lakini wapi. Kuna siku napigiwa kalazwa. Nikaenda kumcheck kakonda balaa. Nikampigia jamaa hata hakutikisika kabisa. Ikabidi nichukue mzigo. Walikuwa na mdogo wake pale, ikabidi nijipe majukumu. Alikaa kama siku 4 akarudi home.
Alivorudi home kila nikitoka lindoni namtembelea nahakikisha amekula napiga nae story ila nilisema sitaweza zungumzia ishu ya W. Naikumbukwe tayari alishaanza maandalizi ya harusi kabisa. Siku zikaenda, dada wa watu hata hasikii la mtu anamwulizia W.
Baadaye akaenda mkoa (akasema anaondoka Dar jumla) anaomba amuag W (nikacheka nikasema haiwezekani). Wakati huu jamaa anahudhuria mafunzo ya ndoa. Basi bana akauza vitu akaondoka zake. Ila tuliendelea kuwasiliana. Kila muda anamwulizia W. Baadaye nikamdanganya yuko nje kusoma. Akahamaki, sasa kulikuwa na ugumu gani kuniambia toka mwanzo.
Siku zilienda D akarudishwa Dar baada ya boss wake kumtaka arudi. Alinipigia kuwa anakuja Dar ila atafikia kwa boss kwanza nikamwambia karibu. Hapo ni almost miaka 2. Ikumbukwe huyu W alihangaika sana ila alikuwa hajapata mtoto. Siku moja nikamwambia D tunaenda sehemu fulani kupiga vyombo wewe njoo kama imekuwa ajali tu. Na uonyeshe kama hukujua. Ila sasa nilimwambia jamaa alisha oa so anatakiwa kubehave.
Kama nilivomwelekeza akaja pale, hata hakuonyesha kushituka. Wakasalimiana pale story zikaendelea mara ulipotelea wapi mara sijui nini. Yeye alikuwa hanywi jamaa kupoza kamwagizia juice chakula cha kushiba, jioni akaenda kwake (alishapanga).
Sasa kumbe walipeana namba pale wakaendelea kuwasiliana tena. Jamaa akafufua tena. Mimi hata sijui na sikuambiwa tena. Siku moja nakutana nae naona ana mimba ya kama ya miezi 7 nauliza vipi anacheka tu anasema ya W. Ikumbukwe bado hajafanikiwa kupata mtoto na yule wife wake.
Sasa wiki jana kajifungua mapacha wawili wakiume copy ya jamaa kabisa. Jamaa kachanganyikiwa. Ana furaha na huzuni vimechanganyikana. Demu aliachishwa kazi na amepewa dada wa kazi. Mama yake amemwambia waoane tu hata kama ni bi mdogo na huyu D hana shida.
Sasa shida mke wake hawezi kubali hilo na yy hataki kutengana nae. Alimtaarifu mama ake (W) akafurahi sana. Sasa ni kama kila mtu anajua kasoro wife wake. Trend inaonyesha atajua soon. Sasa tumepiga hesabu tumwambie ukweli au tumfiche aje kujua mwenyewe? W anataka mimi niongee taratibu na wife wake. Nimegoma aisee.
Bado tuko njia panda. Assume ni wewe hapa unatokaje?
Huyu jamaa yangu wa siku nyingi (tumwite W) alikuwa na demu wake (tumwite D) wa kanda ya kati huko. Huyu binti alimpenda sana jamaa. Yaani alishaniambia nikiwa nachati nae private sio mara moja (Nampenda sana rafiki yako ila naona hata hanipi muda).
Inshort jamaa alikuwa anapiga tu siku ziende ukizingatia kuwa mtarajiwa alikuwa nje kimasomo. Nilijua hawezi muoa ila sikuwahi kumwambia ila yeye kila wakikosana ananipigia eti shemu W sijui nini na nini! Mi nampa pole nampigia jamaa nasolve yanaisha.
Mara hamadi demu wa nje akarudi, ikabidi jamaa ahame kimya kimya pale home akapanga mbali kidogo. Nilipata shida sana mana jamaa alinipa onyo nisije mwambia D. Yaani D alichanganyikiwa alikuwa anafanya kazi sehemu akaacha kazi akawa anashinda analala ndani hali chakula analia tu. Kila akipoa ananipigia simu nimwambie aliko W. Mimi sikutaka kuvunja kiapo nilimwambia atulie atulie ajipe muda lakini wapi. Kuna siku napigiwa kalazwa. Nikaenda kumcheck kakonda balaa. Nikampigia jamaa hata hakutikisika kabisa. Ikabidi nichukue mzigo. Walikuwa na mdogo wake pale, ikabidi nijipe majukumu. Alikaa kama siku 4 akarudi home.
Alivorudi home kila nikitoka lindoni namtembelea nahakikisha amekula napiga nae story ila nilisema sitaweza zungumzia ishu ya W. Naikumbukwe tayari alishaanza maandalizi ya harusi kabisa. Siku zikaenda, dada wa watu hata hasikii la mtu anamwulizia W.
Baadaye akaenda mkoa (akasema anaondoka Dar jumla) anaomba amuag W (nikacheka nikasema haiwezekani). Wakati huu jamaa anahudhuria mafunzo ya ndoa. Basi bana akauza vitu akaondoka zake. Ila tuliendelea kuwasiliana. Kila muda anamwulizia W. Baadaye nikamdanganya yuko nje kusoma. Akahamaki, sasa kulikuwa na ugumu gani kuniambia toka mwanzo.
Siku zilienda D akarudishwa Dar baada ya boss wake kumtaka arudi. Alinipigia kuwa anakuja Dar ila atafikia kwa boss kwanza nikamwambia karibu. Hapo ni almost miaka 2. Ikumbukwe huyu W alihangaika sana ila alikuwa hajapata mtoto. Siku moja nikamwambia D tunaenda sehemu fulani kupiga vyombo wewe njoo kama imekuwa ajali tu. Na uonyeshe kama hukujua. Ila sasa nilimwambia jamaa alisha oa so anatakiwa kubehave.
Kama nilivomwelekeza akaja pale, hata hakuonyesha kushituka. Wakasalimiana pale story zikaendelea mara ulipotelea wapi mara sijui nini. Yeye alikuwa hanywi jamaa kupoza kamwagizia juice chakula cha kushiba, jioni akaenda kwake (alishapanga).
Sasa kumbe walipeana namba pale wakaendelea kuwasiliana tena. Jamaa akafufua tena. Mimi hata sijui na sikuambiwa tena. Siku moja nakutana nae naona ana mimba ya kama ya miezi 7 nauliza vipi anacheka tu anasema ya W. Ikumbukwe bado hajafanikiwa kupata mtoto na yule wife wake.
Sasa wiki jana kajifungua mapacha wawili wakiume copy ya jamaa kabisa. Jamaa kachanganyikiwa. Ana furaha na huzuni vimechanganyikana. Demu aliachishwa kazi na amepewa dada wa kazi. Mama yake amemwambia waoane tu hata kama ni bi mdogo na huyu D hana shida.
Sasa shida mke wake hawezi kubali hilo na yy hataki kutengana nae. Alimtaarifu mama ake (W) akafurahi sana. Sasa ni kama kila mtu anajua kasoro wife wake. Trend inaonyesha atajua soon. Sasa tumepiga hesabu tumwambie ukweli au tumfiche aje kujua mwenyewe? W anataka mimi niongee taratibu na wife wake. Nimegoma aisee.
Bado tuko njia panda. Assume ni wewe hapa unatokaje?