Unawezaje kujilinda na radi wakati wa mvua kubwa? Kuzima data kunaeupusha kupigwa na radi? Kufahamu hayo na mengine mengi soma uzi huu

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,812
11,988
radii.jpg

JamiiForums imefanya mahojiano na Rose Senyagwa, Mtaalam na Mchambuzi wa Hali ya Hewa kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA), ambapo alieleza kwa kirefu nini watu wanatakiwa kufanya ili kujilinda pale kunapokuwa na radi

====

Radi ni nini?
Radi ni umeme, umeme huu unatoka katika mawingu na hasa katika wingu linaloitwa wingu anga, wingu linalorefuka kwenda juu kwa mfano wa kichuguu, na kwa kawaida linakuwa na barafu ndani yake. Sasa pale ambapo wingu na wingu likigongana, zile barafu zinagongana na kutoa umeme. Mvua za barafu hutokea mawingu haya yanapokuwa mazito na kushuka chini kama mvua ambayo ndio inajulikana kama mvua ya mawe.

Umeme huo wa radi unapotokea unaweza kwenda sehemu yoyote, inaweza kutoka kwenye wingu kwenda juu, kwenda kwenye wingu jingine, au kutoka kwenye wingu na kuja ardhini. Inapokuja ardhini ndio inasababisha madhara kwa binadamu na viumbe vingine pamoja na vitu vingine ardhini, lakini ikichukua uelekeo mwingine inakuwa haina madhara kwa binadamu.

Kama radi inapiga unatakiwa kuepuka mambo gani?
Kama radi inapiga si salama kujificha/kujikinga chini ya miti mirefu kwasababu kwa kawaida radi ikipiga chaji ya umeme inapotoka kwenye wingu inaenda uelekeo wowote (yaani haichagui) kitu cha kwanza kirefu kuliko vyote katika eneo hilo itakachokutana nayo itapiga hapo.

Lakini pia miti miti ina uwezo wa kusafirisha umeme. Lakini pia minara au kitu chochote kirefu sio salama kujikinga chini yake radi inapopiga, hii inajumuisha pia nguzo za umeme, hata transfoma

Pia kunapokuwa na radi haishauriwi kutembea katika maji yanayotiririka au yaliyotuama. Mfano madimbwi au maji yanayotembea barabarani, sehemu zenye maji kama mtoni, ziwani au kwenye mabwawa, hii ni sababu radi inaweza ikawa imepiga kwenye eneo fulani ardhini au chanzo cha maji, ule umeme wa radi utasafiri kufuata uelekeo wa maji. Kwahiyo mtu unapokuw aunatembea barabarani maji yanatiririka haushairiwi kukanyaga maji hayo sababu huwezi kujua kama maji hayo yana umeme.

Mbali na hilo haishauriwi kutumia vifaa vya umeme au vinavyokamata mionzi mfano simu/Kompyuta au laptop, TV, redio, friji nk sababu vinaingiliana na radi kupitia mionzi, ambapo inaweza kusafirisha mionzi na radi na hivyo kusababisha kupigwa na shoti.

Nyumba na majengo mengine yana mfumo wa kulinda radi?
Majengo huwa yanawekewa mfumo ya kuzuia radi kupiga kwenye majengo (Erthing) ambapo radi ikipiga mfumo huo hufanya chaji ya umeme kupelekwa uelekeo wa ardhini badala ya kupiga kwenye jengo, hivyo ni vizuri kwa nyumba pamoja na majengo mengine kuwekewa mfumo huo

Mvua inayoambatana na radi inaponyesha ni vizuri uwe salama, kaa nyumbani tulia kama hakuna ulazima sababu radi inaweza kupiga sehemu yoyote na kama utakuwa kwenye maeneo hayo hatarishi ni rahisi kupigwa na radi sababu ni mazingira yanayokaribisha radi.

Nguo nyekundu zina uhusian gani na radi?
Nguo nyekundu au nguo yenye rangi yoyote haina uhusiano wowote na radi, ni imaji iliyojengeka kwa watu. Mtaalamu anasema hata yeye aliwahi kuambiwa hivyo akiwa mtoto na walikuwa na tabia ya kuwakimbia watu wanaokuwa wamevaa nguo nyekundu wakati radi inapiga lakini kitaalamu hakuna uhusiano wowote kati ya nguo nyekundu au rangi yoyote na radi.

Je, kuzima data kwenye simu inasaidia kukuepusha kupigwa na radi kupitia kifaa hicho?
Kuzima data inaondoa tu mtandao kwenye simu lakini simu za kawaida zinaweza kuingia, hii inamaanisha mionzi bado inasafiri, hivyo bado unaweza kupigwa na radi ikiwa umezima data kwenye simu yako. Ni vizuri kuizima kabisa au usipokee simu wakati radi inapiga.

Radi zinavyopiga juu wakati ndege pia zinapita na tunajua ndege zinatumia umeme, kwanini huwa haziathiriki/haziguswi?
Radi ni hatari sana kwa usalama wa anga upande wa ndege, kwasababu ndege ikipita kwenye wingu lenye radi na ikatokea ndege inapita halafu radi ikapiga kuna uwezekano mkubwa wa ndege kulipuka.

Kinachofanyika ni kuwa; wingu la radi sio wakati wote litasambaa eneo lote la anga, kunaweza kukawa na mawingu upande mmoja tu wa anga, Rubanikabla hajaanza ruti yake au anapokuwa kwenye ruti yake kuna vifaa lakini pia anapata taarifa za hali ya hewa za kujua hili wingu lipo wapi, hivyo huwa wanalikwepa wingu hilo ili kuepusha madhara.

Kabla hajaruka anapewa tarifa ya hali ya hewa kujua hili wingu lipo uelekeo gani, kwahiyo yeye anapanga mipango kulikwepa wingu hilo, ndio wakati mwingine ruti inakuwa ndefu kidogo sababu analizunguka lile wingu, sababu haifai kukatiza katika wingu hilo.
 

JamiiForums imefanya mahojiano na Rose Senyagwa, Mtaalam na Mchambuzi wa Hali ya Hewa kutoka TMA, ambapo alieleza kwa kirefu nini watu wanatakiwa kufanya ili kujilinda pale kunapokuwa na radi

====

Radi ni nini?

Radi ni umeme, umeme huu unatoka katika mawingu na hasa katika wingu linaloitwa wingu anga, wingu linalorefuka kwenda juu kwa mfano wa kichuguu, na kwa kawaida linakuwa na barafu ndani yake. Sasa pale ambapo wingu na wingu likigongana, zile barafu zinagongana na kutoa umeme. Mvua za barafu hutokea mawingu haya yanapokuwa mazito na kushuka chini kama mvua ambayo ndio inajulikana kama mvua ya mawe.

Umeme huo wa radi unapotokea unaweza kwenda sehemu yoyote, inaweza kutoka kwenye wingu kwenda juu, kwenda kwenye wingu jingine, au kutoka kwenye wingu na kuja ardhini. Inapokuja ardhini ndio inasababisha madhara kwa binadamu na viumbe vingine pamoja na vitu vingine ardhini, lakini ikichukua uelekeo mwingine inakuwa haina madhara kwa binadamu.

Kama radi inapiga unatakiwa kuepuka mambo gani?

Kama radi inapiga si salama kujificha/kujikinga chini ya miti mirefu kwasababu kwa kawaida radi ikipiga chaji ya umeme inapotoka kwenye wingu inaenda uelekeo wowote (yaani haichagui) kitu cha kwanza kirefu kuliko vyote katika eneo hilo itakachokutana nayo itapiga hapo. Lakini pia miti miti ina uwezo wa kusafirisha umeme. Lakini pia minara au kitu chochote kirefu sio salama kujikinga chini yake radi inapopiga, hii inajumuisha pia nguzo za umeme, hata transfoma

Pia kunapokuwa na radi haishauriwi kutembea katika maji yanayotiririka au yaliyotuama. Mfano madimbwi au maji yanayotembea barabarani, sehemu zenye maji kama mtoni, ziwani au kwenye mabwawa, hii ni sababu radi inaweza ikawa imepiga kwenye eneo fulani ardhini au chanzo cha maji, ule umeme wa radi utasafiri kufuata uelekeo wa maji. Kwahiyo mtu unapokuw aunatembea barabarani maji yanatiririka haushairiwi kukanyaga maji hayo sababu huwezi kujua kama maji hayo yana umeme.

Mbali na hilo haishauriwi kutumia vifaa vya umeme au vinavyokamata mionzi mfano simu/Kompyuta au laptop, TV, redio, friji nk sababu vinaingiliana na radi kupitia mionzi, ambapo inaweza kusafirisha mionzi na radi na hivyo kusababisha kupigwa na shoti.

Nyumba na majengo mengine yana mfumo wa kulinda radi?

Majengo huwa yanawekewa mfumo ya kuzuia radi kupiga kwenye majengo (Erthing) ambapo radi ikipiga mfumo huo hufanya chaji ya umeme kupelekwa uelekeo wa ardhini badala ya kupiga kwenye jengo, hivyo ni vizuri kwa nyumba pamoja na majengo mengine kuwekewa mfumo huo

Mvua inayoambatana na radi inaponyesha ni vizuri uwe salama, kaa nyumbani tulia kama hakuna ulazima sababu radi inaweza kupiga sehemu yoyote na kama utakuwa kwenye maeneo hayo hatarishi ni rahisi kupigwa na radi sababu ni mazingira yanayokaribisha radi

Nguo nyekundu zina uhusian gani na radi?

Nguo nyekundu au nguo yenye rangi yoyote haina uhusiano wowote na radi, ni imaji iliyojengeka kwa watu. Mtaalamu anasema hata yeye aliwahi kuambiwa hivyo akiwa mtoto na walikuwa na tabia ya kuwakimbia watu wanaokuwa wamevaa nguo nyekundu wakati radi inapiga lakini kitaalamu hakuna uhusiano wowote kati ya nguo nyekundu au rangi yoyote na radi

Je, kuzima data kwenye simu inasaidia kukuepusha kupigwa na radi kupitia kifaa hicho?

Kuzima data inaondoa tu mtandao kwenye simu lakini simu za kawaida zinaweza kuingia, hii inamaanisha mionzi bado inasafiri, hivyo bado unaweza kupigwa na radi ikiwa umezima data kwenye simu yako. Ni vizuri kuizima kabisa au usipokee simu wakati radi inapiga

Radi zinavyopiga juu wakati ndege pia zinapita na tunajua ndege zinatumia umeme, kwanini huwa haziathiriki/haziguswi?

Radi ni hatari sana kwa usalama wa anga upande wa ndege, kwasababu ndege ikipita kwenye wingu lenye radi na ikatokea ndege inapita halafu radi ikapiga kuna uwezekano mkubwa wa ndege kulipuka. Kinachofanyika ni kuwa; wingu la radi sio wakati wote litasambaa eneo lote la anga, kunaweza kukawa na mawingu upande mmoja tu wa anga, Rubanikabla hajaanza ruti yake au anapokuwa kwenye ruti yake kuna vifaa lakini pia anapata taarifa za hali ya hewa za kujua hili wingu lipo wapi, hivyo huwa wanalikwepa wingu hilo ili kuepusha madhara

Kabla hajaruka anapewa tarifa ya hali ya hewa kujua hili wingu lipo uelekeo gani, kwahiyo yeye anapanga mipango kulikwepa wingu hilo, ndio wakati mwingine ruti inakuwa ndefu kidogo sababu analizunguka lile wingu, sababu haifai kukatiza katika wingu hilo

1. Kuwahoji TMA kuhusu radi ni kujilisha upepo.

2. Kuhusu radi, sana sana kuwahoji wahandisi umeme wabobezi jalalani ubungo pale.
 
Nimesikia matukio mango kuhusu uwepo wa radi toka nikiwa kinda kbisa, radi inatokea wakati wa mvua inapokuwa inanyesha na pia inaweza kutokea kama kukiwa na mawingu ya mvua angani maisha yangu yote sijawahi kusikia mtu kapigwa radi akiwa kwenye gari hata kama anachezea vifaa vya kielectronic kama simu na n.k
naomba kujuzwa inakuja hii
 
Nimetoa mahali kwa mtaalamu, kimalkia lakini kinaeleweka kama unapenda na umeweka nia ya kujifunza!

Do’s and Don’ts – Lightning and Thunderstorm​


  • If the people are in outdoors, they have to need shelter from lightning. Buildings are best for shelter, but if no buildings are available, you can find protection in a cave, ditch, car, hard top automobile or a canyon. Trees are not good cover, since tall trees attract lightning.

  • If you can’t find any shelter, avoid the tallest object in the area. If only isolated trees are nearby, your best protection is to crouch in the open.

  • If you hear thunder, don’t go outside unless absolutely necessary. Remember, by counting the seconds between the lightning flash and the thunder and dividing by 3, you can estimate your distance from the strike (in km).

  • Stay away from anything that could conduct electricity such as radios, toasters, hairdryers and Unplug any electronic equipments before the thunderstorm arrives. This may also include fireplaces, radiators, stoves metal pipes, sinks, and phones.

  • Stay away from window and doors and stay off verandas.

  • Avoid contact with plumbing and metal pipes. Do not wash your hands, do not take a shower, do not wash dishes and do not wash clothes

  • Stay away from TV, plumbing, sinks, tubs, radiators and stoves.

  • Get out of the water. This includes getting off small boats on the water, away from pools, lakes and other water bodies.

  • When you feel electric charge – if your hair stands up or your skin starts to tingle, lightning may be about be strike you. Drop to the ground immediately.

  • Lightning is also a real threat to livestock. Livestock frequently gathers under trees during a thunderstorm, and a single strike can kill many animals. Moving animals into a shelter, preferably an enclosed one that is equipped with a lightning protection system can reduce the risk to livestock.


 
Mimi hapo kwenye mawingu kugongana na kuzalisha umeme nitakuwa wa mwisho kuelewa labda kama kuna kitu kingine kinaongezeka kuzalisha umeme huo,au mtoa maelezo hukumalizia maelezo hadi mwisho.
TMA pia tumieni hiyo fursa ya umeme wa radi shirikianeni na wataalamu wetu toka shirika letu pendwa na mfano kote ukanda wa kusini mwa jagwa la Sahara yaani TANESCO,ili umeme wa radi uunganishwe kwenye gridi ya taifa tuondokane na tatizo la umeme.Kwani kama huo wa radi unapotea tu na wataalamu tukuka tunao.
 
Kwenye ndege siku hakuna hatari ya radi tena,baada ya ugunduzi wa ndege na kuanza kufanya kazi swala la radi lilikuwa changamoto haswa hadi pale wataalamu walipokaa na kulitafutia uvumbuzi.
 

JamiiForums imefanya mahojiano na Rose Senyagwa, Mtaalam na Mchambuzi wa Hali ya Hewa kutoka TMA, ambapo alieleza kwa kirefu nini watu wanatakiwa kufanya ili kujilinda pale kunapokuwa na radi

====

Radi ni nini?

Radi ni umeme, umeme huu unatoka katika mawingu na hasa katika wingu linaloitwa wingu anga, wingu linalorefuka kwenda juu kwa mfano wa kichuguu, na kwa kawaida linakuwa na barafu ndani yake. Sasa pale ambapo wingu na wingu likigongana, zile barafu zinagongana na kutoa umeme. Mvua za barafu hutokea mawingu haya yanapokuwa mazito na kushuka chini kama mvua ambayo ndio inajulikana kama mvua ya mawe.

Umeme huo wa radi unapotokea unaweza kwenda sehemu yoyote, inaweza kutoka kwenye wingu kwenda juu, kwenda kwenye wingu jingine, au kutoka kwenye wingu na kuja ardhini. Inapokuja ardhini ndio inasababisha madhara kwa binadamu na viumbe vingine pamoja na vitu vingine ardhini, lakini ikichukua uelekeo mwingine inakuwa haina madhara kwa binadamu.

Kama radi inapiga unatakiwa kuepuka mambo gani?

Kama radi inapiga si salama kujificha/kujikinga chini ya miti mirefu kwasababu kwa kawaida radi ikipiga chaji ya umeme inapotoka kwenye wingu inaenda uelekeo wowote (yaani haichagui) kitu cha kwanza kirefu kuliko vyote katika eneo hilo itakachokutana nayo itapiga hapo. Lakini pia miti miti ina uwezo wa kusafirisha umeme. Lakini pia minara au kitu chochote kirefu sio salama kujikinga chini yake radi inapopiga, hii inajumuisha pia nguzo za umeme, hata transfoma

Pia kunapokuwa na radi haishauriwi kutembea katika maji yanayotiririka au yaliyotuama. Mfano madimbwi au maji yanayotembea barabarani, sehemu zenye maji kama mtoni, ziwani au kwenye mabwawa, hii ni sababu radi inaweza ikawa imepiga kwenye eneo fulani ardhini au chanzo cha maji, ule umeme wa radi utasafiri kufuata uelekeo wa maji. Kwahiyo mtu unapokuw aunatembea barabarani maji yanatiririka haushairiwi kukanyaga maji hayo sababu huwezi kujua kama maji hayo yana umeme.

Mbali na hilo haishauriwi kutumia vifaa vya umeme au vinavyokamata mionzi mfano simu/Kompyuta au laptop, TV, redio, friji nk sababu vinaingiliana na radi kupitia mionzi, ambapo inaweza kusafirisha mionzi na radi na hivyo kusababisha kupigwa na shoti.

Nyumba na majengo mengine yana mfumo wa kulinda radi?

Majengo huwa yanawekewa mfumo ya kuzuia radi kupiga kwenye majengo (Erthing) ambapo radi ikipiga mfumo huo hufanya chaji ya umeme kupelekwa uelekeo wa ardhini badala ya kupiga kwenye jengo, hivyo ni vizuri kwa nyumba pamoja na majengo mengine kuwekewa mfumo huo

Mvua inayoambatana na radi inaponyesha ni vizuri uwe salama, kaa nyumbani tulia kama hakuna ulazima sababu radi inaweza kupiga sehemu yoyote na kama utakuwa kwenye maeneo hayo hatarishi ni rahisi kupigwa na radi sababu ni mazingira yanayokaribisha radi

Nguo nyekundu zina uhusian gani na radi?

Nguo nyekundu au nguo yenye rangi yoyote haina uhusiano wowote na radi, ni imaji iliyojengeka kwa watu. Mtaalamu anasema hata yeye aliwahi kuambiwa hivyo akiwa mtoto na walikuwa na tabia ya kuwakimbia watu wanaokuwa wamevaa nguo nyekundu wakati radi inapiga lakini kitaalamu hakuna uhusiano wowote kati ya nguo nyekundu au rangi yoyote na radi

Je, kuzima data kwenye simu inasaidia kukuepusha kupigwa na radi kupitia kifaa hicho?

Kuzima data inaondoa tu mtandao kwenye simu lakini simu za kawaida zinaweza kuingia, hii inamaanisha mionzi bado inasafiri, hivyo bado unaweza kupigwa na radi ikiwa umezima data kwenye simu yako. Ni vizuri kuizima kabisa au usipokee simu wakati radi inapiga

Radi zinavyopiga juu wakati ndege pia zinapita na tunajua ndege zinatumia umeme, kwanini huwa haziathiriki/haziguswi?

Radi ni hatari sana kwa usalama wa anga upande wa ndege, kwasababu ndege ikipita kwenye wingu lenye radi na ikatokea ndege inapita halafu radi ikapiga kuna uwezekano mkubwa wa ndege kulipuka. Kinachofanyika ni kuwa; wingu la radi sio wakati wote litasambaa eneo lote la anga, kunaweza kukawa na mawingu upande mmoja tu wa anga, Rubanikabla hajaanza ruti yake au anapokuwa kwenye ruti yake kuna vifaa lakini pia anapata taarifa za hali ya hewa za kujua hili wingu lipo wapi, hivyo huwa wanalikwepa wingu hilo ili kuepusha madhara

Kabla hajaruka anapewa tarifa ya hali ya hewa kujua hili wingu lipo uelekeo gani, kwahiyo yeye anapanga mipango kulikwepa wingu hilo, ndio wakati mwingine ruti inakuwa ndefu kidogo sababu analizunguka lile wingu, sababu haifai kukatiza katika wingu hilo
Umeelezea vizuri ila mengi umetupiga kamba
 
Kuna mwamba alikua anapiga tipper kokotokaribu na nguzo ya umeme sijui hakuuona waya bodi likaugusa huo mzinga wake ulikua sio wa kitoto ilikua Kama bm la Hamas. Dadeki tairi 7 zili bust palepale dereva aliikimbia gari body likawa bado limegusa waya mpaka mchina akaja kushusha body. Umeme ni nyoko
 
HV wale wa kusini nasikiaga wanatengeneza radi na kukutumia mchana kweupe pasipo wingu ama mnvua. Ni ya kweli au uongo
 
Back
Top Bottom