Unafiki huu wa kujitoa ICC

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,632
697,796
Naona kuna mwamko mkubwa sana wa nchi za kiafrika ambazo ni wanachama wa mahakama ya kimataifa ya uhalifu wa kivita kujitoa kwa kisingizio cha kuwa eti wanaoandamwa ni viongozi wa kiafrika tu.

Tangu kuanzishwa kwake mwaka 2002 huku nchi nyingi za kiafrika zikishadadia kwa nguvu sana kati ya kesi 12 zilizotolewa maamuzi 9 ni za viongozi wa Afrika.

Naita ni unafiki kwakuwa viongozi hawa hawawaambii ukweli hao pimbi bwana wakubwa wanaowapeleka watakavyo viongozi wetu haya wenye akili finyu sana.

Wanapopambana kubaki madarakani hata kwa gharama ya damu isiyo na hatia! Wanapominya demokrasia, wanapoua kwa kisingizio cha kuzima uasi na kulinda nchi misaada ya hali na mali miundombinu silaha na vifaa vya kijeshi vyote hivi hupata toka kwa hao hao pimbi waanzilishi wa hiyo mahakama ya uhalifu wa kivita ambayo makao yake makuu yako The Hague nchini Uholanzi.

Leo anakuuzia silaha kwa mlango wa nyuma unapaisha uchumi wake, kisha unatumia hizo silaha kuangamiza wananchi wako na ustawi wa nchi halafu wanakuja mbele kukukamata na kukufungulia mashtaka ya uhalifu wa kivita kwa silaha alizokuuzia mwenyewe na washirikina wake...hovyo kweli hii.

Kwanini wasiwaambie ukweli kwenye hili wanaogopa nini ?kilichotokea Liberia tumekiona Tailor yuko the Hague sasa! Al Bashir wa Sudan wamemkosakosa lakini bado wanamtafuta, kilichotokea Congo kinajulikana Pierre Bemba yuko nyuma ya vyuma, waliobaki wanaendeleza ukatili ule ule! Burundi Rwanda nk nk hali si shwari.

Kujitoa kwenye hii mahakama ni jambo la kinafiki mno lakini pia lenye kutisha kabisa! Hii mahakama iliwapunguza spidi sasa wanajitoa ngoja tuone mwisho wake.
 
Mkuu hawa viongozi wa Afrika wana unafiki sana,kwanza wanajitoa ni kweli kupisha uonevu wa hiyo mahakama au ni njia ya kushikiria madaraka na uonevu juu ya raia wake? maana hapo nawaona ni viongozi ma dikteta ndio wamekomalia kwelikweli
 
Mkuu hawa viongozi wa Afrika wana unafiki sana,kwanza wanajitoa ni kweli kupisha uonevu wa hiyo mahakama au ni njia ya kushikiria madaraka na uonevu juu ya raia wake? maana hapo nawaona ni viongozi ma dikteta ndio wamekomalia kwelikweli
Wana sababu zao za kutisha sana na hii kitu inanipa hofu kubwa kwakuwa huko tuendako huko..!
 
Huu ni mlolongo wenye kitanzi chenye mchanganyiko mkubwa! ni zaidi ya bomu la nucleur
 
Wasipotukazia hivyo tutachinjana kama kuku!

Wanatupa silaha kujilinda, ila sisi tunazitumia kuuana!

Tatizo hapo si mzungu bali sisi wenyewe!

[HASHTAG]#Waafrika[/HASHTAG] & Waarabu ni nuksi sana#
 
Wasipotukazia hivyo tutachinjana kama kuku!

Wanatupa silaha kujilinda, ila sisi tunazitumia kuuana!

Tatizo hapo si mzungu bali sisi wenyewe!

[HASHTAG]#Waafrika[/HASHTAG] & Waarabu ni nuksi sana#
Tunapata picha gani hapa?
1477194990084.jpg
1477195003089.png
European union wauza silaha wakubwa duniani ndio wametoa fungu nono kwa ajili ya mahakama hiyo
Acha uwiano uwe 9/12 sioni hata ndururu ya mwafrika hapo
 
Unajua kipindi viongozi wa kiafrika wanasign kujiunga na hiyo mahakama hawakujua kua haibagui mtu hata wao kama viongozi wanapelekwa. Wao target Yao ilikua kwa wapinzani wao kisiasa kuja kutahamaki wao ndio hasa wateja kwani wengi wao ni wauaji. Sasa wanahaha kujiondoa kwa sababu za kitoto wakati tunajua huku nyumbani wamejiwekea kinga ya kutoshitakiwa kwa kosa lolote. Africans tuna safari ndefu sana kuwa modern society. Pia tunatia aibu sana
 
Unajua kipindi viongozi wa kiafrika wanasign kujiunga na hiyo mahakama hawakujua kua haibagui mtu hata wao kama viongozi wanapelekwa. Wao target Yao ilikua kwa wapinzani wao kisiasa kuja kutahamaki wao ndio hasa wateja kwani wengi wao ni wauaji. Sasa wanahaha kujiondoa kwa sababu za kitoto wakati tunajua huku nyumbani wamejiwekea kinga ya kutoshitakiwa kwa kosa lolote. Africans tuna safari ndefu sana kuwa modern society. Pia tunatia aibu sana
Ona Burundi alivyokurupuka akataka kujitoa haraka haraka lakini akaambiwa asome katiba ya ICC kwanza (kumbe hata walikuwa hawajaisoma) kwamba unatakiwa kwanza utoe notice ya mwaka mmoja ukieleza kusudio la kujitoa ndio mchakato uanze!
Africa kusini baada ya kugundua hilo ndio nao sasa wameanza mchakato wa kujitoa
Wazungu wametutangulia kifikra kujiunga ni rahisi kujitoa sasa! Hao wanaotaka kujitoa watakumbana na vikwazo huko mbeleni vitakavyokwamisha mchakato wa kujitoa kaazi kweli kweli
 
Hii Mahakama ilianzishwa kwa makusudi mema lakini imegeuka kama fimbo ya kuchapia wanyonge.

Kama ICC ingekuwa Mahakama ya kutenda haki, leo hii Bush na Blair wangeshashtakiwa.

Kama vuguvugu la Africa kujitoa ICC litafanikiwa, tutashuhudi makundi mengi sana ya uhasi Africa.Wazungu watafanya kila mbinu kuhakikisha wanawabana viongozi wasiowapenda.
 
Hii Mahakama ilianzishwa kwa makusudi mema lakini imegeuka kama fimbo ya kuchapia wanyonge.

Kama ICC ingekuwa Mahakama ya kutenda haki, leo hii Bush na Blair wangeshashtakiwa.

Kama vuguvugu la Africa kujitoa ICC litafanikiwa, tutashuhudi makundi mengi sana ya uhasi Africa.Wazungu watafanya kila mbinu kuhakikisha wanawabana viongozi wasiowapenda.
CHARMILTON baba mwenye nyumba hashtakiwi, Ukiangalia bajeti ya ICC kwa asilimia 90 no umoja wa ulaya na miundombinu pia na hata makao makuu yako huko kwahiyo hapo unaweza kupata picha pana zaidi
 
Hii Mahakama ilianzishwa kwa makusudi mema lakini imegeuka kama fimbo ya kuchapia wanyonge.

Kama ICC ingekuwa Mahakama ya kutenda haki, leo hii Bush na Blair wangeshashtakiwa.

Kama vuguvugu la Africa kujitoa ICC litafanikiwa, tutashuhudi makundi mengi sana ya uhasi Africa.Wazungu watafanya kila mbinu kuhakikisha wanawabana viongozi wasiowapenda.
Sudan kusini nani anawachochea, burundi, kongo kabila mda wake umeisha bado tu anapiga brah brah. Sisi waafrika tunapenda sana madaraka bila kujali utu. Tutajie mtu aliepelekwa ICC alieonewa. Haya tumejitoa sababu wazungu hawajapelekwa. Mkurunzinza atapekekwa mahakama ipi? Ana kinga katika nchi yake na viongozi wengine wanaoonea wananchi wao je haki zao zitalindwa vipi?
 
Unajua kipindi viongozi wa kiafrika wanasign kujiunga na hiyo mahakama hawakujua kua haibagui mtu hata wao kama viongozi wanapelekwa. Wao target Yao ilikua kwa wapinzani wao kisiasa kuja kutahamaki wao ndio hasa wateja kwani wengi wao ni wauaji. Sasa wanahaha kujiondoa kwa sababu za kitoto wakati tunajua huku nyumbani wamejiwekea kinga ya kutoshitakiwa kwa kosa lolote. Africans tuna safari ndefu sana kuwa modern society. Pia tunatia aibu sana
Saf
 
Sudan kusini nani anawachochea, burundi, kongo kabila mda wake umeisha bado tu anapiga brah brah. Sisi waafrika tunapenda sana madaraka bila kujali utu. Tutajie mtu aliepelekwa ICC alieonewa. Haya tumejitoa sababu wazungu hawajapelekwa. Mkurunzinza atapekekwa mahakama ipi? Ana kinga katika nchi yake na viongozi wengine wanaoonea wananchi wao je haki zao zitalindwa vipi?
CHARMILTON baba mwenye nyumba hashtakiwi, Ukiangalia bajeti ya ICC kwa asilimia 90 no umoja wa ulaya na miundombinu pia na hata makao makuu yako huko kwahiyo hapo unaweza kupata picha pana zaidi
Kwanza kabisa Africa inatakiwa ipatiwe elimu ili ielimike.

Pili, tuwe na demokrasia, uzalendo na utu baina yetu.Halafu tupigane kujipatia uhuru wa kiuchumi ili sisi tuwe na uwezo wa kufanya maamuzi yetu sisi wenyewe.
 
Africa haichangii bajeti ya umoja wa mataifa. Hatujawahi kuipigania kujitoa hata makao makuu ya umoja wa africa tatujajenga tumejengewa na hao wakubwa. Hivi mnyonge yupi ameonewa na ICC. uhuru ni mnyonge? Bashir ni mnyonge? Bemba ni mnyonge? Ruto, mugabe au wakija hapa kwetu kumfuta shein nae ni mnyonge. Mimi na wewe ndio wanyonge as long tunaishi bila kunyanyasa watu ICC haituhusu. ICC itamuhusu mtu au kiongozi anaeamini katika maguvu na sio maridhiano.
 
Back
Top Bottom