Unafiki huu wa kujitoa ICC

Kwanza kabisa Africa inatakiwa ipatiwe elimu ili ielimike.

Pili, tuwe na demokrasia, uzalendo na utu baina yetu.Halafu tupigane kujipatia uhuru wa kiuchumi ili sisi tuwe na uwezo wa kufanya maamuzi yetu sisi wenyewe.
Hiyo elimu itatoka huko huko kwa njia ya ufadhili na misaada
Wazungu hawako tayari hata siku moja kuona Afrika iko huru kiuchumi kifikra na hata mitazamo, bado wanapenda sisi tuwasikilize na kuwategemea wao kwenye kila kitu. ndio maana wako tayari kutupa misaada ya vitu visivyo na tija na vyenye madhara kama silaha lakini sio elimu yenye ukombozi wa kifikra
Hizi tawala magumashi na katili za kiafrika zote zina mkono wa ngozi ya kitimoto. .jamaa wanacheza na akili zetu watakavyo
 
Hiyo elimu itatoka huko huko kwa njia ya ufadhili na misaada
Wazungu hawako tayari hata siku moja kuona Afrika iko huru kiuchumi kifikra na hata mitazamo, bado wanapenda sisi tuwasikilize na kuwategemea wao kwenye kila kitu. ndio maana wako tayari kutupa misaada ya vitu visivyo na tija na vyenye madhara kama silaha lakini sio elimu yenye ukombozi wa kifikra
Hizi tawala magumashi na katili za kiafrika zote zina mkono wa ngozi ya kitimoto. .jamaa wanacheza na akili zetu watakavyo
Kuna haja ya Afrika kuwa wabishi kama NK na Russia, tofauti na hapo hakuna namna.
 
Unasingizia wazungu kukwepa udhaifu wako. Kwani hao wazungu walipewa elimu na bara gani? Na kwa nini wewe bado usubiri uletewe elimu na hao. Sikiliza sisi waafrika hatujawahi kupendana na kujijali. Chukua mfano wa tukio la kagera hivi ile misaada tuliyochangia tuliichangia serikali au wanyonge wenzetu.? Hadi leo mwezi mmoja wale waathirika wamesaidiwa nini?botha alikua right labda sisi bado tuko ktk evolution towards humanity
 
Kuna haja ya Afrika kuwa wabishi kama NK na Russia, tofauti na hapo hakuna namna.
North korea serikali Yao inawekeza zaidi kwa watu wake na hamna brah brah. Hao russia hakuna ubaguzi wa kutoa elimu kwa watu wake kama sisi hapa. Wao hawatoi mkopo wa elimu wao wanatoa elimu. Sisi hata mikopo ni siasa tu. Vyuo vimefungua, serikali wanadai uhakiki wa mikopo siku zote walikuwa wapi.? Haya watoto watasoma mda gani? Afrika haiwezi kukomaa.
 
North korea serikali Yao inawekeza zaidi kwa watu wake na hamna brah brah. Hao russia hakuna ubaguzi wa kutoa elimu kwa watu wake kama sisi hapa. Wao hawatoi mkopo wa elimu wao wanatoa elimu. Sisi hata mikopo ni siasa tu. Vyuo vimefungua, serikali wanadai uhakiki wa mikopo siku zote walikuwa wapi.? Haya watoto watasoma mda gani? Afrika haiwezi kukomaa.
Ukisoma historia za mataifa/jamii zilizofanikiwa kimaendeleo utagundua hakuna waliopita njia tunazopita/tumia.
 
Kuna haja ya Afrika kuwa wabishi kama NK na Russia, tofauti na hapo hakuna namna.

Ili uwe mbishi

1. Uwe na bajeti yako isiyoteteleka 100%
kwetu Africa sidhali hili kuwezekana au la kwa maifa machache sana.

2. Uwe na Sayansi na Teknolojia yako kujitoshereza kiuchumi kwa kila jambo

3. Uwe na masoko yako ilikukidhi mahitaji yako kisera, kiuchumi nk

Hayo yoote kwetu Afrika hayapo.

Haiwezekani kabisa kujisimia sisi wenyewe
 
Ili uwe mbishi

1. Uwe na bajeti yako isiyoteteleka 100%
kwetu Africa sidhali hili kuwezekana au la kwa maifa machache sana.

2. Uwe na Sayansi na Teknolojia yako kujitoshereza kiuchumi kwa kila jambo

3. Uwe na masoko yako ilikukidhi mahitaji yako kisera, kiuchumi nk

Hayo yoote kwetu Afrika hayapo.

Haiwezekani kabisa kujisimia sisi wenyewe
Ningependa sana kama USSR ingekuwa hai ili tuwe na dola mbili kubwa, pengine tungekuwa na option.

Lakini USSR ilishakufa kutokana na sera zao mbovu za kiujamaa.Kwa maana hiyo hatuwezi kuendelea kwa kutegemea kushikwa mikono na wazungu, inabidi tuanzishe misingi yetu ya maendeleo.

Tujijenge sisi wenyewe ili tuweze kusimama huru, kwani wao waliposimama[e.g China] nini kiliwasaidia?
 
Njia sahihi ni ile ya hayati baba wa Taifa Mwl JK Nyerere ambayo sasa imetupwa...Nikijikita hapa kwetu Tanzania

1. Kupeleka vijana wakitanzania kusoma huko ughaibuni kwa maelefu....Tupate teknolojia.....kisha kuwarejesha hapa kulitumikia Taifa

2. kujenga viwanda kwa gharama yoyote nakuwaweka vijana waliopata elimu nje na ndani (mchanganyiko wa waliosoma hapa na waliopelekwa nje kupata uwakilishi na mnyumbuliko wa Teknolojia)

3. kusimamia kwa nguvu zote nidham na uwajibikaji kwenye viwanda kuhakikisha haviendi kwa hasara na havihujumiwi

4. Kuhakikisha wafungwa wote wanatumika kwa faida mikowa yote...kwenye viwanda, mashamba ya kilimo, migodi nk

5. KuhakikishaJKT wanapewa nyenzo na maeneo ya uzalishaji....wanapewa elimu nakushilikishwa 100% kwenye shughuli za uchumi.

6. Kusimamisha usajiri na utowaji leseni za migodi mipya mpaka pale sera nzuri mpya ya madin kwa faida ya Watanzania imepatika nakukubaliwa.

7. Kuacha demokrasia huru ilikuweka mazingira ya watu kukosoa kwa uwazi ilikufanya marekebisho kulingana na wakosoaji, mahitaji ya Taifa na kuendana na wakati.

Hatuwezi kutoka kama
a) Elimu bora =0

b) Teknolojia =0

c) viwanda =0

d) Ushirikishwaji=0

e) Demokrasia = 0

nk.
 
Naona kuna mwamko mkubwa sana wa nchi za kiafrika ambazo ni wanachama wa mahakama ya kimataifa ya uhalifu wa kivita kujitoa kwa kisingizio cha kuwa eti wanaoandamwa ni viongozi wa kiafrika tu
Tangu kuanzishwa kwake mwaka 2002 huku nchi nyingi za kiafrika zikishadadia kwa nguvu sana kati ya kesi 12 zilizotolewa maamuzi 9 ni za viongozi wa Afrika
Naita ni unafiki kwakuwa viongozi hawa hawawaambii ukweli hao pimbi bwana wakubwa wanaowapeleka watakavyo viongozi wetu haya wenye akili finyu sana
Wanapopambana kubaki madarakani hata kwa gharama ya damu isiyo na hatia! Wanapominya demokrasia, wanapoua kwa kisingizio cha kuzima uasi na kulinda nchi misaada ya hali na mali miundombinu silaha na vifaa vya kijeshi vyote hivi hupata toka kwa hao hao pimbi waanzilishi wa hiyo mahakama ya uhalifu wa kivita ambayo makao yake makuu yako The Hague nchini Uholanzi
Leo anakuuzia silaha kwa mlango wa nyuma unapaisha uchumi wake, kisha unatumia hizo silaha kuangamiza wananchi wako na ustawi wa nchi halafu wanakuja mbele kukukamata na kukufungulia mashtaka ya uhalifu wa kivita kwa silaha alizokuuzia mwenyewe na washirikina wake...hovyo kweli hii
Kwanini wasiwaambie ukweli kwenye hili wanaogopa nini ?kilichotokea Liberia tumekiona Tailor yuko the Hague sasa! Al Bashir wa Sudan wamemkosakosa lakini bado wanamtafuta, kilichotokea Congo kinajulikana Pierre Bemba yuko nyuma ya vyuma, waliobaki wanaendeleza ukatili ule ule! Burundi Rwanda nk nk hali si shwari
Kujitoa kwenye hii mahakama ni jambo la kinafiki mno lakini pia lenye kutisha kabisa! Hii mahakama iliwapunguza spidi sasa wanajitoa ngoja tuone mwisho wake
Wakifanikiwa gawa viongozi madikteta wa afrika kujitoa. Bas wananchi waafrika tujiandae kufanywa vyovyote watakavyo mana hawakuwa na wa kuwabana.
Uwepo wa ICC angalao kwa kiwango fulani kumesaidia kupunguza kasi ya uhalifu wa viongozi wetu. Sasa itokee viongozi hawa wawehuru hawahusiki tena na ICC pigeni picha hali itajuwavipi
 
Tukijadili unafiki wa viongozi unaoneka vizuri sana kwa mambo yafuatayo

1. Unafiki nipale wao wanawajibishwa nakupewa adhabu kutokana na udhalimu wao...mfano

-Burund Nkrunziza kaua wengi na bado anauwa

-Sudan Bashir ameua sana daful mpaka tukaifaham huku na bado anauwa

-Uganda, Museven anatawala kwa lazima na nguvu kubwa

-Kenya, Uhuru na makamo wake walisababisha maafa makubwa na bado.....

-Tanzania, haileweki kinachoendelea zanzibar kama ni amani au utawala wa mkono wa chuma

-Zimbabwe, Babu mgabe amepiga nakutesa kiasi kwamba ukiingia mgahawani kupata sahani ya wali uandae Zim dola zaid ya 100,000....uchumi umeharibka vibaya....above 90yrs old bado yupo ikulu...very wondeful..

-DRC, Kabira junior...Katiba anaikanyaga kanakwamba ikulu mali yake....watu wanauwawa nk

nk nk

unafiki wa hawa wakwetu wao kuuwa na kutesa saaafi ila wanapogeuziwa kibano na hiyo mahakama hawataki

Amakweli

MKUKI KWA NGURUWE....kwa mwandamu....
 
Ona Burundi alivyokurupuka akataka kujitoa haraka haraka lakini akaambiwa asome katiba ya ICC kwanza (kumbe hata walikuwa hawajaisoma) kwamba unatakiwa kwanza utoe notice ya mwaka mmoja ukieleza kusudio la kujitoa ndio mchakato uanze!
Africa kusini baada ya kugundua hilo ndio nao sasa wameanza mchakato wa kujitoa
Wazungu wametutangulia kifikra kujiunga ni rahisi kujitoa sasa! Hao wanaotaka kujitoa watakumbana na vikwazo huko mbeleni vitakavyokwamisha mchakato wa kujitoa kaazi kweli kweli
Na kama Nchi zote hapa Africa zimejitoa hivyo vikwazo vitamwathili nani....??
 
Hakuna.umuhimu wa iyo mahakama Afrika.ijitegemee ss hv, Mwl Nyerere aliwah kitoa mfano sema wazee wa zaman hawakumwelewa wakabak kupoga makofi na kucheka.na nina.uhalika wengi wao speech za yule mzee walikuwa hawamuelew wanabak kicheka.tu, alisema
Kuna siku miti midogo porin ilianza kupiga kelele jaman mashoka hayo yanapita, miti mikubwa yako wapi na yanaenda wap, miti midogo ikajib yanakwenda porin, miti mikubwa yana wajomba, miti midogo hapana hayama wajomba, miti mikubwa ikasema.kwa dharau hayana madhara tulieni, siku yanarud miti midogo.kama kawaida ikaanza kupiga.kelele jaman mashoka yanarud, miti mikubwa yako wap? Miti midogo hayo yanapita, miti mikubwa yana wajomba? Miti midogo ikajib ndio yana.wajomba. miti mikubwa ikasema ss tumekwisha wote, wajomba kimaanisha mipini. Nn maana ya huu msemo wa mwl kwa mwenye tafakar zaidi?
 
Tukijadili unafiki wa viongozi unaoneka vizuri sana kwa mambo yafuatayo

1. Unafiki nipale wao wanawajibishwa nakupewa adhabu kutokana na udhalimu wao...mfano

-Burund Nkrunziza kaua wengi na bado anauwa

-Sudan Bashir ameua sana daful mpaka tukaifaham huku na bado anauwa

-Uganda, Museven anatawala kwa lazima na nguvu kubwa

-Kenya, Uhuru na makamo wake walisababisha maafa makubwa na bado.....

-Tanzania, haileweki kinachoendelea zanzibar kama ni amani au utawala wa mkono wa chuma

-Zimbabwe, Babu mgabe amepiga nakutesa kiasi kwamba ukiingia mgahawani kupata sahani ya wali uandae Zim dola zaid ya 100,000....uchumi umeharibka vibaya....above 90yrs old bado yupo ikulu...very wondeful..

-DRC, Kabira junior...Katiba anaikanyaga kanakwamba ikulu mali yake....watu wanauwawa nk

nk nk

unafiki wa hawa wakwetu wao kuuwa na kutesa saaafi ila wanapogeuziwa kibano na hiyo mahakama hawataki

Amakweli

MKUKI KWA NGURUWE....kwa mwandamu....
Marekani na washirika wake pale Libya kaua wangapi....???

Marekani na washirika wake pale Iraq kauwa wangapi....???

Marekani pale Japan Nagashaki na Heshiroma kauwa wangapi...??

Marekani pale Syria alishaua wangapi kabla Vladimir Putin kuingilia....??

Israel walishaua wangapi pale Palestina...??

Bado Somalia, Afghanistan
Nk..........!!!

Lakini unajifanya huoni wala husikii.....
Wewe macho yote Africa tuu
 
Viongozi wa Afrika wanaweza kuwa na matatizo, tena matatizo makubwa sana lakini ICC haina utakatifu wa kuwahukumu hao viongozi wakati wanakunywa juice na Tony Blair na George Bush. Mahakama ya kihuni kabisa.
 
Viongozi wa Afrika wanaweza kuwa na matatizo, tena matatizo makubwa sana lakini ICC haina utakatifu wa kuwahukumu hao viongozi wakati wanakunywa juice na Tony Blair na George Bush. Mahakama ya kihuni kabisa.
Wao ndio wafadhili
Wao ndio walipa mishahara
Wao ndio wenye ardhi
Wao ndio wenye majengo
Wao ndio wenye miundombinu na facilities zote
Kuamini kuwa wanaweza kututendea haki .......
 
Lakini nchi inayokuja kuwa ya kidikteta zaidi ni Tanzania. Endeleeni tu na pambio la nchi ya amani. Msimamo wangu ni kuwa bado nchi hiyo inahitaji kiongozi wa busara kama Lowassa. Nilimuunga mkono Lowassa akiwa CCM na baada ya kutoka CCM na hadi leo najiona nilikuwa sawa. Baadae watu wakianza kutafuta haki aidha kwa maandamano nawaambia mtauliwa kama mende. Subirini hadi 2020 atakapomaliza muda wake.
 
Back
Top Bottom